Al Watani
JF-Expert Member
- Dec 28, 2014
- 20,372
- 30,312
Kaunda alipigwa kwenye sanduku la kura na Fredrick Chiluba.Hamjambo wana jamvi? Hali ni tete kwa rais wa Zambia Edgar Lungu. Rungu la wapiga kura limemshukia huku mpinzani wake mkuu Hakainde Hichilema akizidi kuchanga mbuga kumnyang'anya ikulu. Sisi kama majirani na marafiki tunaangalia kwa jicho la karibu. Je kilichotokea Malawi ambapo upinzani uliingasha serikali iliyoko madarakani kinajirudia Zambia? Je watanzania tunajifunza nini? Inakuwaje viinchi vidogo vinatushinda? Kwa habari zaidi BONYEZA HAPA TAFADHALI
Fredrick Chiluba akapigwa kwenye sanduku la kura na Levy Mwanawasa
Rupiah Banda akapigwa kwenye sanduku la kura na Michael Chilufya Sata.
Edgar Lungu anachapwa kwenye Sanduku la kura na Hakaindi Hichilema.
Lakini Zambia pia ndiyo nchi pekee ambayo marais wawili walifia madarakani na warithi wao walikuja kuondolewa madarakani kwa sanduku la kura.