Je, kuna haja ya kuendelea na mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini Tanzania

chuuma

JF-Expert Member
May 19, 2015
363
557
JE KUNA HAJA YA KUENDELEA NA MFUMO WA VYAMA VINGI NCHINI TANZANIA?

Na Kilawa the Iron

La hasha!
Mh. John Pombe Magufuli Rais wa jamhuri ya Muungano Tanzania alipokuwa akihutubia katika sherehe za miaka 39 ya kuzaliwa kwa chama cha mapinduzi (CCM) zilizofanyika mkoani Singida aliibuwa maswali mengi na mjadala mkubwa kwa wananchi hasa wa vyama vya upinzani na wasomi wa kada
mbalimbali.

Kauli nyingi alizotumia Mh Dr. Magufuli katika maazimisho hayo ziliibuwa mjadala mzito katika mitandao ya kijamii, vijana wengi wa upinzani na wasomi wengi walikosoa vikali kauli za mh Rais lakin pia wapo waliompongeza kwa kauli zake alizozitumia.

Yawezekana Rais alitumia kauli hizo kwa nia njema, au kwa kutokutambua faida na madhara yake katika jamii au alitumia kauli hizo kwa furaha za ushindi aliopewa na kuwa Rais wa awamu ya tano wa jamhuri ya muungano Tanzania.

Moja ya kauli iliyoonekana inamkanganyiko mkubwa na ya kidikteta ni hii hapa nanukuu "Hakuna mtawala yeyote anayependa kutawaliwa, na bahati mbaya atawaliwe na vyama vya hovyo hovyo, vya ajabu ajabu"

Wananchi wengi, wasomi na wasio wasomi walijiuliza kupitia mitandao ya kijamii na hata kwenye vijiwe mbalimbali nilivyopita. walijiuliza
Je kuna haja gani ya kuita nchi yetu ni ya mfumo wa vyama vingi?
Je Rais John Pombe Magufuli amesahau kwamba yeye mwenyewe alisema atakuwa Rais wa wote?

Lakini katika yote hayo wapo walioongeza na kijadili zaidi juu ya sakata la Zanzibar, watu hawa waliendelea kusema yawezekana matokea ya Zanzibar yaliyofutwa na Bwana Jecha ambaye ndiye mwenyekiti wa ZEC yalipangwa na Viongozi wa juu wa CCM kwa kuwa hawapo tayari kutawaliwa. Wakaongeza kwa kusema Mh Rais atangaze tu hadharani kuwa mfumo wa vyama vingi umefutwa ili ijulikane moja badala ya nyingi.

Mh Rais hakuzungumza maneno hayo tu juu yaliyoibua mjadala pia alisema
"Mimi Rais, lakini ni Rais niliyechaguliwa na chama cha mapinduzi.......... Ambayo ukweli serikali hii nimepewa na chama cha mapinduzi....... Kisingekuwa chama cha mapinduzi leo nisingekuwa Rais "

Hakuishia hapo aliongeza kwa kusema"Mimi mh m/kiti nakuhakikishia serikali ninayoiongoza itaendelea kuwa nakuonesha Mshikamano mkubwa na Chama Cha Mapinduzi, Hakuna serikali kama hakuna CCM"

Hapa ndipo palipowadhihirishia wananchi kuwa upinzani si kitu ndani ya Tanzania, na ndio maana wabunge wa upinzani wankamatwa hovyohovyo na polisi, wanachama na baadhi ya viongozi wa upinzani kupigwa, kuumizwa na hata kuuwawa.

Katika haya yote Mh Rais ameonekana kwamba ana dhamira ya kumaliza upinzani na sio kuimarisha demokrasia, kitendo cha kusema serikali ya awamu yake itashikamana na CCM inaonesha kuwa upande wa upinzani hawana nafasi katika nchi yao inayojinasibu kuwa ni ya kidemokrasia.

Anaposema "hakuna serikali kama hakuna CCM"sasa kuna haja gani ya kufanya uchaguzi na kupoteza mabilion ya pesa ilihali wao wanajua watatawala milele. Wanafanya uchaguzi kuridhisha mataifa ya kibepari aua kuridhisha wananchi au?

Kuna haja kubwa kutengeneza katiba mpya ya nchi yetu ili maswala ya kidemkrasia yapewe nafasi badala ya kupuuzwa kama chama tawala kinavyofanya.
Msema kweli ni adui wa wapenda maovu
 
na ndio maana awataki kuachia madaraka zanzibar na pia tuwe wawazi machafuko ndani ya nchi hii si zenj wala bara yataletwa na viongozi wa ccm hilo lipo vuteni subira mtaona
 
Magufuli amesahau kwamba alidandia muujiza wa mwenzake..chama cha mapinduzi walikwiba kura za wananchi...aendelee kujilisha upepo kwa maneno yake yaliyochanganikana na kilevi kiitwacho MADARAKA..Tanzania mpya inakuja..
 
Ndiyo tatizo la kuwa mtawala, badala ya kuwa kiongozi
 
JE KUNA HAJA YA KUENDELEA NA MFUMO WA VYAMA VINGI NCHINI TANZANIA?

Na Kilawa the Iron

Nakubaliana na wewe kuwa kuna haja ya kuwa na Katiba Huru na Madhubiti. Sikubaliani na wewe kuwa JPM kushabakia CCM ni tatizo. Magufuli ni CCM na CCM ni Magufuli.

La hasha!
Mh. John Pombe Magufuli Rais wa jamhuri ya Muungano Tanzania alipokuwa akihutubia katika sherehe za miaka 39 ya kuzaliwa kwa chama cha mapinduzi (CCM) zilizofanyika mkoani Singida aliibuwa maswali mengi na mjadala mkubwa kwa wananchi hasa wa vyama vya upinzani na wasomi wa kada
mbalimbali.

Kauli nyingi alizotumia Mh Dr. Magufuli katika maazimisho hayo ziliibuwa mjadala mzito katika mitandao ya kijamii, vijana wengi wa upinzani na wasomi wengi walikosoa vikali kauli za mh Rais lakin pia wapo waliompongeza kwa kauli zake alizozitumia.

Yawezekana Rais alitumia kauli hizo kwa nia njema, au kwa kutokutambua faida na madhara yake katika jamii au alitumia kauli hizo kwa furaha za ushindi aliopewa na kuwa Rais wa awamu ya tano wa jamhuri ya muungano Tanzania.

Moja ya kauli iliyoonekana inamkanganyiko mkubwa na ya kidikteta ni hii hapa nanukuu "Hakuna mtawala yeyote anayependa kutawaliwa, na bahati mbaya atawaliwe na vyama vya hovyo hovyo, vya ajabu ajabu"

Wananchi wengi, wasomi na wasio wasomi walijiuliza kupitia mitandao ya kijamii na hata kwenye vijiwe mbalimbali nilivyopita. walijiuliza
Je kuna haja gani ya kuita nchi yetu ni ya mfumo wa vyama vingi?
Je Rais John Pombe Magufuli amesahau kwamba yeye mwenyewe alisema atakuwa Rais wa wote?

Lakini katika yote hayo wapo walioongeza na kijadili zaidi juu ya sakata la Zanzibar, watu hawa waliendelea kusema yawezekana matokea ya Zanzibar yaliyofutwa na Bwana Jecha ambaye ndiye mwenyekiti wa ZEC yalipangwa na Viongozi wa juu wa CCM kwa kuwa hawapo tayari kutawaliwa. Wakaongeza kwa kusema Mh Rais atangaze tu hadharani kuwa mfumo wa vyama vingi umefutwa ili ijulikane moja badala ya nyingi.

Mh Rais hakuzungumza maneno hayo tu juu yaliyoibua mjadala pia alisema
"Mimi Rais, lakini ni Rais niliyechaguliwa na chama cha mapinduzi.......... Ambayo ukweli serikali hii nimepewa na chama cha mapinduzi....... Kisingekuwa chama cha mapinduzi leo nisingekuwa Rais "

Hakuishia hapo aliongeza kwa kusema"Mimi mh m/kiti nakuhakikishia serikali ninayoiongoza itaendelea kuwa nakuonesha Mshikamano mkubwa na Chama Cha Mapinduzi, Hakuna serikali kama hakuna CCM"

Hapa ndipo palipowadhihirishia wananchi kuwa upinzani si kitu ndani ya Tanzania, na ndio maana wabunge wa upinzani wankamatwa hovyohovyo na polisi, wanachama na baadhi ya viongozi wa upinzani kupigwa, kuumizwa na hata kuuwawa.

Katika haya yote Mh Rais ameonekana kwamba ana dhamira ya kumaliza upinzani na sio kuimarisha demokrasia, kitendo cha kusema serikali ya awamu yake itashikamana na CCM inaonesha kuwa upande wa upinzani hawana nafasi katika nchi yao inayojinasibu kuwa ni ya kidemokrasia.

Anaposema "hakuna serikali kama hakuna CCM"sasa kuna haja gani ya kufanya uchaguzi na kupoteza mabilion ya pesa ilihali wao wanajua watatawala milele. Wanafanya uchaguzi kuridhisha mataifa ya kibepari aua kuridhisha wananchi au?

Kuna haja kubwa kutengeneza katiba mpya ya nchi yetu ili maswala ya kidemkrasia yapewe nafasi badala ya kupuuzwa kama chama tawala kinavyofanya.
Msema kweli ni adui wa wapenda maovu
 
Kuna mtu alileta uzi juu ya Magufuli kuwa ni mtu wa visasi katika uzi ule jamaa alisisitiza ikiwa Magufuli atakuja kuwa Rais basi watu watakiona cha mtema kuni. Maneno ya mleta uzi yanaanza kuthibitika kidogo dogo sasa.
 
Tukumbuke kuwa waziri mkuu alishasema kuwa Shughuli za kisiasa sasa basi. Uchaguzi umekwisha. Sasa Hapa kazi tu.
Waziri mkuu ndiye mtendaji mkuu wa serikali na alishasema wazi na kwa dhamira kabisa kuwa serikali haitaki shughuli zote za kisiasa kwa sababu uchaguzi umekwisha.
Lakini cha ajabu CCM chama dola na kinachopigana kufa na kupona ili vyama vingine vifutwe hata kwa kuua watanzania wanaofanya siasa zao kikatiba na kuwaacha majangili wanaokiunga mkono chama hicho ili tu kidumu milele kama mungu wa matumbo yao kinapiga siasa za vijembe na kejeli kila kukicha tena kikijifungamanisha na gharama za serikali kwa kuwashirikisha wajumbe kama mawaziri na Rais wao ambaye ni watendaji wanaotumia magari,ulizi na madereva wa serilali.
Tulitegemea CCM kingeonyesha kwa vitendo kumuunga mkono Rais kwa kufuta sherehe za Kuundwa tu kwa CCM na kupeleka fedha hizo kwenye Shule zake za Jumuiya ya Wazazi wa CCM ambazo zipo hoi bin Taabani na nyingine kuwapa mabalozi au wajumbe wa nyumba kumi ili wanunue hata karatasi za matumizi huko kwenye mashina badala yake CCM imeonyesha wazi kuwa haikuwa imeunga na haiungi mkono kubana matumizi kwa serikali ya Magufuli.
CCM na Mwenyekiti wake akiwemo Katibu Mwenezi wamempinga Magufuli kwa vitendo.

Jambo lingine ni lile la Nape akiungwa mkono na wabunge wote wa CCM ambao ni mizigo kwa dunia hii kufuta matangazo ya live kwa bunge eti wanapunguza matumizi lakini Tangu kuzinduliwa kwa kampeni za CCM maarufu kama siku ya kuzaliwa kwa CCM jambo ambalo hata waasisi hawakufanya hivyo Kwa kufanya maadhimisho ya wiki nzima na kuyaonyesha live kwenye vyombo vya habari pia ni kupuuza wito wa rais wa kupunguza matumizi na ule wa kinafiki wa kufutwa kwa matangazo ya live ya Bunge.
CCM ilipaswa pia isionyeshe hayo matangazo yao kupitia TBC na vyombo vingine ili kumuunga mkono waziri wao na serikali yao.
Hii ni moja kati ya sifa za mnafiki kutenda tofauti na anachosema na akiaminiwa haaminiki.

Tunaona kila kukicha CCM wakifanya shughuli za kisiasa kwa kisingizio kuwa wanaunga mkono kauli mbiu ya rais ya hapa kazi tu.
Kule Zanzibar kila siku Sheni na CCM yake wako mitaani kuhamasisha wanaCCM wajitokeze kumchagua awe rais wao CCM na Zanzibar japo ZEC imepiga marufuku kampeni kwa kuwa jecha anajua kuwa wapinzania ndio waliolengwa kuacha shughuli za kisiasa.

CCM imejipanga na serikali yake kurudisha mfumo wa Chama kimoja kwa kurudisha ule utaratibu wa chama kushika hatamu.
Mfano CCM ilijifanya kuunga mkono Magufuli alipofuta sherehe za Uhuru mwaka jana lakini ikijiandaa kufanya sherehe kubwa zaidi ya ile na kwa gharama kubwa zaidi. Huu ni unafiki uliokithiri.

Tujiulize swali dogo tu: Kama Tanzania kuna zaidi ya vyama 18 vilivyosajiliwa na kila chama kikatumia wiki moja kufanya uzinduzi ya wiki ya maadhimisha ya kuzaliwa kwa chama hicha itaku ni Takribani wiki 18 zitakuwa ni za kisiasa tu kila mwaka.Ambayo ni siku 116 . Hizi ni siku nyingi kuliko siku za kampeni ya uchaguzi mkuu.
Je,serikali ya Chama dola na dola lake la kipolisi watakubali kuona vyama vingine vikitumia haki zake za kisiasa kufanya sherehe na maadhimisho yake kama CCM ilivyofanya kitaifa?
Au tutaona sasa serikali na CCM wakija na swaga za uchaguzi umekwisha sasa shughuli za kisiasa basi?
Labda sasa tupewe maana ya shughuli za kisiasa ni nini kwani inaonekana kuwa shughuliza za kisiasa na siasa ni pale tu wapinzani wanapofanya mikutano na makongamano yao tena kwa gharama zisizohusisha bunge wala serikali wala mahakama tofauti na CCM.

Kwa hali hiyo Hapo mnategemea nini tena kama sio kufutwa kwa vyama vingi kimya kimya huku CCM ikirudia enzi zake za chama kushika hatamu!!!?
 
Kufuta upinzani hawawezi kwani haikuwa idea yao ni force toka nje!! Wanachojaribu kufanya ni kuudhoofisha. Kuwa Kiongozi ni mkusanyiko wa mambo mengi sana ila kubwa kuliko yote ni hekima na uwezo wakuona mbali. Mfano Nyerere aliona mbali kwenye mambo mengi e.g kuwaunganisha watanzania ila hakuona mabali kwenye mfumo upi ungeiwezesha tanzania kuwa taifa kubwa, Yeye alichagua ujamaa na ndio uliomuondoa madarakani na ndiye aliyetuletea umaskini huu.....!!! Mwinyi baada ya kuiingiza nchi kwenye capitalism ndio vyama hivi vikaja kwan mfumo unataka hivyo.
Ukiangalia na kumsikiliza Magufuli vizuri kama mtu unayejua hii mifumo vizuri na unayejua namna gani nchi ifanye ili iendelee utagundua mambo mengi sana. Kwanza Utaona ni Rais ambae hajui hata Katiba aliyeapa kuitumikia inasema nini. Pili utaona hajui hata mfumo upi autumie ili aweze kutimiza malengo yake, hivyo utaona anataka ujamaa, huku anataka ubepari wakati huo huo hataki vyote. Tatu Utagundua ni mtu asiyejiamini ndio maana ni mkali sana, na ukali wake ni wakujihami na hataki hata kushauriwa. Nne ni mtu mwenye nia na mzalendo ila hajui afanyeje ndio maana kuna matamko mengi sana bila ufuatiliaji. Tano hajui chanzo cha matatizo yote haya tuliyonayo na ni njia gani kuyatatua. Mfano yeye anajua kunatatizo la wakulima na wafugaji ila anaamini njia ya kulitatua ni kumtisha mkuu wa wilaya na mkoa kwa kuwaambia atawafukuza. Wakati huo huo kuna waziri wa kilimo, ufugaji....!! Yeye hakumtaja. Nini kitatokea hapo? Ni waziri kumshauri Rais awafukuze wakuu hao kwan ndio solution aliyoisuggest rais.
Mambo ni mengi labda sijaweza kuyaeleza vizuri ila naamin mmenielewa! Ninachosubiri kwa hamu sana ni wakimpa uwenyekiti wa chama hapo ndipo mtajua ni mtu wa namna gani. Atazidi kukigawa chama na atakutana na kuendelea kukidhoofisha badala ya kukijenda. Ndio maana Msekwa anataka JK aweke mambo sawa kabda hajampa JPM.
 
Tanzania sio nchini ya mfumo wa vyama vyingi,ni nchini ya mfumo wa chama kimoja,wananchi wanasapoti vyama vyingi wanafilisiwa,wanafugwa na kupotea na viongozi wa dini wamekaa kimya tu
 
Kuna mtu alileta uzi juu ya Magufuli kuwa ni mtu wa visasi katika uzi ule jamaa alisisitiza ikiwa Magufuli atakuja kuwa Rais basi watu watakiona cha mtema kuni. Maneno ya mleta uzi yanaanza kuthibitika kidogo dogo sasa.
Wengine tunashukuru Trump kaja! Acha aendelee na unyanyasaji kwa vyama Vya siasa na raia iko siku atajikuta kawaudhi wenye akili na nguvu za kijeshi. Atajuta kwanini hakufuata KATIBA YA NCHI.
 
Back
Top Bottom