Je, GEORGE KAHAMA na ANDY YOUNG wamegombana?.. Will IKULU Intervene?!

Game Theory

JF-Expert Member
Sep 5, 2006
8,545
833
George Kahama pamoja na akina Rupia ni moja kati ya ma UNTOUCHABLES bongo na wamekuwa immune for such a long time humu JF

Anyway kama mnavyojua kuwa yule bibie kwa jina la JILL amekuwa akiwaendesha puta maofisa wa Ikulu kutaka apewe special access to JK na kuna taarifa kuwa alifanikiwa kuipata namba ya JK ambayo hata mimi ninayo na mwanakijiji anayo vile vile hivyo siyo siri lakini JK amekuwa hataki kuwa involved moja kwa moja na mambo haya bila washauri wake kumwambia details zinaendaje.

Lakini kuna tatizo lingine ambalo limeibuka out of no where...

Mnavyojua akina KAHAMA walikuwa wako very prominent katika mining industry ya Bongo kwa kutumia influence yao na ndio walio wa-accomodate wale Wa-Canada in the 1990's

Kisha kuna kipindi wakawa wako close na hao GOODWORKS ambao kwa kweli credit anapea huyo Mchungaji Charles Stith.
LG18356.jpg


I have managed to connect the dots na kujua kwanini JILL amekuwa halali ma jisimu isio na wakati maalum

SABABU NI HUYU BWANA:

friedman.jpg

Ana itwa BRENT SCOWCROFT na ni:

hebu soma hapa: http://www.scowcroft.com/index.htm


WEST POINT undergrad
COLUMBIA postgrad & PHD
MORMON
INTERNATIONAL RELATIONS SPECIALIST
NATIONAL SECURITY ADVOSOR to: current Bush and Ford,

Bila kusahau kazi yake nyingine alikuwa ni Chairman wa President's Foreign Intelligence Advisory Board ambayo katika mission statement yake inasema ni:


"...provides advice to the President concerning the quality and adequacy of intelligence collection, of analysis and estimates, of counterintelligence, and of other intelligence activities."
Kisha wanaendelea kusema:

"The role of the board: [is] Unique within the government, the PFIAB traditionally has been tasked with providing the President with an independent source of advice on the effectiveness with which the intelligence community is meeting the nation's intelligence needs and the vigor and insight with which the community plans for the future."
source: http://www.whitehouse.gov/pfiab/

Personally nishawahi kumuona huyu mzee SCOWCROFT akizungumza katika duru za mambo ya Kimataifa lakini it never came to my mind kuwa atakuja kuwa prominent bongo kwani nilijua huyu ni mmoja kati ya wale ma architects wa vita kule Iraq.

In short jamaa ni beyond CIA na kampuni yake hii ambayo haina haja ya kupiga hodi kuingia IKULU ni manyoka watupu ambao wameletwa na mheshimiwa GEORGE KAHAMA na hilo ndilo tatizo kubwa linalomkosesha usingizi bwana ANDREW YOUNG ambaye alidhani anaweza kutumia charm na black brotherhood kupata access na kazi toka kwa JK. Sasa looks like CIA aka "THE COMPANY" are in town na access ya IKULU wanayo na sitoshngaa kama JK atakuwa hawapigii wao simu badala ya wao kumtafuta.

GEORGE KAHAMA kawaingiza Tanzania na washasaini mkataba kwa kutumia nafasi yake kama Advisor wa Tanzania Chamber of Energy &Minerals na vile vile kama member wa Tanzania National Business Council na post yake kama post of vice-president of the Tanzanian Royalty Exploration Corp ,

Kutokana na maelezo katika website yao, akina SCOWCROFT hawasemi mengi sana na inawezekana ikawa akina Kahama waliaambia wasifanye makosa kama akina GWI ambayo yameibua maswali mengi kuliko majibu.

Sasa hawa TANZANIA ROYALTY wamewanyima tenda akina Andy Young na wakaamua kuwapatia hawa akina SCOWCROFT GROUP ambayo ni ya mheshimiwa pichani hapo juu. Cha ajabu ni kuwa akina Andy Young walipata vijikazi kule Ghana kwa kumtumia Walter Kansteiner ambaye alikuwa ni Assistant Secretary for African Affairs and currently board member of Jean Raymond Boulle.

Sasa quick search yangu nimegundua kuwa hao Jean Raymond Boulle


Nikapata hili:

http://www.swtriallaw.com/att-werbner/jean-raymond-boulle.html

http://www.globeadvisor.com/servlet/ArticleNews/story/gam/20060508/RTAX08


POINTS OF INTEREST:

1) Hivi kama watu kama hawa wakishapata unprecedented access na ofisi yetu kubwa je sisi tutakuwa na la kusema wakitulazimisha mikataka mingine mibovu?

2) SCOWCROFT group kama kampuni haikatazwi lakini kutokana na nature ya kampuni yeyenyewe what makes you think our national security will not be compromised?

3) Ndio tunataka ma investors lakini at what price? And who will pay that price? Hivi Mheshimiwa MBUNGE kama GEORGE KAHAMA yuko tayari ku compromise our national security kwa sababu ya njaa yake what makes you think wafanyakazi wa chini watashindwa ku-leak mambo kwenye internet?

4) Role ya FOREIGN ni kui-advice serikali katika mambo haya japo TCCIA wanaweza wakawa hawana objection lakini hii inanifanya ni conclude yafuatayo:

a) RADHIA MSUYA ambaye ni mkuu wa kitengo cha NORTH AMERICA & EUROPE pale either alikuwa nawajua hawa lakini akaamua kukaa kimya au walipeleka assessment yake lakini wakaamua kumdharau

b) RASHID OTHMAN inawezekana alipeleka intelligence estimate ya hawa SCOWCROFT lakini IKULU waliamua ku overule kwa hiyo inawezekana hii ikawaondoa Usalama wa Taifa from this web

c) UBALOZI wetu DC someone is or is not doing his job properly na kama ulifanya then katika chain of command kuna walakini

d) BENARD MEMBE kama mtu niliyekuwa ninamtegemea angeweza kuweka hili wazi naye inaonekana amekuwa overruled na IKULU ambako in the wake of recent scandals kuanzia Jenereta la Richmond to Benki kuu wameprove kuwa ni ma incompetents na hawaji na majibu straight kwa walipa kodi na in other words they are out of touch with the reality on the ground.

5) Je nani anafanya vetting ya hizi kampuni zinazoingia Tanzania? Je KAHAMA kama mtu ambaye alikuwa serikalini kwa muda mrefu je anayo 'our national interest at heart' au kwake muhimu ni pesa tuu?

6) Tatizo siyo hizi kampuni bali ni web of secrecy ambazo zina-operate Tanzania and I have a belief kuwa hii inatokana na jinsi walivyo free kufanya walitakalo na serikali yetu inaonekana kuwa imejaa rushwa. Japo wanaona kuwa hawapati bad press internationally lakini this cannot last for long in my opinion

Last but not least washauri wa JK katika masuala ya UCHUMI ni wachemshaji wakubwa mno. Kila mtu anajua hakuna serious African American investor wa kuinvest Bongo kama wangekuwepo basi huyo MCHUNGAJI STITH angewaleta tangu mid 90's
 
Sasa hili wigo ni laajabu sana kwani kwa namna moja au nyingine huyu CLINTON naye yumo au kwani huyu mheshimiwa hapa chini alikuwa anavita sana pesa toka kwa Clinton

"In 1994, President Bill Clinton appointed Young as chairman of the Southern Africa Enterprise Development Fund, a $100 million privately managed fund to provide equity to businesses in 11 countries."
http://aysps.gsu.edu/people/YoungA.htm


'nuff said.

Wazee hii tunaweza kusema ni patronage signed sealed sponsored now delivered.


halafu one would have thought kuwa huyu Andrew Young anayo best interest with Brothers au tuseme black people. Last week alimtukana OBAMA kwa kusema hivi:


He also joked that author Toni Morrison may have been on to something when she referred to former President Bill Clinton as the "first black president."

"Bill is every bit as black as Barack," he said. "He has probably gone out with more black women than Barack."

Exclusive: Andrew Young explains why he is not supporting Obama

hawa ndio matapeli wapya tunaowakaribisha Ikulu na sasa wanaingia mpaka chumbani. Hivi kama kashindwa kuonyesh brotherhood kwa Barack what makes you thin anao uwezo wa kuonyesha brotherhood kwa JK?
 
Good analysis broda

Another Siera Leon, DRC, Dafur,Angola and Iraq is being created in East Africa, sijui tutakuwa wakimbizi kwa nani.

Madini, madini, madini
 
Huyo babu Andrew Young ndio zake hizo, kwani alitimuliwa kwenye Board ya Wal-Mart kwa mambo kama hayo. Popote penye Stith basi Clinton yupo!! Huyo bwana(stith), nasikia ana mradi mkubwa sana wa kujenga nyumba za kuuza(price range $$75000-150000) somewhere in Dar. Ukweli ni kwamba, ni mradi wake na kina Clinton na mtaji wao unapatikana ktk mtkasi shady!!!.
Ama kweli Tanzania imekuwa kichwa cha mwendawazimu.!
 
Hii nchi ni yetu.
kama tunataka maendeleo ni sisi WaTZ wenyewe ndiyo wenye jukumu la kuleta maendeleo.
Kamwe wageni hawataleta maendeleo ya kweli.

Kitendo cha viongozi wengi kuegemea na kuweka matumaini yao kwa wageni ni udhaifu wa kufikiri na kuona mbele.
Ndoto za mendeleo hazina uhusiano sana na cheti cha darasani. Tuna wasomi wengi nchini Tanzania amabao ni magwiji wa kufanya kazi kwa kutumia DESSA(lazima wawe na mahali pa kutazamia).
Viongozi wenye njozi za maendeleo huota maendeleo yenyewe katika sura yake kutoka vichwani mwao si kutoka kwa vichwa vya wengine.

Kwa kushindwa kwao kuwa na njozi za maendeleo katika vichwa vyao wameamua kuweka nchi rehani kwa yeyote mwenye kuwapa mchicha hata kama wanajua fika kwamba wageni hao wataishia kutuachia mashonde katika miradi yao.

Maendeleo siku zote hujificha nyuma ya pazia la ugumu, ni wale tu wenye njozi ziwezazo kupenyeza pazia hilo huutambua njia halisi za kwenda mbele. Viongozi wenye ubongo mlalo na macho mlevi kamwe hawathubutu kupiga fimbo bongo zao kwa nia ya kuzijengea nguvu ya kufikiri.
Akili zao huwatuma kufanya yote yaliyo rahisi hata kama urahisi huo ni kukaba roho vizazi vyaoo wenyewe.

Vijumba viwili vitatu hapa na pale, fedha ya kupeleka kinda Marekani likajifunze kuvuta bangi, wizi na umalaya, shoping dizaini ya mama mtoto na kimada pale London, gari la miguu minne ya nguvu na kuopoa visichana vidogo huku ukijidharirisha navyo kwa manyoya yako meupe kinenani. Na akina mama viajuza hawako nyuma, kutamani kula vitumbua vyao na vivulana vidogo kama kutamani kuku wa kubanikwa mwenye kunyunyizwa chachandu la Kimanzichana, kisa mchicha haramu.

Maendeleo yanakuja kwa kujenga uwezo wa wananchi ndani ya nchi kukua na kufikia kiwango cha kushindana na matajiri wa dunia.

Wageni wanakuja ili kuchuma na kujenga kwao.

Kushi kwangu kote hapa ughaibuni sioni hata mtu mmoja anayetuonea huruma kwa sababu sisi ni masikini. Kila siku nakutana watu wenye kutaka kujua ujinga wetu utakwisha lini? Japo swali hili hawaulizi moja kwa moja.
 
Hata ASHA ROSE MIGIRO hayuko immune sasa teteni na hili nalo
Asha Rose migiro anapewa Zawadi ili iweje? sasa GWI wanazidi kuchachwa lakini kila mtu anajua tayari nchi tushaiuza na kilichobaki ni kupiga soga tuu

mibmp.jpg


The Founder and special advisor on the Board of Directors, and the Sullivan Summit Convener Mrs.Hope Masters handsover an International Service Award to the UN Deputy Secretary General Dr.Asha Rose Migiro during the fifth sullivan Summit Awards Dinner held in Washington DC last week.third left isambassador Andrew Young who is the board chairman for the Sullivan Foundation,and fourth left clapping is the president and CEO of the Sullivan foundation ambassador Howard Jeter.
 
Hii nchi ni yetu.
kama tunataka maendeleo ni sisi WaTZ wenyewe ndiyo wenye jukumu la kuleta maendeleo.
Kamwe wageni hawataleta maendeleo ya kweli.

Kitendo cha viongozi wengi kuegemea na kuweka matumaini yao kwa wageni ni udhaifu wa kufikiri na kuona mbele.
Ndoto za mendeleo hazina uhusiano sana na cheti cha darasani. Tuna wasomi wengi nchini Tanzania amabao ni magwiji wa kufanya kazi kwa kutumia DESSA(lazima wawe na mahali pa kutazamia).
Viongozi wenye njozi za maendeleo huota maendeleo yenyewe katika sura yake kutoka vichwani mwao si kutoka kwa vichwa vya wengine.

Kwa kushindwa kwao kuwa na njozi za maendeleo katika vichwa vyao wameamua kuweka nchi rehani kwa yeyote mwenye kuwapa mchicha hata kama wanajua fika kwamba wageni hao wataishia kutuachia mashonde katika miradi yao.

Maendeleo siku zote hujificha nyuma ya pazia la ugumu, ni wale tu wenye njozi ziwezazo kupenyeza pazia hilo huutambua njia halzisi za kwenda mbele. Viongozi wenye ubongo mlalo na macho mlevi kamwe hawathubutu kupiga fimbo bongo zao kwa nia ya kuzijengea nguvu ya kufikiri.
Akili zao huwatuma kufanya yote yaliyo rahisi hata kama urahisi huo ni kukaba roho kizazi chako mwenyewe.
Vijumba viwili vitatu hapa na pale, fedha ya kupeleka kinda Marekani likajifunze kuvuta bangi na umalaya, shoping dizaini ya mama mtoto na kimada pale London, gari la miguu minne ya nguvu na kuopoa visichana vidogo huku ukijidharirisha navyo kwa manyoya yako meupe.
Maendeleo yanakuja kwa kujenga uwezo wa wananchi ndani ya nchi kukua na kufikia kiwango cha kushindana na matajiri wa dunia.

Wageni wanakuja ili kuchuma na kujenga kwao.

Kushi kwangu kote ughaibuni sioni hata mtu mmoja anayetuonea huruma kwa sababu sisi ni masikini. Kila siku nakutana watu wenye kutaka kujua ujinga wetu utakwisha lini, japo swali hili hawaulizi moja kwa moja.

Hata GEORGE KAHAMA basi?

One would have thought ni mtu ambaye ni makini lakini wapi!
 
Kipimo cha kuelimika siyo Digirii au ukubwa wa madaraka uliyo wahi kushika.
kipimo cha elimu ya mtu ni umahiri wake katika kutatua matatizo ya jamii yake. Elimu haina maana yeyote kama haitasaidia kutatua matatizo.
Kam mtu anasoma ili awe waziri au mkurugenzi kwa nia ya kuwakoga watu huyo hajaelimika bado.

Tofauti katika jamii si kitu cha ajabu na pengine huwa kitu muhimu ili kujenga mvutano wa maendeleo. Lakini tofauti ya mmoja kukaa Ikweta na mwingine Antactica ni tofauti hatari ambayo siku zote huzua upepo mkali katikati. Hata bila kumwita Nabii aje atutabirie, tunajua fika kwamba upepo huo siku zote utavuma kutoka Antactica kwenda Ikweta mpaka joto la ikweta liwe sawa la lile la Antactica.

Si vema kukiabudu kitabu kwa sura ya jarada au Jina lake kiabudiwe kilichoandikwa ndani yake.

Karl Peters aliwafunga kamba babu zetu kwa shanga na vitambaa vya kujifunga viunoni, wakati ule wafalme walikuwa wakitembea nusu uchi au wakijifunga ngozi namagome ya miti. Kuvaa kitamba na mkewe kuulamba shanga lilikuwa jambo la kuukata kwelikweli. Leo hii viongozi wetu wenyewe wanawafuata akina Karl Peters na kutaja bei yetu hata kabla Peters mwenyewe hajawaliza. Wakiambiwa ni majemadari wa vita ya Rushwa na maendeleo ya wananchi kwa mtindo wa kuvishwa kilemba cha makuti wanavimba vichwa na kuwaona hata mama zao kule udongini ni wajinga.
Tutafika kweli?
 
Ikulu asked to intervene in gold mine rights dispute

FINNIGAN WA SIMBEYE
Dar Es Salaam

A DISPUTE over gold mining rights between a local company, Bazo Enterprises and General Supplies, and the Canadian-registered Tanzania Royalty Exploration (TRE) has reached State House with Chief Secretary Philemon Luhanjo now in the role of mediator, it has been learnt.

This follows Luhanjo’s receipt of a letter from Bazo Enterprises owner Yusuf Shekwavi, in which Ministry of Energy and Minerals officials are accused of showing bias in favour of TRE.

Shekwavi is disputing TRE’s acquisition of the Kigosi gold mine and two other unrelated prospecting licences, with registration PL 1775/2001 and PL 2972/2004, from the Tanzania American International Development Corporation (Tanzam 2000 Ltd).

In his letter to the State House chief secretary dated April 4 this year with reference number BEGS/ST/07/04/2, the Bazo Enterprises proprietor said he had lost confidence in the commissioner of minerals at the ministry, Dr Peter Kafumu, following what he (Shekwavi) referred to as biased actions in favour of TRE vice-president Joseph Kahama.

Shekwavi asserted that after meeting ’’exclusively’’ with Kahama, Dr Kafumu then unilaterally postponed a scheduled meeting between himself and both disputing parties in a questionable manner.

’’The ministry’s legal counsel told me that Mr Joseph Kahama would call the commissioner to fix another date for our joint meeting. It is frustrating to note that Mr Kahama should fix the date for the joint meeting, and not the commissioner,’’ Shekwavi said in his letter to Luhanjo.

He criticized Dr Kafumu’s decision to meet Kahama and his lawyer alone before the joint meeting initially scheduled for February 28 this year, requesting Luhanjo to intervene and make direct contact with TRE chairman and chief executive officer James Sinclair.

Efforts to reach Luhanjo or other State House officials on latest developments concerning the issue had proved futile by the time we went to press yesterday.

Source: ThisDay
 
Kimya cha wana JF kimenitisha, nilitegemea watu wangekuja na maoni mbali mbali kuhusu hili lakini assumption yangu ni kuwa:
either

Nimeenda too deep for your normal taste(yaani sijaipoliticise)

Au mnaogopa kutia neno kuhusu huyu GEORGE KAHAMA

either way i am not sure kama kuna uhumihi wa kuendelea kumwaga data za namna hii manaan nilikuwa na zingine kuhusu waingereza wanvyoitia Umasikini Tanzania kupitia DFID pale Dar lakini naona its not worth it

Anyway thanks MADILU kwa mchango wako
 
Tunasoma na ku synthesize GAME THEORY....
SIO KUKURUPUKA...MAMBO MAZITO HAYO UNAYOSEMA!
 
Game Haya mambo ni makubwa
na mtu hupaswi kuchukulia juu juu

Na kama kuna lototte unaweza kuendelea kutupatia mkuu
 
Kimya cha wana JF kimenitisha, nilitegemea watu wangekuja na maoni mbali mbali kuhusu hili lakini assumption yangu ni kuwa:
either

Nimeenda too deep for your normal taste(yaani sijaipoliticise)

Au mnaogopa kutia neno kuhusu huyu GEORGE KAHAMA

either way i am not sure kama kuna uhumihi wa kuendelea kumwaga data za namna hii manaan nilikuwa na zingine kuhusu waingereza wanvyoitia Umasikini Tanzania kupitia DFID pale Dar lakini naona its not worth it

Anyway thanks MADILU kwa mchango wako

Game,
Kutoa ni moyo... na Elimu haina mwisho wala matabaka...
Basi, wee tenda uonalo linafaa kwa jamii yako na nafsi yako.

SteveD.
 
Rafiki yangu sisi wengine tuna amini in deep focusing! sasa kama hatujakaa sawa ume give up sio vema nakushauri toa yote uliyo nayo moyoni then tutajaribu kuunganisha na mengi tu yanayotusibu huku tuliko ila tofauti yetu waTz ni kubwa sana inapofikia kuongea mambo ya maana kwa maslahi ya taifa hili sio kuwa hatujui mambo lakini hatutoi muda wa kutosha kushughulikia nchi yetu, najua kweli wengi umaskini umezidi tunashughulikia chakula lakini sasa tunasahau hata chakula kinaamuliwa na hawa wenye kumiliki shares zetu nchini.

binafsi najuta sana nchi hii kuanguka mikononi mwa kikwete, kwakweli kikwete anao upeo mdogo sana kushughulikia mabo ya uchumi katika nchi hii halafu kikwete wakati anahaha kuutafuta urais alijikabidhi sana kwa weupe ndio maana hawa kina George kahama wanashtuka kwa hali aliyoingia nayo madarakani, unajua wakati kikwete anacampaign wengi walijua atawabeba wale waliompa tough lakini alikuwa tayari amenunuliwa ili akifika tu afanye yale yanayotakiwa na kina CLINTON sasa hivi TZ kuna mnyukano mkubwa sana kwa ahadi za huyu kikwete kwa weupe hao alipokuja waziri mkuu wa canada haikuwa ziara nyepesi kama vyombo vyetu vilivyoripoti bali ni kubomolewa kwa ngome ya makampuni ya marekani na canada kuna kitu kimewagonganisha haya majitu, na hata hii inayoitwa kamati ya madini inatafutwa ili kumfunga paka kengele ili asilaumiwe kikwete bali mapendekezo ya kamati kikwete anayahitaji kujifichia ili afanye kinyume na yale aliyowaahidi waliomfadhili.

njama zote za kampuni za kuwekeza nchini wakati wa mkapa ziliongozwa na G KAHAMA lakini kutahamaki huyu kahama amelizwa na mtandao wa Rostam ambao unataka kuvuruga network ya KAHAMA sasa biashara hii itakuwa ngumu sana na tarajia siri nyingi sana ku leak kadri wanavyotofautiana .
kama unayo mengine tujulishe usikate tamaa maana kufa na jambo ni fedheha kwa maiti wewe yaweke tutachangia kadri tunavyoweza.

naomaba kama kuna mtu anaweza kufatilia safari za Rostam ajaribu kuangalia kila mwezi huyu mtu yuyko canada kuna mradi anaelekea kuukamilisha siku sio nyingi mkataba mpya utasainiwa!
 
Miye naendelea kuchimba hapa! Hii issue itakuja kuwa moto moto! Sasa Kahama gets into the picture! Hiyo Tanzania Ryalty Exploration nimeshaanza kupata data zake! Hoho!
 
Jamani hii connecting the dots imekuwa TAMU SANA!
Kuna thread moja imeanzishwa kutoka gazeti la this day about hiyo TRE na akina Kahama very interesting. Sasa naomba nimwage info kidogo! Alafu admin aunganishe thread hizi mbili!
haya naenda kubandika information kwenye thread ile nyingine
 
Haya information kuhusu Tanzania Royalty Exploration, Mzee MKJJ as always you are right!
Website: www.TanzanianRoyaltyExploration.com
Fax: (604) 669-8915
News Release - August 24, 2007

Tanzanian Royalty Enters Into Contract Negotiations For Remaining Nickel Licenses in Tanzania with company from People’s Republic of China

Tanzanian Royalty Exploration Corporation (AMEX: TRE / TSX: TNX) is pleased to announce that it has entered into contract negotiations with a company from the People's Republic of China (the "PRC Company") for the remainder of its nickel licenses in the Kagera/Kabanga nickel belt in Tanzania.

The 12 licenses that are presently subject to contract negotiations comprise the entire 4,482 square kilometres portfolio of nickel licences held by Tanzanian Royalty in the Kagera/Kabanga nickel belt.

The decision to enter into contract negotiations for the licenses at this stage follows the signing of a Letter of Intent (LOI) with the PRC Company in May 2007. The LOI granted the PRC Company an exclusivity period of 150 days to evaluate the properties within the context of concluding option agreements that are acceptable to both parties.

According to Tanzanian Royalty Chairman and CEO, Jim Sinclair, “The Chinese have moved quickly to expedite their due diligence on these properties given the highly competitive environment that exists in Tanzania for quality mineral projects of this nature.”

“We have certainly been impressed with their field capabilities and their obvious determination to acquire and exploit the potential of mineral assets in Tanzania that serve their national interests.”

While there is no guarantee that negotiations between Tanzanian Royalty and the PRC Company will lead to the signing of any formal contracts, Sinclair emphasized that the Chinese interest in Tanzania is genuine and reflects the nation’s strategy of securing long term sources of supply for key commodities such as nickel, copper, gold and other industrial metals. “The Chinese have a long history in Tanzania but their business priorities have changed in recent years with industrial commodities leapfrogging to the forefront,” he noted.

Tanzanian Royalty Exploration Corporation is a unique, publicly-traded, financial minerals exploration company whose business strategy is to develop royalty income under partnership arrangements from its world class gold, diamond and nickel assets in the Lake Victoria Greenstone and Kabanga/Kagera Nickel Belts of Tanzania.

Respectfully Submitted,

“James E. Sinclair”
James E. Sinclair
Chairman and Chief Executive Officer


For further information, please contact Investor Relations at 1-800-811-3855
Visit our website: www.TanzanianRoyaltyExploration.com
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom