Je, intelijensia ya mkuu inayaona haya?

singojr

JF-Expert Member
Oct 28, 2014
5,307
6,883
Urais ni taasis kubwa yenye mkono mrefu inayoweza kufika kona yoyote ya nchi kupata habari sahihi kwa wakati sahihi.
Lakini kwa hali inavyoendea nchini naanza kupata shaka na intelligence na watu wanaompa taarifa rais.

Kwanza rais kila siku anahubiri kuwa wanaoisoma namba ni wavivu na mafisadi, hivi kweli taarifa sahihi zinamfikia kuwa wakulima na wanyonge ambao wanajituma katika shughuli zao ndo wananyanyasika huku hakuna fisadi hata mmoja kwenye hao tunaowasikia anaisoma namba? Mahakama imeanzishwa lakini hakuna kesi hata moja ya maana tumeisikia sasa ilikuwa na haja gani kuanzishwa.

Pili ajira, je serikali ilipokuwa inaahidi ajira kwa vijana wakati wa kampeni haikujua vijana wanatakiwa kujiajiri hivi hatuwezi kuajiri huku tunaendelea na uhakiki wa watumishi hewa?, intelligensia inajua ni kiasi gani serikali inapoteza kwa kutoajiri wafanyakazi kwenye taasisi mbalimbali? Maana hawaajiriwi kusaidia serikali bali kuleta faida serikalini.

Tatu, serikali inatambua kuwa raia wengi wanaombea rais afeli ili abadilishe muolekeo wake qa kutokushaurika? Au bado wanakaa kukariri kwamba huku mtaani bado wapendwa na kusifiwa kama watetezi wa wanyonge.Inajua kuwa wazee wazalendo walisiolipwa mafao yao hawana imani tena na serikali, inajua kuwa vijana wanaofanya kazi kwa mkataba na hawajapata mafao yao hawasikilizi tena habari za "serikali ya wanyonge" inafahamu kwamba wanafunzi waliokosa mkopo na watu wa kagera hawawatazami kama walivyowatazama awali.

Ni wakati serikali iache michezo ya kuigiza na matamko yasiyo na tija ni wakati wa serikali kukubali walipotea waanze upya kwa kushughulikia matatizo ya wananchi. Sio kuhangaika na ndege, mahakama ya mafisadi na sheria kandamizi za habari. Tunataka tuambiwe tulime mazao gani maana no viwanda gani vinajengwa na sio ubabaishaji.
 
Hamtaisha lawama!!! Mwambieni white air awarekebishie hali. Mmejenga roho na ujasiri kama wa shetani kabla hajatupwa duniani!!!
 
Hamtaisha lawama!!! Mwambieni white air awarekebishie hali. Mmejenga roho na ujasiri kama wa shetani kabla hajatupwa duniani!!!
Kumbe hadi nyie mnatamani rais awe mwingine poleni. Malaika mkuu ameasi
 
Hao wanajidaganya yani fisadi aisome number kivipi wanaoumia wengi ni wale wakipato cha chini na wasio jua kesho yao inakuwaje pamoja na wakulima ambao ni more than 80%. Sasa nikisikia hyo kauli ya wajanja na mafisadi huwa nashangaa hawa wanasiasa
 
Hao wanajidaganya yani fisadi aisome number kivipi wanaoumia wengi ni wale wakipato cha chini na wasio jua kesho yao inakuwaje pamoja na wakulima ambao ni more than 80%. Sasa nikisikia hyo kauli ya wajanja na mafisadi huwa nashangaa hawa wanasiasa
Tunaambiwa wako kwenye mikono salama. Hivi fisadi ni ntu wa kuwekwa kwenye mikono salama?
 
Tuwe wakweli hapa hakuna hata fisadi mmoja atakayeishi kama shetani, Ukiwa fisadi lazima uwe na account za benki nchi tofauti. Kutakuwa na mirija flani imefungwa au kupungua kufanya ufisadi lakini hela lazima iingie kwa fisadi. Ukweli mwenye kuishi maisha ya shetani ni masikini ya Mungu hana akiba hata hapa nchini achia nchi za nje.
 
Tuwe wakweli hapa hakuna hata fisadi mmoja atakayeishi kama shetani, Ukiwa fisadi lazima uwe na account za benki nchi tofauti. Kutakuwa na mirija flani imefungwa au kupungua kufanya ufisadi lakini hela lazima iingie kwa fisadi. Ukweli mwenye kuishi maisha ya shetani ni masikini ya Mungu hana akiba hata hapa nchini achia nchi za nje.
Hawa wa vyeti feki sijaona hata mmoja alieshikwa hadi sahivi heqa ndo siamini kabisaaa maana mishahara inayolipwa iko pale pale
 
Yeye hajaribiwi...ukipeleka tu rambirambi imekula kwako!
Kapiga zote.jpg
 
Maswali kama haya ya mleta maada ilipaswa kuyauliza 2020 sasa ivi ndio kwanza asubui hata hakujakucha ila baadhi ya viwanda vimeanza kujengwa uwe unaangalia TBC 1 mwaka mmoja wa Rais ingawa, tv haipendwi na wengi kwakuwa inarudiarudia vipindi, jaribu kuangalia utaona hii serikali imefanya nini?
 
Back
Top Bottom