WINGER_TEREZA
JF-Expert Member
- Jul 31, 2015
- 242
- 450
Habari, Juzi Mh. Rais, Mh. Samia Suluhu Hassan ameteua wakuu wa mikoa wa mikoa yote ya Tanzania bara na miongoni ya walioteuliwa ni aliyekuwa mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja General Charles Mbuge kuwa mkuu wa Mkoa wa Kagera akichukua nafasi ya Brigedia Generali Marco Kaguti ambaye ameteuliwa kuwa mkuu wa Mkoa wa Mara.
Mara nyingi kwenye ziara za viongozi wakuu wa Serikali, hususani Mh. Raisi, huwa anaambatana na viongozi wakuu wa vyombo vyote vya ulinzi na usalama kuanzia CDF, IGP, DGTISS, Commissioner wa Magereza, Uhamiaji, Commissioner wa Jeshi la Zimamoto, Mkuu wa PCCB na Mkuu wa Mamlaka ya kupambana na dawa za kulevya huko mikoani ili kuthibitisha uwepo wa kiongozi mkuu wa nchi.
Nimeshuhudia mara CDF, General Venance Mabeyo, akiwapigia salute "viongozi wa kisiasa" hasa wakuu wa Mikoa na wakuu wa Wilaya mfano nilikuwa Kisarawe kupitia TV wakati wa ziara ya "Mwendazake" akizindua mradi wa maji nakushuhudia CDF, General Mabeyo, akimpigia salute Mkuu wa Wilaya hiyo, Miss Joketi Mwegelo. Hili kwa viongozi hawa ambao siyo Askari sidhani kama linashida sana (Ingawa halileti maana vipi IGP AU CDF ampigie Salute raia - but sio mada yangu kwa leo so tuachane nayo) ila shida naiona itakuwaje siku CDF ambaye ni General akiwa Kagera atampigia Salute Mkuu wa Mkoa huo ambaye ni Meja General? Hii imekaaje wanajukwaa au Meja General atampigia Salute Mkuu wake, hapa hata sielewi?
Asante.
Mara nyingi kwenye ziara za viongozi wakuu wa Serikali, hususani Mh. Raisi, huwa anaambatana na viongozi wakuu wa vyombo vyote vya ulinzi na usalama kuanzia CDF, IGP, DGTISS, Commissioner wa Magereza, Uhamiaji, Commissioner wa Jeshi la Zimamoto, Mkuu wa PCCB na Mkuu wa Mamlaka ya kupambana na dawa za kulevya huko mikoani ili kuthibitisha uwepo wa kiongozi mkuu wa nchi.
Nimeshuhudia mara CDF, General Venance Mabeyo, akiwapigia salute "viongozi wa kisiasa" hasa wakuu wa Mikoa na wakuu wa Wilaya mfano nilikuwa Kisarawe kupitia TV wakati wa ziara ya "Mwendazake" akizindua mradi wa maji nakushuhudia CDF, General Mabeyo, akimpigia salute Mkuu wa Wilaya hiyo, Miss Joketi Mwegelo. Hili kwa viongozi hawa ambao siyo Askari sidhani kama linashida sana (Ingawa halileti maana vipi IGP AU CDF ampigie Salute raia - but sio mada yangu kwa leo so tuachane nayo) ila shida naiona itakuwaje siku CDF ambaye ni General akiwa Kagera atampigia Salute Mkuu wa Mkoa huo ambaye ni Meja General? Hii imekaaje wanajukwaa au Meja General atampigia Salute Mkuu wake, hapa hata sielewi?
Asante.