JE huu ni uungwana????????

kunyamba barabaran kimya kimya uku unatembea alafu unajifanya hakuna kitu kimetokea..
 
kwenye vituo vya daladala kuwauzia wenzio mishikaki ya nyama ya paka kisa umeitia ndimu na tangawizi inanukia kama mbuzi
 
kumfundisha mwanao nidhamu mpaka akitaka kufungua mlango wa friji anapiga hodi
 
kubadilisha majina ya timu za wenzako mara arsenane,chelthree,liverfour
 
kumkosoa mtu kwa kutumia kabila lake''we mhaya ebu njoo hapa! hivi we mwanamke utaacha lini tabia zako za kihaya??''
 
'' we konda ebu shusha hapo kwenye nyumba yenye geti la kijani!''utafikiri gari umekodisha
 
kudharau kazi za wenzako ''yani mtoto amefeli mnashindwa ata kumpeleka ualimu''
 
kualika watu baa alafu badala ya kuzungusha round we unazungusha pembetatu, yani wewe,demu wako na shemejio
 
kumfukuzia msichana mpaka kanisani,alafu unajifanya unampa ofa ya kumtolea sadaka eti''usihofu dada acha tu nitatoa na ya kwako''
 
kuingia ofisi za watu na t-shirt lako limeandikwa ''kama vp nipotezee''
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom