Je, huu ndio mwisho wa maridhiano ya CHADEMA na CCM?

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
116,416
215,176
Kamati Kuu ya Chadema iliyoketi siku chache zilizopita imetoka na maazimio kadha wa kadha yenye lengo la kujenga Demokrasia na kuimarisha Utawala wa Sheria Nchini Tanzania .

Maazimio ya kamati kuu hiyo ambayo kiuhalisia ni KAMA DIRA YA TAIFA yalisubiriwa kwa hamu kubwa karibu Dunia nzima , na sasa maazimio hayo yamewekwa hadharani kupitia Mkutano wa Waandishi wa Habari na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Salum Mwalimu .

Baadhi ya maazimio ambayo kimsingi yanagusa moja kwa moja Uhai wa Mazungumzo ya Maridhiano ni pamoja na Sharti la kuondolewa kwa Wabunge wanaoitwa COVID 19 , Wakiongozwa na Halima Mdee , hawa waliingizwa bungeni kinyume cha sheria kwa lengo la KUWADANGANYA WAFADHILI ILI WAONE KWAMBA TANZANIA KUNA DEMOKRASIA YA VYAMA VINGI ILI SERIKALI IPEWE MISAADA , Chadema inataka maridhiano yaendelee baada mamluki hawa kuondolewa bungeni maana walishavuliwa uanachama wa Chadema .

Azimio lingine kabambe kutoka Chadema linahusu KUONDOLEWA KWA ZUIO HARAMU LA MIKUTANO YA HADHARA , ikumbukwe kwamba mikutano ya hadhara na maandamano ni haki iliyo ndani ya Katiba ya Nchi .

MWL NYERERE aliwahi kunukuliwa huko nyuma akitamka kwamba CHAMA CHA SIASA NI MABARABARANI NA MAJUKWAANI , hapa alimaanisha kwamba uhai wa chama chochote cha siasa uko kwenye maandamano na mikutano ya hadhara .

Sasa Swali letu ni hili , kwa Masharti haya ambayo ni kitanzi kwa ccm , Je Maridhiano yatadumu , au ccm itaweka mpira kwapani ?
 
Viongozi wa sasa wa CCM wanaishi kwa mazoea tu na huku uhai wa chama chao ukitegemea mbeleko ya vyombo vya dola. Kinasita mno kuruhisu vyama makini kama CDM kufanya mikutano yake kwa wananchi ili kunadi sera zao kwa wanamchi bila vikwazo vyovyote.

Salama ya muda mfupi ya CCM ipo kwa kuliegemea kundi kubwa la watu ambao hawana uelewa wa kina juu ya madhaifu yake, kupitwa na wakati, kufubaa na kuchoka kwa sera mbovu za chama hiki kikongwe, ambazo haziendani na matakwa halisi ya nyakati wa zama za sasa hivi

Marufuku haramu ilyowekwa ya kuvizuia vyama makini kunadi sera zao, ni kitanzi kwao kwa kuwa ni ubabaishaji wao utakuja tu kuwekwa wazi mbele ya kundi hili. Na endapo kundi hili likija kuelimishwa na kujitambua hapo ndipo rasilimali za nchi zitakuwa mikononi na kwa faida ya wananchi waliokuwa wengi, na wala siyo kwa manufaa ya kundi dogo la watawala hawa wa CCM hii ya sasa.

Jambo moja la kusikitisha ni kwamba mashabikii na wapenzi wengi wa CCM hawaambiliki kabisa kwa kuwa hawana jukwaa rasmi ya kuweza kutambua madhila wanayoletewa na chama chao. Kazi yao ni kushabikia viongozi wao huku wao wakiwa wemepigika mno kimaisha na huku wengi wao wakiishi kwa kubangaiza tu. Mathalani, teuzi zote mpya wala haziwahusu wao japokuwa wana sifa za kiushindani, bali ni watoto wa vigogo, ndugu ama jamaa zao tu ndiyo wanaofikiriwa.

Lakini unamkuta mtu anajitoa ufahamu na wala haoni upendeleo huu, anajua chama hiki kina wenyewe lakini bado kiunafiki anajionyesha kuwa anakiunga mkono. Watu hawa ni lazima watambue chama ambacho kinawabagua hata wafia itikadi zake, hakiwezi kuruhusu haki ya kikatiba kufanya mikutano vya ushindani. Kwa sababu wana hofu kuwa wamezoea kula vibudu, kwa hiyo vya kuchinja ni mtihani mkubwa kwao.
 
Kamati Kuu ya Chadema iliyoketi siku chache zilizopita imetoka na maazimio kadha wa kadha yenye lengo la kujenga Demokrasia na kuimarisha Utawala wa Sheria Nchini Tanzania .

Maazimio ya kamati kuu hiyo ambayo kiuhalisia ni KAMA DIRA YA TAIFA yalisubiriwa kwa hamu kubwa karibu Dunia nzima , na sasa maazimio hayo yamewekwa hadharani kupitia Mkutano wa Waandishi wa Habari na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Salum Mwalimu .

Baadhi ya maazimio ambayo kimsingi yanagusa moja kwa moja Uhai wa Mazungumzo ya Maridhiano ni pamoja na Sharti la kuondolewa kwa Wabunge wanaoitwa COVID 19 , Wakiongozwa na Halima Mdee , hawa waliingizwa bungeni kinyume cha sheria kwa lengo la KUWADANGANYA WAFADHILI ILI WAONE KWAMBA TANZANIA KUNA DEMOKRASIA YA VYAMA VINGI ILI SERIKALI IPEWE MISAADA , Chadema inataka maridhiano yaendelee baada mamluki hawa kuondolewa bungeni maana walishavuliwa uanachama wa Chadema .

Azimio lingine kabambe kutoka Chadema linahusu KUONDOLEWA KWA ZUIO HARAMU LA MIKUTANO YA HADHARA , ikumbukwe kwamba mikutano ya hadhara na maandamano ni haki iliyo ndani ya Katiba ya Nchi .

Sasa Swali letu ni hili , kwa Masharti haya ambayo ni kitanzi kwa ccm , Je Maridhiano yatadumu , au ccm itaweka mpira kwapani ?
Nonsense, baada ya asali waliyolamba kwisha ndio mnakurupuka na maazimio. Genge la hovyo kabisa hili saccos.
 
Kamati Kuu ya Chadema iliyoketi siku chache zilizopita imetoka na maazimio kadha wa kadha yenye lengo la kujenga Demokrasia na kuimarisha Utawala wa Sheria Nchini Tanzania .

Maazimio ya kamati kuu hiyo ambayo kiuhalisia ni KAMA DIRA YA TAIFA yalisubiriwa kwa hamu kubwa karibu Dunia nzima , na sasa maazimio hayo yamewekwa hadharani kupitia Mkutano wa Waandishi wa Habari na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Salum Mwalimu .

Baadhi ya maazimio ambayo kimsingi yanagusa moja kwa moja Uhai wa Mazungumzo ya Maridhiano ni pamoja na Sharti la kuondolewa kwa Wabunge wanaoitwa COVID 19 , Wakiongozwa na Halima Mdee , hawa waliingizwa bungeni kinyume cha sheria kwa lengo la KUWADANGANYA WAFADHILI ILI WAONE KWAMBA TANZANIA KUNA DEMOKRASIA YA VYAMA VINGI ILI SERIKALI IPEWE MISAADA , Chadema inataka maridhiano yaendelee baada mamluki hawa kuondolewa bungeni maana walishavuliwa uanachama wa Chadema .

Azimio lingine kabambe kutoka Chadema linahusu KUONDOLEWA KWA ZUIO HARAMU LA MIKUTANO YA HADHARA , ikumbukwe kwamba mikutano ya hadhara na maandamano ni haki iliyo ndani ya Katiba ya Nchi .

Sasa Swali letu ni hili , kwa Masharti haya ambayo ni kitanzi kwa ccm , Je Maridhiano yatadumu , au ccm itaweka mpira kwapani ?
Hiyo ni kamati ya harusi ya mwajuma ndala ndefu na Juma bonge
 
Sasa Swali letu ni hili , kwa Masharti haya ambayo ni kitanzi kwa ccm , Je Maridhiano yatadumu , au ccm itaweka mpira kwapani ?
Mkuu 'Erythrocyte', mbona jibu la swali ni rahisi?

Ngoja nikupe 'hint," kwani Samia anasimamia wapi kuhusu maswala hayo?

Katika mambo yote yanayozungumzwa kwenye hayo yanayoitwa "maridhiano", hakuna hata moja ambalo Samia ameweka 'commitment' juu yake, kwamba kuna uhakika wa kulitimiza. Badala yake, kwenye maswala yote "ananunua muda", kupteza lengo kiujanjaujanja tu!

Kwa hiyo, kama CHADEMA wanayo mipango yao, hawana budi ya kufuata programu yao badala ya kupotezewa muda.
 
Kamati Kuu ya Chadema iliyoketi siku chache zilizopita imetoka na maazimio kadha wa kadha yenye lengo la kujenga Demokrasia
Demokrasia ya kweli huanzia ndani!
na kuimarisha Utawala wa Sheria Nchini Tanzania .
Kwa kuingilia kesi iliyoko mahakamani?
Maazimio ya kamati kuu hiyo ambayo ni DIRA YA TAIFA yalisubiriwa kwa hamu kubwa karibu Dunia nzima
Hapa ni kweli maana ni chama cha dunia mzima!
Baadhi ya maazimio ambayo kimsingi yanagusa moja kwa moja Uhai wa Mazungumzo ya Maridhiano ni pamoja na Sharti la kuondolewa kwa Wabunge wanaoitwa COVID 19 ,
Kumbe kuna mazungumzo ya maridhiano?. Kumbe maridhiano hayo ya sharti la kuondolewa hao wabunge halali 19?.
Wakiongozwa na Halima Mdee , hawa waliingizwa bungeni kinyume cha sheria
Jambo lolote likifanyika kinyume cha sheria, utatuzi wake ni kwa sheria kufuatwa, na hatua ya kwanza ni kuripoti kwenye vyombo vya sheria, vipi hili lilifanyika?. Chadema mliripoti popote?.
kwa lengo la KUWADANGANYA WAFADHILI ILI WAONE KWAMBA TANZANIA KUNA DEMOKRASIA YA VYAMA VINGI ILI SERIKALI IPEWE MISAADA ,
Duh...!.
Chadema inataka maridhiano yaendelee baada mamluki hawa kuondolewa bungeni
Chadema si nimesema haiutambui uchaguzi na kuuita ni uchafuzi, inahitaji maridhiano ili iweje?. Halafu makamanda walio ipigania Chadema kwa machozi, jasho na damu, leo ni kuitwa mamluki?! Makamanda walioigharimia CHADEMA kwa machozi, jasho na damu, leo ni wakuitwa wasaliti? Karma Haitawaacha salama, itawatandika tu
maana walishavuliwa uanachama wa Chadema.
Maadam Chadema ina katiba yake ambayo imeweka utaratibu wa kuwavua uanachama wanachama wake, jee utaratibu wa kuwavua uanachama ulifuatwa?.
Azimio lingine kabambe kutoka Chadema linahusu KUONDOLEWA KWA ZUIO HARAMU LA MIKUTANO YA HADHARA , ikumbukwe kwamba mikutano ya hadhara na maandamano ni haki iliyo ndani ya Katiba ya Nchi .
Hapa ni kweli zuio lile ni haramu na kinyume cha katiba. Kumbe katiba ikivunjwa, suluhisho ni kutafuta maridhiano kwa mazungumzo?! Nilidhani Chadema kama chama makini ile tuu katiba ya nchi imekiukwa wangechukua hatua stahiki Hoja ya Udikteta wa Magufuli: Tundu Lissu isn't Right. Haupingwi kwa kupaza sauti kupiga tu Kelele!
Sasa Swali letu ni hili , kwa Masharti haya ambayo ni kitanzi kwa ccm , Je Maridhiano yatadumu , au ccm itaweka mpira kwapani ?
Hiki ni swali la msingi sana.
P
 
Demokrasia ya kweli huanzia ndani!

Kwa kuingilia kesi iliyoko mahakamani?

Hapa ni kweli maana ni chama cha dunia mzima!

Kumbe kuna mazungumzo ya maridhiano?. Kumbe maridhiano hayo ya sharti la kuondolewa hao wabunge halali 19?.

Jambo lolote likifanyika kinyume cha sheria, utatuzi wake ni kwa sheria kufuatwa, na hatua ya kwanza ni kuripoti kwenye vyombo vya sheria, vipi hili lilifanyika?. Chadema mliripoti popote?.

Duh...!.

Chadema si nimesema haiutambui uchaguzi na kuuita ni uchafuzi, inahitaji maridhiano ili iweje?. Halafu makamanda walio ipigania Chadema kwa machozi, jasho na damu, leo ni kuitwa mamluki?! Makamanda walioigharimia CHADEMA kwa machozi, jasho na damu, leo ni wakuitwa wasaliti? Karma Haitawaacha salama, itawatandika tu

Maadam Chadema ina katiba yake ambayo imeweka utaratibu wa kuwavua uanachama wanachama wake, jee utaratibu wa kuwavua uanachama ulifuatwa?.

Hapa ni kweli zuio lile ni haramu na kinyume cha katiba. Kumbe katiba ikivunjwa, suluhisho ni kutafuta maridhiano kwa mazungumzo?! Nilidhani Chadema kama chama makini ile tuu katiba ya nchi imekiukwa wangechukua hatua stahiki Hoja ya Udikteta wa Magufuli: Tundu Lissu isn't Right. Haupingwi kwa kupaza sauti kupiga tu Kelele!

Hiki ni swali la msingi sana.
P
1. Ni kweli demokrasia ya kweli huanzia ndani, kama una rafiki yako ambaye hakutendewa haki kule Chadema tutajie, ila asiwe yule wa ACT, huyo alijitakia majanga yakamkuta kwa ujuaji wake, ndumilakuwili.

2. Kesi mahakamani kuingiliwa ni sawa, kwasababu huwezi kuvunja sheria moja, huku ukikimbilia sheria nyingine kwa interest zako, huu ni ubinafsi. Wale wanawake sio wawakilishi wa chama chochote, kule bungeni wanafanya nini? na kwa precedence za case zilizotokea nyuma, na sheria, wale hawana exception yoyote.

3. Kuhusu suala la kuwaripoti hao jamaa kwenye vyombo vya sheria, huko kungekuwa kupotezeana muda tu, kama tunavyoona muda ukipotezwa kwa Spika kuendelea kuwatetea kule bungeni kinyume cha sheria, hizo taasisi za CCM haziaminiki sana, hasa kama kesi zinazokuwepo ni against interest za CCM.

4. Chadema hata kama haiutambui ule "uchafuzi" wa 2020, suala la maridhiano haliko "centred" kwenye jambo moja, yapo mengi yanayohitaji mazungumzo, mfano;

- Mikutano ya hadhara kwa vyama vya upinzani.

- Wanachama wengi wa Chadema wanaoshikiliwa magerezani maeneo mbalimbali nchini.

- Kurejesha kuaminiana baina ya vyama vya upinzani na CCM.

- Kupewa haki zao wale wote walio dhulumiwa. mfano Lissu, na kuhakikishiwa usalama wao wale waliokimbia nchi ili warudi nyumbani, Lissu, Lema, nk.
 
Mkuu 'Erythrocyte', mbona jibu la swali ni rahisi?

Ngoja nikupe 'hint," kwani Samia anasimamia wapi kuhusu maswala hayo?

Katika mambo yote yanayozungumzwa kwenye hayo yanayoitwa "maridhiano", hakuna hata moja ambalo Samia ameweka 'commitment' juu yake, kwamba kuna uhakika wa kulitimiza. Badala yake, kwenye maswala yote "ananunua muda", kupteza lengo kiujanjaujanja tu!

Kwa hiyo, kama CHADEMA wanayo mipango yao, hawana budi ya kufuata programu yao badala ya kupotezewa muda.
Anapoteza muda hadi MWAKA wa uchaguzi mkuu!!ili aweke mazingira ya chama kushinda!anajaribu Bahati yake!happy hajui hakuna uchaguzi BILA KATIBA MPYA!!SIO jukumu la chadema wala CCM la kuamua mstakabali wa Katiba ya nchi hii bali WANANCHI wenye nchi!!
 
1. Ni kweli demokrasia ya kweli huanzia ndani, kama una rafiki yako ambaye hakutendewa haki kule Chadema tutajie, ila asiwe yule wa ACT huyo alijitakia majanga yakamkuta kwa ujuaji wake.
No sio issue ya urafiki, mimi ni mtetezi tuu wa haki za wote nikitetea haki ya Chadema kuwawajibisha wanachama wake ambao ni watovu wa nidhamu ikiwemo kuwatimua, kwa vile katiba ya Chadema imeweka utaratibu wa kuwavua uanachama wanachama wake ambao ni watovu wa nidhamu ikiwemo kuwatimua, then wanachama wanao adhibiwa na kutimuliwa waadhibiwe kwa haki na kutimuliwa kwa haki kwa kufuata kanuni na utaratibu ikiwemo mamlaka halali za nidhamu na sio zile kangaroo courts.
2. Kesi mahakamani kuingiliwa ni sawa, kwasababu huwezi kuvunja sheria huku ukijidai kufuata sheria, wale wanawake sio wawakilishi wa chama chochote, kule bungeni wanafanya nini, na kwa precedence zilizotokea nyuma, wale hawana exception yoyote.
Kuna kitu kinaitwa timing, nikikuzabua kibao au hata nikikubaka, wewe usipolalamika rasmi utaonekana umeridhia!. Na baada ya kukutenda, nikianza mimi kukimbilia mahakamani kukulalamikia umenitenda wewe ndio utapata sweka lupango mpaka ije kuthibitishwa kumbe mchokozi ni mimi, it will take time and by that time you'll have suffered much!.

Hili jambo la wabunge 19 ni simple and straight forward if Chadema would have done the right thing.
  1. Hatua ya kwanza baada ya wabunge hao 19 kuapishwa ni kwa Chadema kufanya an internal due process to establish the authenticity ya barua za uteuzi wao.
  2. Baada ya kubaini hakuna any official letters or official correspondents kati ya Chadema na NEC, then huo ni uthibitisho kuwa majina yale ya hao wabunge, yamepelekwa kwa forged documents hivyo hiyo ni forgery ambayo ni kosa la jinai.
  3. Hatua ya tatu ilikuwa ni kuripoti polisi ili uchunguzi wa kijinai kufanyika na kuwaarifu NEC na Spika
  4. Jeshi la polisi ndio mamlaka pekee nchini Tanzania yenye kuweza kufanya uchunguzi wa kijinai, hivyo NEC wangelazimika kuzionyesha hizo barua za uteuzi za Chadema ambazo ni forged kuthibitisha jinsi ya forgery imetendeka.
  5. Baada ya uthibitisho wa forgery NEC inakuwa haina jinsi bali kutengua uteuzi wao na kumjulisha Spika. Hili jambo lingekuwa limekwisha siku nyingi!.
3. Kuhusu suala la kuwaripoti hao jamaa kwenye vyombo vya sheria, huko kungekuwa kupotezeana muda tu, kama tunavyoona muda ukipotezwa kwa Spika kuendelea kuwatetea kule bungeni, hizo taasisi za CCM haziaminiki sana, hasa kama kesi zinazokuwepo ni against interest za CCM.
Kwa hili naomba tuu kuheshimu mawazo yako, ila kiukweli kabisa CHADEMA Chama cha Ajabu Sana!.Kwenda Mahakamani Kwa Non Issue, Serious Issue ya Katiba ni UKUTA!.
P
 
No sio issue ya urafiki, mimi ni mtetezi tuu wa haki za wote nikitetea haki ya Chadema kuwawajibisha wanachama wake ambao ni watovu wa nidhamu ikiwemo kuwatimua, kwa vile katiba ya Chadema imeweka utaratibu wa kuwavua uanachama wanachama wake ambao ni watovu wa nidhamu ikiwemo kuwatimua, then wanachama wanao adhibiwa na kutimuliwa waadhibiwe kwa haki na kutimuliwa kwa haki kwa kufuata kanuni na utaratibu ikiwemo mamlaka halali za nidhamu na sio zile kangaroo courts.

Kuna kitu kinaitwa timing, nikikuzabua kibao au hata nikikubaka, wewe usipolalamika rasmi utaonekana umeridhia!. Na baada ya kukutenda, nikianza mimi kukimbilia mahakamani kukulalamikia umenitenda wewe ndio utapata sweka lupango mpaka ije kuthibitishwa kumbe mchokozi ni mimi, it will take time and by that time you'll have suffered much!.

Hili jambo la wabunge 19 ni simple and straight forward if Chadema would have done the right thing.
  1. Hatua ya kwanza baada ya wabunge hao 19 kuapishwa ni kwa Chadema kufanya an internal due process to establish the authenticity ya barua za uteuzi wao.
  2. Baada ya kubaini hakuna any official letters or official correspondents kati ya Chadema na NEC, then huo ni uthibitisho kuwa majina yale ya hao wabunge, yamepelekwa kwa forged documents hivyo hiyo ni forgery ambayo ni kosa la jinai.
  3. Hatua ya tatu ilikuwa ni kuripoti polisi ili uchunguzi wa kijinai kufanyika na kuwaarifu NEC na Spika
  4. Jeshi la polisi ndio mamlaka pekee nchini Tanzania yenye kuweza kufanya uchunguzi wa kijinai, hivyo NEC wangelazimika kuzionyesha hizo barua za uteuzi za Chadema ambazo ni forged kuthibitisha jinsi ya forgery imetendeka.
  5. Baada ya uthibitisho wa forgery NEC inakuwa haina jinsi bali kutengua uteuzi wao na kumjulisha Spika. Hili jambo lingekuwa limekwisha siku nyingi!.

Kwa hili naomba tuu kuheshimu mawazo yako, ila kiukweli kabisa CHADEMA Chama cha Ajabu Sana!.Kwenda Mahakamani Kwa Non Issue, Serious Issue ya Katiba ni UKUTA!.
P
- Nakushangaa kwanini hizo "Kangaroo Courts" unazilalamikia, ikiwa hao waliokuwa wanachama wao walikubaliana na taratibu za taasisi yao, wakazijua fika sheria zao, chini ya hizo "Kangaroo Courts", na wakakubali kuzitii ndio maana wakapewa uanachama.

Hapo nakuona una ajenda ya siri.

- Kuhusu hilo suala la timing, nalo sioni hoja yako.

Kwasababu, hao jamaa hawajaviziwa, walikosea, wakaitwa kujitetea, lakini wakaingia mitini.

Baada ya hapo taratibu zikafuatwa kuwawajibisha, na Chadema kama taasisi yenye taratibu na sheria zake, zilizokubaliwa na kusajiliwa na msajili wa vyama, inastahili kuheshimiwa maamuzi yake, lakini kinachofanyika sasa na bunge, ni kuyadharau maamuzi ya vikao halali vya Chadema kama taasisi.

Kwa muktadha huu, unawataka Chadema waende mahakamani kufanya nini? kama bunge limeshindwa kuheshimu maamuzi halali ya vikao vya Chadema kwa manufaa ya CCM, hizo mahakama ndio zitawaheshimu Chadema watapokwenda kutafuta ukweli wa forgery?

Hii ni precedence mbaya wanayoi-set wenyewe bila kujua, tabia zao zinawafanya watu wapoteze imani kwao.
 
15 Reactions
Reply
Back
Top Bottom