Je, Harmonize alifanya uamuzi sahihi kuuza nyumba zake 3 katika harakati za kujitoa WCB? Wewe ungefanyaje?

DocJayGroup

JF-Expert Member
Jan 17, 2020
1,654
3,319
Harmonize anapambana ili aweze kuachana kabisa na WCB. Alitakiwa kulipa shs milioni 500 ili aweze kuwa msanii huria na kufanya kazi zake kama yeye mwenyewe. Jambo ambalo linamaanisha kwamba kama msanii huria, fedha yote atakayoipata katika kazi zake za sanaa itakuwa ni yake.

Alivyokuwa chini ya WCB alikuwa ni kama mwajiriwa chini ya Diamond na akawa analipwa sio kama mmiliki wa kazi ila kama mwajiriwa wa WCB. Tatizo ni kwamba kutokana na taarifa za MCL, bado hajaweza kuwa msanii huria kwa asilimia zote. Inaonekana bado hajamaliza deni la WCB. Jamaa alishauza nyumba zake pekee ili atoke WCB. Ila sasa deni inaonekana bado halijaisha. Atauza nini tena sasa? Je unavyoona wewe alifanya jambo sahihi kuuza investments zake hizo? Kama ni wewe ungefanyaje?

NB: Muziki na Sanaa ni kazi ngumu. Inahitaji fedha nyingi kufanikiwa. Inaonekana Harmonize sasa atakuwa na madeni makubwa ambayo huwa yanasababisha matatizo ya kifedha. Atapitia wakati mgumu kuwezesha record label yake ya Konde Gang kufanikiwa kwa kiasi kikubwa. Pamoja na yote, tunamuombea kwa Mungu afanikiwe kwa sababu mafanikio ya Mtz mmoja, ni mafanikio yetu wote.

Harmo.jpg
 
Nyumba tatu zilikua wapi ? Huyu msanii alikua na nyumba moja tu madale hizo mbili zilikua wapi?

Sent using Jamii Forums mobile app
Harmonize ametoa hiyo taarifa alipohojiwa na watu kadhaa including MCL, Millard Ayo etc. Nenda Youtube utaona yeye mwenyewe akitoa hio taarifa
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2020-01-18 at 2.42.42 PM.jpeg
    WhatsApp Image 2020-01-18 at 2.42.42 PM.jpeg
    57.4 KB · Views: 6
Kwani aliposaini mkataba hakuona kwamba utamnyima uhuru? Ni muhimu kufikiri sana kabla ya kufanya maamuzi hasa mambo ya mikataba
Kwani huo mkataba aliusaini lini?

Yawezekana mtu alisainishwa akiwa underground sasa hayupo huko tena Ila terms za mkataba bado zilezile na haoni uwezekano wa mkataba kupitiwa upya.
 
Hizo nyumba zilikua wapi?
Mkataba wake ungeisha lini?
Ulikua na thamani kiasi gani?
Ikiweza kuuweka hapa itakua poa sana!
Mkataba wake ulikuwa wa miaka 10 na aliusaini mwaka 2015. Kwa hio ametoka akiwa amemaliza miaka minne ya mkataba wake huo. 2019 ni miaka 4 tokea asaini mkataba huo na WCB.

Mkataba ulikuwa unamlipa kwama mwajiriwa thamani ya mapato anayoingizia WCB. Kwa hio yeye anaimba, anarekodi nyimbo, na anafanya matamasha pamoja na collabo na artists wengine. Hela anayoingizia WCB ya faida wakitoa hela wametumia katika promosheni, usafiri, na gharama nyingine, analipwa asilimia yake hio faida.
 
Kwani huo mkataba aliusaini lini?

Yawezekana mtu alisainishwa akiwa underground sasa hayupo huko tena Ila terms za mkataba bado zilezile na haoni uwezekano wa mkataba kupitiwa upya.
Mkataba wake ulikuwa wa miaka 10 na aliusaini mwaka 2015. Malipo yake yalikuwa ni asilimia ya profit anayoingizia WCB baada ya WCB kutoa hela wanayomlipa kusafiri, kuandaa matamasha, kurekodi nyimbo, kufanya music videos, kuleta wasanii wengine wafanye collabo naye n.k. Kwa sasa itabidi yeye ndio akohoe hio hela yote ya kuendeleza usanii. Kazi iko
 
DocJayGroup,

Huo mkataba ulikua na thamani ya sh ngapi? Kama katumilia miaka 4 na kabakiza 6 analipa million 500 basis. Mkataba wake ulikua na thamani zaidi ya Billion 1.

Kwa biashara gani inayofanyika kwenye music industry Tanzania mkataba use na thamani hiyo?
Kwa mkataba huo Harmonize alikua anainhizia kampuni zaidi ya 1.5bilion kwa miaka 10.

KAMBA HII AISEE
 
Kwani huo mkataba aliusaini lini?

Yawezekana mtu alisainishwa akiwa underground sasa hayupo huko tena Ila terms za mkataba bado zilezile na haoni uwezekano wa mkataba kupitiwa upya.
Jamaa anasema.mkataba kasaini 2015. Bado miaka 6 mkataba uishe anatakiwa alipe million 500 kuvunja mkataba maama yake ni kua kwa miaka 10 ya mkataba Harmonize lazima aingize WCB kama 1.5bilion kama thamani ya mkataba.
Kwa biashara gani kwenye music industry ya Tanzania?
 
Back
Top Bottom