Boko haram
JF-Expert Member
- Nov 7, 2011
- 3,253
- 1,229
Kuna kauli zinazozungumzwa kila siku kwamba watu wanatakiwa kutenganisha dini na siasa na ugomvi mkubwa kati ya kikundi cha uamsho na serikali ya mapinduzi ya zanzibar ni suala la kutenganisha dini na siasa, katika mihadhara ya uamsho sheikh farid alisema kwa mujibu wa dini ya uislamu huwezi kutenganisha kati ya dini na siasa kwasababu dini ya uislamu ni mfumo kamili wa maisha ya binadamu ;1 kwamfano masuala ya hukumu mwizi anapoiba hukumu yake nini nini 2 masuala ya mirathi 3 masuala ya biashara na hata mitume wote walitumwa kwa wafalme ambao kwasasa ni kama unavyowazungumzia maraisi hata suleiman alikua nabii na mfalme kwahiyo na yeye alichanganya dini na siasa?