Je, Kipeperushi Hiki cha CCM Kimesajiliwa? Mbona Kinapotosha Wananchi?

Chakaza

JF-Expert Member
Mar 10, 2007
39,794
71,214
Ni utaratibu uliowekwa na Tume (NEC) kuwa vipeperushi vyote vinavyohusiana na uchaguzi lazima vikaguliwe na kupitishwa kabla ya matumizi.

Majuzi Tume imetoa karatasi ya mfano ya kupigia kura ikiwa na mpangilio wa majina yote ya wagombea yatakavyokuwa. Lakini CCM wameichukua na kuihariri na wanaitumia kuwaelekeza watu jinsi ya kupiga kura huku wakiwa wamekata picha na maelezo ya wagombea mwiba kwao.

James Mbatia alihukumiwa kusimamishwa kampeni kwa kosa hilo lakini jana amefutiwa adhabu hiyo, jee yalikuwa ni maandalizi kwa Magufuli kupewa nafasi ya kuvunja sheria hiyo ya kutumia kipeperushi bila kusajiliwa?

Mbona hawa Makamishna wa Tume wanajifedhehesha utadhani hakuna maisha mengine baada ya uchaguzi?

Kipeperushi hicho ni upotoshaji mkubwa sana, na kwa vile wafuasi wengi wa CCM ni maamuma sio rahisi kugundua.

JamiiForums-1587798088.jpg
 
Hicho kipeperushi kina shida gani?Si mfano wa karatasi ya kupigia kura!!!! Mwambie jirani zako watu wote bila kujali makabila waweke Tick ✓ kwa Mgombea Urais namba moja wasihangaike kabisa na wengine.
It seems hujui taratibu za uchaguzi. Waraka wowote unaotumika kwenye kampeni ama peingine popote kuhusu uchaguzi inabidi uwe umesajiliwa na tume.
 
Kazi ya wasimamizi wa uchaguzi ni pamoja na kuwaelekeza wananchi. Kikubwa ni kujua CCM ni Nambari one
 
Na nyie si mkate mumtangaze mgombea wenu, badala ya kupiga kampeni na kutangaza Sera zenu, nyie mnahangaika na CCM
 
Mfano si na nyie mlipewa na tume, hata siku ya matokeo mtasingizia tume hivihivi, au ndo mmeanza kujiandaa kisaikolojia
 
Tume imeona na itakaa kimya maana inajua. Ndio maana huwa sioni mantiki ya Tume kuongozwa na Jaji.
Majaji wanapata image mbaya sana kupitia uongozi wa vyombo kama Tume ya uchaguzi. Matendo yao na ethics za taaluma na kazi zao viko overshadowed na matakwa ya wana siasa
 
Acha kilialia nenda kafanye homework yako, CCM wako kazini na makini na ndiyo maana wanashinda, ninyi ujuaji mwingi matokeo yake wagombea wenu kibao wameengeuliwa kwa kushindwa tu kujaza fomu, aibu kwenu.
 
Ni utaratibu uliowekwa na Tume (NEC) kuwa vipeperushi vyote vya kuhusiana na uchaguzi lazima vikaguliwe na kupitishwa kabla ya matumizi.

Majuzi Tume imetoa karatasi ya mfano ya kupigia kura ikiwa na mpangilio wa majina yote yatakavyo kuwa. Lakini CCM wameichukua na kuihariri na wanaitumia kuwaelekeza watu jinsi ya kupiga kura huku wakiwa wamekata picha na maelezo ya wagombea mwiba kwao.

James Mbatia alihukumiwa kusimamishwa kampeni kwa kosa hilo lakini jana amefutiwa adhabu hiyo, jee yalikuwa ni maandalizi kwa Magufuli kupewa nafasi ya kuvunja sheria hiyo ya kutimia kipeperushi bila kusajiliwa?

Mbona hawa Makamishna wa Tume wanajifedhehesha utadhani hakuna maisha mengine baada ya uchaguzi?

Kipeperushi hicho ni upotoshaji mkubwa sana, na kwa vile wafuasi wengi wa CCM ni maamuma sio rahisi kugundua.
IMG-20201021-WA0034.jpg
 
Chombo cha Mabeberu, samaki wanaogelea mbaaali hawataki kusogelea simu

Mwaka huu CHADEMA mkipata 20%mkatambike.
 
Back
Top Bottom