coscated
JF-Expert Member
- Nov 17, 2010
- 2,919
- 1,968
Ndivyo unavyoamini mkuu?
Wengi hamuelewi majukumu ya mwanaume hasa anapoamua kuwa Baba wa familia,nimekuwa na rafiki zangu ambao wanaendekeza huu umwamba ila kila wakati jasho lao hulitumia kwa maumivu makali sana mf:yupo mmoja siku hiyo anaogopa kupokea simu ananiambia niipokee mimi nidanganye amesahau simu kisa anayepiga ni ma.laya wake aliyemuahidi kumlipia kodi miezi 6 Tabata (yeye mwenyewe anaishi chumba na sebule Tegeta na familia) acha mizinga ya saloon etc na maendeleo hana.
Ukitoa kuogopa dhambi ya uzinzi kutulia na mwanamke mmoja kuna manufaa sana (wachache wamefanikiwa kuyajua),kwanza unakuwa huru mimi simu zangu muda wowote mahali popote mke wangu anashika passwords zote anazijua wakati mwengine nikiwa mbali hutoa yeye maelezo,kufanya sex iliyo safi na kwa uhuru,salama na ya furaha,wakati fulani bado mgeni kwenye ndoa mke wangu alipojifungua first born wetu nikaiga kutoka nje nilikutana na ex ujinga ujinga nikajaa,hofu hofu nimevaa mipira nikiwaza gharama nilizotumia mpaka kukamilisha hiyo mission nikaona ni ujinga,ukishakuwa na watoto wawili+ (though ninao wawili bado nitaongeza Mungu akipenda najiona niko aged 50) najua ndoto zao nimezibeba mimi kutumia pesa 100K pasi na manufaa siioni faida yake zaidi nitawaza niifanyie nini kwa kesho yao au bora waitumie wao kuvaa kula ada etc.
Kuwa muaminifu kwenye ndoa hukupa amani ya maisha,muda wote nyumba inatamalaki furaha mke anacheka watoto wanafurahi hakuna hisia mbaya dhidi yako watoto wanaijua ratiba ya Baba yao kurudi nyumbani ni furaha sana unaingia home watoto wanakufurahia na wanakupa taarifa siku yao ilivyoisha najua hata siku sipo wataukumbuka uwepo wangu (ukiwa mzinzi haya yote utayafanya muda gani wakati ukirudi wamelala?)