Je, kama wewe ndiye mwenye gari utampa tena lifti mtu huyu?

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Apr 29, 2016
20,744
25,439
ETI?
Upo kituo cha daladala, usafiri ni mgumu, mara unamuona mtu unayemfahamu akiwa na gari lake... unampungia mkono kuomba lifti.
Anakupakia na safari inaendelea... mbele kidogo gari lake linazima, anashuka na kuhangaika nalo. Unashuka na kumwambia una haraka unamuacha hapo.
'Aisee ngoja nikuache mi' nna haraka zangu'
Unaenda kituo cha mbele na kusimama tena ukingoja basi kuwahi mambo yako. Humuulizi hata tatizo ni nini, husaidii hata kusukuma kidogo, wala humuagi kistaarabu kuwa inakulazimu kuwahi uendako.
Ukiwa umedoda tena hapo kituoni, ghafla unamuona aliyekupa lifti akija na gari lake. Kumbe limewaka!
Je, utaomba tena lifti?
Kama wewe ndiye mwenye gari utampa tena lifti mtu huyo?

Urahisi wa kuomba tena lifti na kupewa tena lifti unategemeana na namna ulivyoachana na mtu aliyepatwa na tatizo baada ya kukusaidia.
Wengi tunapoona mtu hana msaada tena kwetu, tunakata mawasiliano haraka sana, hatuonyeshi hata juhudi ndogo ya kutaka kusaidia, hatukumbuki fadhila, na tunasahau shida hazina mwisho.
Dunia hii inazunguka rafiki, katika namna ya ajabu sana unaweza kujikuta ukihitaji tena lifti ya mtu uliyepata kuona hana msaada tena kwako.
Jifunze kuagana na watu vizuri unapoona unatakiwa kuwa mbali nao. Pengine anaweza kuwa alikusaidia ukiwa chini na leo uko juu, unasahau hata kumjulia hali mara moja kwa mwaka kwa kuwa hana msaada tena kwako, yawezekana siku moja ukarudi chini kwa kasi na ukamhitaji mtu huyo huyo akusitiri tena.
Waswahili wanasema usinyee kambi!!
Unapoondoka mahali palipokusitiri, jitahidi kuondoka kwa amani iwe rahisi kwako kurudi. Usione kama hutomhitaji mtu tena, maisha huwa yanajua kutushushua kwelikweli!
Ila turudi kwenye swali utaomba tena lifti au utampa tena lifti baada ya yote 😃😃😃.
 
ETI?
Upo kituo cha daladala, usafiri ni mgumu, mara unamuona mtu unayemfahamu akiwa na gari lake... unampungia mkono kuomba lifti.
Anakupakia na safari inaendelea... mbele kidogo gari lake linazima, anashuka na kuhangaika nalo. Unashuka na kumwambia una haraka unamuacha hapo.
'Aisee ngoja nikuache mi' nna haraka zangu'
Unaenda kituo cha mbele na kusimama tena ukingoja basi kuwahi mambo yako. Humuulizi hata tatizo ni nini, husaidii hata kusukuma kidogo, wala humuagi kistaarabu kuwa inakulazimu kuwahi uendako.
Ukiwa umedoda tena hapo kituoni, ghafla unamuona aliyekupa lifti akija na gari lake. Kumbe limewaka!
Je, utaomba tena lifti?
Kama wewe ndiye mwenye gari utampa tena lifti mtu huyo?

Urahisi wa kuomba tena lifti na kupewa tena lifti unategemeana na namna ulivyoachana na mtu aliyepatwa na tatizo baada ya kukusaidia.
Wengi tunapoona mtu hana msaada tena kwetu, tunakata mawasiliano haraka sana, hatuonyeshi hata juhudi ndogo ya kutaka kusaidia, hatukumbuki fadhila, na tunasahau shida hazina mwisho.
Dunia hii inazunguka rafiki, katika namna ya ajabu sana unaweza kujikuta ukihitaji tena lifti ya mtu uliyepata kuona hana msaada tena kwako.
Jifunze kuagana na watu vizuri unapoona unatakiwa kuwa mbali nao. Pengine anaweza kuwa alikusaidia ukiwa chini na leo uko juu, unasahau hata kumjulia hali mara moja kwa mwaka kwa kuwa hana msaada tena kwako, yawezekana siku moja ukarudi chini kwa kasi na ukamhitaji mtu huyo huyo akusitiri tena.
Waswahili wanasema usinyee kambi!!
Unapoondoka mahali palipokusitiri, jitahidi kuondoka kwa amani iwe rahisi kwako kurudi. Usione kama hutomhitaji mtu tena, maisha huwa yanajua kutushushua kwelikweli!
Ila turudi kwenye swali utaomba tena lifti au utampa tena lifti baada ya yote 😃😃😃.

Mafumbo ya nini?
Kama hutaki na lifti yako , tutaenenda na nguvu zetu
 
Binafsi mtu akinipa lift ikatokea shida njiani tunakomaa wote hadi solution ipatikane, ilishanitokea kama mara 2.

Hata kama hauna utaalamu wa ufundi lkn uwepo wako ni support tosha na at the end unaweza ukatoa msaada fulani ulio ndani ya uwezo wako.
Hongera
 
Sasa kama gari lako bovu, unicheleweshe safari zangu, nikusubiri gari liwake hadi saa ngapi, ndo maana nilikaa stand kusubiri usafiri usio na shombo. Yaani unipe lifti ninyanyasike kisa m gari wako mbovu...we komaa na matatizo yako mi naendelea.
Wengine mnapenda kutoa lifti ili msaidiwe mkipata matatizo njiani.
Ujanja ni kutoa nauli tu kwenye usafiri wa umma. Ikiharibika njiani mnatafuta usafiri mwingine mambo yanaendelea
 
Wakuu mie niliwahi kuachwa hivihivi na jamaa kwenye kapori ukitoka wilaya ya bukombe katikati kabla hujafika pale Mbogwe Mkoa wa Geita, jamaa nilimchukua nyakanazi na anaenda Nzega nilipofika kwenye kapori hako tair ikapata pancha nikashuka nipige jeck nibadilishe tairi wakati nahangaika jamaa akaniambia ana haraka hapo ni kama saa 4 usiku akaondoka mie nikabaki mwenyewe bahati nzuri jamaa mmoja nae kaja yupo peke yake kasimama kanisaidia kubadilisha tair tukaondoka tukapita kahama na mji wa kagongwa ndio tunaelekea isaka kumbe jamaa waliomchukua walikuwa wanaenda maeneo hayo wakamshsha mie nikafika akapiga mkono nikasimama kucheki ni abiria yuleyule nilichokifanya nikamwambia kama una 20000 elfu mpaka nzega twende kama huna baki alilia nami nikakomaa kanitoa kumi na tano ndio nikamchukua wakati nauli kutoka kahama to nzega ni elfu tano tu alisema hatarudia tena
 
ETI?
Upo kituo cha daladala, usafiri ni mgumu, mara unamuona mtu unayemfahamu akiwa na gari lake... unampungia mkono kuomba lifti.
Anakupakia na safari inaendelea... mbele kidogo gari lake linazima, anashuka na kuhangaika nalo. Unashuka na kumwambia una haraka unamuacha hapo.
'Aisee ngoja nikuache mi' nna haraka zangu'
Unaenda kituo cha mbele na kusimama tena ukingoja basi kuwahi mambo yako. Humuulizi hata tatizo ni nini, husaidii hata kusukuma kidogo, wala humuagi kistaarabu kuwa inakulazimu kuwahi uendako.
Ukiwa umedoda tena hapo kituoni, ghafla unamuona aliyekupa lifti akija na gari lake. Kumbe limewaka!
Je, utaomba tena lifti?
Kama wewe ndiye mwenye gari utampa tena lifti mtu huyo?

Urahisi wa kuomba tena lifti na kupewa tena lifti unategemeana na namna ulivyoachana na mtu aliyepatwa na tatizo baada ya kukusaidia.
Wengi tunapoona mtu hana msaada tena kwetu, tunakata mawasiliano haraka sana, hatuonyeshi hata juhudi ndogo ya kutaka kusaidia, hatukumbuki fadhila, na tunasahau shida hazina mwisho.
Dunia hii inazunguka rafiki, katika namna ya ajabu sana unaweza kujikuta ukihitaji tena lifti ya mtu uliyepata kuona hana msaada tena kwako.
Jifunze kuagana na watu vizuri unapoona unatakiwa kuwa mbali nao. Pengine anaweza kuwa alikusaidia ukiwa chini na leo uko juu, unasahau hata kumjulia hali mara moja kwa mwaka kwa kuwa hana msaada tena kwako, yawezekana siku moja ukarudi chini kwa kasi na ukamhitaji mtu huyo huyo akusitiri tena.
Waswahili wanasema usinyee kambi!!
Unapoondoka mahali palipokusitiri, jitahidi kuondoka kwa amani iwe rahisi kwako kurudi. Usione kama hutomhitaji mtu tena, maisha huwa yanajua kutushushua kwelikweli!
Ila turudi kwenye swali utaomba tena lifti au utampa tena lifti baada ya yote 😃😃😃.
Huyo akipewa lift, linazima tena.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom