Je,hatujengi Ukabila Kwa Kila Mtu Kwenda Kulongea Kwao?

Pezzonovante

JF-Expert Member
May 1, 2008
638
41
Ebu Oneni Picha Kwa Kubwa Japo Si Nzuri ,naona Sasa Kama Tunapelekwa Kwenye Ukabila Pole Pole Na Watu Hawa Walioishiwa Sera Na Mitaji Ya Kisiasa,ebu Angalia Lowasa Alipotemwa Akaenda Jimboni Kwake Kutushitaki,kwamba Tuna Mwaonea Yeye Ni Safi,kwanini Nasema Anatushitaki Kwani Bungeni Kuna Mwakilishi Wako Pale, So Wanaenda Jenga Chuki Dhidi Ya Makabila Na Wawakilishi Wa Mijmbo Mengine Naye 50cent Alikwenda Kwa Wanazengo(wananchi} Kwa Mantiki Hiyohiyo Na Haijapita Muda Hata Damu Za Ngombe Walio Uwawa Kule Jimboni Kwa Akina 50cent Azijakauka,oooh Bubu Naye Kaenda Kusema Kwao Lupaso Na Watu Wakawa Wanamshangilia Kwa Namana Nyingine Wako Pamoja Naye,akina Che Mwali Katika Vita Hii,je Si Kwamba Nchi Sasa Inaingizwa Kiujanja Kwenye Vinyongo Vya Umajimbo Na Ukabila .
 
Nilianzisha thread kama hii lakini yenye kichwa cha habari..."Mafisadi wakamatwe-Wasirusiwe kuligawa Taifa"
All in all ni kweli wanafanya hivyo na inaelekea ni mpango wao na Serikali ili wawagawe wananchi na hivyo kujijengea mazingira na mwonekano at least kisaikolojia kuwa wao si mafisadi.
Na pia ni mwanzo wa tahadhari kwa upinzani kuwa inawezekana wananchi hao hao wakawarudisha mafisadi madarakani!
Hilo liko wazi na ndio maana msimamo wangu toka awali kuanzia kina Ballali ni kuwa wakamatwe!
 
..at the end of the day ukweli utajulikana tu.

..sijasikia kama Mkapa,Chenge,au Lowassa, wamewataja kwa makabila yao hao wanaodai kwamba wanawasingizia.

..wananchi wa Lupaso,Monduli,Bariadi,.. wakiwa hamnazo ndipo chuki za kikabila zinaweza kuwepo.
 
Nilianzisha thread kama hii lakini yenye kichwa cha habari..."Mafisadi wakamatwe-Wasirusiwe kuligawa Taifa"
All in all ni kweli wanafanya hivyo na inaelekea ni mpango wao na Serikali ili wawagawe wananchi na hivyo kujijengea mazingira na mwonekano at least kisaikolojia kuwa wao si mafisadi.
Na pia ni mwanzo wa tahadhari kwa upinzani kuwa inawezekana wananchi hao hao wakawarudisha mafisadi madarakani!
Hilo liko wazi na ndio maana msimamo wangu toka awali kuanzia kina Ballali ni kuwa wakamatwe!
SASA WANATAKA TUWE KAMA IVORY COST MAMBO YA EAST COST NA WEST COST, BLUE CONER AND RED CONER ,COCASIAN NA CUSHIAT OOOH WAIT A MEANIET WAMECHELEWA.
 
soma hapa


HABARI MPYA KITAIFA DAR MIKOANI TAHARIRI MAKALA MICHEZO
jumatatu, 26 mei 2008

Pekua Tovuti





Gazeti la Jana
Matangazo
Bei zetu
Wasiliana nasi
Tuma habari




Zitto atuma waraka kwa JK

na Kulwa Karedia


HUKUMU ya mahakama kuruhusu watu kugombea nafasi za uongozi kama wagombea binafsi, imemsukuma Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, kuchukua hatua zaidi ili kuhakikisha Watanzania wanaifaidi haki hiyo ya kidemokrasia.

Ili kuhakikisha kuwa suala la mgombea binafsi linaingizwa katika mifumo halali wa uchaguzi na sheria za nchi, Zitto amemwandikia Rais Jakaya Kikwete pamoja na Bunge, akionyesha dhamira yake ya kutaka kuwasilisha muswada binafsi wa mabadiliko ya Katiba.

Akizungumza na gazeti hili, Zitto alisema kuwa suala la mgombea binafsi limecheleweshwa mno na anadhamiria kuhakikisha kuwa linapewa msukumo ili Watanzania wapate uhuru wa kuwania nafasi za uongozi.

Katika barua hiyo ya Mei 19 ambayo Tanzania Daima imepata nakala yake, Zitto alisema utekelezaji wa uamuzi huo utabadilisha mfumo wa uchaguzi nchini na ili utekelezeke, yanahitajika marekebisho ya Katiba ya nchi na sheria za uchaguzi.

"Kwa barua hii, natoa taarifa kuwa nina nia ya kuwasilisha bungeni muswada wa sheria za kurekebisha Katiba ya nchi na sheria za uchaguzi, hivyo naomba wataalamu wa ofisi yako waniandalie muswada huo," anasema Zitto katika barua hiyo.

Katika barua hiyo, anamkumbusha Rais Kikwete kuwa kwa mara ya kwanza alimwandikia barua Mei 31 mwaka jana, akimjulisha uamuzi wa Mahakama ya Rufaa kuhusu wagombea binafsi na umuhimu wa kubadili mfumo wa uchaguzi, lakini hakupata majibu ya msingi.

"Katika barua yangu hiyo nilishauri umuhimu wa kufanya mabadiliko makubwa katika mfumo wetu wa uchaguzi, ili kuendana na si tu hukumu ile ya Mahakama Kuu kuruhusu wagombea binafsi, bali pia kuweka mazingira ya kisiasa ambayo yanatoa fursa kwa vyama kushindana kwa mujibu wa sera zao na hivyo kuimarisha asasi hizo muhimu za kidemokrasia," alisema Zitto.

Alisema anarudia kuandika barua kwa mara ya pili baada ya serikali kushindwa rufaa iliyokata kupinga hukumu ya Mahakama Kuu iliyotoka mapema mwaka 2006.

"Narudia ushauri wangu kwa serikali kukubali kufanya mabadiliko makubwa katika mfumo wa uchaguzi, ili kukabiliana na changamoto za sasa na za baadaye za kisiasa nchini kwetu, lengo likiwa ni kuimarisha mfumo wa vyama vingi," alisema.

Alisema kama wana siasa hawatakuwa makini, maamuzi ya mahakama yanaweza kuudhoofisha mfumo wa vyama vingi nchini na demokrasia kuparaganyika kabisa.

"Hatari ninayoiona ni kuwa kuruhusu wagombea binafsi bila kuwa na mfumo unaohakikisha uimara wa mfumo wa vyama vingi, kunaweza kupeleka nchi kuongozwa na kundi dogo lisilo na udhibiti," alisema Zitto katika barua hiyo.

Alisema anaishauri serikali isipoteze muda kwa ajili ya kukata rufaa kuhusu uamuzi wa Mahakama ya Rufaa kutupilia mbali rufaa ya serikali dhidi ya kuruhusu wagombea binafsi katika nyadhifa za kisiasa.

Katika barua hiyo, Zitto amependekeza mapendekezo matano, akitaka Bunge liwe na aina zifuatazo za wabunge.

Alisema aina ya kwanza ya wabunge ni wabunge waliochaguliwa kuwakilisha mamlaka za Serikali za Mitaa.

Mamlaka hizo sasa zitatamkwa na Katiba, nazo ni halmashauri za wilaya, manispaa na miji.

"Hivi sasa nchini kuna mamlaka za serikali za mitaa zipatazo 124 kwa upande wa Tanzania Bara, hivyo hapa tunaweza kupata wabunge 124 wa kuchaguliwa moja kwa moja na wananchi, kundi hili ni dhahiri wagombea wataruhusiwa kikatiba na sheria ya uchaguzi itaweka masharti ya ushiriki wao," alisema Zitto.

Alisema kwa upande wa Zanzibar wabunge wa kuchaguliwa watokane na wilaya za kiutawala za sasa, ambapo jumla ya wabunge 10 watapatikana.

Pendekezo la tatu, ametaka wabunge wa mikoa kwa Tanzania Bara watakuwa sawa na idadi ya wabunge wanaotokana na mamlaka za halmashauri za wilaya, ambao idadi yao itakuwa 124.

"Kwa upande wa Zanzibar ili kulinda matakwa ya Katiba, idadi ya wabunge wanapaswa kutopungua 50 kama ilivyo sasa, wabunge 40 watatokana na kundi hili la wabunge wa mikoa," alisema.

Alisema mikoa itagawiwa wabunge kutokana na uwiano wa wananchi waliojindikisha kupiga kura katika mkoa husika na mgawo huo utakuwa ukirejewa kila baada ya miaka kumi.

Pendekezo la nne, Zitto alisema ni wabunge wanawake, ambao watakuwa asilimia 30 ya wabunge wanaotokana na makundi matatu ya juu kwa mujibu wa mfumo wa sasa.

Wakati pendekezo la tano, mbunge huyo kijana alisema ni wabunge watano kutoka Baraza la Wawakilishi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Spika kama si mbunge.

"Ndugu Rais kwa mapendekezo haya tunaweza kutoa uhuru kwa raia wa Tanzania mwenye sifa na bila kujali kama ni mwanachama au si mwanachama wa chama cha siasa kugombea ubunge na hata udiwani," alisema.

Alisema mapendekezo hayo yanaangalia umuhimu wa vyama vya siasa kubaki nguzo muhimu ya demokrasia nchini, kugawa viti vya ubunge kwa vyama kutokana na uwiano wa kura ambazo chama kimepata, kutafanya vyama kujimaarisha na kutoa sera bora zaidi na ushindani mkubwa.

"Kwa mapendekezo haya tutakuwa na asimilia 40 ya wabunge wote wanawake bila ya kujumlisha wabunge wanawake watakaochaguliwa kutoka katika mamlaka za serikali za mitaa moja kwa moja kama kina Gertrude Mongela, Beatrice Shelukindo, Zainab Gama na Jenista Mhagama, hivyo tunaweza kufikia asilimia 50 ya wabunge wanawake iwapo vyama vya siasa vitateua wagombea 24 tu kati ya 124 wa mamlaka zilizopo sasa na kushinda," alisema.

Alisema kwa mapendekezo hayo, Tume ya Taifa ya Uchaguzi haitakuwa na kazi ya kugawa mipaka ya majimbo tena, bali mipaka itatokana na tangazo la rais la kutangaza mamlaka za serikali za mitaa.

"Mapendekezo haya yanaondoa nafasi ya rais kuteua wabunge, na badala yake Katiba ifanyiwe marekebisho ili rais aweze kuteua baraza la mawaziri nje ya wabunge ili wadhibitishwe na Bunge," alisema.

Katika hali hiyo, Zitto alisema: "Ndugu Rais nakuomba uiagize serikali yako kuandaa mapendekezo ya mabadiliko ya mfumo wa uchaguzi na kuitisha mjadala mpana wa kitaifa kupitia asasi kama vile RIDET ili kupata maoni ya Watanzania wengi zaidi na hivyo kuboresha demokrasia," alisema.

Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salvatory Rweyemamu, alipoulizwa kama ofisi yake imepokea barua hiyo, hakukubali wala kukataa.

"Ndugu yangu sijui kama barua hiyo imefika au la, nakuomba uwasiliane na Katibu wa Bunge, anaweza kukupa maelezo zaidi kama ombi lake litakuwa limewekwa kwenye Order Paper au unaweza ‘kumkoti Zitto mwenyewe,"' alisema Rweyemamu.

Nakala ya barua hiyo imesambazwa kwa Spika wa Bunge, Samuel Sitta, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Hamad Rashid Mohamed, Waziri wa Katiba na Sheria na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa.

juu
Maoni ya Wasomaji
Maoni yanayotolewa na wasomaji wa safu hii ni ya kwao na sio maoni ya kampuni ya Freemedia Ltd. Aidha sio maoni ya mtunzi au mwandishi wa habari au makala husika hapo juu. Maoni haya hayajahakikiwa wala kuafikiwa na kampuni ya Freemedia Ltd.
Maoni 55 yameshatolewa. (Nawe toa maoni yako!)

Binafsi nakubaliana na mawazo na mbunge wetu 'yosso' Mh Kabwe, Z.Z. Nahitaji kuwasiliana nawe privately! tafadhali naomba anuani yako ya barua-pepe. Itume kupitia anuani yangu tajwa hapo juu.

na Ndugu, Dar - Tanzania, - 26.05.08 @ 08:24 | #13314

Marekebisho ya ujumbe wangu wa kwanza;
Badili neno la tano katika ujumbe huo, badala ya kusomeka 'na' isomeke 'ya'. Kisha anuani yangu ni 'lijangu08@yahoo.com'.

na Ndugu, Dar - Tanzania, - 26.05.08 @ 08:32 | #13319

Maoni yako Zitto ni mazuri sana lakini sasa kuna wasi wasi wa Nchi maskini kuwa na wabunge wengine namna hii .Nadhani kuwe na mabadiliko lakini sasa Nchi inaweza kupata mzigo wa kuwa na wabumge 400 ambao hatuna sababu hata moja ya kuwa nao .

Rais akumbuke kwamba hatutaki wabunge wa kuteuliwa akina Meghji .Kila mmoja apitie katika ballot box .Wabunge wa Rais pia hawana haja .

Tuwe na wagombea binafsi na wa Vyama watu wapate uhuru wa kuamua na mabadiliko ya Katiba haya ndiyo muhimu kabisa kabisa .

na Chifu Ihunyo, Tanzania, - 26.05.08 @ 08:36 | #13320

Mabadilike ya katiba ndio msingi wa kuimarisha mfumo mzima wa Demokrasia wa mfumo wa kiuchaguzi wa mfumo wa vyama vingi pamoja na wagombea binafsi,huu mfumo wa sasa ni wa danganya toto ndo maana hata chaguzi nyingi zilizopita vyama vya upinzani vinashindwa kutokana na hali ya kikatiba iliyopo.Zitto vilevile kumbuka kupigania kuundwa kwa Tume Huru ya Uchaguzi ambayohaitakuwa na maslahi yeyote na Chama chechote,tofauti na ilivyo sasa Tume ya uchaguzi ni mali ya ccm,Zitto liangaliye sana hilo kwani ndo utakuwa mwanzo wa uimarishaji wa Demokrasi ya mifumo yote ya upatikanaji wa viongozi wa kisiasa katika nchi yetu ya Tanzania.

na Israel J.Mwakapembati, Tanzania, - 26.05.08 @ 09:15 | #13324

Maoni ya Zito ni mazuri sana sana sana. Namuona kama mtu wa kwanza kuongelea hoja ya ugombea binafsi kwa faida zake na madhara yake, nhivyo kutoa mwlwkwo wa hekima sahihi inayotakiwa katika kuruhusu ugombea binafsi kuepuka hatari ya kundi dogo lisilodhibitika kutawala nchi. Marafiki wachache wenye nguvu ya fedha wanaweza kujiamualia mambo na kujikita madarakani.

Maoni ya zito ni muhimu sana kuzingatiwa. Hata hivyo nimshauri zito kupunguza ukubwa wa bunge kwenye pendekezo lake, kadiri ya umasikini wa nchi.

na Bernard Mukasa, Sumbawanga, - 26.05.08 @ 09:30 | #13326

Mabadiliko ni lazima,tutumie fursa hii kufanya mambo kwa uwazi zaidi, na Mungu atatusaidia kama tunanuia kutenda haki kwa watu kinyume na hapo taifa litazidi kulia na kunungunika kila kukicha.

Vyama vimetupumbaza muda mrefu kwa ukiritimba wa kuogopa kuhoji wakubwa wa vyama hivyo, nafasi sasa iko wazi.
hongera zitto watanzania tujifunze kwa ndugu huyu.

na Focus Laurent, Bunda, - 26.05.08 @ 09:33 | #13327

Safi sana Zito. Wewe unafikiria kwanza kabla ya kuongea. Siyo kama wachangiaji wengine waliochangia ugombea binafsi waliobaki na kelele zisizo na hoja oooh CCM inaogopa itameguka, oohh aijui nini.

Wote jifunzeni toka kwa zito.

na mviziaji, Bongo, - 26.05.08 @ 09:33 | #13328

Hivi ninyi mnaomsifia Zitto amefanya nini? Tangu wananchi wanapiga kelele, REDET pia imewaambia nendeni vijijini ameshatembelea vijijiji vingapi na amefungua matawi mangapi? Si wapinzai wanamangamanga tu Dar es Salaam. Mara sijui US. Hivi hamjifunzi ya KITETO? Mkaenda kama watalii, wananchi hawajawafahamu vizuri, JAMANI TUTASEMA MARA NGAPI AKINA ZITTO MUELEWI. Lazima muwe strategic, hebu angalia Obam alivyopanga mikakati yake. Hamna dira ninyi wapinzani. Jukwaani na vyombo vya habari ndio mtaongeza wanacha.

Mnauza sura tu na majina kwenye vyombo vya habari. Mbona hamtupatii vijiji vingapi mmetembelea Tanzania yote na mawawi mangapi mmefungua. Hizi ndizo habari tunazotaka kusikia, kwamba mnafahamika vijijini kwenye wapiga kura wengi.

Mnabaki tu kubadilishana kwenye Tv na Magazeti, mara Mbowe, halafu Zitto, halafu Slaa, halafu Limpumba. Afadhali hata Mrema anaonekana anajua analofanya. Sasa hivi anaenda vijijini, akina Zitto kuuza sura kwenye magazeti na Tv, hamfiki mbali, katiba mmefikiwa wapi mliyosema mtashughlika nayo. Zibeni tu masikio, wekeni pamba, mtayapata mengi ya Kiteto msipoenda vijijini kuanzia sasa.

na ki, mn, - 26.05.08 @ 09:45 | #13333

Zitto nakupongeza na ninaunga mkono sula la kubadili katiba, hii ndiyo kero ya nchi yetu, ni kuweka viraka katika katibia mpaka inachakaa. Pia suala la mgombea binafsi, kulikataa ni kuwanyima watu uhuru. Serikali inajihami nini? Si ni nchi ya Demokrais, sasa CCM na serikali wanaogopa nini? Ndugu yangu, Zitto naomba tuwasiliane kwa email yangu hapo juu kwa tafakari zaidi juu ya nchi yetu tajiri lakini watu wake maskini. Inahitaji kukombolewa tena. Watanzania wenye mapenzi mema , hizi ndizo hoja za kuunga mkono za kizalendo kweli kweli, si za kifisadi za wizi wa mali ya umma.Jerusalem 26/5/08

na Fr. mapunda Baptiste, Israel - Jerusalem, - 26.05.08 @ 09:49 | #13335

Zitto ni mtu makini sana! Hata sasa hivi yuko kwenye Jimbo lake, anatembelea vijiji. Lakini pia ni lazima awe Dar, Tanzania iko Dar! Bila kuweka sawa mambo ya Dar, ni vigumu kuyaweza ya vijijini.

Padri Baptiste Mapunda, na mini naomba kuwasiliana na wewe. E-mail yangu: pkarugendo@yahoo.com

na karugendo, Tanzania, - 26.05.08 @ 10:29 | #13341

It's obvious that a dumb man will have no verbal say on this!!!

na bubu - 26.05.08 @ 10:32 | #13343

HV WE UNAEJIITA KI MN UNA AKILI AU UMEJAZA MAJI2 HUKO KICHWANI? WE UNAWATETEA HAO CCM WAMEKUSAIDIA NINI TANGU UMEZALIWA? WA2 2NAJITAHIDI KUPINGA VTA UFISADI KILA SIKU WE UNAWATETEA CCM KAMA UMEKOSA KI2 CHA KUSEMA ACHA KUTOA MAONI YA KIPUUZI KIAC HICHO ******* WEWE.

na MDERE, TZ-ATOWN, - 26.05.08 @ 11:06 | #13347

HV WE UNAEJIITA KI MN UNA AKILI AU UMEJAZA MAJI2 HUKO KICHWANI? WE UNAWATETEA HAO CCM WAMEKUSAIDIA NINI TANGU UMEZALIWA? WA2 2NAJITAHIDI KUPINGA VTA UFISADI KILA SIKU WE UNAWATETEA CCM KAMA UMEKOSA KI2 CHA KUSEMA ACHA KUTOA MAONI YA KIPUUZI KIAC HICHO ****** WEWE.

na MDERE, TZ-ATOWN, - 26.05.08 @ 11:10 | #13348

HV WE UNAEJIITA KI MN UNA AKILI AU UMEJAZA MAJI2 HUKO KICHWANI? WE UNAWATETEA HAO CCM WAMEKUSAIDIA NINI TANGU UMEZALIWA? WA2 2NAJITAHIDI KUPINGA VTA UFISADI KILA SIKU WE UNAWATETEA CCM KAMA UMEKOSA KI2 CHA KUSEMA ACHA KUTOA MAONI YA KIPUUZI KIAC HICHO ****** WEWE.

na MDERE, TZ-ATOWN, - 26.05.08 @ 11:10 | #13349

MAWAZO YA MBUNGE CHIPUKIZI NI MAZURI.
UNAJUA UNAPOKUWA KIJANA WAWEZA KUWA NA NDOTO NYINGI YA KUFANYA MAMBO MENGI SABABU UNAJISIKIA UNA NGUVU.
WATANZANIA LAZIMA TUWE "REALISTIC."
BILA KUWA REALISTIC TUTAKUWA TUNALAZIMISHA MAMBO AMBAYO HAYATATUSAIDIA KULETA MAENDELEO.
MBUNGE ZITTO BADO ANASISITIZA UGOMBEA WA MTU BINAFSI. KUHUSU SWALA HILI TUNAPASWA KUPIMA NA KUELEZA FAIDA NA HASARA ZAKE NA KUJUA FAIDA NI KUBWA ZAIDI AU HASARA NI KUBWA ZAIDI: NA HASA UKIZINGATIA UCHUMI, MUDA WA KUFANYA KAZI WA WANANCHI N.K.
INGAWA KUWA NA MGOMBEA BINAFSI NI HAKI YA MSINGI KWA RAIA, KWA UPANDE WANGU NAONA WATANZANIA KUWA NA SUBIRA. MGOMBEA BINAFSI ATAKUWA WA MAANA WAKATI ASILIMIA KUBWA YA WATANZANIA WATAJUA ELIMU YA URAIA NA SI KUFUATA MKUMBO.
-HALAFU TUSISAHAU KUPIMA MAENDELEO YA VYAMA VYETU VYA UPINZANI: VINAKUA AU VINADUMAA.
KITU CHA MAANA CHA VIONGOZI WA UPINZANI WANACHOPASWA KUKAZANIA NI NAMNA GANI KUJENGA NA KUIMARISHA VYAMA VYA UPINZANI: VIKUE KAMA CCM, KUJITEGEMEA KIUCHUMI.
VYAMA VYA UPINZANI CHADEMA AU NCCR MAGEUZI: KIMOJAWAPO KINGELISHINDA UCHAGUZI NA KUTAKIWA KUUNDA SERIKALI WAKATI HUU, LABDA NCHI INGELIONGOZWA NA VIONGOZI MBUMBUMBU WASIOJUA SIASA. MFANO UKITAJA CHADEMA: WATU WANA MAWAZO YA MBOWE, ZITTO, SLAA. SASA WAAMBIE WAUNDE BARAZA LA MAWAZIRI. CHAMA HIKI KILISHA MWOMBA MTANZANIA FULANI ETI KWA KUWA AMESOMA, LAKINI HANA WAZO LA SIASA AGOMBEE UBUNGE HUKO MOSHI VIJIJINI.
KWA MANTIKI HIYO KABWE, DEMOKRASIA HAITAJENGWA KWA IDADI YA WABUNGE, KWANZA TUOMBE RUZUKU HATA NCHI ZA NJE KUIMARISHA VYAMA NA HASA MASHAMBANI AU VIJIJINI AMBAKO HAWAJUI ELIMU YA URAIA.
KUHUSU ASILIMIA YA WABUNGE AKINA MAMA: MIMI NAONA VIONGOZI WENGINE WANATUMIA AKINA MAMA KAMA KAMPEINI. TUKUMBUKE KWAMBA AKINA MAMA WATAINULIWA KWANZA KWA KUPEWA ELIMU YA KUTOSHA NA KUJUA HAKI ZAO. HAINA MAANA KUMPELEKA MAMA BUNGENI AMBAYE HAJUI HATA WAJIBU WA BUNGE NI NINI.
-JUA NINYI WABUNGE MNATUMIA FEDHA NYINGI KULIKO HATA WASOMI WANAOHANGAIKA MUDA WOTE. SASA KUONGEZA IDADI YA WABUNGE NI KUNYONYA WANANCHI.
TUSISAHAU PIA KUKUA KWA SIASA KUNAENDA SAMBAMBA NA KUKUA KWA UCHUMI.
TANZANIA INATAKA KUJENGA MFUMO WA SIASA AMBAO UTAKUWA NA BAJETI KUBWA KULIKO MAMBO MENGINE YA MAENDELEO.
BE REALISTIC: WAKATI MWINGINE TUNAWEZA KUSOMA SANA TUKABAKI NA NADHARIA TU KICHWANI!!!!!!

na Madaha - 26.05.08 @ 11:32 | #13351

Mdere hujui unachobwabwaja, acha wenye akili ya kuchambua wakufahamishe ujumbe niliokusudia. Tukiwa na watu kama wewe Mdere nchi haiendelei, unadhani kutoa sifa ndio kusaidia. Kwa taarifa yako hujui usemalo, kama huamini mwite mtu alieenda shule ukatafsirie ujumbe wangu.

Ninataka akina Zitto wafanye kazi, sio wauze sura. Unadhani bila kwenda vijijini watapata kura. Unaijua Mdere ripoti ya REDET. Haya niambie inamaana gani halafu inaambie wapinzani wametumia uelewa wake vipi. Mdere hujakua kiakili bado. Hujui ninachoongea. Kura nyingi ziko vijijini. Na nitaendelea kuwazomea wapinzani kama hawatupi ripoti wametembelea vijiji vingapi na wamepata wanachama wangapi. Unajua ya Kiteto wewe Mdere? Wewe msahaulifu kama panzi una kichwa cha panzi. Mwite Zitto akusaidie kusoma hapa, yeye ataelewa ninachosema.

na ki, mn, - 26.05.08 @ 11:35 | #13353

hivi mijitu mingine sijui ina akili au tope haya we unaeiponda CCM hivyo vyama vingine vimekufanyia nini.
huu nimtindio au kwani kila analosema zitto ni la maana mnataka kuiingiza nchi hii ktk matatizo halafu mtakaokuwa wa kwanza kuwageuka ni nyie mnaotoa maoni[****].

na kaka, tz[udsm]dsm, - 26.05.08 @ 11:44 | #13356

Ni kweli kina Mdere ndiyo wanaorudisha nchi nyuma. Kila siku CCM wimbo ni huo huo. Hoja ya wagombea binafsi ni hoja ya wanasiasa. Wanatafuta namna ya kugawana jinsi ya kuingia bungeni na Ikulu. Lakini hoja ya Ki ni kwamba wananchi wa kawaida wanafaidika vipi na wagombea binafsi. Tunajua Zitto katumwa na Mengi. Ni hao hao wanataka tu kuingia bungeni. Hivi bunge la watu 300 linaongeza tija yoyote kwa Watanzania? Let us be realistic. Watu kama akina Mdere wanapandia tu hoja. Hapa siyo siasa bali faida na manufaa ya wananchi. Ufisadi upigwe vita, na wanaoupiga vita wapo CCM na wengine nje ya CCM. Ni ujinga kusema waliomo CCM hawapigi vita ufisadi, ni kukosa akili.

na mwandamizi, Dar, - 26.05.08 @ 11:53 | #13357

Umelonga Mhe.Kabwe. Ni kama umeotea. Umejuwa nyakati na majira. Ni kweli, wakati sasa umefika wa kuwa wawazi. kama sisi waTz tungekuwa tunajali nchi bila kuegemea upande wowote, ulikuwa ni wakati wakusikiliza sauti hii ya Mhe Zitto. Bwana huyu ametembe nje ya nchi ameona tayari mifumo ya nchi zingine zinavyoendeshwa kikatiba na ameona yalivyo na mapungufu katiba ya nchi yetu. Mambo yanabadilika kadri siku zinavyosonga mbele. Haturudi nyuma. Mifumo mingine sasa imepitwa na wakati. Mifumo ya Mbungu kuwa ndiye pia Waziri. Mtunga sheria na Mtendaji kwa wakati mmoja. Ajira mbili kwa wakati mmoja. Kweli busara nayo pia inadai ya Mhe. Zitto kusikilizwa kwa manufaa ya wengi. Isichukuliwe eti yamependekezwa na mpizani, bali ichukuliwe kuwa pendekezo la Mtanzania wa kizazi kipya. Ushauri ni ushauri unaweza kutoa hata kwa adui ukausikliza na kuutendea kazi. Ya EPA si yametusaidia????? mbona yametoa upinzani.

na Msafiri Muelewa, Mwanza, - 26.05.08 @ 12:11 | #13361

Maoni ya Mh. Zitto Kabwe ni mazuri na hasa la kurekebisha katiba na kanuni za tume ya uchaguzi ili ziendane na mabadiliko ya katiba yatakayofanyika. Ni ukweli usio pingika kwamba Tanzania tunahitaji tume huru ya uchaguzi isiyo egemea upande wowote tofauti na ilivyo sasa kwa tume zetu za uchaguzi Tz bara na visiwani. Lakini suala la ukubwa wa bunge kiasi kile siliafiki, ni bora pesa hiyo itumike katika kuwekeza kwenye rasilimali watu ( elimu, hospitali na miundombinu) kuliko kulipa wabunge wapatao 400 ilihali waliopo wanatosha.

na Peres Joshua, Dar es salaam, - 26.05.08 @ 12:11 | #13363

Ndugu Madaha,
Kwa bahati mbaya wengi wetu tunaona mabaya ya "chukua chako mapema", lakini bado tunawapigia kura kwa sababu ya pilau, tshirt au kipannde kimoja cha kanga yenye sura zao.
Pamoja na kuwaeleza waende vijijini hata nawe ndugu yangu kama unaona watawala hatutendei haki, sote kwa pamoja tutafute solution siyo kuwaachia akina Zitto tu.

na mabula - 26.05.08 @ 12:31 | #13370

Ndugu zangu watoa maoni, hususan Ki MN, Mdere,Madaha, mbona sioni hoja zenu? Mbona sioni mapendekezo yenu. Mlingoja Zitto atoe mapendekezo yake muanze kumlima vijembe. Hapa hapatakiwi ushabiki wa vyama. Hoja hii ni ya msingi wala haihitaji vijembe bali kutoa maoni kwa sababu tayari mjadala uko wazi. Toa mapendekezo yako.

Kumbukeni kwamba wakati wa ukomnbozi ni sasa kama asemavyo Mtikila. Hili la Zitto kamalingetoka kwa Rais, nini ungekuwa msimamo wenu? Pendekezo limetolewa, kama lina kasoro au mapungufu, sahihisheni na tuiunge mkono hoja hiyo na kuishinikiza mamlaka husika kuipeleka Bungeni ijadiliwe. Lakini ukweli utabaki palepale, wakati umefika Katiba yetu uzungumziwe na ikiwezekana ibadilishwe ili iendane na zama hizi za demokrasia shirikishi na utawala bora. Namuomba Rais asijali inakotoka pendekezo hili ila ajiri unyeti wa wakati na pendekezo lenyewe. Tuachanena U-ccm, U-chadema, u-cuf. Vyote hivi ni vyama na viongozi wake ni waTz wenye uwezo wa kuogoza nchi. Kama katoto kama Joseph Kabila kanasimamia linchi kama DRC, sembuse na watu wazima waliobobea kielimu na kisiasa kama Profesa Lipumba, Profesa Sengondo, Mchumi Kabwe Zitto, Dr Slaa, wanasheria machachari kama Lisu, Marando na wengine. Mnapende ili uweze kuongoza lazima uwe ccm? tukifikiri hivyo tutakuwa tumechelewa. Angalia mwanasiasa chipukizi Obama wa Marekani anavyowahenyesha wanasiasa waliobobea?

Ndugu zangu, kumbukeni hakuna shule au darasa wanakofundisha ma Waziri au Marais. Hizi ni nafasi za uongozi ambazo zinahitaji hekima na busara tu.

na Sultan Mosi, Pemba, - 26.05.08 @ 12:47 | #13373

Ha ha ha, Naanza kwa kicheko, unayejiita kaka na mwandamizi msidhani kuwa ninamapenzi na chama mie siangalii sura, unadhani maelezo yangu dhidi ya Mdere ni kuitetea CCM, kumbe hata ninyi hamjanielewa, mmechemsha.

Sasa ni hivi mie napenda demokrasia. Ujumbe niliokusudia ni mzuri sana kwa Zitto na Kambi ya upinzani, maneno niliyotumia kuwa wanauza sura siyo kwenye TV na magazeti sio kuwa nawachukia. Nilikuwa nawapa changamoto wahakikishe wanaenda vijijini kueneza demokrasia. Kwa hiyo unayejiita kaka na mwandamizi mmenoa, nanyi mlihitaji mtu awatafsirie ujumbe niliokusudia. Mdere umenipata sasa ujumbe wangu? inahitaji shule kidogo.

Haya sasa ngoja niseme hivi, Waheshimiwa Zitto, Slaa, Mbowe, Lipumba n.k, nawaambia hivi mwende vijijini kueneza demokrasia, wananchi wawafahamu vizuri. Tumieni ripoti ya REDET kufanya kazi, kura nyingi ziko vijijini. Tunataka kwenye majukwaa mtuambie pia mmetembelea vijiji vingapi na mmepata wanachama wangapi. You are over doing it opposition parties by staying in towns, a lot of votes are in rural areas, go there now. You have also to learn a lesson from Kiteto election, stay in villages, you get me Zitto and your colleagues? Bahati mbaya sijui kulugha chenu ningewaambia labda mngenielewa. Zitto come out on this arena and respond on my challenges

na ki, mn, - 26.05.08 @ 12:56 | #13377

WE KI MN NAONA 2KUTAFUTIE MKOA UENDE UKAWADANGANYE MADUNGAYEMBE WENZAKO WANAOSIFIA CCM TANGU UHURU WAKATI UNAKULA MLO M1 KWA CKU BARABARA HAINA LAMI TANGU NCHI IMMEKUA HURU BUT UNACHANGIA KODI DAILY UNAPOENDA KUNUNUA BIDHAA YOYOTE DUKANI AU HUJUI MAANA YA VAT(VALUE ADDED TAX) KWANZA UNAONEKANA HUFUATILII VYOMBO VYA HABARI HUJUI YALIYOTOKEA CHUO HV MAJUZI NENDA KAMUULIZE MUKANDALA MAANA NI BOGA MWENZAKO YANI WE UNGEKUWEPO CHUO 2NGEKUITA SHOGA AU 2NGEKUCHOMA MOTO HAPA MABIBO WE HUTAKI MABADILIKO UNAKUA CONSERVATIVE DAILY UNACHOLINDA NINI SASA?PONGO KWELI WEWE FANYA BADILIKO FASTA KM WENZAKO WA KENYA UKIWAONA NAO WA KINA ZITO WANABORONGA WATOE NAO WARUDISHE CCM SASA KAMA HA2WAPI NAFASI TUTAJUAJE KAMA NI WABAYA KICHWA CHAKO KAMA CHA KARUNGUYEYE WEWE.BE DYNAMIC ALWAYS

na MDERE, UDSM.B.COM, - 26.05.08 @ 13:00 | #13379

Pole sana Mdere, kumbe unasoma B com, mwombe anayesoma sanaa akusaidia Mdere. Ingekuwa mtoto ningekwambia hujajua kujisafisha ukitoka kujisaidia. Samahani wasomaji, ninamlazimisha Mdere aelewe hoja yangu, naomba umpe nafasi Zitto aje kujibu hoja yangu.

Inaonekana hiyo B. COM inakuharibu unafikri katika mstari uliyonyooka.
Kwa ufipi ni Zitto na wapinzani lazima waende vijijini, watake wasitake ili kupata wanachama na kufundisha demokrasia. Jamani Mdere hii inahitaji digrii kuelewa, usiaibishe kisomo cha UDSM Bwana. Zitto msaidie huyu kijana hanielewi kabisa

na ki, mn, - 26.05.08 @ 13:14 | #13383

We, Mdere na ki,mn mnagombania nini? Zitto ni mwanaume, sielewi kwa upande wenu, kama huridhii hoja ya mwenzio basi kaa kimya manake naye amechangia kwa upeo wake. Mume mmoja wake wengi hiyo inakubalika. Nawe Zitto watimizie haja yao walioko jirani yako kama jinsia ni tofauti. Zitto upo? Mi sikupendi.

na Kisima, Mza-Tz, - 26.05.08 @ 13:32 | #13387

we wewe unayejiita kaka hujui usemalo nafikiri ni mmojawapo wa watoto wa mafisadi unaona ccm ndo baba na mama,lakini hufikirii hii nchi inavyoliwa,nchi itaingiaje kwenye matata wakati ndo wigo wa demokrasia unapanuka?wazazi wako wakiishakudanganya ya kuwa vyama vingi vinaleta machafuko na wewe mbichwa unavimba bila ya uchambuzi makini,shauri yako.

na john, Tz, - 26.05.08 @ 13:33 | #13388

WANASOMA SIASA KAWATAFUTE WEWE UWAELIMISHE ILI WATAKAPOMALIZA HIZO DEGREE ZAO WAKAWAELIMISHE NDUGU ZAO HUKO VIJIJINI WAPATE MAENDELEO.SAWA CKATAI KUA WAPINZANI LAZIMA WAENDE RURAL AREAS LAKINI KAMA2 WEWE UPO MJINI UMEPATA ELIMU KIDOGO KWA IMANI HUTAKI MABADILIKO UNADHANI HAO WA VIJIJINI WATAWEZA KUBADILIKA,EMBU KUA MWANA MAGEUZI BWANA WATANZANIA WENZETU KULE VIJIJINI WAPATE MAENDELEO WAJIONE KAMA NAO WAPO DUNIANI NA WAIFURAHIE TANZANIA YAO.JUA KWAMBA HK MJINI 2LIPO HAKUNA SHIDA,SHIDA ZIPO VIJIJNI EEE BWANA BADILIKA.NADHANI UMENIPATA NA UMENIELEWA.SHWAAAAAAAAARI

na MDERE, UDSM .B.COM, - 26.05.08 @ 13:36 | #13389

nampongeza sana mh.Zitto kwa kazi nzuri anayofanya ya kutetea wananchi wote kama alivyotumwa kikamilifu. wazo la kuwasilishwa mswada huo pamoja na marekebisho ya sheria za uchaguzi ni mzuri na nitaomba wananchi wote wamuunge mkono ili demokrsia iweze kushamiri vizuri zaidi hapa nchini. Mungu akulinde na akuongoze vema zaidi Zitto na wote wenye mapenzi mema na nchi yetu, hasa Dr.Slaa.

na Pris, Dodoma/tanzania, - 26.05.08 @ 13:44 | #13391

nampongeza sana mh.Zitto kwa kazi nzuri anayofanya ya kutetea wananchi wote kama alivyotumwa kikamilifu. wazo la kuwasilishwa mswada huo pamoja na marekebisho ya sheria za uchaguzi ni mzuri na nitaomba wananchi wote wamuunge mkono ili demokrsia iweze kushamiri vizuri zaidi hapa nchini. Mungu akulinde na akuongoze vema zaidi Zitto na wote wenye mapenzi mema na nchi yetu, hasa Dr.Slaa.

na Pris, Dodoma/tanzania, - 26.05.08 @ 13:44 | #13392

Wewe kisima hapa tunaongelea maslahi ya nchi. Wapinzani waende vijijini kupata wanachama, wewe unaleta vitu vya ajabu.

Wewe Kisima Na. #13387 afadhari umejisema mwenyewe unapakuliwa na wanaume ndio maana ya jina lako. Ningekuwa kijana mdogo ningekutukana ningekwambia jina lako ni kisima, kwenye a ya kisima nikaondoa naweka i, hili ndilo jina lako. Na ndio unaishi kwa jina lako hilo. Hapa tunatoa hoja wewe unatukana? Moderator umemwona huyo mwenye jina lenye mwelekeo wa jinsia ya kike?. Si unaona jina lake limekaa kihasara hasara?

Ho

na ki, tu, - 26.05.08 @ 13:47 | #13393

Wewe kisima hapa tunaongelea maslahi ya nchi. Wapinzani waende vijijini kupata wanachama, wewe unaleta vitu vya ajabu.

Wewe Kisima Na. #13387 afadhari umejisema mwenyewe unapakuliwa na wanaume ndio maana ya jina lako. Ningekuwa kijana mdogo ningekutukana ningekwambia jina lako ni kisima, kwenye a ya kisima nikaondoa naweka i, hili ndilo jina lako. Na ndio unaishi kwa jina lako hilo. Hapa tunatoa hoja wewe unatukana? Moderator umemwona huyo mwenye jina lenye mwelekeo wa jinsia ya kike?. Si unaona jina lake limekaa kihasara hasara?

na ki, mn, - 26.05.08 @ 13:51 | #13395

Mimi nadhani sasa umefika wakati tubadili katiba ili wabunge wawe wanaishi katika majimbo yao ya uchaguzi ili wawafanyie kazi wananchi waliowachagua badala ya sasa hivi. Tatitizo letu wananchi ni usimamizi mbaya wa pesa za maendeleo, matumizi mabaya ya madaraka kwa wafanyakazi wa serikali na kukosekana uhamasishaji wa kutosha ili kuleta maendeleo kulingana na rasilimali zilizopo eneo husika. Kwa kuwa wabunge tumewaajiri kwa kazi ya kuhakikisha maendeleo ya wananchi yanapatikana kwa kufanya yote niliyoeleza hapo juu na siyo kwenda ******* na kupiga miayo tu bungeni, nadhani sasa umefika wakati wa kuwalizimisha kuwepo kwenye vituo vyao vya kazi (majimboni) muda wote.Hivi inakuwaje muajiriwa anamua lini aende ofisini na akafanye nini kwa muuajiri wake (wananchi), hivi ni wapi mmeona mtu analipwa pesa nyingi kama za ubunge halafu afanye kazi kama wanavyofanya wabunge kupitia magazeti, redio na TV? mfano mzuri mmeona wakati wafanyakazi wanadai nyongeza ya mishahara mipya (80,000)kwani baadhi ya waajiri waliongeza muda wa kufanya kazi ili kuleta tija. Hawa jamaa wanafanan, wawe upinzani au watawala mara nyingi wanajali maslahi yao binafsi, vyama vyao na kuwasahau wananchi. Ni kweli katiba ibadilishwe baadhi ya maeneo ili kuleta mageuzi katika shughuli za wabunge na siyo kujaza watu ambao kwangu mimi naona hawana faida yeyote.Ubunge ni kazi inayolipa sana kuliko hata uhadhiri chuo kikuu hivyo wananchi pia tupime kazi wanazofanya wabunge ofisini kwao (majimboni) badala ya kuwashabikia kwani tumeshawashabikia sana tangu nchi ipate uhuru mtpaka leo bado hamna kasi ya maana. Nionavyo mimi ni lazima tuwape masharti wabunge wetu kama wanataka kazi na siyo kuwaachia watulishe uppuzi wao ili waendelee kubaki madarakani huku wananchi tunaatabika.

na Kibera, tanzania, - 26.05.08 @ 14:00 | #13401

Mtake msitake Zitto lazima aende vijijini ili tuwapate wenzetu wanaohongwa khanga na kofia,na kuuza kadi za kupigia kura kwa shs 2000/= tu toka kwa wakala wa ccm.Bila kuelimishwa hata Zitto aseme na afanye nini ni bure.
MSIPINGE.
Nilisha sema kila mmoja wetu awe na jukumu kuhakikisha baba yake,mama yake,kaka nk wote wasiwape kura hii mijitu mifisadi ya kutupwa.Nyinyi ndio mnaotuangusha hamna mawasiliano na ndugu zenu vijini mmewatupa toka mliposoma mkapata kazi matokeo yake wanasubiri miaka 5 ili wapate khanga,au kofia au shs 2000/=.Tunachosema wakina Slaa na Zitto sawa waende lakini pia jukumu kubwa ni la kila mmoja wetu.

INAWEZEKANA HII MIJITU KUNGOKA KAMA MHOGO WA MASIKA.PLAY YOUR PART.

na yuli, USA, - 26.05.08 @ 14:10 | #13404

Zito kaongelea ugombea binafsi Tanzania. Hjaongelea CHADEMA wala CCM. Mbona wengine mmeanza kulambania vyama? Vimeingiaje kwenye hoja hii?

na Bernard Mukasa, Sumbawanga, - 26.05.08 @ 14:17 | #13406

Sultan Mosi wa Pemba #13373 mawazo yako ni sawa lakini umemalizia vibaya. Hakuna shule ya urais wala uwaziri, lakini elimu ni muhimu ikifuatana na hekima na busara. Obama kasomea sheria Harvard. Wenzake waliodharau elimu, nusu wako jela kwa wizi na uhalifu. Tuchague viongozi wenye elimu nzuri pamoja na hekima na busara.

na J. Bendera., Hamburg, Germany., - 26.05.08 @ 14:18 | #13407

Sasa wale ambao walikuwa hawanielewi angalieni wenye akili zao zimetulia na kuchambua mambo. Bravo Kibera, Congratulation Yuli. Ninyi vichwa. Wengine kusema bila concentration na kuelewa. Ukweli ni kwamba hata kama bado katiba itakuwa haijaweka vizuri, tunapopambana na wanyonyaji katika nchi lazima tuwalazimishe wapinzani waende vijijini. Tuwazomee wasipoenda vijijini.

Anayetoka kijijini kutupatia taarifa amevuna wanachama wangapi ndiye tumpigie makofi. Ukweli ni kwamba hatutaki ya Kiteto yarudie, wakati ni sasa wapinzani waende vijijini, wasiranderande mijini, kura ni vijijiji.

Hongera tena yuli wa USA na Kibera kwa kunielewa. Zitto na wenzeke, kiguu na njia kijijini kuelimisha demokrasia na kuvuna wanachama, hamna chaguo. Sisi wana demokrasia hatutawapigia makofi mijini, labda mnapoleta taarifa za vijiji mlivyotembelea na kutuambia bado vingapi na mmepata wanachama wangapi

na ki, mn, - 26.05.08 @ 14:23 | #13408

Mimi naona badala ya kujadili ccm,Chadema na kumsifu Kabwe tukae na kujadili nini faida na hasara ya wagomnea binafsi.

Kabwe Zitto yaonekana ktk barua yake yeye ameeleza ktk mazingira kuwa inatoa uhuru na haki kwa baadhi ya Watanzania kugombea.

Lakini mimi naona iko hasara na faida zaidi ya hili lililoelezwa na kabwe na yeye hajabainisha hasara zake.

Wadau naomba tuchangie.

na Joram Kiango, DSM/Tanzania, - 26.05.08 @ 14:26 | #13410

Huku usukumani tuna msemo usemao,KUSIKIA KWA ***** HADI DAMU ITOKE MASIKIONI.Sasa Watanzania ni kama ***** hawasikii hadiCCM ianze kukamata watu na ku-wauza nje ndo watajua hili li chama halina nia ya kutupatia maisha bora. Jukumu la kuelimisha watu wa vijijini sio la vyama vya upinzani ni la serikali,itoe elimu ya uraia.Leo hii huko vijijini kuna watu bado wanajua rais ni Nyerere.

na kakaa, mwanza, - 26.05.08 @ 15:03 | #13412

Natoa changamoto (Public Lecture ya bure bila malipo) kwa vyombo vya habari vya Tz, viwe kila siku vinatoa majina ya viongozi wote wa siasa hasa wale wa ngazi za juu kila siku wako wapi na wanafanya nini. Mwisho wa mwezi wanatoa analysis akina nani walienda vijijini nani hawakwenda. Nashangaa hawa wabunifu wa jamii forum hawajagundua njia hii ya kulazimisha wapinzani waende vijijini kufundisha demokrasia.

Sasa mimi leo nawapa Lecture waandishi wote wa habari wa Tz, pamoja na Jamii forum. Kuanzia wiki kesho nitaangalia walioelewa somo langu. Yaani andaeni scheme (a table)ya viongozi wakuu wa vyama vya upinzani - Mwenyekiti, Makatibu, Waenezi, n.k. Inaonesha jina, chama, wadhifa, yupi wapi, amefanya nini kila siku. Mwisho wa mwezi au kila baada ya wiki mbili tunaona akina nani walienda vijijini kufundisha demokrasia na akina nani walikuwa wanarandaranda mijini. Walioenda vijijini wakirudi kutupa taarifa - wamepta wanachama wangapi tunawapongeza. Wale ambao wanarandaranda na kuuza sura tunawazomea ili nao wafanye vizuri. Mmenielewa wanafunzi wangu, jamii forum na waandishi wote wa habari mpo? Aliye nielewa ajitokeze asemi sisi hapa tutatekelza mpo. Wengine tumekosa tu nafasi za kuongoza lakini we kichwa moto- Ona darasa hilo na uone watakavyochapa kazi.


Rafiki Joram Kiango unataka kusema wagombea binafsi watapokea pesa za shetani. Of course inawezekana, lakini inawekwa tu misingi- kwamba source za kugombea zinakuwa zinachangwa kama wanavyochangiwa akina Obama.

Wagombea binafsi watalazimisha vyama kuchagua watu watakatifu, wasio mafisadi. Hata wagombea wa vyama bado wananunuliwa na wafanya biashara hasa waasia. Halafu wanawatumia kama remote, wao kutenda maelekezo wanapata kwa wale waliowanunua. Kuanzia uchaguzi unaokuja kila chama kitoe hesabu ya pesa inazozitumia na iseme imezipata wapi. Vilevile kwa wagombea binafsi. Jamani hamnipigii tu makofi, au mna wivu. Mie sina unchoyo- lecture bila malipo- kwa heri.

?

na ki, mn, - 26.05.08 @ 15:06 | #13413

Pamoja na kukupongeza Mhe. Zitto kwa hatua hii nuzi, pia ni wakati muafaka serikali ikafahamu kuwa ni haki ya kila Mtanzania kugombea ili kuchaguliwa si lazima kupitia kwenye Chama chochote.

Kila la kheri.

na Hillary N. Mkony, Tanzania, - 26.05.08 @ 15:08 | #13414

WANAOAMBIWA WAKUBALI KUAMBIWA,WAO HAWAJUI KUWA HAWAJUI. LAKINI SI HIVYO NI WAJINGA.

na KINYA, ZENJI, - 26.05.08 @ 15:29 | #13416

NAKUBALIANA NA WATOA MAONI WAKISISITIZA VIONGOZI WA UPINZANI KWENDA VIJIJINI SIO KUWA "OPPORTUNISTS" KWA KASORO ZILIZOPO.
TANZANIA TUNAYO BAHATI YA KUJIFUNZA TOKA NCHI JIRANI AMBAZO VYAMA VYA UPINZANI VIMECHUKUA MADARAKA, MFANO: ZAMBIA, NA KENYA. NI NCHI PEKEE ZA KIAFRIKA AMBAZO TAYARI VYAMA VYA UPINZANI VIMESHINDA. NA TUMEONA MATOKEO YAKE? SABABU YA WANANCHI KUKOSA KUANDALIWA TANGU NGAZI ZA MASHAMBANI, MAMBO YANABAKI VILE VILE. ANAYESHINDA ANAJIKUTA ANASAIDIANA NA VIONGOZI WALE WALE WALIOKUWA NA KASHFA ZA UFISADI. MFANO: UNAAMINI KWAMBA PR. SAITOTI ALIHUSISHWA NA KASHFA TANGU UTAWALA WA MOI. HALAFU UPINZANI UKAMKUMBATIA TENA!
SAFARI NI NDEFU!!
CCM ITAENDELEA KUSHINDA. SUBIRI IWAWAJIBISHE MAFISADI HIVI KARIBUNI.

na Askari wa mwavuli - 26.05.08 @ 15:38 | #13417

Huyu Ki ni ****** kweli kweli. Mwanzoni alipokuwa anamlazimisha Mdere na Mwandamizi wakubaliane na mawazo yake nilidhani anazo, kumbe hakuna kitu ndani ya kichwa!Angalia alichoandika kwenye maoni #13413 hiyo ndiyo busara yake.Yaani watu wengine bwana, analzimisha watu wakubali upuuzi wake kwa kujaribu kuonyesha kuwa ni hoja ya msingi kumbe amejaa pumba tupu.
Huyu ki nimegundua kuwa ndiye anayeuza sura hapa kwenye mtandao.Lakini asife moyo aendelee kuwasoma wenye vichwa vilivyotulia siku moja nayeye ataweza kutoa maoni yenye akili.

na Peter Pierre, tz, - 26.05.08 @ 16:08 | #13421

We piere hujui kitu. Wenye akili wameshapata ujumbe utaona utakavyofanyiwa kazi. Maelezo mengine ilikuwa ni staili ya presentation ili msomaji asichoke kwa sababu niliandika mengi.

Kama unadhani ninaongea utani kasome jamii forum utaona wameanzisha thread, wanalalamika kuwa vyama vya upinzani ni wazembe hawaendi vijijiji. Kwa hiyo hapa nimetoa mbinu za kuwalazimisha wapinzani waende vijijini. Ninarudia kila siku orodha, Mbowe, Slaa, Lipumba, sijui Mwenezi, jina la chama, yupi wapi, anafanya nini. Wanaoleta ripoti ya kuvuna wanachama tunawapongeza. Wanaorandaranda mijiji tunawazomea hadi wakatuletee taarifa, wamavuna wanachama wangapi, na bado vijiji vingapi. Mwisho wa mwezi tunatangaza wazembe na wawajibikaji wa kufundisha Demokrasia vijijiji.

Tatizo lako piere, badala ya kusoma ujumbe umeangalia namna nilivyokuwa siwachoshi. Unakumbuka staili ya hotaba za Nyerere, utani wa kutosha kwenye hotaba watu, hawachoki. Ila usiseme najilinganisha na Nyerere ile namba Nyingine.

Jamani vyombo vya habari, jamii forum kazi kwenu. front page kila siku summary za viongozi wa upinzani, wameende vijiji gani. Ngoja nikwambie Piere, mbinu hii wataichukia viongozi wa upinzani wazembe kama walivyosema jamii forum. Ila sasa tunawasimamia kwa kuwawekea summary kila siku.

Zitto akileta akitoka Sumbawanga huko ndani akituambia nimepata wanachama 10,000. Tunasukuma gari lake. Akiuza sura mjini tunamwambia data inasema wewe mzembe katuletee kwanza wanachama. Mmesikia wanahabari, from page summary viongozi wapinzani wanafanya nini. Tuone kama hawatafanya kazi na kama wanachama hawatapta. Hatutaki ya Kiteto yarudie, huwezi kupata kura kwa kutalii wakati wa uchaguzi tu. LAZIMA wapinzani tuwafundishe namna ya kufanya kazi. Wameshindwa kufanya kazi bila kusukumwa, sasa tunawalazimisha kufanya kazi. Naomba wanahabari fanyeni hilo kuanzia wiki kesho. Kazi kwao wazembe, wataona cha moto, data kila mwezi au kila baada ya wiki mbili

na ki, tu, - 26.05.08 @ 16:43 | #13425

We piere hujui kitu. Wenye akili wameshapata ujumbe utaona utakavyofanyiwa kazi. Maelezo mengine ilikuwa ni staili ya presentation ili msomaji asichoke kwa sababu niliandika mengi.

Kama unadhani ninaongea utani kasome jamii forum utaona wameanzisha thread, wanalalamika kuwa vyama vya upinzani ni wazembe hawaendi vijijiji. Kwa hiyo hapa nimetoa mbinu za kuwalazimisha wapinzani waende vijijini. Ninarudia kila siku orodha, Mbowe, Slaa, Lipumba, sijui Mwenezi, jina la chama, yupi wapi, anafanya nini. Wanaoleta ripoti ya kuvuna wanachama tunawapongeza. Wanaorandaranda mijiji tunawazomea hadi wakatuletee taarifa, wamavuna wanachama wangapi, na bado vijiji vingapi. Mwisho wa mwezi tunatangaza wazembe na wawajibikaji wa kufundisha Demokrasia vijijiji.

Tatizo lako piere, badala ya kusoma ujumbe umeangalia namna nilivyokuwa siwachoshi. Unakumbuka staili ya hotaba za Nyerere, utani wa kutosha kwenye hotaba watu, hawachoki. Ila usiseme najilinganisha na Nyerere ile namba Nyingine.

Jamani vyombo vya habari, jamii forum kazi kwenu. front page kila siku summary za viongozi wa upinzani, wameende vijiji gani. Ngoja nikwambie Piere, mbinu hii wataichukia viongozi wa upinzani wazembe kama walivyosema jamii forum. Ila sasa tunawasimamia kwa kuwawekea summary kila siku.

Zitto akileta akitoka Sumbawanga huko ndani akituambia nimepata wanachama 10,000. Tunasukuma gari lake. Akiuza sura mjini tunamwambia data inasema wewe mzembe katuletee kwanza wanachama. Mmesikia wanahabari, from page summary viongozi wapinzani wanafanya nini. Tuone kama hawatafanya kazi na kama wanachama hawatapta. Hatutaki ya Kiteto yarudie, huwezi kupata kura kwa kutalii wakati wa uchaguzi tu. LAZIMA wapinzani tuwafundishe namna ya kufanya kazi. Wameshindwa kufanya kazi bila kusukumwa, sasa tunawalazimisha kufanya kazi. Naomba wanahabari fanyeni hilo kuanzia wiki kesho. Kazi kwao wazembe, wataona cha moto, data kila mwezi au kila baada ya wiki mbili

na ki, mn, - 26.05.08 @ 16:51 | #13426

HONGERA SANA ZITO KWA KUWA NA MAWAZO AMBAYO NI WABUNGE WACHACHE WENYE AKILI HIYO

MABADILIKO YA KATIBA NI JAMBO AMBALO KWA MTANZANIA MWENYE KUELEWA NA KUSOMA ALAMA ZANYAKATI ATAONA NI JAMBO LA BUSARA.

SASA NDUGU YANGU ZITO MOTO UMESHAUANZISHA ENDELEA NAO TAFUTA WADAU PITA MTAA HADI MTAA UKILIONGELEA HILI KAMA MLIVYOFANYA KATIKA KUWAFUNGUA WANANCHI MASWALA YA UFISADI, TUKO NYUMA YAKO.

SASA IMEFIKA WAKATI WATZD KUELEWA KUWA HATUKO TENA KATIKA UTAWALA WA CHAMA KIMOJA TUNACHOTAKA NI UKWELI NA UWAZI KATIKA SERIKALI NA SERIKALI INAYOWAJALI MASIKINI SIO SERIKALI INAYOJALI WEZI WA FEDHA NA KODI ZA WANANCHI.

WATU WALISEMA CCM NI CHAMA CHA MAJAMBAZI

WENGINE WALISEMA CCM NI CHAMA CHA MAFIA

SASA TUNAONA KUWA WAMEZAA JINA JIPYA AMBALO NI CHAMA CHA MAFISADI

HAYA SISI HATUYATAKI

TUNATAKA KUONA KILA MTANZANIA ANAFAIDI MATUNDA YA NCHI YAKE NA SI WACHACHE.

HIVI KWELI UNAMTEUA ZAKHIA MEGHI UNAMPA UWAZIRI WA FEDHA ANAHARIBU NA HATA YALE AMBAYO YALIKUWA MACHACHE MAZURI HALAFU ANAZUNGUMZA KAMA VILE CHEREKO KUTETEA UCHAFU WAKE.

KATIBA IBADILISHWE NA RAISI AWE NA UWANJA MPANA WA KUTEUA HAWA WASHAURI WAKE.

ZITO KOMAAA KAKA WEWE NI NGUZO CHANGA LAKINI KUWA MACHO NA MAFIA AU MAFISADI

NB

AMINA CHIFUPA ALIKUFA KIFO CHA UTATA

MORINGE SOKOINE NAYE ALIPITIA NJIA HIYO HIYO YA UTATA

KOLIMBA HORRACE BILA KUULIZA

BALLAL DAUDI NAYE KIFO CHAKE NI UTATA UMZITO

KOMBE JENERAL HADI SASA TUNAJUA SERIKALI INAHUSIKA KIFO CHAKE MWULIZE MREMA AGUSTINA ATAKUPA STORY

SASA ZITO NDUGU YANGU KAZA BUTI TUKO NYUMA YAKO AMSHA HAPO JUUU SIO KWAMBA NAKUTISHA HUO NDIO UANAUME.

BONGO WAKIONA UNATAKA KUSHIKA MASILAHI YAO WANAKUPA KUBWA KAMA NDUGU ZETU HAPO JUUU



na MTANZANIA HALISI, TANZANIA, - 26.05.08 @ 16:57 | #13428

HONGERA SANA ZITO KWA KUWA NA MAWAZO AMBAYO NI WABUNGE WACHACHE WENYE AKILI HIYO

MABADILIKO YA KATIBA NI JAMBO AMBALO KWA MTANZANIA MWENYE KUELEWA NA KUSOMA ALAMA ZANYAKATI ATAONA NI JAMBO LA BUSARA.

SASA NDUGU YANGU ZITO MOTO UMESHAUANZISHA ENDELEA NAO TAFUTA WADAU PITA MTAA HADI MTAA UKILIONGELEA HILI KAMA MLIVYOFANYA KATIKA KUWAFUNGUA WANANCHI MASWALA YA UFISADI, TUKO NYUMA YAKO.

SASA IMEFIKA WAKATI WATZD KUELEWA KUWA HATUKO TENA KATIKA UTAWALA WA CHAMA KIMOJA TUNACHOTAKA NI UKWELI NA UWAZI KATIKA SERIKALI NA SERIKALI INAYOWAJALI MASIKINI SIO SERIKALI INAYOJALI WEZI WA FEDHA NA KODI ZA WANANCHI.

WATU WALISEMA CCM NI CHAMA CHA MAJAMBAZI

WENGINE WALISEMA CCM NI CHAMA CHA MAFIA

SASA TUNAONA KUWA WAMEZAA JINA JIPYA AMBALO NI CHAMA CHA MAFISADI

HAYA SISI HATUYATAKI

TUNATAKA KUONA KILA MTANZANIA ANAFAIDI MATUNDA YA NCHI YAKE NA SI WACHACHE.

HIVI KWELI UNAMTEUA ZAKHIA MEGHI UNAMPA UWAZIRI WA FEDHA ANAHARIBU NA HATA YALE AMBAYO YALIKUWA MACHACHE MAZURI HALAFU ANAZUNGUMZA KAMA VILE CHEREKO KUTETEA UCHAFU WAKE.

KATIBA IBADILISHWE NA RAISI AWE NA UWANJA MPANA WA KUTEUA HAWA WASHAURI WAKE.

ZITO KOMAAA KAKA WEWE NI NGUZO CHANGA LAKINI KUWA MACHO NA MAFIA AU MAFISADI

NB

AMINA CHIFUPA ALIKUFA KIFO CHA UTATA

MORINGE SOKOINE NAYE ALIPITIA NJIA HIYO HIYO YA UTATA

KOLIMBA HORRACE BILA KUULIZA

BALLAL DAUDI NAYE KIFO CHAKE NI UTATA UMZITO

KOMBE JENERAL HADI SASA TUNAJUA SERIKALI INAHUSIKA KIFO CHAKE MWULIZE MREMA AGUSTINA ATAKUPA STORY

SASA ZITO NDUGU YANGU KAZA BUTI TUKO NYUMA YAKO AMSHA HAPO JUUU SIO KWAMBA NAKUTISHA HUO NDIO UANAUME.

BONGO WAKIONA UNATAKA KUSHIKA MASILAHI YAO WANAKUPA KUBWA KAMA NDUGU ZETU HAPO JUUU



na MTANZANIA HALISI, TANZANIA, - 26.05.08 @ 16:57 | #13429

Vijana naona sasa mnakiuka maadili ya gazeti.Mtandao unasomwa dunia nzima .Mjaribu kutueleza yaliyo ya busara.Hoja ziwekwe katika hali ya kusomeka kwa maelewano ,na si maneno ya tafsiri ya ******.Hoja ni jinsi gani vyama vinaweza kuungwa mkono na watu wengi, ili viweze kushindana na CCM.tunajua katika vyama kuna mambo mengi.Hata kikichaguliwa chama chochote ,kula ni lazima.Kwasababu Wote wanaoingia kwenye vyama ,ni watu waliyo na mawazo tofauti .Kunawanaotaka uongozi kwa faida .Na kuna wale wenye uzalendo na uchungu na nchi.Hawa kuwafahamu ni vigumu.Kuwepo mgombea binafsi ,hili i gumu.Ukweli ni kuwa tuimarishe vyama.Na viwe vichache,Wahusika waende mpaka vijijini wazungumze,Nini watawafanyia wananchi.Kisha wananchi waamue.Wagombea wafahamike,naona hili litasaidia watu kuelewa makosa ya chama tawala .Lakini uchaguzi uanapofika, eti ndio watu wanachangamka kuwaburuza watu , huyu ndiye mgombea wa chama fulani.Wananchi lazima wataona ni danganya toto.Naungana na mwandishi anaesisitiza kuwa vyama pinzani,viende vijijini vikajinadi ,wananchi wawaelewe.Kwa hivi sasa lazima watawaunga mkono.Mambo ya kuwepo vyama mjini ndiyo sababu chama tawala kinawasambaratisha wapinzani,kwakutojieleza kwa wananchi.

na mtzmwenyeuchunngu, tz, - 26.05.08 @ 17:52 | #13435

Watanzania tutaongea sana lkn ni wazi kua tunataka si mabadiliko tu ya maneno kwenye TV na magazeti bali mabadiliko kivitendo hasa vijijini.Nini cha kufanya [1]kura ya maoni i.e tuamue ni constitution ipi tunataka,kwani hii iliyopo inawapa favor kubwa CCM,kama tuonavyo ZNZ mtu akishinda hata zaidi ya kura 1 yeye ndio anaunda serikali,hata kichaa ataona kuna walakini.
[2]Tume huru ya uchaguzi inayokubalika na wote.[3]watanzania tuache uvivu,rushwa,kuombaomba mpaka mosquito nets,tuwe waaminifu,tufanye kazi kwa ajili ya kizaji kipya"next generations,kwani tusitegemea kujenga Hong Kong au Rome kwa 5 years.Tunapenda maisha ya kifahari kuliko wanaotupa misaada.
[4]wandishi tuongelee zaidi kupanda na kushuka kwa uchumu,education,science n,k.kwani politics haitufikishi mbali,Tusipende kujikuza kupitia newspapers.Watz pamoja na JK kuungwa mkono ati ni hodari wa kuomba misaada nje lkn hakuna cha bure,Mnajua misada hulipwa?mnajua kua hakuna nchi iliyo wahi kwenda mbele hata kwa hatua 1 kwa ajili ya misaada.TENA ikumbukwe Tanzania ni nchi inayoongoza kwa kuombaomba,kupewa misaada,the same time ni nchi inayoongoza duniani kwa kula misaada.Ni nchi inayoongoza kwa kutafuta wawekezaji,ni nchi inayoongoza kwa wawekezaji kutajirika kuliko walivyokua hawatarajii.muhimu tu uwe colored na usijui kuongea kiswahili.

na window XP, P.R,CHINA, - 26.05.08 @ 18:08 | #13436

Window wa China unamaana ili mradi tu uongee kama Ponjoro, utaikamua Tanzania kama wanavyoikamua maponjoro wa Tz wenye uraia wa UK, Canada, Marekani na Iran. Halafu wanataka uraia wa nchi nyingi ili watuzike kabisa watanzania, yaani tubakie tu kwenda Jahanamu.

na in, p, - 26.05.08 @ 18:38 | #13440

Kwa watu waliokombolewa na kukomaa kifikra, watu wanaoweza kusema ndio katika ndio, au hapana katika hapana, mawazo kama haya ndiyo yanakuwa yanaeleweka. Wapo watu wanaotumia safu hii kuponda Vyama badala ya kutafuta ukweli na kutumia safu hii kutoa maoni ya kuelimisha jamii. Binafsi naona Hoja ya Zitto ni ya msingi sana lakini inaeleweka kwa wenye akili timamu, wanaoona nchi yetu inavyoenda. Wala hawapendi kujipendekeza kwa CCM ili kutafuta maslahi binafsi bali wanasema hivyo kwa manufaaa ya jamii ya watanzania kama anavyofanya Zitto. Zitto usiogope we endelea na vijijini tutakusaidia unafahamika kwanza kuliko Rais mwenyewe.

na Isango, Singida, - 26.05.08 @ 20:47 | #13447

Namshukuru Bw ZITO kwa hoja yake nzuri,ingependeza serikali ifike mahali ikubaliane na mawazo yanayojenga ikiwa ni kwa maslahi ya nchi.Huwa nasoma sana magazeti ya nyumbani na nafurahi kuona changamoto hizo.KILA LA KHERI.

na Uronu Mmbasha, North carolina Moyok USA., - 27.05.08 @ 04:00 | #13455

Kwanza nashauri kwa wachangiaji wa hii tovuti...ACHENI ****** NA KULUMBANA BILA SABABU CHANGIA HOJA!
Hongera Mchungaji Mtikila kwa kuanzisha hoja ya mgombea binafsi pale mjini Dodoma miaka michache iliyopita. Hii ni hoja ya msingi kwani KATIBA imetamka bayana haja ya kuwa na mgombea binafsi.Mawazo ya Kijana Zitto nayo ni mazuri sana. Wito wangu kwa wanaharakati:Mabadiriko yoyote ya Katiba na Sheria zake ni vizuri yakafanyika kwa kutazama historia ya nchi yetu, lakini pia MASLAHI ya TAIFA. Kukua kwa Democrasia peke yake bila uzalendo na uadilifu wa dhati kwa nchi ni sawa na zero. Angalia mfano wa nchi za mashariki ya Asia (east Asian tigers)zimepiga hatua sana kiuchumi; Wala hazikuwa na Democrasia bali uzalendo wa hali ya juu wa viongozi,watumishi na wananchi kwa ujumla. Nchi hizo zipo kwenye kundi la Developmental State na si Democratic State. Ni kweli kwamba Democrasia ni nzuri kwa maendeleo ya Taifa kwani inahusisha ushirikishwaji wa jamii katika kila shughuli (siasa, uchumi nk)LAKINI pia ikumbukwe kuwa Democrasia ni sehemu ya UTANDAWAZI ambapo kwa nchi changa kama TZ ambayo sayansi na technolojia vimepita mbali hatufaidiki na chochote ila kuendelea KUPORWA rasilimali zetu (madini,sekta ya fedha na biashara nk). Kwa sababu hiyo ndiyo maana viongozi wa nchi kama Taiwani na South Korea walikata democrasia na kujichagulia muundo wao wa utawala ...Developmental State!
Sisemi kwamba Democrasia ni mbaya katika kuleta maendeleo ya nchi changa kama TZ: Bali uangalifu MKUBWA unatakiwa katika kufanya mabadiliko ya Katiba na Sheria zetu. Kikubwa ni UZALENDO & UADIRIFU kwa NCHI na JAMII tuache undugunisation katika kazi! Achaguliwe mtumishi mwenye SIFA na UWEZO badala ya patronage and clientele! Tabia kubwa iliyojengeka miongoni mwetu ni kutaka kufaidika (binafsi) kwanza kabla ya kuzalisha. Watu wanageuza mali za umma kuwa binafsi! Katika mazingira kama hayo hapo juu unatarajia democrasia itafanya nini kubalisha maisha ya Mtanzania? Kumbuka mashirika ya umma yalikufa kutokana na Umimi na Undugunisation, na hivyo ndivyo hali ya nchi hii ilivyo sasa!Pitapita huko maaofisini (wizarani, kwenye taasisi mbalimbali za serikali, ofisi za mikoa au halmashauri za wilaya/miji/municipal)utaona jinsi watu walivyojiinga kiundugu ndugu na kufanya kazi kiundugu!
JAMII tuache woga: jumuiya za dini, makundi mbali mbali ya jamii yana jukumu kubwa ktk kuchochea maendeleo na kubadilisha mfumo wa siasa wa nchi. Hebu angalia ni Watz wangapi waliojitokeza kupambana na ufisadi! ni wachache sana! Inakuwaje raia wa UK waandamane kwa ajili yetu wakati sisi wenyewe tukiwa TUNASHANGAA SHANGAA kana kwamba HATUPO! Kwani hili Taifa ni la Dr. Slaa peke na hao wachache wenzake?
Mwisho Democrasia peke yake haiwezi kubalisha chochote kwa jinsi tabia na mfumo wa utawala ulivyo sasa TZ.Mabadiliko ya Katiba na Sheria za Uchaguzi ni mazuri lakini yaangalie UFANISI wa kazi na MASLAHI ya TAIFA!
Tuchape kazi kwa bidii!

na Donald, Australia, - 27.05.08 @ 06:20 | #13459

Donald umesema ukweli, watanzania watu wa maneno na kulaumu tu. Zito katoa hoja ya wagombea binafsi, angalia maoni ya wengi hapo juu. Wabongo tuache porojo za mitaani, hazitufikishi popote, hata hao wagombea binafsi wakija, kama mtindo wenyewe ukiendelea hivi tutaendelea kuwa maskini milele na kuendelea kuilaumu serikali kila kukicha. TUCHAPE KAZI KWA BIDII TUTAFANIKIWA.

na Dadili, Tz, - 27.05.08 @ 10:46 | #13491
Andika maoni yako:

Jina:


Barua-pepe:


Mji/Nchi:


Maoni:




Habari Mpya | Kitaifa | Dar | Mikoani | Tahariri | Makala | Michezo | Matangazo | Webmaster
Copyright 2008 © FreeMedia Ltd.
Free media limited
mtaa wa Mkwepu na Makunganya, jengo la Bilicanas, gorofa ya kwanza, SLP 15261, Dar es salaam, Tanzania
simu +255-22-2126233 • faksi +255-22-2126234 • Selula 0713 296570
MFUMO WA UCHAGUZI TULIO NAO UNAKARIBISHA UKABILA, MAJIMBO MENGINE YANKABILA MOJA TUU, KAMA MAJIMBO YA RUNGWE , NA IRINGA VIJIJINI, MTU ANAWEZA KUWA JIMBONI KWAKE KWA KISINGIZIO CHA MAJUKUMU YA UBUNGE KUMBE NI UKABILA ANAENDEKEZA,

MFUMO WA UCHAGUZI ANAOPENDEKEZA ZITO KABWE UTAONDOA KABISA DHANA YA UKABILA
 
soma hapa


HABARI MPYA KITAIFA DAR MIKOANI TAHARIRI MAKALA MICHEZO
jumatatu, 26 mei 2008

Pekua Tovuti





Gazeti la Jana
Matangazo
Bei zetu
Wasiliana nasi
Tuma habari




Zitto atuma waraka kwa JK

na Kulwa Karedia


HUKUMU ya mahakama kuruhusu watu kugombea nafasi za uongozi kama wagombea binafsi, imemsukuma Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, kuchukua hatua zaidi ili kuhakikisha Watanzania wanaifaidi haki hiyo ya kidemokrasia.

Ili kuhakikisha kuwa suala la mgombea binafsi linaingizwa katika mifumo halali wa uchaguzi na sheria za nchi, Zitto amemwandikia Rais Jakaya Kikwete pamoja na Bunge, akionyesha dhamira yake ya kutaka kuwasilisha muswada binafsi wa mabadiliko ya Katiba.

Akizungumza na gazeti hili, Zitto alisema kuwa suala la mgombea binafsi limecheleweshwa mno na anadhamiria kuhakikisha kuwa linapewa msukumo ili Watanzania wapate uhuru wa kuwania nafasi za uongozi.

Katika barua hiyo ya Mei 19 ambayo Tanzania Daima imepata nakala yake, Zitto alisema utekelezaji wa uamuzi huo utabadilisha mfumo wa uchaguzi nchini na ili utekelezeke, yanahitajika marekebisho ya Katiba ya nchi na sheria za uchaguzi.

“Kwa barua hii, natoa taarifa kuwa nina nia ya kuwasilisha bungeni muswada wa sheria za kurekebisha Katiba ya nchi na sheria za uchaguzi, hivyo naomba wataalamu wa ofisi yako waniandalie muswada huo,” anasema Zitto katika barua hiyo.

Katika barua hiyo, anamkumbusha Rais Kikwete kuwa kwa mara ya kwanza alimwandikia barua Mei 31 mwaka jana, akimjulisha uamuzi wa Mahakama ya Rufaa kuhusu wagombea binafsi na umuhimu wa kubadili mfumo wa uchaguzi, lakini hakupata majibu ya msingi.

“Katika barua yangu hiyo nilishauri umuhimu wa kufanya mabadiliko makubwa katika mfumo wetu wa uchaguzi, ili kuendana na si tu hukumu ile ya Mahakama Kuu kuruhusu wagombea binafsi, bali pia kuweka mazingira ya kisiasa ambayo yanatoa fursa kwa vyama kushindana kwa mujibu wa sera zao na hivyo kuimarisha asasi hizo muhimu za kidemokrasia,” alisema Zitto.

Alisema anarudia kuandika barua kwa mara ya pili baada ya serikali kushindwa rufaa iliyokata kupinga hukumu ya Mahakama Kuu iliyotoka mapema mwaka 2006.

“Narudia ushauri wangu kwa serikali kukubali kufanya mabadiliko makubwa katika mfumo wa uchaguzi, ili kukabiliana na changamoto za sasa na za baadaye za kisiasa nchini kwetu, lengo likiwa ni kuimarisha mfumo wa vyama vingi,” alisema.

Alisema kama wana siasa hawatakuwa makini, maamuzi ya mahakama yanaweza kuudhoofisha mfumo wa vyama vingi nchini na demokrasia kuparaganyika kabisa.

“Hatari ninayoiona ni kuwa kuruhusu wagombea binafsi bila kuwa na mfumo unaohakikisha uimara wa mfumo wa vyama vingi, kunaweza kupeleka nchi kuongozwa na kundi dogo lisilo na udhibiti,” alisema Zitto katika barua hiyo.

Alisema anaishauri serikali isipoteze muda kwa ajili ya kukata rufaa kuhusu uamuzi wa Mahakama ya Rufaa kutupilia mbali rufaa ya serikali dhidi ya kuruhusu wagombea binafsi katika nyadhifa za kisiasa.

Katika barua hiyo, Zitto amependekeza mapendekezo matano, akitaka Bunge liwe na aina zifuatazo za wabunge.

Alisema aina ya kwanza ya wabunge ni wabunge waliochaguliwa kuwakilisha mamlaka za Serikali za Mitaa.

Mamlaka hizo sasa zitatamkwa na Katiba, nazo ni halmashauri za wilaya, manispaa na miji.

“Hivi sasa nchini kuna mamlaka za serikali za mitaa zipatazo 124 kwa upande wa Tanzania Bara, hivyo hapa tunaweza kupata wabunge 124 wa kuchaguliwa moja kwa moja na wananchi, kundi hili ni dhahiri wagombea wataruhusiwa kikatiba na sheria ya uchaguzi itaweka masharti ya ushiriki wao,” alisema Zitto.

Alisema kwa upande wa Zanzibar wabunge wa kuchaguliwa watokane na wilaya za kiutawala za sasa, ambapo jumla ya wabunge 10 watapatikana.

Pendekezo la tatu, ametaka wabunge wa mikoa kwa Tanzania Bara watakuwa sawa na idadi ya wabunge wanaotokana na mamlaka za halmashauri za wilaya, ambao idadi yao itakuwa 124.

“Kwa upande wa Zanzibar ili kulinda matakwa ya Katiba, idadi ya wabunge wanapaswa kutopungua 50 kama ilivyo sasa, wabunge 40 watatokana na kundi hili la wabunge wa mikoa,” alisema.

Alisema mikoa itagawiwa wabunge kutokana na uwiano wa wananchi waliojindikisha kupiga kura katika mkoa husika na mgawo huo utakuwa ukirejewa kila baada ya miaka kumi.

Pendekezo la nne, Zitto alisema ni wabunge wanawake, ambao watakuwa asilimia 30 ya wabunge wanaotokana na makundi matatu ya juu kwa mujibu wa mfumo wa sasa.

Wakati pendekezo la tano, mbunge huyo kijana alisema ni wabunge watano kutoka Baraza la Wawakilishi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Spika kama si mbunge.

“Ndugu Rais kwa mapendekezo haya tunaweza kutoa uhuru kwa raia wa Tanzania mwenye sifa na bila kujali kama ni mwanachama au si mwanachama wa chama cha siasa kugombea ubunge na hata udiwani,” alisema.

Alisema mapendekezo hayo yanaangalia umuhimu wa vyama vya siasa kubaki nguzo muhimu ya demokrasia nchini, kugawa viti vya ubunge kwa vyama kutokana na uwiano wa kura ambazo chama kimepata, kutafanya vyama kujimaarisha na kutoa sera bora zaidi na ushindani mkubwa.

“Kwa mapendekezo haya tutakuwa na asimilia 40 ya wabunge wote wanawake bila ya kujumlisha wabunge wanawake watakaochaguliwa kutoka katika mamlaka za serikali za mitaa moja kwa moja kama kina Gertrude Mongela, Beatrice Shelukindo, Zainab Gama na Jenista Mhagama, hivyo tunaweza kufikia asilimia 50 ya wabunge wanawake iwapo vyama vya siasa vitateua wagombea 24 tu kati ya 124 wa mamlaka zilizopo sasa na kushinda,” alisema.

Alisema kwa mapendekezo hayo, Tume ya Taifa ya Uchaguzi haitakuwa na kazi ya kugawa mipaka ya majimbo tena, bali mipaka itatokana na tangazo la rais la kutangaza mamlaka za serikali za mitaa.

“Mapendekezo haya yanaondoa nafasi ya rais kuteua wabunge, na badala yake Katiba ifanyiwe marekebisho ili rais aweze kuteua baraza la mawaziri nje ya wabunge ili wadhibitishwe na Bunge,” alisema.

Katika hali hiyo, Zitto alisema: “Ndugu Rais nakuomba uiagize serikali yako kuandaa mapendekezo ya mabadiliko ya mfumo wa uchaguzi na kuitisha mjadala mpana wa kitaifa kupitia asasi kama vile RIDET ili kupata maoni ya Watanzania wengi zaidi na hivyo kuboresha demokrasia,” alisema.

Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salvatory Rweyemamu, alipoulizwa kama ofisi yake imepokea barua hiyo, hakukubali wala kukataa.

“Ndugu yangu sijui kama barua hiyo imefika au la, nakuomba uwasiliane na Katibu wa Bunge, anaweza kukupa maelezo zaidi kama ombi lake litakuwa limewekwa kwenye Order Paper au unaweza ‘kumkoti Zitto mwenyewe,”’ alisema Rweyemamu.

Nakala ya barua hiyo imesambazwa kwa Spika wa Bunge, Samuel Sitta, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Hamad Rashid Mohamed, Waziri wa Katiba na Sheria na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa.

juu
Maoni ya Wasomaji
Maoni yanayotolewa na wasomaji wa safu hii ni ya kwao na sio maoni ya kampuni ya Freemedia Ltd. Aidha sio maoni ya mtunzi au mwandishi wa habari au makala husika hapo juu. Maoni haya hayajahakikiwa wala kuafikiwa na kampuni ya Freemedia Ltd.
Maoni 55 yameshatolewa. (Nawe toa maoni yako!)

Binafsi nakubaliana na mawazo na mbunge wetu 'yosso' Mh Kabwe, Z.Z. Nahitaji kuwasiliana nawe privately! tafadhali naomba anuani yako ya barua-pepe. Itume kupitia anuani yangu tajwa hapo juu.

na Ndugu, Dar - Tanzania, - 26.05.08 @ 08:24 | #13314

Marekebisho ya ujumbe wangu wa kwanza;
Badili neno la tano katika ujumbe huo, badala ya kusomeka 'na' isomeke 'ya'. Kisha anuani yangu ni 'lijangu08@yahoo.com'.

na Ndugu, Dar - Tanzania, - 26.05.08 @ 08:32 | #13319

Maoni yako Zitto ni mazuri sana lakini sasa kuna wasi wasi wa Nchi maskini kuwa na wabunge wengine namna hii .Nadhani kuwe na mabadiliko lakini sasa Nchi inaweza kupata mzigo wa kuwa na wabumge 400 ambao hatuna sababu hata moja ya kuwa nao .

Rais akumbuke kwamba hatutaki wabunge wa kuteuliwa akina Meghji .Kila mmoja apitie katika ballot box .Wabunge wa Rais pia hawana haja .

Tuwe na wagombea binafsi na wa Vyama watu wapate uhuru wa kuamua na mabadiliko ya Katiba haya ndiyo muhimu kabisa kabisa .

na Chifu Ihunyo, Tanzania, - 26.05.08 @ 08:36 | #13320

Mabadilike ya katiba ndio msingi wa kuimarisha mfumo mzima wa Demokrasia wa mfumo wa kiuchaguzi wa mfumo wa vyama vingi pamoja na wagombea binafsi,huu mfumo wa sasa ni wa danganya toto ndo maana hata chaguzi nyingi zilizopita vyama vya upinzani vinashindwa kutokana na hali ya kikatiba iliyopo.Zitto vilevile kumbuka kupigania kuundwa kwa Tume Huru ya Uchaguzi ambayohaitakuwa na maslahi yeyote na Chama chechote,tofauti na ilivyo sasa Tume ya uchaguzi ni mali ya ccm,Zitto liangaliye sana hilo kwani ndo utakuwa mwanzo wa uimarishaji wa Demokrasi ya mifumo yote ya upatikanaji wa viongozi wa kisiasa katika nchi yetu ya Tanzania.

na Israel J.Mwakapembati, Tanzania, - 26.05.08 @ 09:15 | #13324

Maoni ya Zito ni mazuri sana sana sana. Namuona kama mtu wa kwanza kuongelea hoja ya ugombea binafsi kwa faida zake na madhara yake, nhivyo kutoa mwlwkwo wa hekima sahihi inayotakiwa katika kuruhusu ugombea binafsi kuepuka hatari ya kundi dogo lisilodhibitika kutawala nchi. Marafiki wachache wenye nguvu ya fedha wanaweza kujiamualia mambo na kujikita madarakani.

Maoni ya zito ni muhimu sana kuzingatiwa. Hata hivyo nimshauri zito kupunguza ukubwa wa bunge kwenye pendekezo lake, kadiri ya umasikini wa nchi.

na Bernard Mukasa, Sumbawanga, - 26.05.08 @ 09:30 | #13326

Mabadiliko ni lazima,tutumie fursa hii kufanya mambo kwa uwazi zaidi, na Mungu atatusaidia kama tunanuia kutenda haki kwa watu kinyume na hapo taifa litazidi kulia na kunungunika kila kukicha.

Vyama vimetupumbaza muda mrefu kwa ukiritimba wa kuogopa kuhoji wakubwa wa vyama hivyo, nafasi sasa iko wazi.
hongera zitto watanzania tujifunze kwa ndugu huyu.

na Focus Laurent, Bunda, - 26.05.08 @ 09:33 | #13327

Safi sana Zito. Wewe unafikiria kwanza kabla ya kuongea. Siyo kama wachangiaji wengine waliochangia ugombea binafsi waliobaki na kelele zisizo na hoja oooh CCM inaogopa itameguka, oohh aijui nini.

Wote jifunzeni toka kwa zito.

na mviziaji, Bongo, - 26.05.08 @ 09:33 | #13328

Hivi ninyi mnaomsifia Zitto amefanya nini? Tangu wananchi wanapiga kelele, REDET pia imewaambia nendeni vijijini ameshatembelea vijijiji vingapi na amefungua matawi mangapi? Si wapinzai wanamangamanga tu Dar es Salaam. Mara sijui US. Hivi hamjifunzi ya KITETO? Mkaenda kama watalii, wananchi hawajawafahamu vizuri, JAMANI TUTASEMA MARA NGAPI AKINA ZITTO MUELEWI. Lazima muwe strategic, hebu angalia Obam alivyopanga mikakati yake. Hamna dira ninyi wapinzani. Jukwaani na vyombo vya habari ndio mtaongeza wanacha.

Mnauza sura tu na majina kwenye vyombo vya habari. Mbona hamtupatii vijiji vingapi mmetembelea Tanzania yote na mawawi mangapi mmefungua. Hizi ndizo habari tunazotaka kusikia, kwamba mnafahamika vijijini kwenye wapiga kura wengi.

Mnabaki tu kubadilishana kwenye Tv na Magazeti, mara Mbowe, halafu Zitto, halafu Slaa, halafu Limpumba. Afadhali hata Mrema anaonekana anajua analofanya. Sasa hivi anaenda vijijini, akina Zitto kuuza sura kwenye magazeti na Tv, hamfiki mbali, katiba mmefikiwa wapi mliyosema mtashughlika nayo. Zibeni tu masikio, wekeni pamba, mtayapata mengi ya Kiteto msipoenda vijijini kuanzia sasa.

na ki, mn, - 26.05.08 @ 09:45 | #13333

Zitto nakupongeza na ninaunga mkono sula la kubadili katiba, hii ndiyo kero ya nchi yetu, ni kuweka viraka katika katibia mpaka inachakaa. Pia suala la mgombea binafsi, kulikataa ni kuwanyima watu uhuru. Serikali inajihami nini? Si ni nchi ya Demokrais, sasa CCM na serikali wanaogopa nini? Ndugu yangu, Zitto naomba tuwasiliane kwa email yangu hapo juu kwa tafakari zaidi juu ya nchi yetu tajiri lakini watu wake maskini. Inahitaji kukombolewa tena. Watanzania wenye mapenzi mema , hizi ndizo hoja za kuunga mkono za kizalendo kweli kweli, si za kifisadi za wizi wa mali ya umma.Jerusalem 26/5/08

na Fr. mapunda Baptiste, Israel - Jerusalem, - 26.05.08 @ 09:49 | #13335

Zitto ni mtu makini sana! Hata sasa hivi yuko kwenye Jimbo lake, anatembelea vijiji. Lakini pia ni lazima awe Dar, Tanzania iko Dar! Bila kuweka sawa mambo ya Dar, ni vigumu kuyaweza ya vijijini.

Padri Baptiste Mapunda, na mini naomba kuwasiliana na wewe. E-mail yangu: pkarugendo@yahoo.com

na karugendo, Tanzania, - 26.05.08 @ 10:29 | #13341

It's obvious that a dumb man will have no verbal say on this!!!

na bubu - 26.05.08 @ 10:32 | #13343

HV WE UNAEJIITA KI MN UNA AKILI AU UMEJAZA MAJI2 HUKO KICHWANI? WE UNAWATETEA HAO CCM WAMEKUSAIDIA NINI TANGU UMEZALIWA? WA2 2NAJITAHIDI KUPINGA VTA UFISADI KILA SIKU WE UNAWATETEA CCM KAMA UMEKOSA KI2 CHA KUSEMA ACHA KUTOA MAONI YA KIPUUZI KIAC HICHO ******* WEWE.

na MDERE, TZ-ATOWN, - 26.05.08 @ 11:06 | #13347

HV WE UNAEJIITA KI MN UNA AKILI AU UMEJAZA MAJI2 HUKO KICHWANI? WE UNAWATETEA HAO CCM WAMEKUSAIDIA NINI TANGU UMEZALIWA? WA2 2NAJITAHIDI KUPINGA VTA UFISADI KILA SIKU WE UNAWATETEA CCM KAMA UMEKOSA KI2 CHA KUSEMA ACHA KUTOA MAONI YA KIPUUZI KIAC HICHO ****** WEWE.

na MDERE, TZ-ATOWN, - 26.05.08 @ 11:10 | #13348

HV WE UNAEJIITA KI MN UNA AKILI AU UMEJAZA MAJI2 HUKO KICHWANI? WE UNAWATETEA HAO CCM WAMEKUSAIDIA NINI TANGU UMEZALIWA? WA2 2NAJITAHIDI KUPINGA VTA UFISADI KILA SIKU WE UNAWATETEA CCM KAMA UMEKOSA KI2 CHA KUSEMA ACHA KUTOA MAONI YA KIPUUZI KIAC HICHO ****** WEWE.

na MDERE, TZ-ATOWN, - 26.05.08 @ 11:10 | #13349

MAWAZO YA MBUNGE CHIPUKIZI NI MAZURI.
UNAJUA UNAPOKUWA KIJANA WAWEZA KUWA NA NDOTO NYINGI YA KUFANYA MAMBO MENGI SABABU UNAJISIKIA UNA NGUVU.
WATANZANIA LAZIMA TUWE "REALISTIC."
BILA KUWA REALISTIC TUTAKUWA TUNALAZIMISHA MAMBO AMBAYO HAYATATUSAIDIA KULETA MAENDELEO.
MBUNGE ZITTO BADO ANASISITIZA UGOMBEA WA MTU BINAFSI. KUHUSU SWALA HILI TUNAPASWA KUPIMA NA KUELEZA FAIDA NA HASARA ZAKE NA KUJUA FAIDA NI KUBWA ZAIDI AU HASARA NI KUBWA ZAIDI: NA HASA UKIZINGATIA UCHUMI, MUDA WA KUFANYA KAZI WA WANANCHI N.K.
INGAWA KUWA NA MGOMBEA BINAFSI NI HAKI YA MSINGI KWA RAIA, KWA UPANDE WANGU NAONA WATANZANIA KUWA NA SUBIRA. MGOMBEA BINAFSI ATAKUWA WA MAANA WAKATI ASILIMIA KUBWA YA WATANZANIA WATAJUA ELIMU YA URAIA NA SI KUFUATA MKUMBO.
-HALAFU TUSISAHAU KUPIMA MAENDELEO YA VYAMA VYETU VYA UPINZANI: VINAKUA AU VINADUMAA.
KITU CHA MAANA CHA VIONGOZI WA UPINZANI WANACHOPASWA KUKAZANIA NI NAMNA GANI KUJENGA NA KUIMARISHA VYAMA VYA UPINZANI: VIKUE KAMA CCM, KUJITEGEMEA KIUCHUMI.
VYAMA VYA UPINZANI CHADEMA AU NCCR MAGEUZI: KIMOJAWAPO KINGELISHINDA UCHAGUZI NA KUTAKIWA KUUNDA SERIKALI WAKATI HUU, LABDA NCHI INGELIONGOZWA NA VIONGOZI MBUMBUMBU WASIOJUA SIASA. MFANO UKITAJA CHADEMA: WATU WANA MAWAZO YA MBOWE, ZITTO, SLAA. SASA WAAMBIE WAUNDE BARAZA LA MAWAZIRI. CHAMA HIKI KILISHA MWOMBA MTANZANIA FULANI ETI KWA KUWA AMESOMA, LAKINI HANA WAZO LA SIASA AGOMBEE UBUNGE HUKO MOSHI VIJIJINI.
KWA MANTIKI HIYO KABWE, DEMOKRASIA HAITAJENGWA KWA IDADI YA WABUNGE, KWANZA TUOMBE RUZUKU HATA NCHI ZA NJE KUIMARISHA VYAMA NA HASA MASHAMBANI AU VIJIJINI AMBAKO HAWAJUI ELIMU YA URAIA.
KUHUSU ASILIMIA YA WABUNGE AKINA MAMA: MIMI NAONA VIONGOZI WENGINE WANATUMIA AKINA MAMA KAMA KAMPEINI. TUKUMBUKE KWAMBA AKINA MAMA WATAINULIWA KWANZA KWA KUPEWA ELIMU YA KUTOSHA NA KUJUA HAKI ZAO. HAINA MAANA KUMPELEKA MAMA BUNGENI AMBAYE HAJUI HATA WAJIBU WA BUNGE NI NINI.
-JUA NINYI WABUNGE MNATUMIA FEDHA NYINGI KULIKO HATA WASOMI WANAOHANGAIKA MUDA WOTE. SASA KUONGEZA IDADI YA WABUNGE NI KUNYONYA WANANCHI.
TUSISAHAU PIA KUKUA KWA SIASA KUNAENDA SAMBAMBA NA KUKUA KWA UCHUMI.
TANZANIA INATAKA KUJENGA MFUMO WA SIASA AMBAO UTAKUWA NA BAJETI KUBWA KULIKO MAMBO MENGINE YA MAENDELEO.
BE REALISTIC: WAKATI MWINGINE TUNAWEZA KUSOMA SANA TUKABAKI NA NADHARIA TU KICHWANI!!!!!!

na Madaha - 26.05.08 @ 11:32 | #13351

Mdere hujui unachobwabwaja, acha wenye akili ya kuchambua wakufahamishe ujumbe niliokusudia. Tukiwa na watu kama wewe Mdere nchi haiendelei, unadhani kutoa sifa ndio kusaidia. Kwa taarifa yako hujui usemalo, kama huamini mwite mtu alieenda shule ukatafsirie ujumbe wangu.

Ninataka akina Zitto wafanye kazi, sio wauze sura. Unadhani bila kwenda vijijini watapata kura. Unaijua Mdere ripoti ya REDET. Haya niambie inamaana gani halafu inaambie wapinzani wametumia uelewa wake vipi. Mdere hujakua kiakili bado. Hujui ninachoongea. Kura nyingi ziko vijijini. Na nitaendelea kuwazomea wapinzani kama hawatupi ripoti wametembelea vijiji vingapi na wamepata wanachama wangapi. Unajua ya Kiteto wewe Mdere? Wewe msahaulifu kama panzi una kichwa cha panzi. Mwite Zitto akusaidie kusoma hapa, yeye ataelewa ninachosema.

na ki, mn, - 26.05.08 @ 11:35 | #13353

hivi mijitu mingine sijui ina akili au tope haya we unaeiponda CCM hivyo vyama vingine vimekufanyia nini.
huu nimtindio au kwani kila analosema zitto ni la maana mnataka kuiingiza nchi hii ktk matatizo halafu mtakaokuwa wa kwanza kuwageuka ni nyie mnaotoa maoni[****].

na kaka, tz[udsm]dsm, - 26.05.08 @ 11:44 | #13356

Ni kweli kina Mdere ndiyo wanaorudisha nchi nyuma. Kila siku CCM wimbo ni huo huo. Hoja ya wagombea binafsi ni hoja ya wanasiasa. Wanatafuta namna ya kugawana jinsi ya kuingia bungeni na Ikulu. Lakini hoja ya Ki ni kwamba wananchi wa kawaida wanafaidika vipi na wagombea binafsi. Tunajua Zitto katumwa na Mengi. Ni hao hao wanataka tu kuingia bungeni. Hivi bunge la watu 300 linaongeza tija yoyote kwa Watanzania? Let us be realistic. Watu kama akina Mdere wanapandia tu hoja. Hapa siyo siasa bali faida na manufaa ya wananchi. Ufisadi upigwe vita, na wanaoupiga vita wapo CCM na wengine nje ya CCM. Ni ujinga kusema waliomo CCM hawapigi vita ufisadi, ni kukosa akili.

na mwandamizi, Dar, - 26.05.08 @ 11:53 | #13357

Umelonga Mhe.Kabwe. Ni kama umeotea. Umejuwa nyakati na majira. Ni kweli, wakati sasa umefika wa kuwa wawazi. kama sisi waTz tungekuwa tunajali nchi bila kuegemea upande wowote, ulikuwa ni wakati wakusikiliza sauti hii ya Mhe Zitto. Bwana huyu ametembe nje ya nchi ameona tayari mifumo ya nchi zingine zinavyoendeshwa kikatiba na ameona yalivyo na mapungufu katiba ya nchi yetu. Mambo yanabadilika kadri siku zinavyosonga mbele. Haturudi nyuma. Mifumo mingine sasa imepitwa na wakati. Mifumo ya Mbungu kuwa ndiye pia Waziri. Mtunga sheria na Mtendaji kwa wakati mmoja. Ajira mbili kwa wakati mmoja. Kweli busara nayo pia inadai ya Mhe. Zitto kusikilizwa kwa manufaa ya wengi. Isichukuliwe eti yamependekezwa na mpizani, bali ichukuliwe kuwa pendekezo la Mtanzania wa kizazi kipya. Ushauri ni ushauri unaweza kutoa hata kwa adui ukausikliza na kuutendea kazi. Ya EPA si yametusaidia????? mbona yametoa upinzani.

na Msafiri Muelewa, Mwanza, - 26.05.08 @ 12:11 | #13361

Maoni ya Mh. Zitto Kabwe ni mazuri na hasa la kurekebisha katiba na kanuni za tume ya uchaguzi ili ziendane na mabadiliko ya katiba yatakayofanyika. Ni ukweli usio pingika kwamba Tanzania tunahitaji tume huru ya uchaguzi isiyo egemea upande wowote tofauti na ilivyo sasa kwa tume zetu za uchaguzi Tz bara na visiwani. Lakini suala la ukubwa wa bunge kiasi kile siliafiki, ni bora pesa hiyo itumike katika kuwekeza kwenye rasilimali watu ( elimu, hospitali na miundombinu) kuliko kulipa wabunge wapatao 400 ilihali waliopo wanatosha.

na Peres Joshua, Dar es salaam, - 26.05.08 @ 12:11 | #13363

Ndugu Madaha,
Kwa bahati mbaya wengi wetu tunaona mabaya ya "chukua chako mapema", lakini bado tunawapigia kura kwa sababu ya pilau, tshirt au kipannde kimoja cha kanga yenye sura zao.
Pamoja na kuwaeleza waende vijijini hata nawe ndugu yangu kama unaona watawala hatutendei haki, sote kwa pamoja tutafute solution siyo kuwaachia akina Zitto tu.

na mabula - 26.05.08 @ 12:31 | #13370

Ndugu zangu watoa maoni, hususan Ki MN, Mdere,Madaha, mbona sioni hoja zenu? Mbona sioni mapendekezo yenu. Mlingoja Zitto atoe mapendekezo yake muanze kumlima vijembe. Hapa hapatakiwi ushabiki wa vyama. Hoja hii ni ya msingi wala haihitaji vijembe bali kutoa maoni kwa sababu tayari mjadala uko wazi. Toa mapendekezo yako.

Kumbukeni kwamba wakati wa ukomnbozi ni sasa kama asemavyo Mtikila. Hili la Zitto kamalingetoka kwa Rais, nini ungekuwa msimamo wenu? Pendekezo limetolewa, kama lina kasoro au mapungufu, sahihisheni na tuiunge mkono hoja hiyo na kuishinikiza mamlaka husika kuipeleka Bungeni ijadiliwe. Lakini ukweli utabaki palepale, wakati umefika Katiba yetu uzungumziwe na ikiwezekana ibadilishwe ili iendane na zama hizi za demokrasia shirikishi na utawala bora. Namuomba Rais asijali inakotoka pendekezo hili ila ajiri unyeti wa wakati na pendekezo lenyewe. Tuachanena U-ccm, U-chadema, u-cuf. Vyote hivi ni vyama na viongozi wake ni waTz wenye uwezo wa kuogoza nchi. Kama katoto kama Joseph Kabila kanasimamia linchi kama DRC, sembuse na watu wazima waliobobea kielimu na kisiasa kama Profesa Lipumba, Profesa Sengondo, Mchumi Kabwe Zitto, Dr Slaa, wanasheria machachari kama Lisu, Marando na wengine. Mnapende ili uweze kuongoza lazima uwe ccm? tukifikiri hivyo tutakuwa tumechelewa. Angalia mwanasiasa chipukizi Obama wa Marekani anavyowahenyesha wanasiasa waliobobea?

Ndugu zangu, kumbukeni hakuna shule au darasa wanakofundisha ma Waziri au Marais. Hizi ni nafasi za uongozi ambazo zinahitaji hekima na busara tu.

na Sultan Mosi, Pemba, - 26.05.08 @ 12:47 | #13373

Ha ha ha, Naanza kwa kicheko, unayejiita kaka na mwandamizi msidhani kuwa ninamapenzi na chama mie siangalii sura, unadhani maelezo yangu dhidi ya Mdere ni kuitetea CCM, kumbe hata ninyi hamjanielewa, mmechemsha.

Sasa ni hivi mie napenda demokrasia. Ujumbe niliokusudia ni mzuri sana kwa Zitto na Kambi ya upinzani, maneno niliyotumia kuwa wanauza sura siyo kwenye TV na magazeti sio kuwa nawachukia. Nilikuwa nawapa changamoto wahakikishe wanaenda vijijini kueneza demokrasia. Kwa hiyo unayejiita kaka na mwandamizi mmenoa, nanyi mlihitaji mtu awatafsirie ujumbe niliokusudia. Mdere umenipata sasa ujumbe wangu? inahitaji shule kidogo.

Haya sasa ngoja niseme hivi, Waheshimiwa Zitto, Slaa, Mbowe, Lipumba n.k, nawaambia hivi mwende vijijini kueneza demokrasia, wananchi wawafahamu vizuri. Tumieni ripoti ya REDET kufanya kazi, kura nyingi ziko vijijini. Tunataka kwenye majukwaa mtuambie pia mmetembelea vijiji vingapi na mmepata wanachama wangapi. You are over doing it opposition parties by staying in towns, a lot of votes are in rural areas, go there now. You have also to learn a lesson from Kiteto election, stay in villages, you get me Zitto and your colleagues? Bahati mbaya sijui kulugha chenu ningewaambia labda mngenielewa. Zitto come out on this arena and respond on my challenges

na ki, mn, - 26.05.08 @ 12:56 | #13377

WE KI MN NAONA 2KUTAFUTIE MKOA UENDE UKAWADANGANYE MADUNGAYEMBE WENZAKO WANAOSIFIA CCM TANGU UHURU WAKATI UNAKULA MLO M1 KWA CKU BARABARA HAINA LAMI TANGU NCHI IMMEKUA HURU BUT UNACHANGIA KODI DAILY UNAPOENDA KUNUNUA BIDHAA YOYOTE DUKANI AU HUJUI MAANA YA VAT(VALUE ADDED TAX) KWANZA UNAONEKANA HUFUATILII VYOMBO VYA HABARI HUJUI YALIYOTOKEA CHUO HV MAJUZI NENDA KAMUULIZE MUKANDALA MAANA NI BOGA MWENZAKO YANI WE UNGEKUWEPO CHUO 2NGEKUITA SHOGA AU 2NGEKUCHOMA MOTO HAPA MABIBO WE HUTAKI MABADILIKO UNAKUA CONSERVATIVE DAILY UNACHOLINDA NINI SASA?PONGO KWELI WEWE FANYA BADILIKO FASTA KM WENZAKO WA KENYA UKIWAONA NAO WA KINA ZITO WANABORONGA WATOE NAO WARUDISHE CCM SASA KAMA HA2WAPI NAFASI TUTAJUAJE KAMA NI WABAYA KICHWA CHAKO KAMA CHA KARUNGUYEYE WEWE.BE DYNAMIC ALWAYS

na MDERE, UDSM.B.COM, - 26.05.08 @ 13:00 | #13379

Pole sana Mdere, kumbe unasoma B com, mwombe anayesoma sanaa akusaidia Mdere. Ingekuwa mtoto ningekwambia hujajua kujisafisha ukitoka kujisaidia. Samahani wasomaji, ninamlazimisha Mdere aelewe hoja yangu, naomba umpe nafasi Zitto aje kujibu hoja yangu.

Inaonekana hiyo B. COM inakuharibu unafikri katika mstari uliyonyooka.
Kwa ufipi ni Zitto na wapinzani lazima waende vijijini, watake wasitake ili kupata wanachama na kufundisha demokrasia. Jamani Mdere hii inahitaji digrii kuelewa, usiaibishe kisomo cha UDSM Bwana. Zitto msaidie huyu kijana hanielewi kabisa

na ki, mn, - 26.05.08 @ 13:14 | #13383

We, Mdere na ki,mn mnagombania nini? Zitto ni mwanaume, sielewi kwa upande wenu, kama huridhii hoja ya mwenzio basi kaa kimya manake naye amechangia kwa upeo wake. Mume mmoja wake wengi hiyo inakubalika. Nawe Zitto watimizie haja yao walioko jirani yako kama jinsia ni tofauti. Zitto upo? Mi sikupendi.

na Kisima, Mza-Tz, - 26.05.08 @ 13:32 | #13387

we wewe unayejiita kaka hujui usemalo nafikiri ni mmojawapo wa watoto wa mafisadi unaona ccm ndo baba na mama,lakini hufikirii hii nchi inavyoliwa,nchi itaingiaje kwenye matata wakati ndo wigo wa demokrasia unapanuka?wazazi wako wakiishakudanganya ya kuwa vyama vingi vinaleta machafuko na wewe mbichwa unavimba bila ya uchambuzi makini,shauri yako.

na john, Tz, - 26.05.08 @ 13:33 | #13388

WANASOMA SIASA KAWATAFUTE WEWE UWAELIMISHE ILI WATAKAPOMALIZA HIZO DEGREE ZAO WAKAWAELIMISHE NDUGU ZAO HUKO VIJIJINI WAPATE MAENDELEO.SAWA CKATAI KUA WAPINZANI LAZIMA WAENDE RURAL AREAS LAKINI KAMA2 WEWE UPO MJINI UMEPATA ELIMU KIDOGO KWA IMANI HUTAKI MABADILIKO UNADHANI HAO WA VIJIJINI WATAWEZA KUBADILIKA,EMBU KUA MWANA MAGEUZI BWANA WATANZANIA WENZETU KULE VIJIJINI WAPATE MAENDELEO WAJIONE KAMA NAO WAPO DUNIANI NA WAIFURAHIE TANZANIA YAO.JUA KWAMBA HK MJINI 2LIPO HAKUNA SHIDA,SHIDA ZIPO VIJIJNI EEE BWANA BADILIKA.NADHANI UMENIPATA NA UMENIELEWA.SHWAAAAAAAAARI

na MDERE, UDSM .B.COM, - 26.05.08 @ 13:36 | #13389

nampongeza sana mh.Zitto kwa kazi nzuri anayofanya ya kutetea wananchi wote kama alivyotumwa kikamilifu. wazo la kuwasilishwa mswada huo pamoja na marekebisho ya sheria za uchaguzi ni mzuri na nitaomba wananchi wote wamuunge mkono ili demokrsia iweze kushamiri vizuri zaidi hapa nchini. Mungu akulinde na akuongoze vema zaidi Zitto na wote wenye mapenzi mema na nchi yetu, hasa Dr.Slaa.

na Pris, Dodoma/tanzania, - 26.05.08 @ 13:44 | #13391

nampongeza sana mh.Zitto kwa kazi nzuri anayofanya ya kutetea wananchi wote kama alivyotumwa kikamilifu. wazo la kuwasilishwa mswada huo pamoja na marekebisho ya sheria za uchaguzi ni mzuri na nitaomba wananchi wote wamuunge mkono ili demokrsia iweze kushamiri vizuri zaidi hapa nchini. Mungu akulinde na akuongoze vema zaidi Zitto na wote wenye mapenzi mema na nchi yetu, hasa Dr.Slaa.

na Pris, Dodoma/tanzania, - 26.05.08 @ 13:44 | #13392

Wewe kisima hapa tunaongelea maslahi ya nchi. Wapinzani waende vijijini kupata wanachama, wewe unaleta vitu vya ajabu.

Wewe Kisima Na. #13387 afadhari umejisema mwenyewe unapakuliwa na wanaume ndio maana ya jina lako. Ningekuwa kijana mdogo ningekutukana ningekwambia jina lako ni kisima, kwenye a ya kisima nikaondoa naweka i, hili ndilo jina lako. Na ndio unaishi kwa jina lako hilo. Hapa tunatoa hoja wewe unatukana? Moderator umemwona huyo mwenye jina lenye mwelekeo wa jinsia ya kike?. Si unaona jina lake limekaa kihasara hasara?

Ho

na ki, tu, - 26.05.08 @ 13:47 | #13393

Wewe kisima hapa tunaongelea maslahi ya nchi. Wapinzani waende vijijini kupata wanachama, wewe unaleta vitu vya ajabu.

Wewe Kisima Na. #13387 afadhari umejisema mwenyewe unapakuliwa na wanaume ndio maana ya jina lako. Ningekuwa kijana mdogo ningekutukana ningekwambia jina lako ni kisima, kwenye a ya kisima nikaondoa naweka i, hili ndilo jina lako. Na ndio unaishi kwa jina lako hilo. Hapa tunatoa hoja wewe unatukana? Moderator umemwona huyo mwenye jina lenye mwelekeo wa jinsia ya kike?. Si unaona jina lake limekaa kihasara hasara?

na ki, mn, - 26.05.08 @ 13:51 | #13395

Mimi nadhani sasa umefika wakati tubadili katiba ili wabunge wawe wanaishi katika majimbo yao ya uchaguzi ili wawafanyie kazi wananchi waliowachagua badala ya sasa hivi. Tatitizo letu wananchi ni usimamizi mbaya wa pesa za maendeleo, matumizi mabaya ya madaraka kwa wafanyakazi wa serikali na kukosekana uhamasishaji wa kutosha ili kuleta maendeleo kulingana na rasilimali zilizopo eneo husika. Kwa kuwa wabunge tumewaajiri kwa kazi ya kuhakikisha maendeleo ya wananchi yanapatikana kwa kufanya yote niliyoeleza hapo juu na siyo kwenda ******* na kupiga miayo tu bungeni, nadhani sasa umefika wakati wa kuwalizimisha kuwepo kwenye vituo vyao vya kazi (majimboni) muda wote.Hivi inakuwaje muajiriwa anamua lini aende ofisini na akafanye nini kwa muuajiri wake (wananchi), hivi ni wapi mmeona mtu analipwa pesa nyingi kama za ubunge halafu afanye kazi kama wanavyofanya wabunge kupitia magazeti, redio na TV? mfano mzuri mmeona wakati wafanyakazi wanadai nyongeza ya mishahara mipya (80,000)kwani baadhi ya waajiri waliongeza muda wa kufanya kazi ili kuleta tija. Hawa jamaa wanafanan, wawe upinzani au watawala mara nyingi wanajali maslahi yao binafsi, vyama vyao na kuwasahau wananchi. Ni kweli katiba ibadilishwe baadhi ya maeneo ili kuleta mageuzi katika shughuli za wabunge na siyo kujaza watu ambao kwangu mimi naona hawana faida yeyote.Ubunge ni kazi inayolipa sana kuliko hata uhadhiri chuo kikuu hivyo wananchi pia tupime kazi wanazofanya wabunge ofisini kwao (majimboni) badala ya kuwashabikia kwani tumeshawashabikia sana tangu nchi ipate uhuru mtpaka leo bado hamna kasi ya maana. Nionavyo mimi ni lazima tuwape masharti wabunge wetu kama wanataka kazi na siyo kuwaachia watulishe uppuzi wao ili waendelee kubaki madarakani huku wananchi tunaatabika.

na Kibera, tanzania, - 26.05.08 @ 14:00 | #13401

Mtake msitake Zitto lazima aende vijijini ili tuwapate wenzetu wanaohongwa khanga na kofia,na kuuza kadi za kupigia kura kwa shs 2000/= tu toka kwa wakala wa ccm.Bila kuelimishwa hata Zitto aseme na afanye nini ni bure.
MSIPINGE.
Nilisha sema kila mmoja wetu awe na jukumu kuhakikisha baba yake,mama yake,kaka nk wote wasiwape kura hii mijitu mifisadi ya kutupwa.Nyinyi ndio mnaotuangusha hamna mawasiliano na ndugu zenu vijini mmewatupa toka mliposoma mkapata kazi matokeo yake wanasubiri miaka 5 ili wapate khanga,au kofia au shs 2000/=.Tunachosema wakina Slaa na Zitto sawa waende lakini pia jukumu kubwa ni la kila mmoja wetu.

INAWEZEKANA HII MIJITU KUNGOKA KAMA MHOGO WA MASIKA.PLAY YOUR PART.

na yuli, USA, - 26.05.08 @ 14:10 | #13404

Zito kaongelea ugombea binafsi Tanzania. Hjaongelea CHADEMA wala CCM. Mbona wengine mmeanza kulambania vyama? Vimeingiaje kwenye hoja hii?

na Bernard Mukasa, Sumbawanga, - 26.05.08 @ 14:17 | #13406

Sultan Mosi wa Pemba #13373 mawazo yako ni sawa lakini umemalizia vibaya. Hakuna shule ya urais wala uwaziri, lakini elimu ni muhimu ikifuatana na hekima na busara. Obama kasomea sheria Harvard. Wenzake waliodharau elimu, nusu wako jela kwa wizi na uhalifu. Tuchague viongozi wenye elimu nzuri pamoja na hekima na busara.

na J. Bendera., Hamburg, Germany., - 26.05.08 @ 14:18 | #13407

Sasa wale ambao walikuwa hawanielewi angalieni wenye akili zao zimetulia na kuchambua mambo. Bravo Kibera, Congratulation Yuli. Ninyi vichwa. Wengine kusema bila concentration na kuelewa. Ukweli ni kwamba hata kama bado katiba itakuwa haijaweka vizuri, tunapopambana na wanyonyaji katika nchi lazima tuwalazimishe wapinzani waende vijijini. Tuwazomee wasipoenda vijijini.

Anayetoka kijijini kutupatia taarifa amevuna wanachama wangapi ndiye tumpigie makofi. Ukweli ni kwamba hatutaki ya Kiteto yarudie, wakati ni sasa wapinzani waende vijijini, wasiranderande mijini, kura ni vijijiji.

Hongera tena yuli wa USA na Kibera kwa kunielewa. Zitto na wenzeke, kiguu na njia kijijini kuelimisha demokrasia na kuvuna wanachama, hamna chaguo. Sisi wana demokrasia hatutawapigia makofi mijini, labda mnapoleta taarifa za vijiji mlivyotembelea na kutuambia bado vingapi na mmepata wanachama wangapi

na ki, mn, - 26.05.08 @ 14:23 | #13408

Mimi naona badala ya kujadili ccm,Chadema na kumsifu Kabwe tukae na kujadili nini faida na hasara ya wagomnea binafsi.

Kabwe Zitto yaonekana ktk barua yake yeye ameeleza ktk mazingira kuwa inatoa uhuru na haki kwa baadhi ya Watanzania kugombea.

Lakini mimi naona iko hasara na faida zaidi ya hili lililoelezwa na kabwe na yeye hajabainisha hasara zake.

Wadau naomba tuchangie.

na Joram Kiango, DSM/Tanzania, - 26.05.08 @ 14:26 | #13410

Huku usukumani tuna msemo usemao,KUSIKIA KWA ***** HADI DAMU ITOKE MASIKIONI.Sasa Watanzania ni kama ***** hawasikii hadiCCM ianze kukamata watu na ku-wauza nje ndo watajua hili li chama halina nia ya kutupatia maisha bora. Jukumu la kuelimisha watu wa vijijini sio la vyama vya upinzani ni la serikali,itoe elimu ya uraia.Leo hii huko vijijini kuna watu bado wanajua rais ni Nyerere.

na kakaa, mwanza, - 26.05.08 @ 15:03 | #13412

Natoa changamoto (Public Lecture ya bure bila malipo) kwa vyombo vya habari vya Tz, viwe kila siku vinatoa majina ya viongozi wote wa siasa hasa wale wa ngazi za juu kila siku wako wapi na wanafanya nini. Mwisho wa mwezi wanatoa analysis akina nani walienda vijijini nani hawakwenda. Nashangaa hawa wabunifu wa jamii forum hawajagundua njia hii ya kulazimisha wapinzani waende vijijini kufundisha demokrasia.

Sasa mimi leo nawapa Lecture waandishi wote wa habari wa Tz, pamoja na Jamii forum. Kuanzia wiki kesho nitaangalia walioelewa somo langu. Yaani andaeni scheme (a table)ya viongozi wakuu wa vyama vya upinzani - Mwenyekiti, Makatibu, Waenezi, n.k. Inaonesha jina, chama, wadhifa, yupi wapi, amefanya nini kila siku. Mwisho wa mwezi au kila baada ya wiki mbili tunaona akina nani walienda vijijini kufundisha demokrasia na akina nani walikuwa wanarandaranda mijini. Walioenda vijijini wakirudi kutupa taarifa - wamepta wanachama wangapi tunawapongeza. Wale ambao wanarandaranda na kuuza sura tunawazomea ili nao wafanye vizuri. Mmenielewa wanafunzi wangu, jamii forum na waandishi wote wa habari mpo? Aliye nielewa ajitokeze asemi sisi hapa tutatekelza mpo. Wengine tumekosa tu nafasi za kuongoza lakini we kichwa moto- Ona darasa hilo na uone watakavyochapa kazi.


Rafiki Joram Kiango unataka kusema wagombea binafsi watapokea pesa za shetani. Of course inawezekana, lakini inawekwa tu misingi- kwamba source za kugombea zinakuwa zinachangwa kama wanavyochangiwa akina Obama.

Wagombea binafsi watalazimisha vyama kuchagua watu watakatifu, wasio mafisadi. Hata wagombea wa vyama bado wananunuliwa na wafanya biashara hasa waasia. Halafu wanawatumia kama remote, wao kutenda maelekezo wanapata kwa wale waliowanunua. Kuanzia uchaguzi unaokuja kila chama kitoe hesabu ya pesa inazozitumia na iseme imezipata wapi. Vilevile kwa wagombea binafsi. Jamani hamnipigii tu makofi, au mna wivu. Mie sina unchoyo- lecture bila malipo- kwa heri.

?

na ki, mn, - 26.05.08 @ 15:06 | #13413

Pamoja na kukupongeza Mhe. Zitto kwa hatua hii nuzi, pia ni wakati muafaka serikali ikafahamu kuwa ni haki ya kila Mtanzania kugombea ili kuchaguliwa si lazima kupitia kwenye Chama chochote.

Kila la kheri.

na Hillary N. Mkony, Tanzania, - 26.05.08 @ 15:08 | #13414

WANAOAMBIWA WAKUBALI KUAMBIWA,WAO HAWAJUI KUWA HAWAJUI. LAKINI SI HIVYO NI WAJINGA.

na KINYA, ZENJI, - 26.05.08 @ 15:29 | #13416

NAKUBALIANA NA WATOA MAONI WAKISISITIZA VIONGOZI WA UPINZANI KWENDA VIJIJINI SIO KUWA "OPPORTUNISTS" KWA KASORO ZILIZOPO.
TANZANIA TUNAYO BAHATI YA KUJIFUNZA TOKA NCHI JIRANI AMBAZO VYAMA VYA UPINZANI VIMECHUKUA MADARAKA, MFANO: ZAMBIA, NA KENYA. NI NCHI PEKEE ZA KIAFRIKA AMBAZO TAYARI VYAMA VYA UPINZANI VIMESHINDA. NA TUMEONA MATOKEO YAKE? SABABU YA WANANCHI KUKOSA KUANDALIWA TANGU NGAZI ZA MASHAMBANI, MAMBO YANABAKI VILE VILE. ANAYESHINDA ANAJIKUTA ANASAIDIANA NA VIONGOZI WALE WALE WALIOKUWA NA KASHFA ZA UFISADI. MFANO: UNAAMINI KWAMBA PR. SAITOTI ALIHUSISHWA NA KASHFA TANGU UTAWALA WA MOI. HALAFU UPINZANI UKAMKUMBATIA TENA!
SAFARI NI NDEFU!!
CCM ITAENDELEA KUSHINDA. SUBIRI IWAWAJIBISHE MAFISADI HIVI KARIBUNI.

na Askari wa mwavuli - 26.05.08 @ 15:38 | #13417

Huyu Ki ni ****** kweli kweli. Mwanzoni alipokuwa anamlazimisha Mdere na Mwandamizi wakubaliane na mawazo yake nilidhani anazo, kumbe hakuna kitu ndani ya kichwa!Angalia alichoandika kwenye maoni #13413 hiyo ndiyo busara yake.Yaani watu wengine bwana, analzimisha watu wakubali upuuzi wake kwa kujaribu kuonyesha kuwa ni hoja ya msingi kumbe amejaa pumba tupu.
Huyu ki nimegundua kuwa ndiye anayeuza sura hapa kwenye mtandao.Lakini asife moyo aendelee kuwasoma wenye vichwa vilivyotulia siku moja nayeye ataweza kutoa maoni yenye akili.

na Peter Pierre, tz, - 26.05.08 @ 16:08 | #13421

We piere hujui kitu. Wenye akili wameshapata ujumbe utaona utakavyofanyiwa kazi. Maelezo mengine ilikuwa ni staili ya presentation ili msomaji asichoke kwa sababu niliandika mengi.

Kama unadhani ninaongea utani kasome jamii forum utaona wameanzisha thread, wanalalamika kuwa vyama vya upinzani ni wazembe hawaendi vijijiji. Kwa hiyo hapa nimetoa mbinu za kuwalazimisha wapinzani waende vijijini. Ninarudia kila siku orodha, Mbowe, Slaa, Lipumba, sijui Mwenezi, jina la chama, yupi wapi, anafanya nini. Wanaoleta ripoti ya kuvuna wanachama tunawapongeza. Wanaorandaranda mijiji tunawazomea hadi wakatuletee taarifa, wamavuna wanachama wangapi, na bado vijiji vingapi. Mwisho wa mwezi tunatangaza wazembe na wawajibikaji wa kufundisha Demokrasia vijijiji.

Tatizo lako piere, badala ya kusoma ujumbe umeangalia namna nilivyokuwa siwachoshi. Unakumbuka staili ya hotaba za Nyerere, utani wa kutosha kwenye hotaba watu, hawachoki. Ila usiseme najilinganisha na Nyerere ile namba Nyingine.

Jamani vyombo vya habari, jamii forum kazi kwenu. front page kila siku summary za viongozi wa upinzani, wameende vijiji gani. Ngoja nikwambie Piere, mbinu hii wataichukia viongozi wa upinzani wazembe kama walivyosema jamii forum. Ila sasa tunawasimamia kwa kuwawekea summary kila siku.

Zitto akileta akitoka Sumbawanga huko ndani akituambia nimepata wanachama 10,000. Tunasukuma gari lake. Akiuza sura mjini tunamwambia data inasema wewe mzembe katuletee kwanza wanachama. Mmesikia wanahabari, from page summary viongozi wapinzani wanafanya nini. Tuone kama hawatafanya kazi na kama wanachama hawatapta. Hatutaki ya Kiteto yarudie, huwezi kupata kura kwa kutalii wakati wa uchaguzi tu. LAZIMA wapinzani tuwafundishe namna ya kufanya kazi. Wameshindwa kufanya kazi bila kusukumwa, sasa tunawalazimisha kufanya kazi. Naomba wanahabari fanyeni hilo kuanzia wiki kesho. Kazi kwao wazembe, wataona cha moto, data kila mwezi au kila baada ya wiki mbili

na ki, tu, - 26.05.08 @ 16:43 | #13425

We piere hujui kitu. Wenye akili wameshapata ujumbe utaona utakavyofanyiwa kazi. Maelezo mengine ilikuwa ni staili ya presentation ili msomaji asichoke kwa sababu niliandika mengi.

Kama unadhani ninaongea utani kasome jamii forum utaona wameanzisha thread, wanalalamika kuwa vyama vya upinzani ni wazembe hawaendi vijijiji. Kwa hiyo hapa nimetoa mbinu za kuwalazimisha wapinzani waende vijijini. Ninarudia kila siku orodha, Mbowe, Slaa, Lipumba, sijui Mwenezi, jina la chama, yupi wapi, anafanya nini. Wanaoleta ripoti ya kuvuna wanachama tunawapongeza. Wanaorandaranda mijiji tunawazomea hadi wakatuletee taarifa, wamavuna wanachama wangapi, na bado vijiji vingapi. Mwisho wa mwezi tunatangaza wazembe na wawajibikaji wa kufundisha Demokrasia vijijiji.

Tatizo lako piere, badala ya kusoma ujumbe umeangalia namna nilivyokuwa siwachoshi. Unakumbuka staili ya hotaba za Nyerere, utani wa kutosha kwenye hotaba watu, hawachoki. Ila usiseme najilinganisha na Nyerere ile namba Nyingine.

Jamani vyombo vya habari, jamii forum kazi kwenu. front page kila siku summary za viongozi wa upinzani, wameende vijiji gani. Ngoja nikwambie Piere, mbinu hii wataichukia viongozi wa upinzani wazembe kama walivyosema jamii forum. Ila sasa tunawasimamia kwa kuwawekea summary kila siku.

Zitto akileta akitoka Sumbawanga huko ndani akituambia nimepata wanachama 10,000. Tunasukuma gari lake. Akiuza sura mjini tunamwambia data inasema wewe mzembe katuletee kwanza wanachama. Mmesikia wanahabari, from page summary viongozi wapinzani wanafanya nini. Tuone kama hawatafanya kazi na kama wanachama hawatapta. Hatutaki ya Kiteto yarudie, huwezi kupata kura kwa kutalii wakati wa uchaguzi tu. LAZIMA wapinzani tuwafundishe namna ya kufanya kazi. Wameshindwa kufanya kazi bila kusukumwa, sasa tunawalazimisha kufanya kazi. Naomba wanahabari fanyeni hilo kuanzia wiki kesho. Kazi kwao wazembe, wataona cha moto, data kila mwezi au kila baada ya wiki mbili

na ki, mn, - 26.05.08 @ 16:51 | #13426

HONGERA SANA ZITO KWA KUWA NA MAWAZO AMBAYO NI WABUNGE WACHACHE WENYE AKILI HIYO

MABADILIKO YA KATIBA NI JAMBO AMBALO KWA MTANZANIA MWENYE KUELEWA NA KUSOMA ALAMA ZANYAKATI ATAONA NI JAMBO LA BUSARA.

SASA NDUGU YANGU ZITO MOTO UMESHAUANZISHA ENDELEA NAO TAFUTA WADAU PITA MTAA HADI MTAA UKILIONGELEA HILI KAMA MLIVYOFANYA KATIKA KUWAFUNGUA WANANCHI MASWALA YA UFISADI, TUKO NYUMA YAKO.

SASA IMEFIKA WAKATI WATZD KUELEWA KUWA HATUKO TENA KATIKA UTAWALA WA CHAMA KIMOJA TUNACHOTAKA NI UKWELI NA UWAZI KATIKA SERIKALI NA SERIKALI INAYOWAJALI MASIKINI SIO SERIKALI INAYOJALI WEZI WA FEDHA NA KODI ZA WANANCHI.

WATU WALISEMA CCM NI CHAMA CHA MAJAMBAZI

WENGINE WALISEMA CCM NI CHAMA CHA MAFIA

SASA TUNAONA KUWA WAMEZAA JINA JIPYA AMBALO NI CHAMA CHA MAFISADI

HAYA SISI HATUYATAKI

TUNATAKA KUONA KILA MTANZANIA ANAFAIDI MATUNDA YA NCHI YAKE NA SI WACHACHE.

HIVI KWELI UNAMTEUA ZAKHIA MEGHI UNAMPA UWAZIRI WA FEDHA ANAHARIBU NA HATA YALE AMBAYO YALIKUWA MACHACHE MAZURI HALAFU ANAZUNGUMZA KAMA VILE CHEREKO KUTETEA UCHAFU WAKE.

KATIBA IBADILISHWE NA RAISI AWE NA UWANJA MPANA WA KUTEUA HAWA WASHAURI WAKE.

ZITO KOMAAA KAKA WEWE NI NGUZO CHANGA LAKINI KUWA MACHO NA MAFIA AU MAFISADI

NB

AMINA CHIFUPA ALIKUFA KIFO CHA UTATA

MORINGE SOKOINE NAYE ALIPITIA NJIA HIYO HIYO YA UTATA

KOLIMBA HORRACE BILA KUULIZA

BALLAL DAUDI NAYE KIFO CHAKE NI UTATA UMZITO

KOMBE JENERAL HADI SASA TUNAJUA SERIKALI INAHUSIKA KIFO CHAKE MWULIZE MREMA AGUSTINA ATAKUPA STORY

SASA ZITO NDUGU YANGU KAZA BUTI TUKO NYUMA YAKO AMSHA HAPO JUUU SIO KWAMBA NAKUTISHA HUO NDIO UANAUME.

BONGO WAKIONA UNATAKA KUSHIKA MASILAHI YAO WANAKUPA KUBWA KAMA NDUGU ZETU HAPO JUUU



na MTANZANIA HALISI, TANZANIA, - 26.05.08 @ 16:57 | #13428

HONGERA SANA ZITO KWA KUWA NA MAWAZO AMBAYO NI WABUNGE WACHACHE WENYE AKILI HIYO

MABADILIKO YA KATIBA NI JAMBO AMBALO KWA MTANZANIA MWENYE KUELEWA NA KUSOMA ALAMA ZANYAKATI ATAONA NI JAMBO LA BUSARA.

SASA NDUGU YANGU ZITO MOTO UMESHAUANZISHA ENDELEA NAO TAFUTA WADAU PITA MTAA HADI MTAA UKILIONGELEA HILI KAMA MLIVYOFANYA KATIKA KUWAFUNGUA WANANCHI MASWALA YA UFISADI, TUKO NYUMA YAKO.

SASA IMEFIKA WAKATI WATZD KUELEWA KUWA HATUKO TENA KATIKA UTAWALA WA CHAMA KIMOJA TUNACHOTAKA NI UKWELI NA UWAZI KATIKA SERIKALI NA SERIKALI INAYOWAJALI MASIKINI SIO SERIKALI INAYOJALI WEZI WA FEDHA NA KODI ZA WANANCHI.

WATU WALISEMA CCM NI CHAMA CHA MAJAMBAZI

WENGINE WALISEMA CCM NI CHAMA CHA MAFIA

SASA TUNAONA KUWA WAMEZAA JINA JIPYA AMBALO NI CHAMA CHA MAFISADI

HAYA SISI HATUYATAKI

TUNATAKA KUONA KILA MTANZANIA ANAFAIDI MATUNDA YA NCHI YAKE NA SI WACHACHE.

HIVI KWELI UNAMTEUA ZAKHIA MEGHI UNAMPA UWAZIRI WA FEDHA ANAHARIBU NA HATA YALE AMBAYO YALIKUWA MACHACHE MAZURI HALAFU ANAZUNGUMZA KAMA VILE CHEREKO KUTETEA UCHAFU WAKE.

KATIBA IBADILISHWE NA RAISI AWE NA UWANJA MPANA WA KUTEUA HAWA WASHAURI WAKE.

ZITO KOMAAA KAKA WEWE NI NGUZO CHANGA LAKINI KUWA MACHO NA MAFIA AU MAFISADI

NB

AMINA CHIFUPA ALIKUFA KIFO CHA UTATA

MORINGE SOKOINE NAYE ALIPITIA NJIA HIYO HIYO YA UTATA

KOLIMBA HORRACE BILA KUULIZA

BALLAL DAUDI NAYE KIFO CHAKE NI UTATA UMZITO

KOMBE JENERAL HADI SASA TUNAJUA SERIKALI INAHUSIKA KIFO CHAKE MWULIZE MREMA AGUSTINA ATAKUPA STORY

SASA ZITO NDUGU YANGU KAZA BUTI TUKO NYUMA YAKO AMSHA HAPO JUUU SIO KWAMBA NAKUTISHA HUO NDIO UANAUME.

BONGO WAKIONA UNATAKA KUSHIKA MASILAHI YAO WANAKUPA KUBWA KAMA NDUGU ZETU HAPO JUUU



na MTANZANIA HALISI, TANZANIA, - 26.05.08 @ 16:57 | #13429

Vijana naona sasa mnakiuka maadili ya gazeti.Mtandao unasomwa dunia nzima .Mjaribu kutueleza yaliyo ya busara.Hoja ziwekwe katika hali ya kusomeka kwa maelewano ,na si maneno ya tafsiri ya ******.Hoja ni jinsi gani vyama vinaweza kuungwa mkono na watu wengi, ili viweze kushindana na CCM.tunajua katika vyama kuna mambo mengi.Hata kikichaguliwa chama chochote ,kula ni lazima.Kwasababu Wote wanaoingia kwenye vyama ,ni watu waliyo na mawazo tofauti .Kunawanaotaka uongozi kwa faida .Na kuna wale wenye uzalendo na uchungu na nchi.Hawa kuwafahamu ni vigumu.Kuwepo mgombea binafsi ,hili i gumu.Ukweli ni kuwa tuimarishe vyama.Na viwe vichache,Wahusika waende mpaka vijijini wazungumze,Nini watawafanyia wananchi.Kisha wananchi waamue.Wagombea wafahamike,naona hili litasaidia watu kuelewa makosa ya chama tawala .Lakini uchaguzi uanapofika, eti ndio watu wanachangamka kuwaburuza watu , huyu ndiye mgombea wa chama fulani.Wananchi lazima wataona ni danganya toto.Naungana na mwandishi anaesisitiza kuwa vyama pinzani,viende vijijini vikajinadi ,wananchi wawaelewe.Kwa hivi sasa lazima watawaunga mkono.Mambo ya kuwepo vyama mjini ndiyo sababu chama tawala kinawasambaratisha wapinzani,kwakutojieleza kwa wananchi.

na mtzmwenyeuchunngu, tz, - 26.05.08 @ 17:52 | #13435

Watanzania tutaongea sana lkn ni wazi kua tunataka si mabadiliko tu ya maneno kwenye TV na magazeti bali mabadiliko kivitendo hasa vijijini.Nini cha kufanya [1]kura ya maoni i.e tuamue ni constitution ipi tunataka,kwani hii iliyopo inawapa favor kubwa CCM,kama tuonavyo ZNZ mtu akishinda hata zaidi ya kura 1 yeye ndio anaunda serikali,hata kichaa ataona kuna walakini.
[2]Tume huru ya uchaguzi inayokubalika na wote.[3]watanzania tuache uvivu,rushwa,kuombaomba mpaka mosquito nets,tuwe waaminifu,tufanye kazi kwa ajili ya kizaji kipya"next generations,kwani tusitegemea kujenga Hong Kong au Rome kwa 5 years.Tunapenda maisha ya kifahari kuliko wanaotupa misaada.
[4]wandishi tuongelee zaidi kupanda na kushuka kwa uchumu,education,science n,k.kwani politics haitufikishi mbali,Tusipende kujikuza kupitia newspapers.Watz pamoja na JK kuungwa mkono ati ni hodari wa kuomba misaada nje lkn hakuna cha bure,Mnajua misada hulipwa?mnajua kua hakuna nchi iliyo wahi kwenda mbele hata kwa hatua 1 kwa ajili ya misaada.TENA ikumbukwe Tanzania ni nchi inayoongoza kwa kuombaomba,kupewa misaada,the same time ni nchi inayoongoza duniani kwa kula misaada.Ni nchi inayoongoza kwa kutafuta wawekezaji,ni nchi inayoongoza kwa wawekezaji kutajirika kuliko walivyokua hawatarajii.muhimu tu uwe colored na usijui kuongea kiswahili.

na window XP, P.R,CHINA, - 26.05.08 @ 18:08 | #13436

Window wa China unamaana ili mradi tu uongee kama Ponjoro, utaikamua Tanzania kama wanavyoikamua maponjoro wa Tz wenye uraia wa UK, Canada, Marekani na Iran. Halafu wanataka uraia wa nchi nyingi ili watuzike kabisa watanzania, yaani tubakie tu kwenda Jahanamu.

na in, p, - 26.05.08 @ 18:38 | #13440

Kwa watu waliokombolewa na kukomaa kifikra, watu wanaoweza kusema ndio katika ndio, au hapana katika hapana, mawazo kama haya ndiyo yanakuwa yanaeleweka. Wapo watu wanaotumia safu hii kuponda Vyama badala ya kutafuta ukweli na kutumia safu hii kutoa maoni ya kuelimisha jamii. Binafsi naona Hoja ya Zitto ni ya msingi sana lakini inaeleweka kwa wenye akili timamu, wanaoona nchi yetu inavyoenda. Wala hawapendi kujipendekeza kwa CCM ili kutafuta maslahi binafsi bali wanasema hivyo kwa manufaaa ya jamii ya watanzania kama anavyofanya Zitto. Zitto usiogope we endelea na vijijini tutakusaidia unafahamika kwanza kuliko Rais mwenyewe.

na Isango, Singida, - 26.05.08 @ 20:47 | #13447

Namshukuru Bw ZITO kwa hoja yake nzuri,ingependeza serikali ifike mahali ikubaliane na mawazo yanayojenga ikiwa ni kwa maslahi ya nchi.Huwa nasoma sana magazeti ya nyumbani na nafurahi kuona changamoto hizo.KILA LA KHERI.

na Uronu Mmbasha, North carolina Moyok USA., - 27.05.08 @ 04:00 | #13455

Kwanza nashauri kwa wachangiaji wa hii tovuti...ACHENI ****** NA KULUMBANA BILA SABABU CHANGIA HOJA!
Hongera Mchungaji Mtikila kwa kuanzisha hoja ya mgombea binafsi pale mjini Dodoma miaka michache iliyopita. Hii ni hoja ya msingi kwani KATIBA imetamka bayana haja ya kuwa na mgombea binafsi.Mawazo ya Kijana Zitto nayo ni mazuri sana. Wito wangu kwa wanaharakati:Mabadiriko yoyote ya Katiba na Sheria zake ni vizuri yakafanyika kwa kutazama historia ya nchi yetu, lakini pia MASLAHI ya TAIFA. Kukua kwa Democrasia peke yake bila uzalendo na uadilifu wa dhati kwa nchi ni sawa na zero. Angalia mfano wa nchi za mashariki ya Asia (east Asian tigers)zimepiga hatua sana kiuchumi; Wala hazikuwa na Democrasia bali uzalendo wa hali ya juu wa viongozi,watumishi na wananchi kwa ujumla. Nchi hizo zipo kwenye kundi la Developmental State na si Democratic State. Ni kweli kwamba Democrasia ni nzuri kwa maendeleo ya Taifa kwani inahusisha ushirikishwaji wa jamii katika kila shughuli (siasa, uchumi nk)LAKINI pia ikumbukwe kuwa Democrasia ni sehemu ya UTANDAWAZI ambapo kwa nchi changa kama TZ ambayo sayansi na technolojia vimepita mbali hatufaidiki na chochote ila kuendelea KUPORWA rasilimali zetu (madini,sekta ya fedha na biashara nk). Kwa sababu hiyo ndiyo maana viongozi wa nchi kama Taiwani na South Korea walikata democrasia na kujichagulia muundo wao wa utawala ...Developmental State!
Sisemi kwamba Democrasia ni mbaya katika kuleta maendeleo ya nchi changa kama TZ: Bali uangalifu MKUBWA unatakiwa katika kufanya mabadiliko ya Katiba na Sheria zetu. Kikubwa ni UZALENDO & UADIRIFU kwa NCHI na JAMII tuache undugunisation katika kazi! Achaguliwe mtumishi mwenye SIFA na UWEZO badala ya patronage and clientele! Tabia kubwa iliyojengeka miongoni mwetu ni kutaka kufaidika (binafsi) kwanza kabla ya kuzalisha. Watu wanageuza mali za umma kuwa binafsi! Katika mazingira kama hayo hapo juu unatarajia democrasia itafanya nini kubalisha maisha ya Mtanzania? Kumbuka mashirika ya umma yalikufa kutokana na Umimi na Undugunisation, na hivyo ndivyo hali ya nchi hii ilivyo sasa!Pitapita huko maaofisini (wizarani, kwenye taasisi mbalimbali za serikali, ofisi za mikoa au halmashauri za wilaya/miji/municipal)utaona jinsi watu walivyojiinga kiundugu ndugu na kufanya kazi kiundugu!
JAMII tuache woga: jumuiya za dini, makundi mbali mbali ya jamii yana jukumu kubwa ktk kuchochea maendeleo na kubadilisha mfumo wa siasa wa nchi. Hebu angalia ni Watz wangapi waliojitokeza kupambana na ufisadi! ni wachache sana! Inakuwaje raia wa UK waandamane kwa ajili yetu wakati sisi wenyewe tukiwa TUNASHANGAA SHANGAA kana kwamba HATUPO! Kwani hili Taifa ni la Dr. Slaa peke na hao wachache wenzake?
Mwisho Democrasia peke yake haiwezi kubalisha chochote kwa jinsi tabia na mfumo wa utawala ulivyo sasa TZ.Mabadiliko ya Katiba na Sheria za Uchaguzi ni mazuri lakini yaangalie UFANISI wa kazi na MASLAHI ya TAIFA!
Tuchape kazi kwa bidii!

na Donald, Australia, - 27.05.08 @ 06:20 | #13459

Donald umesema ukweli, watanzania watu wa maneno na kulaumu tu. Zito katoa hoja ya wagombea binafsi, angalia maoni ya wengi hapo juu. Wabongo tuache porojo za mitaani, hazitufikishi popote, hata hao wagombea binafsi wakija, kama mtindo wenyewe ukiendelea hivi tutaendelea kuwa maskini milele na kuendelea kuilaumu serikali kila kukicha. TUCHAPE KAZI KWA BIDII TUTAFANIKIWA.

na Dadili, Tz, - 27.05.08 @ 10:46 | #13491
Andika maoni yako:

Jina:


Barua-pepe:


Mji/Nchi:


Maoni:




Habari Mpya | Kitaifa | Dar | Mikoani | Tahariri | Makala | Michezo | Matangazo | Webmaster
Copyright 2008 © FreeMedia Ltd.
Free media limited
mtaa wa Mkwepu na Makunganya, jengo la Bilicanas, gorofa ya kwanza, SLP 15261, Dar es salaam, Tanzania
simu +255-22-2126233 • faksi +255-22-2126234 • Selula 0713 296570
MFUMO WA UCHAGUZI TULIO NAO UNAKARIBISHA UKABILA, MAJIMBO MENGINE YANKABILA MOJA TUU, KAMA MAJIMBO YA RUNGWE , NA IRINGA VIJIJINI, MTU ANAWEZA KUWA JIMBONI KWAKE KWA KISINGIZIO CHA MAJUKUMU YA UBUNGE KUMBE NI UKABILA ANAENDEKEZA,

MFUMO WA UCHAGUZI ANAOPENDEKEZA ZITO KABWE UTAONDOA KABISA DHANA YA UKABILA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom