Je, Hivi ni kweli kuna baadhi ya sabuni za Unga huwa zinapausha nguo ukizitumia zaidi ya mara moja au mara kwa mara?

commm

JF-Expert Member
Sep 6, 2019
1,674
1,905
Wakuu habari za Wakati huu

Twende kwenye mada

Nilikuwa nahitaji kufahamu kama ni kweli kuna baadhi ya Sabuni za Unga unapozitumia mara kwa mara au zaidi ya mara moja huwa zinapausha Nguo?

Kama ni kweli, Je ni Kampuni ipi ambayo Sabuni zao huwa zina Ubora ambao pia hauna athari kwa mtumiaji.
 
Wakuu habari za Wakati huu

Twende kwenye mada

Nilikua nahitaji kufahamu kama ni kweli kuna baadhi ya Sabuni za Unga unapozitumia mara kwa mara au zaidi ya mara moja huwa zinapausha Nguo?

Kama ni kweli, Je ni Kampuni ipi ambayo Sabuni zao huwa zina Ubora ambao pia hauna athari kwa mtumiaji.
Nguo zinazo chuja rangi tumia sabuni ya kipande badala ya unga
 
Wakuu habari za Wakati huu

Twende kwenye mada

Nilikua nahitaji kufahamu kama ni kweli kuna baadhi ya Sabuni za Unga unapozitumia mara kwa mara au zaidi ya mara moja huwa zinapausha Nguo?

Kama ni kweli, Je ni Kampuni ipi ambayo Sabuni zao huwa zina Ubora ambao pia hauna athari kwa mtumiaji.

Epuka kuloweka nguo muda mrefu
 
Wakuu habari za Wakati huu

Twende kwenye mada

Nilikua nahitaji kufahamu kama ni kweli kuna baadhi ya Sabuni za Unga unapozitumia mara kwa mara au zaidi ya mara moja huwa zinapausha Nguo?

Kama ni kweli, Je ni Kampuni ipi ambayo Sabuni zao huwa zina Ubora ambao pia hauna athari kwa mtumiaji.
Sababu ingine, Epuka kuanika nguo muda mrefu juani, nguo ikishaanza kukauka zihamishie kivulini
 
Nguo za vitenge na zile unazozipenda Sana..unazifua kwa SABUNI ya kipande ya JAMAA... Unasuuza na maji mengi povu lisibaki kwa nguo..

Kwa SABUNI ya unga..nguo zako nzuri...huziloweki..yaani ukishafikicha povu..unafua fasta..ikiwezekana fua Moja Moja..Suuza na Kama Kuna kivuli Anika kwa kivuli

Mimi amabae sijaingia uchumi wakati .hua natumia mbinu hii kufanya nguo zangu chache nzuri zidumu
 
Sabuni za gharama ndo huwa nzuri... halafu cha ajabu zile za zamani ambazo zilikuwa za kawaaida kipindi kile eti sasahivi ndo za bei

OMO
TOSS
Na sabuni nyingine za zamani hususani za bluu
 
Zamani nlikua naangalia Matangazo mtoto kachafua nguo Mama anaweka kwenye maji ya omo.. nakutoa Ina ng'aaa..

Nikawa nafua nguo za mtoto Miaka 6..hivi..kwa omo...AISEE NILIFIKICHA nikasema Kweli Hawa wamatangazo Wana lao jambo
 
Back
Top Bottom