Je kukwea pipa kwa jk juzi kunaonesha kuyadharau maandamano ya chadema?

Nhunda

Member
Feb 4, 2011
17
1
Ndugu wanajamii suala hili limekuwa likinipa taabu sana, inawezekanaje Rais kuondoka nchini wakati nchi yake ikiwa katika wakati fulani mgumu aidha kisiasa au kijamii. Raisi Kikwete mara baada tu ya mabomu kulipuka kule gongo la mboto aliondoka nchini, sasa hivi pia kaona maandamano yamepamba moto huko kanda ya ziwa kaondoka nchini.

Swali linakunja; Je hali hii inamaanisha kuwa JK anayadharau matukio haya au hukimbia kwenda kupumzisha akili nje ya nchi? naomba maoni yako mwana JF.
 
Nashindwa kuelewa uzalendo wa viongozi wetu wakiongozwa na Kikwete,huu ndio wakati muafaka kwake kukaa nyumbani na kama kuna haja ya kuwepo kwenye hiyo mikutano au majadiliano angeweza tu kumtuma kiongozi yeyote yule wa nhiniyake kama alivyowahi kufanya hivyo wakati wa kampeni kwenye kikao cha umoja wa mataifa kwa kumtuma waziri mkuu Pinda kwenda kumuwakilisha.Inaonekana hajali matatizo ya watanzania ambao wanaishi kwa taabu na shida kubwa.
Suala la kudharau maandamano si kweli bali anawadharau wananchi wake anaowaongoza.
 
Hiyo nikweli inaonesha yeye anaonekana kuwajali zaidi wananchi wakati anawaomba kura baada ya hapo maslahi yake anayatanguliza mbele zaidi, wananchi watafakari juu ya hili.
 
Huyu mzee JK nchi imemshinda kuongoza hata yeye anatambua, so anapopata opportunity ya kwenda nje anafurahi sana cuz anapumzisha akili yake.
 
Ref: bintimkongwe

Baba wafamilia anayeiacha familia katika mtafaruko nakuondoka zake, je huyo ni baba mwema?, je anajali familia yake, je anastahili kuigwa?. tafakari
 
aondoke akae hata mwaka mzima ili michongo ya kifisadi ikuli ipungue au icheleweshwe kiaina.
Hamna anachotusaidia zaidi ya kutuharibia.
 
Mimi nadhani JK hamuamini Waziri wa mambo ya nje ndiyo maana safari kwake zimekuwa haziishi. Labda bado anadhani yeye ni waziri wa mambo ya nchi za nje. Kweli inasikitisha, kumtuma waziri ni cost effective kuliko Rais kila siku kiguu na njia.
 
Anakimbia siku tisa huyo anaona zinakaribia kuyoyoma na hajui nn kitatokea,

kama mmeweza kugundua mara baada ya kutokea tukio au likikaribia kutokea tukio lolote baya basi Mkuu wa Kaya huondoka nchini,nia yake ni kujisafisha km hakuusika vile
Rejea ,tukio la Arusha,ujio wa Al Adawi,Mabom ya Gongo la mboto na mengine mengi ya nyuma na pia yatayofuatia
 
Wana JF Safari za Raisi siyo dharura ni kitu ambacho kimethibitishwa na kipo kwenye "Calendar" yake. Kama alipewa mwaliko labda miezi mitatu kabla ya siku ya tukio, akakubali na akawekwa kwenye ratiba ya wazungumzaji mnataka aingie mitini? Kero za wananchi zinazowazilishwa na maandamano ya CDM zitashughulikiwa na Mawaziri wa Kisekta kama zina mashiko mfano Suala la Sukari tayari Waziri wa biashara analifanyia kazi; suala la DOWANS nadhani hata kwenye hotuba yake hajalizungumzia ila alisisitiza sheria ya manunuzi ifuatwe kwenye hotuba.
 
Ndugu wanajamii suala hili limekuwa likinipa taabu sana, inawezekanaje Rais kuondoka nchini wakati nchi yake ikiwa katika wakati fulani mgumu aidha kisiasa au kijamii. Raisi Kikwete mara baada tu ya mabomu kulipuka kule gongo la mboto aliondoka nchini, sasa hivi pia kaona maandamano yamepamba moto huko kanda ya ziwa kaondoka nchini.

Swali linakunja; Je hali hii inamaanisha kuwa JK anayadharau matukio haya au hukimbia kwenda kupumzisha akili nje ya nchi? naomba maoni yako mwana JF.


Acha kuwa na upungufu wa mawazo ndani ya the home of big thinkers.....i dont think this is an issue you can put as a post.

Kumbuka rais wa nchi ana majukum mengi na mengine inabidi aya deligate kwa wasaidizi wake, uwepo wake nchini sio suruhisho ya matatizo, kama rais wa nchi bado anaweza kufanya utekelezaji wa shughuli za serikali na maamuzi hata kama yuko nje ya nchi kwa kuagiza cha kufanya.

Tujaribu kujadili maswala muhim ya nchi na hasa root problem. Root problem yetu hapa nchi hii ni kuwa hatuna viongozi waadilifu na wenye dhamira ya mabadiliko katika jamii, tatizo hapa ni hiki chama na muhimu tunakiondoaje na tunaweka watu gani wataofaa zaidi kusaidia kutatua matatizo yetu. Mambo ya kusafiri amedharua au asiposafiri wala hayasaidii kujadili hapa, muhimu tunapataje hawa viongozi wazuri au tunaiwekaje chadema madarakani basi!
 
Anaenda kupumzika paris afu atapitia jamaica kny bembea apunguze mawazo maana siku tisa tayari
 
Kuondoka na kuacha matatizo nyumbani ni aina ya defence mechanism ya kukwepa wajibu. Ni muoga wa kukabili matatizo/ shida za nchi. Njia rahisi ni kujifanya busy na mambo ambayo hayampi pressure kv. mikutano ya kimataifa, kusuluhisha migogoro ya wengine, nk. Hawezi kukaa na kutulia nyumbani kwa vile kufanya hivyo kutamfanya akae mkabala na matatizo ya taifa ambayo hana uwezo nayo. Njia rahisi ni kusafiri.
 
kuna mtu yoyote anakeep record ya safari zake?naomba tuzirecord ili tuzijumlishe mwisho wa mwaka wa kalenda maana amecharuka na safari,kweli mjasiri haachi asili halafu hichi kijamaa hakioni aibu bwana,..watu wamekisema kuhusu ushamba wake wakupenda ndege lakini hakomi,naanza kuungana na watu wanaohoji uwezo wa watu wapwani kuoongoza nchi,..jk stop those trips already,..aaaagh!!
 
Ndugu wanajamii suala hili limekuwa likinipa taabu sana, inawezekanaje Rais kuondoka nchini wakati nchi yake ikiwa katika wakati fulani mgumu aidha kisiasa au kijamii. Raisi Kikwete mara baada tu ya mabomu kulipuka kule gongo la mboto aliondoka nchini, sasa hivi pia kaona maandamano yamepamba moto huko kanda ya ziwa kaondoka nchini.

Swali linakunja; Je hali hii inamaanisha kuwa JK anayadharau matukio haya au hukimbia kwenda kupumzisha akili nje ya nchi? naomba maoni yako mwana JF.

kukimbia matatizo!!
 
Ref:Bless the 12

What you have demonstrated here is true, but you have failed to capture what was intended (root cause) to be discussed in the main topic. Hapa tulichokuwa tunajaribu kuangalia nijinsi mtu anavyo weza kukwepa majukumu yake kwakwenda ziara za nje kwa mfano baada ya mabomu ya Gongo la mboto kunahoja nyingi ziliibuka ambazo kimsingi kwa kiongozi anayejiamini zilihitaji majibu au kutolewa ufafanuzi, lakini kwa kisingizio ('' nilikuwa safarini'') mpaka sasa zinaelea mioyoni mwa watanzania bila majibu.

Hapa sio kwamba ninamaanisha asiende ziara lakini tunacho kiangalia niuwezo wa kupima uzito wa mambo kwa mfano 'utokea msiba nyumbani kwenu ndugu yako kafariki halafu kukawa kuna wito ulikuja, siku hiyo ya msiba inatakiwa uende nyumbani kwao mkeo (ukweni kwako) kwenda kuwasuluhisha shemeji zako wanagombania mashamba ya uridhi, je kwa akiri ya kawaida utauacha msiba na kwenda kuhudhuria kikao ukweni kwako?
 
Sasa watanzania wengi tumeondoa ujinga huyo bwana anakwepa majukumu kijanja namchukia kiana
 
Back
Top Bottom