Je, haki zipi mwajiriwa nastahili kwenye shirika la kimataifa?

kemaro

New Member
Jul 8, 2020
2
3
Mimi ni mwajiriwa kwenye shirika moja la kimataifa, hili shirika lilitoa mikataba kwa wafanyakazi , lakini moja ya vipengele havijaorodheshwa kwenye mikataba wala havipo kwenye internal regulations japo tunapewa, mfano house allowance; hela ya kujikimu mtu anapoanza kazi , n.k.

Naomba msaada wa kisheria kama kuna mtu anajua?

1. Je, mwajiriwa anapewa house allowance kwa sheria ipi kwenye mashirika ya kimataifa?

2. Je, idadi ya wiki kwenye mwezi ni ngapi kisheria? (Huyu wa kwetu anasema masaa ya kazi kwa mwezi 195 akiwa na maana anachukua 30/4=4.3 kwa hiyo mwezi una wiki 4.3 afu ndo anazidisha na 45×4.3 anapata masaa 195. Je kisheria week ina siku ngapi na kipengele kipi sheria inaelezea haya mambo.

3. Nilishafanya mashirika mengi mengi kazi , kwenye mashirika mengne ukifika unarudishiwa nauli yako , japo hapa hawarudishi ! Je yale mashirika yanatumia sheria gani kurudisha nauli za wafanyakazi wao wanapoenda kuanza kazi.

4. Kwa msaada kama kuna mtu anaweza kunisaidia international labor law na Tanzania labor law in private sector /international organization zinazooperate ndani ya Tanzania zinatumia sheria gani.

Natanguliza shukurani zangu
 
Back
Top Bottom