Je,inawezekana mkaazisha huusiano wa kimapenzi kwa kupitia cm?

twenty2

JF-Expert Member
May 20, 2011
296
32
watu wengi nikiwauliza kuhusu kujenga huusiano kwenye cm kama inawezekana,wanajibu ndio,je na nyinyi washilika wenzangu mnaionaje?
 
Inawezekana lakini inabidi uwe makini sana coz kwenye simu watu wengi huwa wanapretend sana kuwa na characters ambazo si zao. I have a friend of mine ambae alipata boyfriend kupitia kwenye simu. Kabla hajamkubalia alinidokezea kidogo mi nikamwambia amkubalie tu kama rafiki wa kawaida mpaka pale watakapokuja kuonana na kila mtu akaridhika na mwenzake ndo waanzishe huo uhusiano wao. Ye akachagua kutokusubiri coz alikolea kwelikweli. Sasa kimbembe kimetokea pale walipoonana live, mwenzangu jitu si hilo! Yaani pande la baba alafu limemzidi sana kiumri adi mi mwenyewe nilishangaa kwakweli, jinsi alivokuwa anaongea kwenye simu na nilivyomuona ni tofauti kabisa. Zimepita siku mbili rafiki yangu akamtosa huyo jamaa, wee nusura amuue, alimkaba koo huku akisisitiza eti kwanini amempotezea mda kiasi hicho? Ni mengi yaliendelea ila nataka kusema kuwa unapoamua kumdate mtu kwenye simu ni lazima uwe mwangalifu sana kwa sababu unachokitarajia unaweza usikipate. Hivyo vimaneno vitamu vitamu na vivocha visikudanganye!
 
Inawezekana. Ila inabidi kuwa makini unaweza kuta ni jambazi at! Mwisho wa siku inakula kwako.
 
Kuna rafiki yangu alikutana na mumewe kwenyee kukosea namba, aliita taxi, yaani ikachelewa,akatuma msg unanichelewesha Aport,ikaenda kwa mkaka mtanashati, akamwambia pole umekosea namba, ila mie pia naelekea aport, akamuuliza unakaawapi? Msichana akajibu tangi bovu,kijana anakaa tegeta,ndege wanasafiria moja kwenda mwanza, looo wakapitiana, kilichoendelea huko ni historia,wameoana na wana mtoto mmoja, kwa hiyo wakati mwingine huwa ina work out,ila sio nara nyingi,ni golden chance
Inawezekana lakini
inabidi uwe makini sana coz kwenye simu watu wengi huwa wanapretend sana kuwa na characters ambazo si zao. I have a friend of mine ambae alipata boyfriend kupitia kwenye simu. Kabla hajamkubalia alinidokezea kidogo mi nikamwambia amkubalie tu kama rafiki wa kawaida mpaka pale watakapokuja kuonana na kila mtu akaridhika na mwenzake ndo waanzishe huo uhusiano wao. Ye akachagua kutokusubiri coz alikolea kwelikweli. Sasa kimbembe kimetokea pale walipoonana live, mwenzangu jitu si hilo! Yaani pande la baba alafu limemzidi sana kiumri adi mi mwenyewe nilishangaa kwakweli, jinsi alivokuwa anaongea kwenye simu na nilivyomuona ni tofauti kabisa. Zimepita siku mbili rafiki yangu akamtosa huyo jamaa, wee nusura amuue, alimkaba koo huku akisisitiza eti kwanini amempotezea mda kiasi hicho? Ni mengi yaliendelea ila nataka kusema kuwa unapoamua kumdate mtu kwenye simu ni lazima uwe mwangalifu sana kwa sababu unachokitarajia unaweza usikipate. Hivyo vimaneno vitamu vitamu na vivocha visikudanganye!
<br />
<br />
 
watu wengi nikiwauliza kuhusu kujenga huusiano kwenye cm kama inawezekana,wanajibu ndio,je na nyinyi washilika wenzangu mnaionaje?
<br />
<br />
Mkuu hiyo hutokea sana tu! Mimi kuna swaiba yangu mkubwa ana Gf wake ambaye mwanzo wao wa kimapenzi ni kupitia simu! Wamewasiliana kwa miezi 6 pasipo kujuana sura, na mpaka sasa wanaishi vyema!
 
Kuna rafiki yangu alikutana na mumewe kwenyee kukosea namba, aliita taxi, yaani ikachelewa,akatuma msg unanichelewesha Aport,ikaenda kwa mkaka mtanashati, akamwambia pole umekosea namba, ila mie pia naelekea aport, akamuuliza unakaawapi? Msichana akajibu tangi bovu,kijana anakaa tegeta,ndege wanasafiria moja kwenda mwanza, looo wakapitiana, kilichoendelea huko ni historia,wameoana na wana mtoto mmoja, kwa hiyo wakati mwingine huwa ina work out,ila sio nara nyingi,ni golden chance&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;
<br />
<br />
Ni kweli kabisa huwa inatokea watu wanapendana kupitia simu na hatimae wanatengeneza maisha mazuri, kwani huwezi jua mpenzi wako wakweli utakutana nae wapi. Ila sometimes pia ni full magumashi!!
 
Samahani kuna neno lakiswahili""koma"" cheki kwenye kamusi
nakupenda sana usifike huko
 
Mwenzenu Mwaka 2000 Shemeji yangu alipewa simu aina ya Ericcson a1018s kama zawadi kwenye harusi, simu ikuwa kubwa flani hivi. Shemeji akaiweka ikawa inatumika kama simu ya pale nyumbani sababu hakupenda kutumia ule MSHINDI. Ikawa ile simu usiku mie nabaki nayo asubuhi inarudi sebuleni. Kuna siku jioni nikakuta miscall km mbili namba siijui! nikaandika sms "mambo" ikajibiwa ya kwanza ya pili...... kumbe walikuwa wanafunzi wa kike wawili, majina yao nayahifadhi, Mmoja Msomali mwingine Mtoto wa Kichaga bana! walikuwa form five wakati huo, tulichat sana usiku tunapigiana simu kila siku usiku tunaongea lkn hatukuweza panga kukutana. wakamaliza form six, Mtoto wa kisomali akaenda kusoma Ulaya, huyu ndo alikuwa mstari wa mbele sana kchat na mimi. alipoondoka ikawa ndo mwisho wa mawasiliano naye. Huyu aliyebaki tukaendelea kuchat naye na baadaye yeye kaingia University of Dar es salaam campus ya Muhimbili. ilikuwa kila asubuhi, mchana, jioni ni Hi!!/mambo hapo sijamtongoza wala nini ni km friend tuu. Mwaka 2002 nikapata kazi!! tukaendelea kuwasiliana naye, tunataniana kila mmoja anamwambia mwenzie mipango yake ya baadaye!! hii iliendelea mpaka 2003 ndo kwa mara ya kwanza tukapanga tukutane!! mitaa ya Posta nikamwona tukaongea sana mtoto alikuwa mzuri rangi ya chocolate, hana makuu!! nikawa namtania Doc mtarajiwa ukiwa doctor ntakuja unichome sindano ya MOYO hahaha

Mwanzoni Kwa kweli sikupenda kumuumiza huyu dada sababu tayari nilikuwa na mtu ambaye alinibana vilivyo, huyu dada ni mstaarabu sana na tuliendelea kuchat kwa sana. mwaka 2004 nikahamia gheto hapa ndo mambo yakaanza kuharibika, huyu mpenzi wangu akawa anakuja kupiga mbonji gheto sometimes a week nzima. Kuna siku nikamtania huyu dada kwa sms kwamba it has been long enough just chatting lets try have a date! ooops she was so excited! hakuamini, the next day akapiga simu km saa moja jioni nipo gheto na huyu mchumba wangu, tukaongea vizuri huku mchumba wangu akisikiliza kwa makini, hatukuongea vitu vibaya kwa kweli, na nikamwambia ukweli kwamba huyu ni rafiki yangu yupo chuoni muhimbili anasoma, kumbe mwenzangu hakupenda akaiba ile namba siku ya pili alipoondoka akampigia yule dada akamtukana sawa sawa! dah kwa kweli iliniuma sana!! alipokuja kuniuliza mbona GF wako ananitukana wakati sina kosa? she was a good friend!! nikamwomba msamaha basi akawa not happy at all!! akawa sasa anapiga muda anajua niko job ananisalimia. Mawasiliano yakawa yanapungua na baadaye akabadilisha na namba kabsaaa!! saasa hivi ni DOc kabsaa na huwa namuona kwenye baadhi ya matangazo ya madaktari wa MEWATA! nahisi sikumtendea jema! lkn ntafanyaje? na nimeshaoa, na nadhani na yeye keshaolewa, basi km yupo JF anisamehe tuu, shughuli za ujana si mchezo, SIMU ILITUKUTANISHA lkn haikuwa Mpango wa mungu!!!!
 
Inawezekana,ila inakuwa shida pale mwenzio anapokuwa kapewa namba na m2 anayekujuwa au yeye mwenyewe anakujuwa akatafuta namba yk.Hata kuendesha,tuwe wa angalifu xna
 
Back
Top Bottom