Elections 2010 Je kuna haja ya kupiga kura Tanzania?

QUALITY

JF-Expert Member
Sep 27, 2010
853
115
Uchaguzi wa mwaka huu unatupatia mafunzo mengi sana. Matokeo ya udiwani na ubunge katika majimbo mengi yameishatangzwa. Katika majimbo mengi, hakukuwa na ulalamishi kwa sababu karatasi kutoka kwa mawakala zimetumika kujumlisha matokeo. Katika majimbo mengine kumwkuwa na fujo kwa sababu fulani akishinda, kura hazitangazwi. Mfano ni Ubungo, Kawe, Nyamahana n.k. Mpaka kura zihesabiwe mara tatu tatu. kama karatasi zilizotumika kuhesabu na kusainiwa na mawakala zipo, ya nini kuhesabu upya? Halafu kujumlisha kura ni zoezi la dakika kati ya 30 na 60, iweje itumie siku mbili au zaidi? wanatumia calculator au kuhesabu vidole?

Hapa kuna hoja kubwa ya kufanyia kazi. Kama kura za kina Mnyika zinachezewa inawezekana ni kwa sababu wakurugenzi wenyewe wanahofia kutamka kura hizo maana watapoteza kazi.

kwa jimbo la Segerea, ni tusi kwa wapiga kura kumtangaza Mahanga Makongoro. Mahanga kutangazwa mshindi ni kuwambia wapiga kura wa jimbo la segerea hawakuwa na haja ya kwenda kujipanga na kupiga kura kwa mtu wanayemtaka (Mpendazoe) na kisha wao wanamtangaza aliyeshindwa kuwa ndiye mshindi. Hapo haki iko wapi?

Halafu hapo ni katika jimbo ambalo ni dogo na ni rahisi kufuatilia kwa karatasi toka kwa mawakala. Je kwa rais ambaye karatasi hizo hatunazo? ufuatiliaji katika nafasi ya Urais unaweza kufanyikaje kwa usahihi? Je siyo nafasi ya kuwakatisha tamaa wapiga kura ili waseme "Hata nikipiga kura, zitaibiwa". Ili watawala, waendelee kutawala milele.

Mimi nadhani watanzania watapiga kura tutakapokuwa na tume huru ya Uchaguzi na tusitumie wakurugenzi wa Halmashauri kusimamia uchaguzi ambao wameteuliwa na Rais!!
 
Bado kuna haja kupiga kura.

Kama watu wasingepiga kura hawa wabunge walioshinda (kwa vyama vyote) tungewapataje?
 
You have a point, but Lakini kwanini maamuzi ya wananchi hayaheshimiwi? kweli wanaoshindwa na kuchakachua wana nia ya kuwawakilisha watanzania au wana lao jambo?
 
Kuna haja ya kupiga kura lakini baada ya wizi wa kishindo sijui kama watu watajitokeza kupiga kura tena hasa kwa Tanzania bara
 
Zamani nilikuwa sioni umuhimu. Lakini nakwambia kuna mapinduzi makubwa sana. Elimu tu, na matumaini mapya vitawafanya watu waone umuhimu wa kupiga kura kiasi ambacho wezi wataumbuka na kuiba watashindwa. Sivunjiki moyo tena kupiga kura maana matumaini yapo karibu sana.
 
Naomba nieleze habari ambayo nimeikumbuka baada ya kusikia matokeo ya Urais. Habari yenyewe iko hivi:

Wakati kampeni zimepamba moto huku maeneo ya Babati vijijini, siku moja nilikuwa na katibu wa Tawi la CCM katika sherehe. Wakati tunajadiliana juu ya ushindi ambao anaweza kuupata Dr. Slaa katika uchaguzi wa Oktoba 2010, yule katibu wa CCM alituambia jambo ambalo leo nikilikumbuka natamani nilie.

Yule katibu wa CCM alituambia kuwa Mkuu wa wilaya ya Babati aliwambia viongozi wa CCM katika tawi hilo kwenye vikao vya ndani kuwa "msihangaike na kura ya urais kwani hizo zipo tayari ila ninyi hangaikeni na kura za madiwani na mbunge kwani hao ndiyo watu wenu". Kwa matokeo haya ya sasa ambayo Jk ana kura nyingi ambazo zinamshangaza kila mmoja, nina kosa la kusema.

Hakika demokrasia imebakwa, Watanzania tumebakwa tena mchana. Kama mimi ni mwongo.....
 
Haja ya kupiga kura ipo, tena ni haki ya msingi kabisa ya kila MTANZANIA kama Bunge litasimamia mabadiliko ya KATIBA iwe ya vyama vingi kuliko hii ya sasa ni chama kimoja. Bila kubadilisha katiba tutakuwa tunatwanga maji kwenye kinu.
 
Nakubaliana na maneno yako muungwana Quality.

Kuwahamasisha wananchi waache shughuli zao ili wajiandikishe, kushiriki mchakato wa kampeni na hatimaye kupiga kura BILA YA KUWA NA UTARATIBU TIMAMU KABISA WA KUJUA NANI MSHINDI, Nasema kwa kwa KINYWA KIPANA kwamba hiyo NI KAZI BURE. Sawasawa kabisa na KUTWANGA MAJI KWENE KINU. Vyama vyote vya upinzani vinavyojali mustakabali wa nchi hii viliangalie hili kwa kina katika chaguzi zijazo. Visijitumbukize kwene chaguzi kwa mihemuko na wala visiwachoshe watz kama hazina mikakati ya kuondoa udhaifu huu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom