Je, kufuatia utetezi wa Spika Ndugai kwa wabunge wa Chadema kuna haja ya wabunge hao kukata rufaa baraza kuu kudai Uanachama!

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
82,750
139,541
Spika Ndugai amesema yeye ameshawaapisha wabunge 19 wa Chadema na kwamba kamwe hatawafukuza kwa sababu akiwafukuza dunia nzima itamshangaa na ataingizwa kwenye orodha ya maajabu ya dunia.

Kufuatia kauli hii ya Spika Ndugai kuna haja tena ya Halima Mdee na wenzake 18 kuhangaika kudai kurejeshewa uanachama wao huko CHADEMA?

Maendeleo hayana vyama!
 
Wanawake 19 Hawana Wasi Wasi Wowote
Ccm Ikiwa Upande Wako Unadhani Nini Kitatokea!
Hapo Sasa Hivi Ndiyo Kwenye Kilima Kinashushwa
Kwenye Bonde Panajazwa!!!😀😁😂😅😄😐😃
Nasema Uongo Ndugu Zangu
Ndiyo Ukweli Wenyewe
 
Chadema wameshafanya jukumu lao, basi. Kazi ya kumtoa mtu bungeni au kumbakisha kwa sababu yoyote ile iwe inafuata sheria au inakiuka si jukumu la chadema.

Sijasikia wala kuona popote chadema wamesema akina Halima wafutwe ubunge. Hili ni suala la kikatiba, kuwa Mbunge kwa tiketi ya chama, na si takwa la chadema.

Mjue tu pamoja na kushangilia, kuwabakiza hao bungeni ni kuvunja waziwazi sheria za nchi, na kwakuwa awamu hii si jambo geni kuvunja sheria, hakuna wa kushangaa.
 
Nilivyomsikia anasema vile,nikajua Mchezo umeisha
Mahakama,chadema hawatoki,tume uchaguzi ndo hakuna jipya,
alafu ni kama calculated move,Huku ACT Wamemaliza znz,huku bara wamemaliza kesi pia..
Acha kujifariji wale wameshafukuzwa tayari, chadema wameshamaliza kazi yao ata wakiendelea kwenda bungeni ni uthibitisho serekali ya magufuli haifuati katiba
 
Acha kujifariji wale wameshafukuzwa tayari, chadema wameshamaliza kazi yao ata wakiendelea kwenda bungeni ni uthibitisho serekali ya magufuli haifuati katiba
Hayo sasa unasema wewe,hilo jambo spika kaliacha kwa Mahakama na Tume iliyopeleka majina,
Mengine yanabaki maneno,
Hilo jambo lilishaisha kabla hata halijaanza,
 
Chadema ni taasis huru inayotambulika kikatiba hawez Pangiwa na mahakama au tume kwenye maamuzi yao, sababu wao wanavigezo vyao vya yupi awe mwanachama au asiye mwanacham
Time will tell mkuu,
Afterall tunazungumzia kauli ya spika,hayo mengine ni speculation tu,
ila tunaofahamu siasa za kitanzania,kwa mbaali,jambo kama lishaisha,
Chadema ndio wataonekana losers,Act walau,
Kuna msemo unasema,Bora kuambulia kitu,kuliko kukosa kabisa..
 
Spika Ndugai amesema yeye ameshawaapisha wabunge 19 wa Chadema na kwamba kamwe hatawafukuza kwa sababu akiwafukuza dunia nzima itamshangaa na ataingizwa kwenye orodha ya maajabu ya dunia.

Kufuatia kauli hii ya Spika Ndugai kuna haja tena ya Halima Mdee na wenzake 18 kuhangaika kudai kurejeshewa uanachama wao huko Chadema?

Maendeleo hayana vyama!
Chandimu bwana, hata hawajui wanataka nn
 
Time will tell mkuu,
Afterall tunazungumzia kauli ya spika,hayo mengine ni speculation tu,
ila tunaofahamu siasa za kitanzania,kwa mbaali,jambo kama lishaisha,
Chadema ndio wataonekana losers,Act walau,
Kuna msemo unasema,Bora kuambulia kitu,kuliko kukosa kabisa..
Spika ndo Nani kwa chadema hawez wapangia kitu Cha kufanya, jaribio lolote ni kukanyaga katiba na sio kuikomoa chadema
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom