Je, Kanga ndio hupiga kelele namna hii? Kanga wangu wanapiga kelele mpaka imekuwa kero kwa majirani

GAZETI

JF-Expert Member
Feb 24, 2011
5,277
6,673
Dah, wakuu nimeamua kujiongeza kwa kufuga kanga, ni mradi mzuril lakini kwa changamoto ninayokutana nayo nimenyoosha mikono.

Nilimwekea kuku wa kwanza mayai 12 ya kanga akatotoa yote lakini wamepona 7 tu. Nikaendelea kuwawekea kuku wengine kwa kuchanganya mayai yao na ya kanga,
Mpaka sasa nina kanga wadogo wadogo 32.

Tatizo ninalolipata hapa ni hawa kanga 7 wakubwa, yaani hayo makelele siyo ya Dunia hii. Acha kabisa ndugu yangu yaani wanapiga makelele mpaka majirani wamekuja kunilalamikia, siyo majirani tu hata mimi mwenyewe nimechemka.

Sasa hawa 7 balaa limekuwa hili wakishafika 100 itakuwaje?

Nipeni uzoefu wafugaji wa Kanga huenda kukawa na namna ya kufanya kudhibiti kelele maana si mchana wala usiku kanga ana kelele tu!
 
Siku nyingine wakipiga hayo makelele turekodie kama hutojali halafu utuwekee humu ili na sisi ambao hatujawahi kushudia tupate cha kusimulia kuhusu hao kanga.
 
🤣🤣🤣🤣🤣Mkuu kwanini hukufanya utafiti kabla ya kuanza? HULALI!!!

Dah, wakuu nimeamua kujiongeza kwa kufuga kanga, ni mradi mzuri
lakini kwa changamoto ninayokutana nayo nimenyoosha mikono.

Nilimwekea kuku wa kwanza mayai 12 ya kanga akatotoa yote lakini wamepona 7 tu,
Nikaendelea kuwawekea kuku wengine kwa kuchanganya mayai yao na ya kanga,
Mpaka sasa nina kanga wadogo wadogo 32.

Tatizo ninalolipata hapa ni hawa kanga 7 wakubwa, yaani hayo makelele siyo ya
Dunia hii, Acha kabisa ndugu yangu yaani wanapiga makelele mpaka majirani
Wamekuja kunilalamikia, siyo majirani tu hata mimi mwenyewe nimechemka.

Sasa hawa 7 balaa limekuwa hili wakishafika 100 itakuwaje?

Nipeni uzoefu wafugaji wa Kanga huenda kukawa na namna ya kufanya kudhibiti
kelele maana si mchana wala usiku kanga ana kelele tu!
 
nishawahi kuwafuga hawa ndege ni balaa..

nilikuwa napenda ugonvi wao, ugomvi wao ni wa wiki nzima au mpka mmoja afe, ila kama unawaachia, siku wakirukwa na akili utaona wanakimbizana kwenye paa, ila wakiwa katika utulivu utawapenda, ni wapole balaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mkuu mimi nimefuga wale weupe na wale wa madoamadoa nilikuwa nao hamsini
wana kelele sana hasa weupe madume siku moja nilishindwa kuvumilia kelele zao nikawauza wote
kiukweli hawafai kufugia karibu na makazi ya watu
niliwatoa nikaweka bata
 
Hakuna dawa ya kuzuia makelele kumbuka hao kanga ni wanyama wa porini hivyo kelele ni jadi. Yako cha msingi uza au kula Mie nilikua nao niliwala wote kwani wana kelele mno si mchana hata usiku wa manane
 
Changamoto kubwa kwa kanga ni vifo vya ghafla kwa vifaranga. Mwanzoni nilichanganyikiwa unakuta kifaranga mzima kabisa akilowa kidogo tu na hata ukimgusa mikono ikiwa na vimajimaji ghafla anaanza kutetemeka na ndani ya nusu saa amekufa. Akipata stress kidogo amekufa.

Tatizo lingine ni udhaifu wa miguu yaani anatambalia tumbo miguu ime paralyze kabisaa na baada ya muda anakufa

Nilikuwa na vifaranga 200 kila siku wanakufa 10-20 mpaka wakabaki 92

Suluhisho:
Nilikwenda kwa mzee daktari dukani nikamueleza nahitaji chanjo ya kanga na nikampa sababu, akaniambia kanga huwa hashambuliwi na magonjwa Kama kuku na hivyo chanjo haina maana ila vifo kwa vifaranga ni kutokana na upungufu mkubwa wa vitamin A. Alinipa aminovet ya kuwachanganyia kwenye maji (bei 6000) niliwapa mchana ule ule siku ya pili walikufa 2 ambao walikuwa dhaifu na siku ya 3 hakuna kifo na ndiyo ukawa mwisho wa vifo.

Hii iminovet unawapa kila siku na wanaipenda sana, ukiwawekea maji pure hawanywi

Asante sana mzee wangu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah, wakuu nimeamua kujiongeza kwa kufuga kanga, ni mradi mzuril lakini kwa changamoto ninayokutana nayo nimenyoosha mikono.

Nilimwekea kuku wa kwanza mayai 12 ya kanga akatotoa yote lakini wamepona 7 tu. Nikaendelea kuwawekea kuku wengine kwa kuchanganya mayai yao na ya kanga,
Mpaka sasa nina kanga wadogo wadogo 32.

Tatizo ninalolipata hapa ni hawa kanga 7 wakubwa, yaani hayo makelele siyo ya Dunia hii. Acha kabisa ndugu yangu yaani wanapiga makelele mpaka majirani wamekuja kunilalamikia, siyo majirani tu hata mimi mwenyewe nimechemka.

Sasa hawa 7 balaa limekuwa hili wakishafika 100 itakuwaje?

Nipeni uzoefu wafugaji wa Kanga huenda kukawa na namna ya kufanya kudhibiti kelele maana si mchana wala usiku kanga ana kelele tu!
Mimi nina miaka zaidi ya kumi nafuga kanga tena mamia, nawapenda sana kwa sababu kama niko safari mke wangu akiwa hayuko nyumbani najua tu kuwa huyu yuko mchepuko, kwa sababu kanga kwa kelele ni masaa 24. Ila uzuri wake ukisikia wamenyamaza ghafla wote basi ujue mjasiriamali a.k.a Mchawi kakutembelea.
 
Back
Top Bottom