Je, Kiswahili kitumike kama lugha ya kufundishia kuanzia shule za sekondari mpaka vyuo vikuu? Jadili

kutumia kiswahili kama lugha ya kufundishia bila kiingereza ni changamoto sana hasa kwa masomo ya sayansi. katika masomo haya kuna dhana (concept) ambazo ni abstract sana na zingine ni concrete na zinamaneno ya kukopa hasa kwenye lugha ya kigriki na kilatini kutokana na watu waliogundua dhana hizo, hivyo kuyabadili maneno yote kuwa katika kiswahili ni kazi kubwa na ngumu na inahitaji kuwa na rasilimali nyingi na za kutosha. lakini pia mtu unaweza kuwa unaelewa kitu katika lugha mama (traditional language) lakini ukashindwa kukitafasili katika lugha ya kiswahili, je utaweza kutafasili hayo maneno ya kigriki na kilatini kuwa katika kiswahili?....binafsi naunga mkono hoja ya serikali katika sera ya elimu ya 2014 kuhusu hlugha ya kufundishia na kujifunzia.....
Tamko.....3.2.19. Lugha ya Taifa ya Kiswahili itatumika kufundishia na
kujifunzia katika ngazi zote za elimu na mafunzo na
Serikali itaweka utaratibu wa kuwezesha matumizi
ya lugha hii kuwa endelevu na yenye ufanisi katika
kuwapatia walengwa elimu na mafunzo yenye tija
kitaifa na kimataifa.

3.2.20. Serikali itaendelea na utaratibu wa kuimarisha
matumizi ya lugha ya Kiingereza katika kufundishia na
kujifunzia, katika ngazi zote za elimu na mafunzo.
 
kiswahi


Kuna watu wanasema kuwa lugha ya kufundishia kwenye mfumo wetu wa Elimu iwe Kiingereza kwa sababu Kiingereza ndo lugha ya dunia na uandishi wa vitabu mbali mbali na ugunduzi wa technologia nyingi ikiwepo kompyuta uko kwenye lugha ya kiingiereza.

Watetezi wa hoja hii wanasema nchi nyingi zlilizoendelea zinatumia kiingereza kwa hivyo sisi tulio nyuma kimaendeleo hatuwezi kuacha kufundisha watoto wetu kwa lugha hiyo ya dunia.

Watetezi wa hoja hii wanasema tusipojifunza kiingereza tutashindwa kuwasiliana na nchi tajiri duniani kama Uingereza, marekani nk ambazo zinatumia kiingereza. Kushindwa kuwasiliana huko kutaathiri mahusiano yetu na nchi Tajiri na mwishowe tutashidwa kufanya biashara na nchi hizo. Kubwa zaidi, hata vijana wetu hawataweza kuajiriwa katika nchi hizo.

Watetezi wengi wa hoja hii ni wanasiasa ambao watoto wao ama wanasoma nje ya nchi ama wako ndani ya nchi lakini kwenye shule za st xyz au accademy ambazo shule zinazotumia kiingereza kama lugha ya kufundishia.

Kwa upande wa pili, Wako wanaosema kiingereza isiwe lugha ya kufundishia kwenye shule na vyuo vyetu. Watetezi wa msimamo huu wengi wao (si wote) ni wataalamu wa vyuo vya juu, wao wanasema kiingereza ifundishwe kama lugha nyingine yo yote kama kifaransa, kichina, kireno, kiarabu nk ili watanzania wawasiliane na watu wengine duniani. Wao wanataka lugha ya kufundishia shuleni na vyuoni iwe kiswahili.

Sababu zao ni kama hizi zifuatazo:

Kwamba wanadai kuwa kisayansi Binadamu yo yote hufikiri kwa kutumia lugha ya kwanza wa wazazi wake, kisha hulazimika kutafsiri lugha hiyo kichwani kama atalazimika kuongea kiingereza na kwamba mchakato huu unarudisha nyuma au unachelewesha ubunifu wa watoto na hivyo tunaishia kuwa na wasomi waliokariri badala ya wasomi wanaoibua vitu vipya.

Matokeo yake wahitimu wa vyuo vikuu hawaji na ugunduzi wo wote mpya na mwisho wa siku wasomi wetu wa kukariri kiingereza wameshindwa kututoa kwenye lindi la umasikini pamoja na rasilimali nyingi tulizo nazo.

Pili, kwa kuwa kiingereza yenyewe ni tabu, wengi wanadhani kuwa wanafunzi wengi wa sekondary wakifika shuleni wanaanza kuhangaika na lugha ya kiingereza matokeo yake uelewa/ufaulu wao kwenye masomo lengwa unaathiriwa.

Watetezi wa hoja hii wanatoa mifano ya nchi kama China, Korea kusini, Malaysia nk ambazo zimeendelea kwa kutumia lugha zao za asili na hawatumii kiingereza hata kwenye mifumo yao ya Elimu. China kwa sasa ndo mkopeshaji wa Marekani.

Kati ya watetezi wa hoja hii wako Dr Martha Qoroo( Dean wa Chuo kikuu cha Dsm) na Jenerali Ulimwengu (mmiliki wa gazeti la Raia Mwema na Raia Tanzania)

Tume ya jaji Warioba kwenye rasimu yao ya pili walitangaza kiswahili kama lugha rasmi ya Taifa lakini hawakusema pia kwamba Kiingereza kisiwe lugha ya kufundishia -- waliipa kiswahili nguvu lakini kuhusu lugha ya kufundishia walikaa kimya.

kwa maneno rahisi akina Warioba walikwepa mjadala huu na kuamua kukaa katikati, japo katikati yao inaelemea upande wa Kiswahili zaidi hata kama ni kwa kiasi kidogo sana.

Wewe una maoni gani na kwa nini?

Wanaotumia kifaransa, Kichina na kihispaniola, kiitaliano wamelazimika kutumia kingereza kama lugha ya kufundishia advanced levels. Kiswahili tupa kulee. kibaki kama somo tu.
 
Mkuu The DR10

Kama wagunduzi wa dhana hizo walikuwa wagiriki na walatini, unadhani walifanya ugunduzi wao kwa lugha ngeni na kuhifadhi kimaandishi kwa lugha wasiyoijua?

Kama walitumia kiingereza ikiwa si lugha mama yao, basi ufahamu kuwa Waingereza walifanya shughuli pevu kuhakikisha ama lugha yao ina tafsiri ya maneno yote ya lugha za wagunduzi au walilazimisha lugha za wagunduzi ziwe na tafsiri ya maneno yote ya kiingereza.

Kama ilivyosemwa na bingwa mmoja hapo juu, utawaza kwa lugha mama tuu, ufanisi wa jambo lolote unalowaza, ili liwe kimatendo ni lazima utumie lugha yako ya kwanza.

Kuhusu kukosea kuandika kiswahili ilhali umezaliwa ndani ya lugha hiyo, hii ipo kila nchi. Kuna waingereza, wamarekani n.k ambao wanaongea kiingereza ila kuandika ni kasheshe, tena kuna maneno ya lugha yao wenyewe hawayajui.

Tunao wataalamu wanaoweza kututafsiria maneno yote ya kitaalamu kutoka lugha ngeni kwenda kwenye kiswahili, au ikibidi kuumba maneno mapya ya kiswahili kwaajili ya taaluma. Hapa lugha ngeni tutajifunza tu for leisure. Wangapi wanaingia hapa, ili shughuli zao ziende wanalazimika kujifunza kiswahili kwaajili ya mawasiliano tuu!!!

Lugha ya kwanza iwe Kiswahili, ya pili Kiswahili
 
mie naona kama kingereza kitaanzia la kwanza,then iendelee hivyo hivyo mpaka chuo kikuu,watoto hawatapata shida wakiwa chuo kikuu,

sio sasa mnawachanganya watoto,wenye benefits ni wale waliosoma english medium schools,

na wa kayumba kubaki kukariri ,lol

toeni hili tabaka
 
..mbona miaka ya zamani kuna watu waliishia darasa la 8 lakini walikuwa wanazunguka Kiingereza na Kiswahili kwa ufasaha kabisa?

..kwanini siku hizi tuna wahitimu hata wa PhD lakini hawakimudu Kiingereza.

..zaidi hivi karibuni kumeibuka kundi kubwa la wasomi wetu ambao hata Kiswahili kinawashinda kuandika.

..miaka ya nyuma sikuwahi kushuhudia mtu aliyesoma mpaka kidato cha nne halafu akawa anachanganya "ra" na "la" ktk uandishi.

..nadhani tatizo lipo ktk MFUMO wetu wa elimu. Naamini lugha zote, Kiingereza na Kiswahili, hazifundishwi kwa kuzingatia masharti ya ufundishaji lugha hizo.

..lingine tunarukia kufundisha biologia, vizikia, kemia, kwa kiingereza kabla ya kuhakikisha mwanafunzi ana uelewa wa kutosha ktk kusoma, kuandika, na kuzungumza, kiingereza.

..kama mwanafunzi hajapewa kitabu cha " introduction to biology -- MacKean" anapojiunga kidato cha kwanza ni vizuri akawa tayari ameshajisomea vitabu vingi vidigo vidogo vya hadithi na tamthilia vya Kiingereza.

..Kwa maoni yangu Watanzania tunapaswa kuzungumza lugha 3 kwa ufasaha. Tujifunze lugha zetu za makabila, pamoja na Kiingereza na Kiswahili.

..Mwisho, napendekeza KIINGEREZA kiendelee kuwa lugha ya kufundishia.

NB.

..tuimarishe MAKTABA ktk shule zetu za msingi na sekondari.

..binafsi nashangaa kabisa kuwa nimesoma shule ya msingi mpaka chuo kikuu na sikuwahi kuazima kitabu ktk maktaba ya shule (msingi + sekondari).

..tujenge utamaduni wa KUJISOMEA vitabu vya hadithi, tamthilia, toka ngazi za chini.

..tufundishe "COMMUNICATION SKILLS" kwa vijana wetu toka wakiwa wadogo.

..tusisitize na tuboreshe ufundishaji wa HESABU, SAYANSI, na TEKNOLOJIA, kuanzia umri mdogo kabisa.

..mwisho, turuhusu watoto wetu wawe watundu-watundu. Hiyo itakuja kuwasaidia ukubwani ktk masomo ya UFUNDI.
 
kutumia kiswahili kama lugha ya kufundishia bila kiingereza ni changamoto sana hasa kwa masomo ya sayansi. katika masomo haya kuna dhana (concept) ambazo ni abstract sana na zingine ni concrete na zinamaneno ya kukopa hasa kwenye lugha ya kigriki na kilatini kutokana na watu waliogundua dhana hizo, hivyo kuyabadili maneno yote kuwa katika kiswahili ni kazi kubwa na ngumu na inahitaji kuwa na rasilimali nyingi na za kutosha. lakini pia mtu unaweza kuwa unaelewa kitu katika lugha mama (traditional language) lakini ukashindwa kukitafasili katika lugha ya kiswahili, je utaweza kutafasili hayo maneno ya kigriki na kilatini kuwa katika kiswahili?....binafsi naunga mkono hoja ya serikali katika sera ya elimu ya 2014 kuhusu hlugha ya kufundishia na kujifunzia.....
Tamko.....3.2.19. Lugha ya Taifa ya Kiswahili itatumika kufundishia na
kujifunzia katika ngazi zote za elimu na mafunzo na
Serikali itaweka utaratibu wa kuwezesha matumizi
ya lugha hii kuwa endelevu na yenye ufanisi katika
kuwapatia walengwa elimu na mafunzo yenye tija
kitaifa na kimataifa.

3.2.20. Serikali itaendelea na utaratibu wa kuimarisha
matumizi ya lugha ya Kiingereza katika kufundishia na
kujifunzia, katika ngazi zote za elimu na mafunzo.
HATA KIINGEREZA MANENO YA KIGIRIKI NA KILIYAACHA KAMA YALIVYOKUA. HATA SISI HATUTATAFRISI NENO PHYSICS KUA KUA NENO TULUTILU, BALI TUTAITAFSIRI KAMA NENO FIZIKIA. mbona PSYCHOLOGY tunajua kama SAIKOLOJIA na hakuna kilichoharibika wala ugumu!!!
 
mie naona kama kingereza kitaanzia la kwanza,then iendelee hivyo hivyo mpaka chuo kikuu,watoto hawatapata shida wakiwa chuo kikuu,

sio sasa mnawachanganya watoto,wenye benefits ni wale waliosoma english medium schools,

na wa kayumba kubaki kukariri ,lol

toeni hili tabaka
Mwazo mazuri sana. Lugha itayotumika kufundishia tangu elimu ya awali, ndio hiyo hiyo itumike mpaka chuo kikuu. Sio hii 'style' ya sasa ya kupokezana. Kwamba ww kiswahili tangulia, mm kiingereza nitakupokea baadae.
 
mie naona kama kingereza kitaanzia la kwanza,then iendelee hivyo hivyo mpaka chuo kikuu,watoto hawatapata shida wakiwa chuo kikuu,

sio sasa mnawachanganya watoto,wenye benefits ni wale waliosoma english medium schools,

na wa kayumba kubaki kukariri ,lol

toeni hili tabaka
Mwazo mazuri sana. Lugha itayotumika kufundishia tangu elimu ya awali, ndio hiyo hiyo itumike mpaka chuo kikuu. Sio hii 'style' ya sasa ya kupokezana. Kwamba ww kiswahili tangulia, mm kiingereza nitakupokea baadae.
 
mie naona kama kingereza kitaanzia la kwanza,then iendelee hivyo hivyo mpaka chuo kikuu,watoto hawatapata shida wakiwa chuo kikuu,

sio sasa mnawachanganya watoto,wenye benefits ni wale waliosoma english medium schools,

na wa kayumba kubaki kukariri ,lol

toeni hili tabaka
Mwazo mazuri sana. Lugha itayotumika kufundishia tangu elimu ya awali, ndio hiyo hiyo itumike mpaka chuo kikuu. Sio hii 'style' ya sasa ya kupokezana. Kwamba ww kiswahili tangulia, mm kiingereza nitakupokea baadae.
 
maarifa huja kwa lugha ya asili... kiswahili kitumike

..wako wengi ambao kiswahili siyo lugha yao ya asili.

..lakini pia tujiulize, mbona kenya wanaweza?

..mbona rwanda wanaongea kinyarwanda na shuleni ni kiingereza? Na sasa wameongeza kiswahili!!

..kwanini sisi tujipunje, kwa kujifunza kiswahili huku tukikitupa mkono kiingereza?
 
Kwa kweli kiswahili bado hakijajitosheleza, sifikirii Kama inawezekana kukitumia kiswahili kuwa ndio lugha ya kufundishia, pia nchi yetu haina uwezo mkubwa ki tecnolojia, tunahitaji kwenda kusoma zaidi katika nchi zilizoendelea, Wachina wana uwezo wa kutengeneza kila Jitu, hii ni hatari sana kufikiria mambo ambayo kwa sasa yatatuletea matatizo makubwa, wafanyakazi wa hoteli ndio kitakuwa kichekesho kikubwa, Menu imeandikwa Kiingereza mfanyakazi anavijua kwa kiswahili, wageni wanavijua kwa kiingereza, Tuache kukurupuka bado muda haujafika.
 
Kiswahili kitukuzwe, lakini kisiwe lugha ya kufundishia. Ningekuwa na madaraka ya kuamua ningesema kuwa kiingereza kiwe lugha kuu ya kufundishia kuanzia darsa la nne, lakini kiswahili kiwe ni compulsory. Yaani mtu hawezi kupata digrii, diploma au cheti cha taaluma yake bila kupasi ujuvi wa lugha ya kiswahili sawasawa hata kama atapasi masomo ya taaluma yake. Lakini hatuwezi kufundisha masomo ya sayansi kwa kiswahili.

"Newton's Laws" zibaki kuwa ni Newton's Laws siku zote kama zilivyotolewa na Newton, siyo tuzigeuze na kuziita kuwa eti ni "Kanuni za Nyutoni." Ingawa hiyo ni tafsiri sahihi katika lugha yetu lakini huwa inapoteza maana yake halisi (lost in translation). Kisayansi kuna laws, principles, theorems, conjectures, lemmas na statements nyinginezo ambazo karibu zote zinatafsiriwa kwa kiswahili kama kanuni ingawa katika sayansi zina maana tofauti!
 
Ha-ha kwahyo wakitumia kiswahili ndo nini sasa ufaulu utaongezeka au? Wataelewa zaidi ? Na sisi tutakuwa na kina plato wetu na ma galileo au ?pathetic wanafunzi wenyewe hawapendi shule lugha cyo factor yoyote.in fact mbna wapo watu wame master English na wame reach potential kubwa.Language ain't the problem attitude towards education is
.
 
Kiswahili bado akijitoshelezi kimisamiati hasa katika maswala ya kisayansi na kiteknolojia, waalimu wafundishe kwa kiingereza ila watoe maelezo kwa kiswahili pale inapobidi
 
lugha na maarifa ni vitu viwili tofauti, lugha unayoijua ni rahisi kukupa maarifa kwani uelewa huwa mwepesi. kiingereza ni lugha ambayo mtu yoyote anaweza kujifunza. mwanasayansi wa kirusi ana maarifa na inawezekana akawa hajui kiingereza hata kidogo. kutokujua lugha ya kiingereza hakuzuiii kuwa na maarifa. dunia ya leo haitaki ujuzi wa lugha inataka watu wenye maarifa, stadi na ujuzi na bahati mbaya sana mfumo wetu wa elimu unaanza kugawa fikira za mwanafunzi tangu siku ya kwanza. ndio maana huwa sishangai kuona watanzania tukiamua kimoja tunafanya kingine (we have split personality) kwa sababu mfumo wa elimu sijui unataka ujue lugha au maarifa.

kiswahili 100% iwe lugha ya kujifunza kwenye ngazi zote za elimu. lugha inakua pale matumizi yake yanapoongezeka. hakuna miujiza. TUNAHITAJI MFUMO WA MAWASILIAIANO UTAKAOFANIKISHA KUPATA MAARIFA, STADI NA UJUZI KWA URAHISI. HATUHITAJI KUONEKANA WAJUZI WAKATI HATUNA MAARIFA, STADI NA UJUZI WA KUTOSHA KUTUWEZESHA KUSHINDANA ULIMWENGUNI.


Kuna watu wanasema kuwa lugha ya kufundishia kwenye mfumo wetu wa Elimu iwe Kiingereza kwa sababu Kiingereza ndo lugha ya dunia na uandishi wa vitabu mbali mbali na ugunduzi wa technologia nyingi ikiwepo kompyuta uko kwenye lugha ya kiingiereza.

Watetezi wa hoja hii wanasema nchi nyingi zlilizoendelea zinatumia kiingereza kwa hivyo sisi tulio nyuma kimaendeleo hatuwezi kuacha kufundisha watoto wetu kwa lugha hiyo ya dunia.

Watetezi wa hoja hii wanasema tusipojifunza kiingereza tutashindwa kuwasiliana na nchi tajiri duniani kama Uingereza, marekani nk ambazo zinatumia kiingereza. Kushindwa kuwasiliana huko kutaathiri mahusiano yetu na nchi Tajiri na mwishowe tutashidwa kufanya biashara na nchi hizo. Kubwa zaidi, hata vijana wetu hawataweza kuajiriwa katika nchi hizo.

Watetezi wengi wa hoja hii ni wanasiasa ambao watoto wao ama wanasoma nje ya nchi ama wako ndani ya nchi lakini kwenye shule za st xyz au accademy ambazo shule zinazotumia kiingereza kama lugha ya kufundishia.

Kwa upande wa pili, Wako wanaosema kiingereza isiwe lugha ya kufundishia kwenye shule na vyuo vyetu. Watetezi wa msimamo huu wengi wao (si wote) ni wataalamu wa vyuo vya juu, wao wanasema kiingereza ifundishwe kama lugha nyingine yo yote kama kifaransa, kichina, kireno, kiarabu nk ili watanzania wawasiliane na watu wengine duniani. Wao wanataka lugha ya kufundishia shuleni na vyuoni iwe kiswahili.

Sababu zao ni kama hizi zifuatazo:

Kwamba wanadai kuwa kisayansi Binadamu yo yote hufikiri kwa kutumia lugha ya kwanza wa wazazi wake, kisha hulazimika kutafsiri lugha hiyo kichwani kama atalazimika kuongea kiingereza na kwamba mchakato huu unarudisha nyuma au unachelewesha ubunifu wa watoto na hivyo tunaishia kuwa na wasomi waliokariri badala ya wasomi wanaoibua vitu vipya.

Matokeo yake wahitimu wa vyuo vikuu hawaji na ugunduzi wo wote mpya na mwisho wa siku wasomi wetu wa kukariri kiingereza wameshindwa kututoa kwenye lindi la umasikini pamoja na rasilimali nyingi tulizo nazo.

Pili, kwa kuwa kiingereza yenyewe ni tabu, wengi wanadhani kuwa wanafunzi wengi wa sekondary wakifika shuleni wanaanza kuhangaika na lugha ya kiingereza matokeo yake uelewa/ufaulu wao kwenye masomo lengwa unaathiriwa.

Watetezi wa hoja hii wanatoa mifano ya nchi kama China, Korea kusini, Malaysia nk ambazo zimeendelea kwa kutumia lugha zao za asili na hawatumii kiingereza hata kwenye mifumo yao ya Elimu. China kwa sasa ndo mkopeshaji wa Marekani.

Kati ya watetezi wa hoja hii wako Dr Martha Qoroo( Dean wa Chuo kikuu cha Dsm) na Jenerali Ulimwengu (mmiliki wa gazeti la Raia Mwema na Raia Tanzania)

Tume ya jaji Warioba kwenye rasimu yao ya pili walitangaza kiswahili kama lugha rasmi ya Taifa lakini hawakusema pia kwamba Kiingereza kisiwe lugha ya kufundishia -- waliipa kiswahili nguvu lakini kuhusu lugha ya kufundishia walikaa kimya.

kwa maneno rahisi akina Warioba walikwepa mjadala huu na kuamua kukaa katikati, japo katikati yao inaelemea upande wa Kiswahili zaidi hata kama ni kwa kiasi kidogo sana.

Wewe una maoni gani na kwa nini?
 
Lugha yetu ya kiswahili ni nzuri sana na hatuna budi kujivunia na kuitukuza,ndio lugha inayotuunganisha kama taifa toka enzi za Mkoloni mpaka sasa.

Lakini kwa upeo wangu, lugha yetu ina uhaba mkubwa sana wa misamiati ya taaluma mbali mbali kuanzia Sheria mpaka Utabibu.

Hizo Nchi zinazotumia lugha zao mama kwa kujifunzia ni kuwa zinajitosheleza kimsamiati ndio maana unaona zinaendelea kuendelea kwa kutumia lugha zao kwenye nyanja zote za kisiasa hadi kiuchumi.

Tukitaka kufika walipo tuanzie kwenye misamiati,halafu mitaala kama baadhi ya wakuu hapa walivyochangia tukifika hapo sasa tutaweza kuanza kupitisha sheria mbali mbali kwa ajili ya kukisimika kiswahili kuwa lugha ya kufundishia.
 


Kuna watu wanasema kuwa lugha ya kufundishia kwenye mfumo wetu wa Elimu iwe Kiingereza kwa sababu Kiingereza ndo lugha ya dunia na uandishi wa vitabu mbali mbali na ugunduzi wa technologia nyingi ikiwepo kompyuta uko kwenye lugha ya kiingiereza.

Watetezi wa hoja hii wanasema nchi nyingi zlilizoendelea zinatumia kiingereza kwa hivyo sisi tulio nyuma kimaendeleo hatuwezi kuacha kufundisha watoto wetu kwa lugha hiyo ya dunia.

Watetezi wa hoja hii wanasema tusipojifunza kiingereza tutashindwa kuwasiliana na nchi tajiri duniani kama Uingereza, marekani nk ambazo zinatumia kiingereza. Kushindwa kuwasiliana huko kutaathiri mahusiano yetu na nchi Tajiri na mwishowe tutashidwa kufanya biashara na nchi hizo. Kubwa zaidi, hata vijana wetu hawataweza kuajiriwa katika nchi hizo.

Watetezi wengi wa hoja hii ni wanasiasa ambao watoto wao ama wanasoma nje ya nchi ama wako ndani ya nchi lakini kwenye shule za st xyz au accademy ambazo shule zinazotumia kiingereza kama lugha ya kufundishia.

Kwa upande wa pili, Wako wanaosema kiingereza isiwe lugha ya kufundishia kwenye shule na vyuo vyetu. Watetezi wa msimamo huu wengi wao (si wote) ni wataalamu wa vyuo vya juu, wao wanasema kiingereza ifundishwe kama lugha nyingine yo yote kama kifaransa, kichina, kireno, kiarabu nk ili watanzania wawasiliane na watu wengine duniani. Wao wanataka lugha ya kufundishia shuleni na vyuoni iwe kiswahili.

Sababu zao ni kama hizi zifuatazo:

Kwamba wanadai kuwa kisayansi Binadamu yo yote hufikiri kwa kutumia lugha ya kwanza wa wazazi wake, kisha hulazimika kutafsiri lugha hiyo kichwani kama atalazimika kuongea kiingereza na kwamba mchakato huu unarudisha nyuma au unachelewesha ubunifu wa watoto na hivyo tunaishia kuwa na wasomi waliokariri badala ya wasomi wanaoibua vitu vipya.

Matokeo yake wahitimu wa vyuo vikuu hawaji na ugunduzi wo wote mpya na mwisho wa siku wasomi wetu wa kukariri kiingereza wameshindwa kututoa kwenye lindi la umasikini pamoja na rasilimali nyingi tulizo nazo.

Pili, kwa kuwa kiingereza yenyewe ni tabu, wengi wanadhani kuwa wanafunzi wengi wa sekondary wakifika shuleni wanaanza kuhangaika na lugha ya kiingereza matokeo yake uelewa/ufaulu wao kwenye masomo lengwa unaathiriwa.

Watetezi wa hoja hii wanatoa mifano ya nchi kama China, Korea kusini, Malaysia nk ambazo zimeendelea kwa kutumia lugha zao za asili na hawatumii kiingereza hata kwenye mifumo yao ya Elimu. China kwa sasa ndo mkopeshaji wa Marekani.

Kati ya watetezi wa hoja hii wako Dr Martha Qoroo( Dean wa Chuo kikuu cha Dsm) na Jenerali Ulimwengu (mmiliki wa gazeti la Raia Mwema na Raia Tanzania)

Tume ya jaji Warioba kwenye rasimu yao ya pili walitangaza kiswahili kama lugha rasmi ya Taifa lakini hawakusema pia kwamba Kiingereza kisiwe lugha ya kufundishia -- waliipa kiswahili nguvu lakini kuhusu lugha ya kufundishia walikaa kimya.

kwa maneno rahisi akina Warioba walikwepa mjadala huu na kuamua kukaa katikati, japo katikati yao inaelemea upande wa Kiswahili zaidi hata kama ni kwa kiasi kidogo sana.

Wewe una maoni gani na kwa nini?

Soma hiki kitabu. Utapata majibu yote juu ya mada hii
http://cas1.elis.ugent.be/avrug/pdf03/neke.pdf
 
achana na kiswshili, ongeza mkakati wa uelewa wa english. pili tuko na wenzetu wa EAC, tusiende kivyetuvyetu, do things in consideration that we are east africans, that should be the spirit
 
Ukitaka kuamini kuwa lugha ya kingereza ndio inapaswa kuwa lugha ya kufundishia kuanzia chekechea hadi chuo kikuu na Kiswahili libaki kama somo kwanza jiulize kwanini mtu asome kiswahili miaka zaidi ya tisa

halafu ndani ya miaka minne analazimishwa kujua kingereza vizuri na anaonekana hana sifa ya kwenda chuo au kusoma sekondari kama hajui kingereza hao hao wanasahau wamemfundisha kwa kiswahili zaidi ya miaka saba!

Kusema ukweli lugha ya kiswahili haitusaidii chochote na haina manufaa yeyote kwetu ndio maana secondary na chuo kikuu inatupwa na kutumika kingereza! Nchi yetu imejaa unafiki mwingi hasa kwenye elimu kama kweli kiswahili kingekuwa na muhimu kingefundishwa hadi chuo kikuu!

Lugha ya kiswahili haiwezi kutumika kwenye ushindani kabisa kwenye nyanja zote za uchumi!
Unaonekana kujadili mada bila ya kuwa na elimu. Unahitaji ujifunze umuhimu wa Kiingereza ni nini na kwanini tunajifunza, halafu ujifunze kuhusu umuhimu wa lugha mama katika elimu. Halafu ndio ujadili. Yaonesha unajadili bila uelewa. Kila lugha kati ya hizi mbili zina umuhimu wake. Tatizo lenu wengi hamjui lugha ipi ina umuhimu gani? Muko na ile imani kuwa Kiingereza ndio kila kitu.
 
Back
Top Bottom