Uchaguzi 2020 Je, Gwajima anaandaliwa kuchukua nafasi ya Mch. Getrude Rwakatare (RIP mama)?

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,633
697,782
Mara kadha nimeshawahi kuuliza kama ni nani anaihujumu CCM na kwanini anafanya hivyo. Nimeandika na mada pia kulihusu hili
Matokeo ya teuzi za ubunge yametoka, hayakuangalia kigezo cha aliyepata kura nyingi za wajumbe na kushika number moja. Hili majibu pekee yana CCM huko kwenye Kamati Kuu.

Tunatambua wote hali ilivyokuwa kwenye mchuano wa wana CCM Kawe; watia nia walikuwa si chini ya 176. Mshindi hakutarajiwa na wengi lakini ndio lilikuwa chaguo la wajumbe.

Serikali yetu haina dini lakini bungeni alipenyezwa mama Getrude Lwakatare aliyekuwa na Kanisa rasmi la Mlima wa Moto. Mama huyu hayupo tena duniani na pengine bado CCM inamhitaji mchungaji mwingine bungeni.

Je, katika wagombea wote 176 CCM wameona Gwajima ndio anafaa? Hivi hata kwa usafi na weledi wa kiroho na kimwili huyu mtu ni chaguo sahihi kweli? Hasa kwa jimbo kama la Kawe!?

Ni Gwajima huyu aliyeshikwa uongo wa kumfufua mwanafunzi wa shule ya msingi Kurasini
Ni Gwajima huyu aliyekamatwa na uongo wa kufufua misukule
Ni Gwajima huyu aliyemtukana kiongozi wa kiroho wa Kanisa Katoliki Tanzania Mhashamu Polycap Pengo
Ni Gwajima huyu aliyeshikwa ugoni na wake za watu ama waumini wake
Ni Gwajima huyu mwenye tuhuma za ngono kila kona
Ni Gwajima huyu aliyetaka kuwatoroka polisi akijifanya mgonjwa wakati alipokuwa anakabiliwa na kesi fulani..begi lake lilikutwa na silaha mbili za moto na risasi zake
Ni Gwajima huyu mwenye kashfa na mwenye misuguano na watu wa kila aina

Kuna baadhi wanasema kapita kwa sababu ya kabila, hii ni dhana lakini inaweza kuwa potofu.

Kuna wanaosema kapita kwakuwa ana waumini wengi sana. Hii ni dhana dhaifu sana kwakuwa hao waumini wake wanatoka sehemu mbalimbali, si wakazi wa Kawe wote. Dhana moja halisi ni moja au mbili:

1. Gwajima ni bilionea kwa viwango vyetu, lakini je ubilionea wake ni sadaka tu? Hana mishe nyingine nyuma ya uchungaji!? Tunafahamu kwa ukubwa wa chama kama CCM ni vigumu mno kuwakwepa wafadhili. Je, Gwajima ni mmojawapo?

2. Gwajima ni sehemu ya mamlaka!? Hili tuliache kama lilivyo.

Vyovyote iwavyo, Gwajima sio chaguo sahihi la mgombea wa kisiasa:

Alishasema wazi kuwa mbunge ni kujishusha kwakuwa yeye ni mtumishi wa Mungu, koleo number 1. Alishawatukania Wakatoliki kiongozi wao, koleo number 2. Hawezi kupata kura za waumini wengine na wa imani nyingine kwakuwa si mwanasiasa ni kiongozi wa dini tena binafsI, koleo number 3.

Hawezi kupata kura zote za waumini wake, wote si wakazi wa Kawe wana kwao na hao wana itikadi tofauti na wana viongozi wao wa kisiasa wanaowakubali, koleo number 4.

Kuna wapinzani wake ndani ya CCM ambao hawajaridhika na uteuzi wake, koleo number 5

Sasa kwanini katika watia nia 176 kachukuliwa yeye!? Je, ni nguvu ya Shekeli!? Muda utasema.

RIP Mchungaji Dr. MB Getrude Lwakatare. Mlima wa Moto umeondoka nao!
 
Wewe si uliletaga uzi hapa ukadai ni za kafara? Najua unamchukia kwakuwa unapo wanga huwa anakutwanga rohoni punguza chuki kijana maisha hayaendi hivyo
Ninini hizo za kafara? Chuki iko wapi hapo!?
 
Mshana Jr,

Waache wafu wapumzike kwa amani usiwataje taje. Alafu hizo kila kona unazozisemea unazijua wewe na alienyuma yako.

Ujue bhana kila mtu ana pande mbili na pia mtu haukumiwi kwa zamani yake. Hayo mambo ya kumtukana Askofu ni ya zamani na alikuwa anapinga mahakama ya kazi sio kwamba hujui unajua ila una kaza ubongo. Na unavyosema kutoroka polisi Sio kweli maana kwa kumbukumbu zangu baada ya kureport central kituo kilichofata ni ICU sasa sijui mtu anaweza kuigiza mpaka kufika ICU?

Hata kipindi kile watu waliongea sana oh tuone oh tuone clip kibao zikasambaa ila leo matokeo yametuchachafya. Wengi walitamani Askofu akose ila ndio kapita sasa kuwa mgombea ubunge wa chama tawala.

Hakuna ubaya wowote wa kiongozi wa dini kuwepo bungeni hata kama ni sheikh. Bungeni ni kwa wote. Na Kawe ndio ishachukuliwa hivyooo
 
Back
Top Bottom