sabuwanka
JF-Expert Member
- Apr 11, 2015
- 690
- 751
Wanabodi, poleni na majukumu pamoja na misiba iliyowakuta wenzetu wa moshi baada ya kukanyagana wakati wakati wakikanyaga mafuta ya upako chini ya neno la unabii kutoka kwa mtumishi mwamposa mnamo 01.02.2020
Pili, naendelea kupongeza juhudi za serikali ya awamu ya tano kwa kuongeza utoaji wa mikopo kwa vijana wa elimu ya juu, sambamba na hilo serikali hii ndiyo imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kusimamia urejeshwaji wa mikopo kwa wanufaika hasa waliohitimimu kwa wingi 2009-2019, hili ni jambo la kupongeza!
Lakini pia kumekuwa na vilio kwa wanufaika walioajiriwa sekta za umma na binafsi juu ya urejeshwaji wa mkopo kwa 15% kwa mwezi toka katika bisic salary zao na tozo mbali mbali zinazoambatana na urejeshwaji wa mkopo huo,
Hivyo napenda wadau kwa ujumla tujadili zoezi hili la ukopaji, na urejeshwaji wa mkopo , je limesaidia kwa kiwango kikubwa kutokomeza umaskini ?hasa kutoa fursa kwa wengine kukopeshwa zaidi?
Mwisho kabisa natoa tahadhari kwa wanufaika wa sasa watumie mikopo kwa uangalifu maana kinachokopeshwa kwa mwezi ni sawa na mshahara utakaopata baada ya kuhitimu kwa mwezi, achilia mbali muda utakaotumika kurejesha deni hilo.
Karibuni
Pili, naendelea kupongeza juhudi za serikali ya awamu ya tano kwa kuongeza utoaji wa mikopo kwa vijana wa elimu ya juu, sambamba na hilo serikali hii ndiyo imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kusimamia urejeshwaji wa mikopo kwa wanufaika hasa waliohitimimu kwa wingi 2009-2019, hili ni jambo la kupongeza!
Lakini pia kumekuwa na vilio kwa wanufaika walioajiriwa sekta za umma na binafsi juu ya urejeshwaji wa mkopo kwa 15% kwa mwezi toka katika bisic salary zao na tozo mbali mbali zinazoambatana na urejeshwaji wa mkopo huo,
Hivyo napenda wadau kwa ujumla tujadili zoezi hili la ukopaji, na urejeshwaji wa mkopo , je limesaidia kwa kiwango kikubwa kutokomeza umaskini ?hasa kutoa fursa kwa wengine kukopeshwa zaidi?
Mwisho kabisa natoa tahadhari kwa wanufaika wa sasa watumie mikopo kwa uangalifu maana kinachokopeshwa kwa mwezi ni sawa na mshahara utakaopata baada ya kuhitimu kwa mwezi, achilia mbali muda utakaotumika kurejesha deni hilo.
Karibuni