Je habari hizi hazihatarishi usalama wa taifa?

Gamba la Nyoka mkuu heshima mbele. Ninavyoelewa mimi taarifa zilizoandikwa hapo haziwezi kuhatarisha usalama wa Taifa kwani hakuna kitu sisi tunachokiiti siri ambacho hakifahamiki na wazungu kwani silaha zenyewe tunanunua kwao halafu kwa umaskini wetu World Bank na IMF huwa wanadodosa juu yA MILITARY SPENDING YETU KABLA HAWAJATUFADHILI MIKOPO; tunalazimika kuwapa taarifa za majeshi yetu!! Taarifa za jeshi letu sio siri tena na ndio maana hata wewe umeweza kuzipata!!! Usalama wa Taifa letu ni jukumu letu mimi na wewe kuwatokomeza hawa mafisadi kwani fisadi kama Rostam anaweza kuliangamiza Taifa letu kwa jinsi alivyowaweka mifukoni viongozi wa nchi yetu!!

Mkuu hapa nadhani hupo sahihi. Tatizo letu sio mataifa makubwa kwani hata siku moja hatuwezi kushindana nao wala kupigana nao. Tatizo hapa ni hawa wenzetu wadogo wadogo wakijua mambo yetu ya ndani ni hatari. Mfano tukitaka kuichapa mfano Kenya au Uganda hivi kama inajua strength ya jeshi letu inaweza kutushinda kwa kujiandaa vilivyo. Natumaini hata hao mataifa makubwa yanayolazimika kujua silaha tulizonao wana miiko yao hawawezi kupablishi details kama hizi
 
Kale kale kautamaduni ka kuhofia usalama wa taifa bado kanaendelea! Leo hii kama ni kuhatarisha usalama wa Taifa ni kuangalia ni jinsi gani maji tunayokunywa yanavyolindwa, umeme tunaoutumia ulivyofinyu kutokana na uongozi mbaya, wizi wa hazina yetu, jinsi mwekezaji anavyopewa mamlaka na nguvu kuliko raia, tunavyoendelea kutegemea misaada, ukimwi, madawa ya kulevya, njaa na ujinga!
 
when they saw much action, even if one was shot down in a case of fratricide fire (it was lost to SA-7s fired by Tanzanian troops).

We shot down one of our own planes? Never knew this.
 
Napata taabu kidogo kuona kama kweli tuna haja ya kuwa na wasi wasi na hizi taarifa. Kama kila kitu sasa hivi kinapatika tu hata kama ni kutoka CIA, iweje tufikirie kuficha habari, eti kwa sababu ni za kijeshi? Kama kuna kitu ambacho tungeweka nguvu nyingi kukificha ni kuwakamata vijana wenye bongo nzuri na kuwatumia vizuri kwa maendeleo ya taifa. Hao ndio wakiamua leo hata kwenye maabara ya nyumbani wanatengeneza kimeta (anthrax) cha kuangamiza nchi nzima. Badala yake nchi imekaa kama nyumba iliyovunjika nguzo yakati. Imelala upande mmoja, ikisubiri nguzo zielemewe idondoke chini. Dunia ya sasa inatakiwa kuangalia suala hilo pia kwa sababu mtu mmoja mmoja au kikundi kwa hali ya sasa ni hatari kuliko taifa moja moja. Kwa hiyo kama Tz itaendelea kulea mafisadi, basi tusishangae baadhi ya vijana wakaanza kufanya vitu vyao hata ikibidi kujilipua. Kwa hiyo usalama wa nchi sasa sidhani kama unategemea sana jeshi kama zamani bali uwezo wa kuangalia mahitaji ya mtu au vikundi vya watu ili wasihatarishe amani. Kwani sisi tunahitaji jeshi lenye nguvu za ajabu sasa hivi?
 
Hiyo habari mbona ni ya kawaida sana. Tena uzuri wa wikipidia hata wewe unaweza kuongeza information zaidi kama unaona kuna kitu kimepunguzwa au kinamiss. Hii ipo kwenye public forums, taarifa za kutisha ni zile walizonazo kwenye facts files zao za siri. Embu tembelea google earth uone mambo, unaweza hata kuona ni ndege ngapi ziko standby pale Ngerengere na ni za aina gani.

Kwa hivyo ndugu yangu usishangae sana ndio dunia ya utandawazi, sio kila information ni classsified, unaweza kujidanganya siri kubwa kumbe wenzako wanaona hiyo ni proper for public consumption.
 
vita sasa viko modern and softsicated, na nchi zilizoendelea hazina haja sana ya kurundika masilaha unakuwa na silaha chache za kujikinga na unakuwa na bajeti kubwa ya emergance, in case vita inatokea lazima uwe unajua supplier wako ni nani na mpinzani wako anatumia nini ambacho hauna and then unapress order, within shorttime unakuwa ok kwa vita
lakini pia cha muhimu sio sana vifaa, bali ni courage na intelligent ya jeshi lako, marekani alipoingia somalia na mashine za kila haina alishindwa vita na wasomali kwa AK47 tu,
vita ya vietnam marekani pamoja na choppers and everygood weapons at that time, lakini walishindwa vita kwa techniques tu za wavietnam,
hata vita ya uganda, waganda walikuwa wanavifaa kuliko TZ lakini ni courage na hardworking ndio ilitufanya tushinde ile vita
lakini tatizo kubwa ninaloliona sasa kwa jeshi la Tanzania ni kitendo cha kumkaribisha Marekani kwenye jeshi, marekani hana historia nzuri ya kupigana vita na jeshi lake ni jeshi la technolojia ya hali ya juu sasa sidhani kwa bajeti yetu ya madafu kama tutaweza kuimudu hiyo technologia, uzuri wa Mchina na Mrusi vifaa vyao ni durable and cheap and very easy to train, kwa hiyo hata wakati vita inaendelea unaweza kununua vifaa na ukatrain watu kuvitumia pasipo na complications nyingi
 
Ha ha haa... Hauruhusiwi kupiga picha Selender Bridge,Central,Lugalo Millitary Base nk vyote vimepitwa na wakati...
 
Salander Bridge

12559942.jpg
 
Huu huu ujinga wa usalama wa taifa kila kitu umetufikisha hapa tulipo.
Wakubwa wa nchi hii wanatuibia kisa usalama wa taifa. Mnakumbuka maneno mengi ya yule waziri fisadi wa fweza akilazimisha kununua rada na ndege ya raisi? kwenye maelezo yake kulikuwa na kitu hiki usalama wa taifa. Matokeo wizi mtupu.
Tuanze kupingana na ujinga huu wa usalama wa taifa.
Kupiga picha usalama wa taifa, kusoma bango usalama wa taifa. Usalama wa taifa ni wetu wote si wa kikundi cha watu.
Nikijua capability ya jeshi letu inanifanya nihatarishe usalama wangu? ujinga na wizi mtupu.
 
... Ila kuna ndege za kivita zetu WaZanzibari ,WaTanganyika mlizichukua bila ya rizaa.True story. :D

Kwani huoni mfano wa USA na Iran kuhusu silaha za nuclear? Zikiwapo USA zinakuwa mahali salama, lakini zikiwa Iran, aaaah, wale jamaa kama ninyi tu, "hawaeleweki"
 
Last edited:
Kama habari zilizo katika post za wikipedia zinaweza kuhatarisha usalama wa taifa letu, basi taifa letu lina matatizo makubwa zaidi kiusalama zaidi ya post za Wikipedia.

Nakusudia kumaanisha kwamba, adui anayetaka kuvamia Tanzania atakuwa na resources zilizo credible zaidi kuliko Wikipedia. kwa hiyo kama Wikipedia wamepata hizi cha kuangalia ni kwamba CIA (and not only their publicly available factbook) wana data gani.

Kwa kweli si siri kwamba umahiri wa kivita hatuna. Tena siku hizi usalama wa taifa wanajitangaza na wamejaa ufisadi ndiyo kabisa hatuna dira wala mwelekeo.
 
Nilikuwa napitia mtandao wa wikipedia, ili kusoma historia ya vita vya Kagera, tahamaki nikakuta webpage moja wanalichambua jeshi la wananchi wa Tanzania kinaga ubaga, nikashituka sana, je hizi habari hazihatarishi usalama wa Taifa?.


Nionavyo, ktk karne hii kwa nchi kama zetu hazina sababu ya kujidai kwamba kuna siri ktk mambo ya Ulinzi. Hivi vifaa vyoye vinanunuliwa nje ya nchi na kusafirishwa na meli za nje ya nchi. Lazima takwimu kama hizi ziko wazi.

Kwa haraka sana utajibiwa na wakuu wa jeshi letu kwamba ni Habari za Hatari, lakini Dunia imebadilika. Huna haja ya kujidai kuficha haya au kuzuia kupiga picha kambi ya Lugalo wakati tunafahamu kuna setilaiti nyingi hewani.
 
Nionavyo, ktk karne hii kwa nchi kama zetu hazina sababu ya kujidai kwamba kuna siri ktk mambo ya Ulinzi. Hivi vifaa vyoye vinanunuliwa nje ya nchi na kusafirishwa na meli za nje ya nchi. Lazima takwimu kama hizi ziko wazi.

Kwa haraka sana utajibiwa na wakuu wa jeshi letu kwamba ni Habari za Hatari, lakini Dunia imebadilika. Huna haja ya kujidai kuficha haya au kuzuia kupiga picha kambi ya Lugalo wakati tunafahamu kuna setilaiti nyingi hewani.

supported;

Kuna silaha tunatengeneza Tanzania? ...NO
Je vifaa kama Rada tunatengeneza Taz...No,
Mafunzo ya wataalamu wetu waliyatoa wapi??... Nchi zilizoendelea,

Sasa kuna kitu gani cha kuficha hapa?

NADHANI TUWAOGOPE WAHUJUMU UCHUMI ZAIDI , KULIKO WAVAMIZI TOA NJE!
 
Hapa ujanja hakuna,
Sisi wataalamu tunao maana watu wanaoweza kutengeneza mabomu au siraha ni wataaramu wetu walioko vyuoni na mainjinia huko mavyuoni wao ndio wanaweza kugundua hizo siraha za maangamizi ukizingatia siraha zinazo angamiza sana ni nzuri kwa taifa maana taifa halitavamiwa.

Sasa tuje kwenye point ya msingi chuo kikuu cha Tanzania ambapo majaribio yoote ya utaalam wetu tunapoweza kufanya sasa hivi wamejenga maduka, Let say wasomi wetu wanataka kujaribu Jet engine ambayo wame itengeneza kwa ajili ya matumizi nisio yajua wataijaribia wapi hiyo Jet wakati sehemu iliokuwa wazi kwa ajili ya kufanyia mambo kama hayo imejengwa maduka na nyumba za kifahari.
Tisa kumi wasomi wetu wakitaka kurutubisha Uranium ili tuondokane na tatizo la umeme watafanyia wapi??
Kwakweli tumependa pesa sasa hata kama Nchi yetu ikiwa haina usiri wowote tukubali maana tumeyataka.

Chuo kikuu cha dar es salaam walitakiwa watengeneze maroketi waanze ya mita mia mpaka km 2000 kisha hizo siraha ziingizwe Jeshini.

Byline: Jennifer Langston

Nov. 7--University researchers have received a grant to help improve jet engines, using a giant tank of baby oil at the INEEL.

The machine at the site, which looks like an oversized aquarium, uses lasers that cut through the clear liquid to precisely measure how fluids like air or water flow around an object.

The Air Force Office of Science Research has awarded a three-year, $315,000 grant to University of Idaho researchers who hope to improve the design of turbine blades in airplane engines.

Turbine blades twist behind the combustion chamber...


Sasa hapa unaona vyuo vya wenzetu wanafanya mambo na wanapata faida sasa sisi hapo udsm utafanyia wapi research kama hiyo? jibu ni hapana maana Jet ikiwashwa on its maxmum speed hayo maduka sijui itakuwa vipi,
model_rocket.jpg

project kama hizi hapa.


Kweli haya mambo huwa ni Siri nakumbuka zamani ulikuwa ukiangalia web ya Navy US utakuta wamekuandikia idadi kamili ya Aircraft Carriers,Amphibious assault ship,Battleship,Nyambizi,Cruisers,Destroyers na Frigates, Lakini infor zote walishatoa hauwezi kujua wana nyambizi ngapi hao jamaa.

Tujitahidi kitechnology tutafika hasa tukiacha ufisadi tukawekeza ktk Technology maana ndio inayo tuchukulia pesa zetu zinapelekwa China na kwingineko.
 
Back
Top Bottom