Je, kati ya aliyeghushi au aliyefuata mafundisho ya uongo yupi anastahili adhabu?

Undava King

JF-Expert Member
Aug 11, 2017
3,140
5,231
Nimekaa nikiyatafakari baadhi ya maandiko ambayo niliyasoma mahali na kubaini mapungufu fulani yenye ka chembechembe ka upotoshaji.

Kisha nikajiuliza swali je, nani atawajibika endapo mawazo yangu yakiwa sahihi (pengine ni ujinga nilionao juu ya tafsiri ya maandiko husika ndo yananifanya nione kuna dosari) juu ya nilichokikisia kuwa hakiko sawa?

Je, ni yule aliyegushi na kuwakosesha wenzake kwa malengo anayoyajua yeye mwenyewe?

Au ni yule aliyefuata mafundisho hayo kwa upofu akiamini ni matakatifu pasipo kuyachunguza undani au uhalali wake?

Au wote watapatwa na adhabu moja ya kutojua sheria siyo kinga dhidi ya kuvunja sheria?

Mfano wa maandiko hayo ni kama haya; naomba kunukuu kifungu kutoka kwenye kitabu kitakatifu cha biblia:-

Sala ya Bwana Luka 11

2 Akawaambia, Msalipo, Semeni, Baba [yetu uliye mbinguni], jina lako litakaswe, ufalme wako uje, [Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni]

3 Utupe siku kwa siku riziki yetu.

4 Utusamehe dhambi zetu kwa kuwa sisi nasi tunamsamehe kila tumwiaye. Na usitutie majaribuni [ lakini tuokoe na yule mwovu]

Utaona kuna maandishi yapo kwenye mabano kwangu binafsi hapo ndipo palipo na utata wenyewe:

1. [Yetu uliye mbinguni] naamini hii ni dhana ya kupotosha yenye lengo la kumwondosha muamini katika mstari wa kujua kuwa Mungu wake yu mahali popote na hata ndani yake pia.

2. [Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni] hii ni kauli mbiu yenye mfanano wa karibu sana na mafundisho ya illuminati (As done below here so above)

3.[lakini tuokoe na yule mwovu] sina cha kueleza hapa ila ni sawa na kumwombea adui (shetani) msamehewe pamoja.(labda kama dhamiri nitofauti na kauli)

Take home value: Hii sala bila ya hivyo vipengele hapo kwenye mabano ina make sense zaidi, hivyo kwa fikra zangu naamini kabla ya kuongezewa vipengele nilivyovibainisha kwa mabano hapo juu ilipaswa kuwa hivyo.
 
QURAN 34 : 31- 33

"Na walisema walio kufuru: Hatutaiamini Qur'ani hii, wala yaliyo kuwa kabla yake. Na ungeli waona madhalimu watapo simamishwa mbele ya Mola wao Mlezi, wakirudishiana maneno wao kwa wao! Wanyonge wakiwaambia walio jivuna (viongozi): Lau kuwa si nyinyi, bila ya shaka tungeli kuwa Waumini sisi".

32. "Walio jivuna (viongozi) watawaambia wanyonge: Kwani sisi ndio tulio kuzuieni na uwongofu baada ya kukujieni? Bali nyinyi wenyewe ni wakosefu. "



33. "Na wanyonge wakawaambia walio jivuna (viongozi): Bali ni vitimbi vyenu vya usiku na mchana, mlipo kuwa mkituamrisha tumkufuru Mwenyezi Mungu, na tumfanyie washirika. Nao wataficha majuto watakapo iona adhabu. Na tutaweka makongwa shingoni mwao walio kufuru. Kwani wanalipwa ila kwa waliyo kuwa wakiyatenda?"


 
QURAN 40: 47-49

47: "Na watapo hojiana huko Motoni, wanyonge (wafuasi) watawaambia walio jitukuza: Hakika sisi tulikuwa wafuasi wenu, basi je, hamtuondolei sehemu ya huu Moto?"



48. "Watasema walio jitukuza: Hakika sote sisi tumo humu humu (motoni)! Kwani Mwenyezi Mungu kesha hukumu baina ya waja!"



49. "Na walio Motoni watawaambia walinzi wa Jahannamu: Mwombeni Mola wenu Mlezi atupunguzie walau siku moja ya adhabu".



50. "Nao watasema: Je! Hawakuwa wakikufikieni Mitume wenu kwa hoja zilio wazi? Watasema: Kwani? (Hapana walifika) Watasema: Basi ombeni! Na maombi ya makafiri hayawi ila ni kupotea bure tu."


 
Nimekaa nikiyatafakari baadhi ya maandiko ambayo niliyasoma mahali na kubaini mapungufu fulani yenye ka chembechembe ka upotoshaji.

Kisha nikajiuliza swali je, nani atawajibika endapo mawazo yangu yakiwa sahihi (pengine ni ujinga nilionao juu ya tafsiri ya maandiko husika ndo yananifanya nione kuna dosari) juu ya nilichokikisia kuwa hakiko sawa?

Je, ni yule aliyegushi na kuwakosesha wenzake kwa malengo anayoyajua yeye mwenyewe?

Au ni yule aliyefuata mafundisho hayo kwa upofu akiamini ni matakatifu pasipo kuyachunguza undani au uhalali wake?

Au wote watapatwa na adhabu moja ya kutojua sheria siyo kinga dhidi ya kuvunja sheria?

Mfano wa maandiko hayo ni kama haya; naomba kunukuu kifungu kutoka kwenye kitabu kitakatifu cha biblia:-

Sala ya Bwana Luka 11

2 Akawaambia, Msalipo, Semeni, Baba [yetu uliye mbinguni], jina lako litakaswe, ufalme wako uje, [Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni]

3 Utupe siku kwa siku riziki yetu.

4 Utusamehe dhambi zetu kwa kuwa sisi nasi tunamsamehe kila tumwiaye. Na usitutie majaribuni [ lakini tuokoe na yule mwovu]

Utaona kuna maandishi yapo kwenye mabano kwangu binafsi hapo ndipo palipo na utata wenyewe:

1. [Yetu uliye mbinguni] naamini hii ni dhana ya kupotosha yenye lengo la kumwondosha muamini katika mstari wa kujua kuwa Mungu wake yu mahali popote na hata ndani yake pia.

2. [Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni] hii ni kauli mbiu yenye mfanano wa karibu sana na mafundisho ya illuminati (As done below here so above)

3.[lakini tuokoe na yule mwovu] sina cha kueleza hapa ila ni sawa na kumwombea adui (shetani) msamehewe pamoja.(labda kama dhamiri nitofauti na kauli)

Take home value: Hii sala bila ya hivyo vipengele hapo kwenye mabano ina make sense zaidi, hivyo kwa fikra zangu naamini kabla ya kuongezewa vipengele nilivyovibainisha kwa mabano hapo juu ilipaswa kuwa hivyo.
Kati ya watu hao wawili, yupi alifanya kwa kudamiria na ni yupi aliyefanya pasipo kudhamiria?
 
Kati ya watu hao wawili, yupi alifanya kwa kudamiria na ni yupi aliyefanya pasipo kudhamiria?
Je, kuna kipimo hicho katika dhambi? Maana ninavyofahamu mimi kulingana na hayo maandiko husika dhambi zote ni sawa.
 
QURAN 40: 47-49

47: "Na watapo hojiana huko Motoni, wanyonge (wafuasi) watawaambia walio jitukuza: Hakika sisi tulikuwa wafuasi wenu, basi je, hamtuondolei sehemu ya huu Moto?"



48. "Watasema walio jitukuza: Hakika sote sisi tumo humu humu (motoni)! Kwani Mwenyezi Mungu kesha hukumu baina ya waja!"



49. "Na walio Motoni watawaambia walinzi wa Jahannamu: Mwombeni Mola wenu Mlezi atupunguzie walau siku moja ya adhabu".



50. "Nao watasema: Je! Hawakuwa wakikufikieni Mitume wenu kwa hoja zilio wazi? Watasema: Kwani? (Hapana walifika) Watasema: Basi ombeni! Na maombi ya makafiri hayawi ila ni kupotea bure tu."


Je, uoni kama maandiko haya yamelenga kuvutia upande mmoja kuwa sahihi (uislamu) na mwingine ni batili (ukristo) pasipo kuwa na hoja ya msingi?

Je, unaweza kututhibitishia uhalali wa Quran kutokughushiwa na binadamu au kueleza baadhi ya uongo katika aya zake?
 
QURAN 2: 2-5

2. "Hiki ni Kitabu kisichokuwa na shaka ndani yake; ni uwongofu kwa wachamungu",



3. "Ambao huyaamini yasiyoonekana na hushika Sala, na hutoa katika tuliyo wapa."



4. "Na ambao wanayaamini yaliyo teremshwa kwako, na yaliyo teremshwa kabla yako; na Akhera wana yakini nayo."



5. "Hao wapo juu ya uwongofu utokao kwa Mola wao Mlezi, na hao ndio walio fanikiwa."
 
QURAN 2: 23-24

23. "Na ikiwa mna shaka kwa hayo tuliyo mteremshia mja wetu basi leteni sura moja ya mfano wake, na muwaite mashahidi wenu (wawasaidie) badala ya Mwenyezi Mungu, ikiwa mnasema kweli."



24. "Na mkitofanya - na wala hamtofanya kamwe - basi uogopeni moto ambao kuni zake ni watu na mawe walio andaliwa hao wanao kanusha. "
 
QURAN 10: 37-40

37. "Na haiwezekani Qur'ani hii kuwa imetungwa na haitoki kwa Mwenyezi Mungu. Lakini hii inasadikisha (vitabu) vilivyo tangulia, na ni ufafanuzi wa Kitabu kisicho na shaka ndani yake, kutokana na Mola Mlezi wa viumbe vyote".



38. "Je! Ndiyo wanasema ameizua (hii Quran)? Sema: Hebu na nyie leteni sura moja mfano wake na muwaite (kukusaidieni) muwawezao, asiye kuwa Mwenyezi Mungu, ikiwa nyinyi mnasema kweli."



39. "Bali wameyakanusha wasio yaelewa elimu yake kabla hayajawajia maelezo yake. Kadhalika walio kabla yao walikanusha vile vile. Basi angalia jinsi ulivyo kuwa mwisho wa madhalimu hao. "



40. "Na miongoni mwao wapo wanao iamini, (hii Quran) na miongoni mwao wapo wasio iamini. Na Mola wako Mlezi anawajua vyema mafisadi."
 
QURAN 3: 2-4

2. "Mwenyezi Mungu, hakuna Mungu ila Yeye Aliye Hai, Msimamizi wa yote milele"



3. "Amekuteremshia Kitabu kwa haki, kinacho sadikisha yaliyo kuwa kabla yake. Na aliteremsha Taurati na Injili "



4. "Kabla yake, ziwe uwongofu kwa watu. Na akateremsha Quran (Furqani). Hakika walio zikanusha Ishara za Mwenyezi Mungu watakuwa na adhabu kali. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na Mwenye kulipa."


 
QURAN 2: 132- 137

132. "Na Ibrahim akawausia wanawe, na pia Yakub (aliwausia wanawe): Enyi wanangu! Hakika Mwenyezi Mungu amekuteulieni Dini hii; basi msife ila nanyi mmekuwa Waislamu, wanyenyekevu."



133. "Je! Mlikuwapo yalipo mfikia Yakub mauti, akawaambia wanawe: Mtamuabudu nani baada yangu? Wakasema: Tutamuabudu Mungu wako na Mungu wa baba zako, Ibrahim na Ismail na Ishaka, Mungu Mmoja tu, na sisi tunasilimu kwake"



134. "Hao ni watu walio kwisha pita. Watapata waliyo yachuma, nanyi mtapata mtakayo yachuma; wala hamtaulizwa nyinyi waliyo kuwa wakiyafanya wao."



135. "Na wakasema: Kuweni Mayahudi au Wakristo ndio mtaongoka. Sema: Bali tunashika mila ya Ibrahim mwongofu, wala hakuwa katika washirikina. "



136. "Semeni: Tumemuamini Mwenyezi Mungu na yale tuliyo teremshiwa sisi, na yaliyo teremshwa kwa Ibrahim na Ismail na Is-hak na Yakub na wajukuu zake, na waliyo pewa Musa na Isa, na pia waliyo pewa Manabii wengine kutoka kwa Mola wao Mlezi; hatubagui yeyote katika hao, na sisi tumesilimu kwake".



137. "Basi wakiamini kama mnavyo amini nyinyi, itakuwa kweli wameongoka. Na wakikengeuka basi wao wamo katika upinzani tu. Na Mwenyezi Mungu atakutosheni kukukingeni na shari yao, na Yeye ndiye Msikizi, Mjuzi. "


 

QURAN 3: 19-20

19. "Bila ya shaka Dini mbele ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu. Na walio pewa Kitabu (kabla ya Quran) hawakuhitalifiana ila baada ya kuwajia ujuzi, kwa sababu ya uhasidi ulio kuwa baina yao. Na anaye zikataa Ishara za Mwenyezi Mungu basi hakika Mwenyezi Mungu ni Mwepesi wa kuhisabu."



20. "Na pindi wakikuhoji, basi sema: Mimi nimeusalimisha uso wangu kumwelekea Mwenyezi Mungu, na kadhaalika walio nifuata. Na waambie walio pewa Kitabu na wasio na kisomo: Je! Mumesilimu? Wakisilimu basi wameongoka. Na wakikengeuka basi juu yako ni kufikisha ujumbe tu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwaona waja wake."
 
Back
Top Bottom