Je, Hashim Thabit aanze maandalizi ya NBA Draft?

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,005
Nilikuwa naangalia mechi ya Connecticut leo, bahati mbaya wamefungwa 70 kwa 69. Mtanzania mwenzetu Hashim anaweza kupata kishawishi cha kwenda NBA. Kusema kweli mwaka huu ameimprove sana katika uchezaji wake ukilinganisha na mwaka jana, kwa maoni yangu arudi tena connecticut kwa mwaka mmoja mwingine kabla ya kwenda NBA katika draft ya 2009 ambayo kama kutakuwa na improvement zaidi mwaka unaokuja atakuwa katika top 5 ya draft ya 2009. Kwa wale Watanzania waliomshauri aendelee na masomo badala ya kwenda NBA nawaomba mumshauri tena, anauwezo wa kuja kuwa kama Hakeem Olajuwon wa Houston Rockets ambaye alikuwa ni tishio katika NBA. Wenzangu mnasemaje?
 
Ni kweli bwana, nilikuwa naicheck mechi, pamoja na kushindwa.....kijana anatia moyo........jina lake limepanda sana mwaka huu........si vibaya kama akiweza kuingia NBA (kitu ambacho sidhani) kama underdog na kujijenga huko huko.......otherwise aendelee tu kuonyesha vitu vyake UCONN
 
Jamaa alipo sasa hivi ni NBA or bust.Kujiandaa kwingine mbele kwa mbele.Miaka haingojei mtu na watu wengine wako geared to rise to the occassion, meaning kama hajitosi NBA anaweza kukaa UCONN miaka mia na bado asiwe tayari kwa NBA.

Nimeona mwenzake wa UCONN yupo kwenye cover la Sports Illustrated this week, they must be doing something right.
 
Mwenye picha ya wazazi wa hasheem thabit atuwekee hapa maana sio kwa kimo kile ..
 
Back
Top Bottom