<br />Inawezekana lakini
inabidi uwe makini sana coz kwenye simu watu wengi huwa wanapretend sana kuwa na characters ambazo si zao. I have a friend of mine ambae alipata boyfriend kupitia kwenye simu. Kabla hajamkubalia alinidokezea kidogo mi nikamwambia amkubalie tu kama rafiki wa kawaida mpaka pale watakapokuja kuonana na kila mtu akaridhika na mwenzake ndo waanzishe huo uhusiano wao. Ye akachagua kutokusubiri coz alikolea kwelikweli. Sasa kimbembe kimetokea pale walipoonana live, mwenzangu jitu si hilo! Yaani pande la baba alafu limemzidi sana kiumri adi mi mwenyewe nilishangaa kwakweli, jinsi alivokuwa anaongea kwenye simu na nilivyomuona ni tofauti kabisa. Zimepita siku mbili rafiki yangu akamtosa huyo jamaa, wee nusura amuue, alimkaba koo huku akisisitiza eti kwanini amempotezea mda kiasi hicho? Ni mengi yaliendelea ila nataka kusema kuwa unapoamua kumdate mtu kwenye simu ni lazima uwe mwangalifu sana kwa sababu unachokitarajia unaweza usikipate. Hivyo vimaneno vitamu vitamu na vivocha visikudanganye!
<br />watu wengi nikiwauliza kuhusu kujenga huusiano kwenye cm kama inawezekana,wanajibu ndio,je na nyinyi washilika wenzangu mnaionaje?
<br />Kuna rafiki yangu alikutana na mumewe kwenyee kukosea namba, aliita taxi, yaani ikachelewa,akatuma msg unanichelewesha Aport,ikaenda kwa mkaka mtanashati, akamwambia pole umekosea namba, ila mie pia naelekea aport, akamuuliza unakaawapi? Msichana akajibu tangi bovu,kijana anakaa tegeta,ndege wanasafiria moja kwenda mwanza, looo wakapitiana, kilichoendelea huko ni historia,wameoana na wana mtoto mmoja, kwa hiyo wakati mwingine huwa ina work out,ila sio nara nyingi,ni golden chance<br /><br />
<br />
Si kwa simu tu hata hapa Jamii Forum waweza pata ndoa