Je, hizi Ratiba nyingi za Kikazi na Mizunguko za Waziri Mkuu Kassim Majaliwa zinazingatia pia na Kujali Afya yake kama Kiongozi Mwandamizi nchini?

Mzukulu

JF-Expert Member
Feb 14, 2020
1,401
2,631
Napenda sana na mno Uchapakazi wake Waziri Mkuu wa sasa ( Awamu hii ya Tano ) Mheshimiwa Kassim Majaliwa Kassim ila kuna mahala kama vile naona hapako sawa hasa upande wa mlundiko wa Ratiba zake nyingi ambazo zinahusisha Kusafiri kwa Gari au Ndege ndani na nje ya nchi pasipo hata Kupumzika.

Je, Kiafya hizi Ratiba zake kuwa nyingi nyingi huku zingine zikiwa ni za ghafla haziwezi kuwa na Athari yoyote ile Kwake? Je, kuna ubaya wowote kama kukiwa na Uwiano sawia wa Ratiba za Kikazi na Mizunguko kati yake Waziri Mkuu Majaliwa na Mabosi zake Wawili Wakuu Mheshimiwa Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan na Mwamba mwenyewe Rais Dkt. Magufuli?

Kuna muda huwa nahisi kuwa huenda Waziri Mkuu huwa analazimishwa kuwa busy Kiratiba na ndiyo maana wala haihitaji uwezo mkubwa wa Kumsoma na Kumjua kuwa mara nyingi tu hata body language yake huonyesha ni Mtu aliyechoka, aliyeelemewa na Ratiba za Kikazi na Mizunguko ila anashidwa tu Kumwambia Boss wake Mkuu Mheshimiwa Rais labda kwa Hofu ya Kung'olewa.

Yaani asubuhi utasikia yupo Ruangwa, mchana yupo Kisiwandui, alasiri yupo mpakani Namanga na Jioni yupo Ikulu ya huko Bunjumbura Burundi.
 
Ndio mtendaji mkuu wa serikali. Mbna hata sisi hatupumuziki mkuu

Akina Sokoine, Jaji Warioba, Mwanadiplomasia Nguli Salim Ahmed Salim, Mzee Cleopa Msuya, Sumaye, Lowassa na Pinda nao walikuwa busy hivi?
 
Mwache apate uzoefu wa kutosha .

Labda anaweza kuwa anaandaliwa kuwa Rais ajaye 2025 - 2030
 
Mwache apate uzoefu wa kutosha .

Labda anaweza kuwa anaandaliwa kuwa Rais ajaye 2025 - 2030

Uzoefu wa Mtu anayeandaliwa kuja kuwa Head of State baadae huwa unaambatana na Ratiba nyingi za Kumchosha na Kumdhoofu hata Kiafya?
 
Je, Kiafya hizi Ratiba zake kuwa nyingi nyingi huku zingine zikiwa ni za ghafla haziwezi kuwa na Athari yoyote ile Kwake
Kila mmoja anaziba shimo lake! Watakuja wengine, kama Albert Einstein alikufa na science inaendelea, sioni tatizo!
 
Uzoefu wa Mtu anayeandaliwa kuja kuwa Head of State baadae huwa unaambatana na Ratiba nyingi za Kumchosha na Kumdhoofu hata Kiafya?
Yeye mwenyewe hajalalamika . Akilalamika ratiba itarekebishwa . Mwache achape kazi .
 
PM ndiye Mtendaji mkuu wa serikali. Kwa hiyo, majukumu yake ni mengi kwa sababu ni ya kiutendaji kama ilivyo nafasi yake yenyewe.

Aidha, kuhusu ratiba ya viongozi wakuu wa nchi akiwamo PM, ni jambo linakuwa limefanyiwa kazi kwa kuzingatia mambo mengi zaidi kuliko unavyofikiri.
 
Kukaa kwenye kiyoyozi na kuongea tu jukwaan ushaona kazi sn wakati watu wapo mgodini kwa laizer hawajui jua linazama saangapi kila siku na hawajui siku watapata mbona hao huwaoni
 
Ni ngumu mtu mwingine kuamini kama kuna mtanzania wa Leo anaweza kuingia kazini saa kumi na mbili hasubuhi,akatoka saa tano usiku na bado akaonekana mvivu.
 
Back
Top Bottom