Je,inaweza kuwa Rais Magufuli ndiye Mfalme Daudi wa kizazi cha sasa?

Pure_sapiens

JF-Expert Member
Dec 25, 2016
2,196
2,020
Daudi aliteuliwa baada ya Sauli....

Mwenyezi Mungu akamwagiza Samweli amteue Sauli kwa kumpaka mafuta ili awe Mfalme wao.Sauli ni nani? Sauli alikuwa mtoto wa Kishi kutoka kabila la Benyamin.

M/Mungu alimkataa Sauli kuwa Mfalme wa wa Israel na kumwambia Samweli chukua haya mafuta ya Zeituni nenda kule Bethlehem kwa mtu aitwaye Yese Nimemchagua mmoja wa vijana wake awe Mfalme.

Samweli alishikwa na woga akasema,"Sauli akisikia mambo hayo ataniua"M/Mungu alimwambia aende tu.Samweli alipofika nyumbani kwa Yese alimwagiza ajitakase yeye na wanawe wote.Samweli akamwambia Yese niitie wanao wote 6 hapa.Samweli alipomwona Eliabu mtoto mkubwa wa Yese akasema.

Kijana huyu anayesimama mbele ya M/Mungu hakika ndiye aliyeteuliwa,Lakini M/Mungu akamwambia "Usiangalie urefu na uzuri wake.Mimi nimemkataa kwani siamui kama wanavyoamua watu.Watu wanaangalia uzuri wa nje tu.Lakini na angalia mioyo" Lakini Samweli akaendelea kuwaita wanawe wote wa Yese M/Mungu alaiendelea kuwaka taa.

Kisha Samweli akamwuliza Yese,"Je huna wana wengine?" Yese akamjibu
"Yuko mwingine na ambaye ndiye mdogo,Lakini amekwenda kuchunga kondoo" Samweli akamwambia"Hatuwezi kutambika mpaka atakapofika" Yese akamtuma mwanawe akamwite.Alipowasili kijana huyo M/Mungu akamwambia Samweli."Huyu ndiye.Mpake mafuta"Samweli akachukuwa mafuta ya Zeituni na kumpaka mafuta mbele ya kaka zake.

Mara roho Mwenyezi Mungu akamwingia Daudi.
[black] Daudi anamwambia Goliath.
Kwa kipindi kirefu waisraeli walikuwa na vita vya Mara kwa Mara na Wafilisti.Siku moja ~Wafilisti walijiandaa kupigana na Waisraeli .Waisrael walikuwa juu ya mlima mmoja na Wafilisti walikuwa juu ya mlima mwingine katikati yao kulikuwa na Bonde.

Shujaa mmoja wa Wafilisti aliyeitwa Goliath,alijitokeza ili kupigana na Waisrael.Goliath alikuwa na urefu wa mita tatu,vazi lake la vita lilikuwa uzito wa kilo hamsini na saba na kofia ya shaba na miguuni alivaa shaba.Mkuki wake ulikuwa na uzito wa kilo saba,mpini wa mkuki huo ulikuwa mnene kama mti wa mfumanguo,Ngao yake ilibebwa na mtu mwingine aliyemtangulia mbele.

Goliath alisimama na kuwatukana Waisrael na Sauli akiwaambia"Mini ni mfilisti halisi.chagueni mtu wenu aje apigane nami.Akishinda na kuniua,sisi tutakuwa watumwa wenu Lakini nikishinda na kumwua ninyi nyote mtakuwa watumwa wetu.Basi Waisrael wote wakaanza kutetemeka kwa hofu.Bila kuogofya Goliath aliendelea kuwatukana Waisrael kwa muda wa siku arubaini,usiku na mchana.

Daudi ajitoa kupigana. Basi siku moja Yese alimtuma Daudi ili kwenda kuwa angalia kaka zake vitani.Daudi alipofika huko,aliwakuta waisreli na Wafilisti wakiwa tayari kushambuliana.Mara akatokea Goliath na kufanya kama alivyozoea Daudi alimsikia Goliath.

Daudi aliposikia maneno ya Goliath aliwauliza watu waliokuwa karibu naye "Je mtu atakayeliua lile jitu la Wafilisti na kuwakomboa waisraeli kutoka dharau zake atapata nini?" Wakamwambia kuwa Mfalme Sauli atamwoza binti yake na Yeye pamoja na ndugu zake hawatakuwa wanalipa kodi.

Daudi akamwambia Sauli kuwa nitakwenda kupambana na Goliath. Watu waliposikia maneno ya Daudi walimcheka,walimdharau na kumkejeli kuwa atashindwa na kufa kifo kibaya sana.Na hali hiyo ilitokana na umbo la Daudi kuwa mdogo.

PAMBANO
Goliath alipomwona Daudi anamjia alimdharau sana akamwuliza"Sasa hiyo fimbo ni ya nini?Unadhani Mimi mbwa?"
Daudi alimaambia"Mimi nakuja kwa jina la Mwenyezi Mungu. Nitakukata kichwa chako na miili ya wanajeshi wako.

Daudi akachukuwa jiwe lake moja na kuliweka kwenye kombeo lake na kulirusha lile jiwe;nalo lilimpiga Goliath kwenye paji lake na uso na kulivunja,ghafla Goliath akaanguka chini akafa.Daudi akachukuwa panga na kukata kichwa na kumpelekea Mfalme.Daudi akawa mshindi Katika vita hii ngumu

Je kupitia kisa hiki cha kweli tunajifunza nini?
Nawasilisha kwenu ndugu zangu...
 
Daudi aliteuliwa baada ya Sauli....

Mwenyezi Mungu akamwagiza Samweli amteue Sauli kwa kumpaka mafuta ili awe Mfalme wao.Sauli ni nani? Sauli alikuwa mtoto wa Kishi kutoka kabila la Benyamin.
M/Mungu alimkataa Sauli kuwa Mfalme wa wa Israel na kumwambia Samweli chukua haya mafuta ya Zeituni nenda kule Bethlehem kwa mtu aitwaye Yese Nimemchagua mmoja wa vijana wake awe Mfalme.
Samweli alishikwa na woga akasema,"Sauli akisikia mambo hayo ataniua"M/Mungu alimwambia aende tu.Samweli alipofika nyumbani kwa Yese alimwagiza ajitakase yeye na wanawe wote.Samweli akamwambia Yese niitie wanao wote 6 hapa.Samweli alipomwona Eliabu mtoto mkubwa wa Yese akasema.Kijana huyu anayesimama mbele ya M/Mungu hakika ndiye aliyeteuliwa,Lakini M/Mungu akamwambia "Usiangalie urefu na uzuri wake.Mimi nimemkataa kwani siamui kama wanavyoamua watu.Watu wanaangalia uzuri wa nje tu.Lakini na angalia mioyo" Lakini Samweli akaendelea kuwaita wanawe wote wa Yese M/Mungu alaiendelea kuwaka taa.

Kisha Samweli akamwuliza Yese,"Je huna wana wengine?" Yese akamjibu
"Yuko mwingine na ambaye ndiye mdogo,Lakini amekwenda kuchunga kondoo" Samweli akamwambia"Hatuwezi kutambika mpaka atakapofika" Yese akamtuma mwanawe akamwite.Alipowasili kijana huyo M/Mungu akamwambia Samweli."Huyu ndiye.Mpake mafuta"Samweli akachukuwa mafuta ya Zeituni na kumpaka mafuta mbele ya kaka zake.
Mara roho Mwenyezi Mungu akamwingia Daudi.
[black] Daudi anamwambia Goliath.
Kwa kipindi kirefu waisraeli walikuwa na vita vya Mara kwa Mara na Wafilisti.Siku moja ~Wafilisti walijiandaa kupigana na Waisraeli .Waisrael walikuwa juu ya mlima mmoja na Wafilisti walikuwa juu ya mlima mwingine katikati yao kulikuwa na Bonde.
Shujaa mmoja wa Wafilisti aliyeitwa Goliath,alijitokeza ili kupigana na Waisrael.Goliath alikuwa na urefu wa mita tatu,vazi lake la vita lilikuwa uzito wa kilo hamsini na saba na kofia ya shaba na miguuni alivaa shaba.Mkuki wake ulikuwa na uzito wa kilo saba,mpini wa mkuki huo ulikuwa mnene kama mti wa mfumanguo,Ngao yake ilibebwa na mtu mwingine aliyemtangulia mbele.Goliath alisimama na kuwatukana Waisrael na Sauli akiwaambia"Mini ni mfilisti halisi.chagueni mtu wenu aje apigane nami.Akishinda na kuniua,sisi tutakuwa watumwa wenu Lakini nikishinda na kumwua ninyi nyote mtakuwa watumwa wetu.Basi Waisrael wote wakaanza kutetemeka kwa hofu.Bila kuogofya Goliath aliendelea kuwatukana Waisrael kwa muda wa siku arubaini,usiku na mchana.
Daudi ajitoa kupigana
Basi siku moja Yese alimtuma Daudi ili kwenda kuwa angalia kaka zake vitani.Daudi alipofika huko,aliwakuta waisreli na Wafilisti wakiwa tayari kushambuliana.Mara akatokea Goliath na kufanya kama alivyozoea Daudi alimsikia Goliath.Daudi aliposikia maneno ya Goliath aliwauliza watu waliokuwa karibu naye "Je mtu atakayeliua lile jitu la Wafilisti na kuwakomboa waisraeli kutoka dharau zake atapata nini?" Wakamwambia kuwa Mfalme Sauli atamwoza binti yake na Yeye pamoja na ndugu zake hawatakuwa wanalipa kodi.
Daudi akamwambia Sauli kuwa nitakwenda kupambana na Goliath. Watu waliposikia maneno ya Daudi walimcheka,walimdharau na kumkejeli kuwa atashindwa na kufa kifo kibaya sana.Na hali hiyo ilitokana na umbo la Daudi kuwa mdogo.
PAMBANO
Goliath alipomwona Daudi anamjia alimdharau sana akamwuliza"Sasa hiyo fimbo ni ya nini?Unadhani Mimi mbwa?"
Daudi alimaambia"Mimi nakuja kwa jina la Mwenyezi Mungu. Nitakukata kichwa chako na miili ya wanajeshi wako.Daudi akachukuwa jiwe lake moja na kuliweka kwenye kombeo lake na kulirusha lile jiwe;nalo lilimpiga Goliath kwenye paji lake na uso na kulivunja,ghafla Goliath akaanguka chini akafa.Daudi akachukuwa panga na kukata kichwa na kumpelekea Mfalme.Daudi akawa mshindi Katika vita hii ngumu
Je kupitia kisa hiki cha kweli tunajifunza nini?
Nawasilisha kwenu ndugu zangu...
Hilo liko wazi kabisa!! NDIO.
Mungu alimuuliza JK, hamna mwingine kweli?? Jk akasema yupo mwingine 'mbugani ila ni mdogo', the rest is history!
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom