Je, Felix Mrema ni kichwa ngumu kiasi hiki?

Pundamilia07

JF-Expert Member
Oct 29, 2007
1,439
54
na Ramadhani Siwayombe, Arusha

MGOGORO sehemu itakapozikwa maiti ya mtoto wa Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Felix Mrema, umechukua sura mpya baada ya mbunge huyo kudaiwa kuondoka hapa nchini kwa kificho na kwenda nchini Marekani kwa lengo la kufanya mazishi nchini humo.

Habari zilizopatikana jijini hapa, jana na kuthibitishwa na ndugu wa marehemu walioko nchini Marekani zinaeleza kuwa mbunge huyo hivi sasa yupo nchini huko kwa lengo la kufanya maziko ya mwanae huko bila kumshirikisha mkewe wa ndoa, Milcah Mrema, aliyeko hapa nchini.

Kutokana na mgogoro uliopo wa wazazi juu ya sehemu atakayozikiwa mwanao, Angel Mrema, 34, maiti imefikisha siku 20, bila kuzikwa.

Akiongea na Tanzania Daima mara baada ya kupata taarifa hizo mama mzazi wa marehemu, Milcah Mrema, alisema nguvu ya fedha aliyonayo mbunge huyo ndiyo inayomnyanyasa na kumkosesha haki zake za msingi.

''Mimi ni mzazi mwenzie ambaye wote kwa pamoja tumefiwa na mtoto wetu na tuna machungu kwa hilo lakini mwenzangu kaamua kuondoka bila hata kuniaga na kwenda huko kufanya taratibu za mazishi bila kunishirikisha.'' Alieleza mama huyo kwa machungu.

Aidha mama mzazi wa marehemu akiongea kwa masikitiko mjini Arusha alisema, kinachomuuma ni kusikia kuwa mazishi yanayotaka kufanyika huko ni kwa njia ya kuchoma moto mwili wa marehemu kutokana na nafasi za kupata makaburi kutokuwepo ambapo ni kinyume na utaratibu wa dini yao Kikristo.

Amesema kuwa licha ya kwenda kinyume na misingi hiyo ya mazishi ya dini pia haki ya kuwa anafanya maombi dhidi ya mtoto wake kwa kutembelea kaburi na kuweka maua inakiukwa kutokana na maamuzi yanayotaka kufanywa na mumewe.

Akizungumza kwa njia ya simu kutoka Marekani katika jimbo la Los Angeles ambako ndiko mwili huo wa marehemu uliko mama mkubwa wa marehemu, Muthike Phyllis Porter, amethibitisha kufika huko kwa mbunge huyo na kuanza taratibu za mazishi.

Muthike ambaye anaishi katika Jimbo la Washington DC nchini Marekani alienda Los Angeles kwa ajili ya kufanya taratibu za kusafirisha mwili huo kuuleta hapa nchini kwa maelekezo ya ndugu yake lakini kufika huko kwa Felix Mrema kumesimamisha mipango hiyo.

Marehemu Angela Mrema, mtoto wa Mbunge wa Arusha Mjini, Felix Mrema, alifariki dunia Desemba 17 mwaka jana nchini Marekani baada ya kupata ajali ya gari Desemba 7; ajali iliyosababisha kufanyiwa upasuaji baada ya kuumia mguu na wakati akiwa katika matibabu hayo, alifariki dunia akiwa katika chumba cha upasuaji.

Mara baada ya kupatikana kwa taarifa za kifo hicho familia ya marehemu iliyopo mjini Arusha wakiwemo baba mzazi wa Marehemu, Felix Mrema, na mkewe Milcah ambaye kwa sasa haishi na mumewe huyo baada ya mbunge huyo kuwa na mke mwingine, kulizuka mvutano wa sehemu utakapozikwa mwili huo.

Katika mgogoro huo, mama mzazi wa marehemu anataka mazishi ya mwili wa mtoto wao uzikwe hapa hapa Arusha, huku baba, Felix Mrema, akitaka shughuli yote ya mazishi kufanyika huko Marekani.

Jitihada za kumpata mbunge huyo kwa njia ya simu ili azungumzie hatua iliyofikiwa juu ya taratibu za mazishi haikuzaa matunda baada ya simu yake kuita bila majibu.
 
Mwanaume unatakiwa uwe na msimamo!! usiyumbishwe na mwanamke katika maamuzi. namshauri arudi na majivu kidogo kwa ajili ya mama.
 
Nadhani hii ishu imekaa kifamilia zaidi,kama wameshindwa kuamua wao ndani ya familia tuwaachie wao,maana nimesoma baadhi ya magazeti yameshaanza kiweka ishu hii kisiasa...Tuwaachie wanafamilia jamani...be blessed
 
..suala la kifamilia hili. si utamaduni wetu kuweka masuala hayo magazetini. tena wala hatuwasaidii kwa kuwaendekeza malumbano haya kwenye vyombo vya habari.

NB:

..huyu mama alianza kwa kuulalamikia ubalozi wa usa nairobi kwamba wamemnyima visa. sasa anamlalamikia mumewe.
 
Ni shu ya kifamili alakini ina mafundisho mengi kwetu hapa na kwa jamii nzima!
Wazazi mnapogombana mzingatie itafika siku mtashindwa kushirikiana katika mambo makubwa na ya msingi kama kifo au ugonjwa.- Wazazi wametengana, baba amebaki na mali zilizochumwa na familia( mke na mume kwa manufaa ya watoto wao); mama ndo keshakuwa mtu mzima amestaafu, watoto ni kama wanajitegemea, baba kachukua a younger woman to enjoy the wealth, the younger woman is really enjoying the wealth!if all was well hakuna kifo basi migogoro hii isingekuwa public issue.

Kifo kimetokea- hili ni jambo kubwa, wazazi badala ya kushirikiana, mwenye mali ndiyo anatumia nguvu ya fedha kumnyanyasa yule asiyekuwa na mali ( pamoja na kwamba wamechuma pamoja), kwa vile mama/mke si mtanzania imebidi kuombea visa kwao Kenya, huko anakosa visa kwa sababu zisizokuwa wazi sana. Anapoomba dadake huko marekani asaidie kuleta mwili huku kwa maziko, baba mwenye fedha anaamua kuruka kwenda marekani kumaliza kila kitu huko. Sababu ya msingi kwanini asisafirishe maiti ije izikwe TZ ni nini? je ni kuendelea kumkomoa mama?
Fundisho:
- Ugomvi wa mke na mume una madhara zaidi ya tunavyodhani
- Wanawake walioolewa muwe macho na makini zaidi maana kuna leo na kesho
-Kina baba wenye kufanya dhuluma mjue mnajiaibisha na pia kuna Mungu!
-Wanawake wenye kuvunja ndoa za watu, ole wenu siku ya kiama!
 
Kama tumejadili ishuz like JK kumcheza ngoma mtoto wake why not hii ambayo kimsingi ina-raise some fundamental questions kuhusu Mheshimiwa Mrema?

Let me ask you guys mnaosema ishu hii imekaa kifamilia zaidi:hivi mtu akimnyanyasa mkewe au mwanae,kwanini vyombo vya sheria vinaweza kuhusishwa?Suala la familia,or a private matter,is not an excuse ya kufanya mambo ya ajabu.

Mtambue pia kwamba anayeweka public habari hizo ni Milcah,mzazi mwenzie Mrema.Sasa mnaposema suala hili ni la kifamilia zaidi wakati mmoja wa wazazi analileta kwenye public arena siwaelewi.

Bottom line is,huyu Mbunge anamuogopa huyo "mkewe mpya" kupita kiasi to an extent ya kupanga mazishi yafanyikie nje ya nchi ili asimuudhi.Well,pengine hilo halituhusu sana lakini another crucial point is,kama kiongozi anaboronga katika maamuzi ndani ya familia yake,what should we expect from him katika uongozi wa umma?
 
Its real painful. Hivi kweli hata kama mmegombana kuna ulazima wa kuwa maadui hasa kukiwa na viuinganishi kama watoto? Kitengo alichofanya huyu mbunge kweli ni cha kinyama na mtu yeyote asijaribu kutetea kaka kulikuwa na uwezo wa mtu wa kuleta huo mwili.

Kitu ninachokiona hapa si mbunge kumuogopa mke mdogo, ni ubabe wa kinyama ambao hata mwenyezi mungu hapendi na adhabu yake tutaiona hapa hapa.

Mtu mwenye maamuzii ya kipuuzi na kinyama kwa mtoto aliyemzaa mwenyewe kwa umma ni shetani. Mafunzo ni mengi hapa hasa kwa wale tulio ndani ya ndoa, tunatarajia au tuliotarikiwa. Tunapofanya maamuzi tushirikiane hatujui nini kiko mbele yetu au la. Kuachana si kutengeneza uadui, you can keep the friendship to make days longer.

Felix tumuombee, repacation ya kitiu alichokifanya ataiona baadae siyo leo wala kesho, yeye anaona amefanya maamuzi mazuri kumbe siyo.
 
Kwa kuongezea, familia nyingi sana zinanyanyasika kwa kivuli cha " maswala ya kifamilia"- unyanyasaji uwe kwa mwanamke, mwanaume,mtoto,kikongwe, ukeketaji, ubakaji miongoni mwa wanafamilia, incest etc yote ni makosa makubwa na yenye kuleta madhara.Ni wakati muafaka wa kuondoa pazia hili la kijinga na kupinga vitendo vyote viovu vinavyotendekeka katika ngazi ya familia na kuendekezwa na jamii.Na inasikitisha zaidi pale vitendo hivi vinapotendwa na viongozi wenye dhamana ya kulinda na kutetea haki za jamii.Viongozi wetu wanapaswa kuongoza kwa mfano bora kuanzia ngazi ya familia zao.Kama JF tutafumbia macho vitendo kama hivi kwa kisingizio cha faragha ya familia basi tutakuwa wanafiki!
 
Naunga mkono kuwa hii ni issue ya kifamilia zaidi ila public interest sababu Baba ni Mhe. Analipwa kwa taxpayers money hivyo anapoteza sehemu ya his right to privacy ili wananchi wajue public na private conduct yake.
Kuzika kwa kuchoma ni moja ya njia za kisasa za body disporsal with body dignity kuliko decent burial with psychologil comfort on the eyes followed by ghasly decomposition in the cofin as long as it takes place iside the burial chamber and no foul smell comes out, hivyo its ok.
Uamuzi wa creamation naamini merehemu mwenyewe ndiye aliyeamua. Msimlaumu Mrema.
The last factor ni 'the Kenyan wife'. Jamani wanawake wa Kenya ni wakorofi sijapata kuona na kwenye misiba ni wababe mfano hakuna. Nilipota kushuhudia kisa cha Maehemu Mzee John Ondolo pale Sinza.
Mzee Ondolo ni Mjaluo wa Tanzania alioa Mkikuyu wa Kenya wakapata watoto 3. Wawili wa kike na mmoja wa kiume. Mwaka 1967, akahamia Tanzania na kununua eneo kubwa pale Sinza. Miaka ya 70 akatengana na mkewe, mama akarudi Kenya na watoto wa kike, baba akabaki Tanzania na mtoto wa kiume. Baadaye baba akaoa mke mwingine Mtanzania na kupata watoto wengine 3.
Mpaka mauti yalipomkuta, alikuwa na familia mpya na mwanae mkubwa wa kiume akijitegemea na familia yake ila wakati anaumwa, akamgawiya kila mtoto ardhi yake na kusisitiza atazikwa Dar.
Baada ya kutokea msiba, akatoka amri Kenya msizike mpaka Mke wa marehemu afike toka Kenya. Tulingoja for Two weeks tukiambiwa mke anawasubiri mabinti zake toka Marekani ndipo waandamane.
After 14 days, akaibuka binti,pekee na wakati huo tumeshatangaziwa mazishi ni kesho. Siku ya Mazishi, yule binti kwa ujasiri mkubwa na macho makavu, akatangaza, wametumwa na mama yao kuichukua- maiti ya mumewe kumpelekea Kenya kwa mazishi, akitoa hoja yeye ndiye mke wa ndoa in total disregard of subsisting family. Ni ugomvi tena ukalipuka na ugomvi mwingine wakitaka hati za ardhi na milki ya mali zake zote!. Baada ya vuta nikuvute, uamuzi ulifikiwa mazishi yakafanyika Dar lakini maiti ilikaa mortual zaidi ya mwezi, kisa Mke Mkenya. Mrema hili ameamua kuliepuka kwa kumake a long story short kwa kumalizia kila kitu Marekani.
 
Naunga mkono kuwa hii ni issue ya kifamilia zaidi ila public interest sababu Baba ni Mhe. Analipwa kwa taxpayers money hivyo anapoteza sehemu ya his right to privacy ili wananchi wajue public na private conduct yake.
Kuzika kwa kuchoma ni moja ya njia za kisasa za body disporsal with body dignity kuliko decent burial with psychologil comfort on the eyes followed by ghasly decomposition in the cofin as long as it takes place iside the burial chamber and no foul smell comes out, hivyo its ok.
Uamuzi wa creamation naamini merehemu mwenyewe ndiye aliyeamua. Msimlaumu Mrema.
The last factor ni 'the Kenyan wife'. Jamani wanawake wa Kenya ni wakorofi sijapata kuona na kwenye misiba ni wababe mfano hakuna. Nilipota kushuhudia kisa cha Maehemu Mzee John Ondolo pale Sinza.Mzee Ondolo ni Mjaluo wa Tanzania alioa Mkikuyu wa Kenya wakapata watoto 3. Wawili wa kike na mmoja wa kiume. Mwaka 1967, akahamia Tanzania na kununua eneo kubwa pale Sinza. Miaka ya 70 akatengana na mkewe, mama akarudi Kenya na watoto wa kike, baba akabaki Tanzania na mtoto wa kiume. Baadaye baba akaoa mke mwingine Mtanzania na kupata watoto wengine 3.
Mpaka mauti yalipomkuta, alikuwa na familia mpya na mwanae mkubwa wa kiume akijitegemea na familia yake ila wakati anaumwa, akamgawiya kila mtoto ardhi yake na kusisitiza atazikwa Dar.
Baada ya kutokea msiba, akatoka amri Kenya msizike mpaka Mke wa marehemu afike toka Kenya. Tulingoja for Two weeks tukiambiwa mke anawasubiri mabinti zake toka Marekani ndipo waandamane.
After 14 days, akaibuka binti,pekee na wakati huo tumeshatangaziwa mazishi ni kesho. Siku ya Mazishi, yule binti kwa ujasiri mkubwa na macho makavu, akatangaza, wametumwa na mama yao kuichukua- maiti ya mumewe kumpelekea Kenya kwa mazishi, akitoa hoja yeye ndiye mke wa ndoa in total disregard of subsisting family. Ni ugomvi tena ukalipuka na ugomvi mwingine wakitaka hati za ardhi na milki ya mali zake zote!. Baada ya vuta nikuvute, uamuzi ulifikiwa mazishi yakafanyika Dar lakini maiti ilikaa mortual zaidi ya mwezi, kisa Mke Mkenya. Mrema hili ameamua kuliepuka kwa kumake a long story short kwa kumalizia kila kitu Marekani.

Naheshimu mawazo yako..
lakini napenda kukusisitizia kuwa chanzo cha yote haya si the kenyan wife factor bali ni a mixture of midlife crisis ambayo mheshimiwa alishindwa kui manage na pia opportunism kwa upande wa mwanamke mpya - sitasema huyu ni mke wa ndoa!Sidhani ni sahihi kuhukumu kuwa wanawake wote wa kenya ni wakorofi.
Kinachotekea kwenye hili ni matokeo ( aftermath) ya ndoa iliyogeuka chungu baada ya mmoja kupata nyumba ndogo.Hakuna haja ya details ambazo kuzileta hapa itakuwa ni kuingilia undani na faragha ya wahusika na itakuwa umbeya!
The bottom line is kunyanyasa na kutumia nguvu ya pesa ambazo pengine hata anayenyanyaswa ana haki nazo japo hana access nazo.Isitoshe huyo mwanamke mwingine naye amemkimbia mumewe na kumfuata mheshimiwa sababu ya pesa!Kwa hiyo hapo hata morally its a wrong start.Ila si juu yetu kuyajadili zaidi.
 
Naunga mkono kuwa hii ni issue ya kifamilia zaidi ila public interest sababu Baba ni Mhe. Analipwa kwa taxpayers money hivyo anapoteza sehemu ya his right to privacy ili wananchi wajue public na private conduct yake.
Kuzika kwa kuchoma ni moja ya njia za kisasa za body disporsal with body dignity kuliko decent burial with psychologil comfort on the eyes followed by ghasly decomposition in the cofin as long as it takes place iside the burial chamber and no foul smell comes out, hivyo its ok.
Uamuzi wa creamation naamini merehemu mwenyewe ndiye aliyeamua. Msimlaumu Mrema.
The last factor ni 'the Kenyan wife'. Jamani wanawake wa Kenya ni wakorofi sijapata kuona na kwenye misiba ni wababe mfano hakuna. Nilipota kushuhudia kisa cha Maehemu Mzee John Ondolo pale Sinza.
Mzee Ondolo ni Mjaluo wa Tanzania alioa Mkikuyu wa Kenya wakapata watoto 3. Wawili wa kike na mmoja wa kiume. Mwaka 1967, akahamia Tanzania na kununua eneo kubwa pale Sinza. Miaka ya 70 akatengana na mkewe, mama akarudi Kenya na watoto wa kike, baba akabaki Tanzania na mtoto wa kiume. Baadaye baba akaoa mke mwingine Mtanzania na kupata watoto wengine 3.
Mpaka mauti yalipomkuta, alikuwa na familia mpya na mwanae mkubwa wa kiume akijitegemea na familia yake ila wakati anaumwa, akamgawiya kila mtoto ardhi yake na kusisitiza atazikwa Dar.
Baada ya kutokea msiba, akatoka amri Kenya msizike mpaka Mke wa marehemu afike toka Kenya. Tulingoja for Two weeks tukiambiwa mke anawasubiri mabinti zake toka Marekani ndipo waandamane.
After 14 days, akaibuka binti,pekee na wakati huo tumeshatangaziwa mazishi ni kesho. Siku ya Mazishi, yule binti kwa ujasiri mkubwa na macho makavu, akatangaza, wametumwa na mama yao kuichukua- maiti ya mumewe kumpelekea Kenya kwa mazishi, akitoa hoja yeye ndiye mke wa ndoa in total disregard of subsisting family. Ni ugomvi tena ukalipuka na ugomvi mwingine wakitaka hati za ardhi na milki ya mali zake zote!. Baada ya vuta nikuvute, uamuzi ulifikiwa mazishi yakafanyika Dar lakini maiti ilikaa mortual zaidi ya mwezi, kisa Mke Mkenya. Mrema hili ameamua kuliepuka kwa kumake a long story short kwa kumalizia kila kitu Marekani.

Hapo umelonga mkulu,tatizo watu wanachangia tu bila kujua ni nini kipo nyuma ya pazia...Tatizo ni kwamba ishu hii imeshaanza kuwekwa kisiasa(kila kitu politiki tuuuuu,inaboa jama),mfanop angalia maoni haya ya wasomaji wa habari hii Maiti ya mtoto wa mbunge yazua mzozo na haya Mbunge aenda Marekani ‘kumzika' bintiye
 
Kama kweli Mh Mrema amekwenda Marekani kufanya mazishi ya mtoto wake bila ya kumaliza tofauti zake na mkewe basi huyu Mheshimiwa hawezi kukwepa kujadiliwa hapa.

Siku zote tumekuwa na desturi za kuwakoma watu hapa mpaka kieleweke hasa tulisema kama hao watu ni 'public figures'. Sababu kubwa ni kuwa tunaamini kiongozi ambaye anasjika ofisi ya umma anapaswa kuwa ni kioo katika jamii yetu ili aweze kuamini kwa yale anayotakiwa kuyatekeleza.

kitendo cha yeye (kwa hali yeyote ile) kuondoka kwenda Marekani na kumwacha Mkewe akilalamika hatuwezi tukanyamaza wakati mheshimiwa mwenyewe hajajitokeza kujibu hizo tuhuma zinazotolewa na huyo mama. Mrema kama kiongozi inaonesha kutokumudu mazingira yake kwa upande wa kusimamia haki ndani ya familia yake. Kuna wengine wamechangia kuwa Mheshimiwa yuko underpressure ya Bi Mdogo, hii inawezekana maana haingii akilini kabisa kutoafikiana na mkeo juu ya hatima ya mazishi ya mtoto ambaye yeye aliibeba mimba kwa muda wa miezi tisa na akjifungua kwa uchungu. Kama jambo hili wakuu wengine wanatakalinyamaziwe basi ni kweli mna-double standards kwani kama ambavyo wameandika wachangiaji wengine kuwa ni public figures ngapi zilijadiliwa kwa mapana na marefu juu ya mambo yao ya ndani?

Mimi sikubaliani kabisa na kitendo cha Mheshimiwa kutoafikiana na mkewe juu ya jambo hili.

Mwisho kwa wale ambao wana-generalize kuwa wanawake wa kikenya wanatabia kama alizozitaja, basi hana budi kutumia neno 'baadhi' kwani ukichulia kuwa wanawake wote wakenya wako hivyo tunakuona wewe si mkweli kwani huna data zilizotafitiwa kisayansi zinazoweza kukupa mamlaka ya kusema hivyo, otherwise ukiendelea na msimamo bila ya data tutakuona umedhamiria kupiga kelele kama za debe tupu
 
Hapo umelonga mkulu,tatizo watu wanachangia tu bila kujua ni nini kipo nyuma ya pazia...Tatizo ni kwamba ishu hii imeshaanza kuwekwa kisiasa(kila kitu politiki tuuuuu,inaboa jama),mfanop angalia maoni haya ya wasomaji wa habari hii Maiti ya mtoto wa mbunge yazua mzozo na haya Mbunge aenda Marekani ‘kumzika’ bintiye

Mkuu kwa heshima zote, nadhani ni sahihi kusema kuwa ishu hii ni multi-dimensional - lina siasa maana mhusika mmoja ni mwanasiasa au public figure.Pia ni la kijamii kwa maana lina mahusiano yakijamii humo ndani.Ni la kisheria kwa maana lina masuala ya haki na wajibu,ni la kidini kwa maana linahusu safari ya mwisho ya mwanadamu.Lina mambo mengi mtambuka.Afterall, what is politics? Everthing in life can be political! Unless wewe na wengine mnaoona tofauti mtujuze zaidi tujue mnaposema siasa mna maana gani.
 
Mkuu kwa heshima zote, nadhani ni sahihi kusema kuwa ishu hii ni multi-dimensional - lina siasa maana mhusika mmoja ni mwanasiasa au public figure.Pia ni la kijamii kwa maana lina mahusiano yakijamii humo ndani.Ni la kisheria kwa maana lina masuala ya haki na wajibu,ni la kidini kwa maana linahusu safari ya mwisho ya mwanadamu.Lina mambo mengi mtambuka.Afterall, what is politics? Everthing in life can be political! Unless wewe na wengine mnaoona tofauti mtujuze zaidi tujue mnaposema siasa mna maana gani.

Nimekuelewa mkuu...Lazima kutakuwa kuna sababu iliyopo nyuma ya sakata hili,kwa nini Mrema akatae mwanae asizikwe Tanzania???,lazima kuna sababu/tatizo hapa,na jibu la tatizo hili wanalo wana familia wenyewe so si busara kuanza kulaumu mojawapo ya pande katika sakata hili bila kujua hasa sababu ya Mrema kuchukua maamuzi hayo....Kuhusu politics ni kwamba nilitaka kuonesha ni jinsi gani habari hii ilivypokelewa na wananchi wengine ambapo wametoa maoni juu ya habari hii na wengine kujaribu kuihusisha moja kwa moja CCM na sakata hili(soma maoni ya wasomaji kwenye link hizo hapo juu)...Otherwise nimekuelewa mkuu na ubarikiwe sana
 
Naunga mkono kuwa hii ni issue ya kifamilia zaidi ila public interest sababu Baba ni Mhe. Analipwa kwa taxpayers money hivyo anapoteza sehemu ya his right to privacy ili wananchi wajue public na private conduct yake.
Kuzika kwa kuchoma ni moja ya njia za kisasa za body disporsal with body dignity kuliko decent burial with psychologil comfort on the eyes followed by ghasly decomposition in the cofin as long as it takes place iside the burial chamber and no foul smell comes out, hivyo its ok.
Uamuzi wa creamation naamini merehemu mwenyewe ndiye aliyeamua. Msimlaumu Mrema.
The last factor ni 'the Kenyan wife'. Jamani wanawake wa Kenya ni wakorofi sijapata kuona na kwenye misiba ni wababe mfano hakuna. Nilipota kushuhudia kisa cha Maehemu Mzee John Ondolo pale Sinza.
Mzee Ondolo ni Mjaluo wa Tanzania alioa Mkikuyu wa Kenya wakapata watoto 3. Wawili wa kike na mmoja wa kiume. Mwaka 1967, akahamia Tanzania na kununua eneo kubwa pale Sinza. Miaka ya 70 akatengana na mkewe, mama akarudi Kenya na watoto wa kike, baba akabaki Tanzania na mtoto wa kiume. Baadaye baba akaoa mke mwingine Mtanzania na kupata watoto wengine 3.
Mpaka mauti yalipomkuta, alikuwa na familia mpya na mwanae mkubwa wa kiume akijitegemea na familia yake ila wakati anaumwa, akamgawiya kila mtoto ardhi yake na kusisitiza atazikwa Dar.
Baada ya kutokea msiba, akatoka amri Kenya msizike mpaka Mke wa marehemu afike toka Kenya. Tulingoja for Two weeks tukiambiwa mke anawasubiri mabinti zake toka Marekani ndipo waandamane.
After 14 days, akaibuka binti,pekee na wakati huo tumeshatangaziwa mazishi ni kesho. Siku ya Mazishi, yule binti kwa ujasiri mkubwa na macho makavu, akatangaza, wametumwa na mama yao kuichukua- maiti ya mumewe kumpelekea Kenya kwa mazishi, akitoa hoja yeye ndiye mke wa ndoa in total disregard of subsisting family. Ni ugomvi tena ukalipuka na ugomvi mwingine wakitaka hati za ardhi na milki ya mali zake zote!. Baada ya vuta nikuvute, uamuzi ulifikiwa mazishi yakafanyika Dar lakini maiti ilikaa mortual zaidi ya mwezi, kisa Mke Mkenya. Mrema hili ameamua kuliepuka kwa kumake a long story short kwa kumalizia kila kitu Marekani.

Pasco! Umetoa mfano usiolingana na ishu inayozungumzwa. Ninatofautiana na wewe katika yafuatayo:

1) Umewakumu waKenya wote kwa kitendo cha Mrs Ondolo. Umehukumu taifa lote kwa kitu ambacho kinaongozwa zaidi na mila za kabila na hulka ya mtu anayehusika. Haukuwatendea haki waKenya.

2) Unadai MKE wa Kikuyu amemtuma BINTI yake aende kwa wakwe zake akadai mwili wa mume waliyetengana miaka mingi iliyopita! Unataka kutuambia kuwa kwa wakikuyu mume anazikwa kwa mke? Huyo mzee Ondolo hakuwa na ndugu wa kiume hadi wakamwachia huyo binti awachanganye? Au unatufanya sisi wote hapa si waafrika? Hatuzipendi baadhi ya mila zetu lakini tunazijua!

3) Unasema mwili ulikaa mortuary kwa zaidi ya mwezi wakati umesema kuwa mlimsubiri mke mkubwa kwa wiki 2! Kwa msisitizo umesema binti aliwasili baada ya 14 days na mazishi yalikuwa kesho yake! Au mwezi wako una siku 14?

4) Kutaka kujua mali za mzazi wako marehemu ni kitu cha kawaida. Wewe kama mtu uliyebobea katika sheria ni lazima ujue kuwa hata wangechukua hati isingewasaidia kitu maana wengine wangeweza kuweka pingamizi katika mabidiliko yoyote ya hati. Unapaswa kujua vile vile kuwa mtu hawezi kuchukua milki mazikoni. Kuna taratibu na kama ndugu wamesoma kidogo wanajua kuna sheria za mirathi. Lakini sishangai kwa mtu ambaye hakuwa karibu na baba yake kutaka kujua mali alizomiliki marehemu. Yeye kama mtoto ana haki unless mzazi wake amemfuta kimaandishi katika mirathi yake!

5) Haujatuambia vile vile kama walipotengana waligawana walichochuma wakati wa ndoa yao? Je, huyo mama alikatiwa sehemu ya lile eneo kubwa la pale Sinza au kama kawaida yetu alitolewa nje na mzee akabaki na eneo lake? Haujatuambia kama marehemu katika mgao aliofanya wa hilo eneo kama aliwakumbuka binti zake?

6)Huyu mama wa marehemu hajaomba mwili wa marehemu ukazikwe kwao Kenya bali anataka ukazikwe kwa mumewe waliyetengana. Mume ndiye anayedai mtoto wake azikwe ugenini. Huyu ni mtu anayetoka katika kabila ambalo hata kuzika Dar es Salaamu wanaona shida hadi wamrudishe marehemu kwao!

7) Mara nyingi sisi wanaume tunajisahau kuwa mwenye uhakika wa uzazi wa mtoto ni mwanamke. Yeye ndiye aliyembeba na ndiye aliyemzaa. Sisi ni wasindikizaji tuu. Kwa hali hiyo si haki kumzuia mama wa mtoto hata kama mmekorofishana vipi kumzika mwanae! Kwa bahati mbaya tabia anayoonyesha huyu mheshimiwa ni kawaida mno kwetu wanaume wakiafrika. Arrogance na ubabe usio na sababu wala mpaka!

Kama alivyosema WomenofSubstanc, mara nyingi tunatumia kisingizio cha mambo ya kifamilia kufanya dhulma. Na mara nyingi tunafanya hivyo kumkomoa yule tuliyetofautiana.

Hata mseme vipi, this thing stinks!

Amandla.....
 


5) Haujatuambia vile vile kama walipotengana waligawana walichochuma wakati wa ndoa yao? Je, huyo mama alikatiwa sehemu ya lile eneo kubwa la pale Sinza au kama kawaida yetu alitolewa nje na mzee akabaki na eneo lake? Haujatuambia kama marehemu katika mgao aliofanya wa hilo eneo kama aliwakumbuka binti zake?

6)Huyu mama wa marehemu hajaomba mwili wa marehemu ukazikwe kwao Kenya bali anataka ukazikwe kwa mumewe waliyetengana. Mume ndiye anayedai mtoto wake azikwe ugenini. Huyu ni mtu anayetoka katika kabila ambalo hata kuzika Dar es Salaamu wanaona shida hadi wamrudishe marehemu kwao!

7) Mara nyingi sisi wanaume tunajisahau kuwa mwenye uhakika wa uzazi wa mtoto ni mwanamke. Yeye ndiye aliyembeba na ndiye aliyemzaa. Sisi ni wasindikizaji tuu. Kwa hali hiyo si haki kumzuia mama wa mtoto hata kama mmekorofishana vipi kumzika mwanae! Kwa bahati mbaya tabia anayoonyesha huyu mheshimiwa ni kawaida mno kwetu wanaume wakiafrika. Arrogance na ubabe usio na sababu wala mpaka!

Kama alivyosema WomenofSubstanc, mara nyingi tunatumia kisingizio cha mambo ya kifamilia kufanya dhulma. Na mara nyingi tunafanya hivyo kumkomoa yule tuliyetofautiana.

Hata mseme vipi, this thing stinks!

Amandla.....

Mkuu nimefurahishwa sana na points zako zote, lakini nimenukuu hizi chache ambazo nadhani zimesimamia kanuni muhimu ya haki!Pia nimefarijika kuona kuwa kuna wanaume wenye kuwa objective linapokuja swala na mahusiano kama hili maana aghalabu wengi hawaoni mapana na marefu ya tatizo.Huliangalia kwa wepesi sana.Ishu hii imenifanya nikumbuka thread za nyuma kuhusu wanawake kulinda ndoa zao zisivunjike kwa kuhofia madhila yatakayowapata watoto wao.Hapa tunaona pia upande mwingine wa shilingi - madhila yanayowapata wanawake wenye kulinda ndoa zao hadi watoto wanapokuwa watu wazima na kujitegemea na wao kubaki bila!Mungu aendelee kuwa na huruma na awaangazie wale wote wenye mioyo ya dhuluma ilainike watende haki.

Uendelee kubarikiwa Mkuu ili uwe kioo kwa jamii.
 
Naunga mkono kuwa hii ni issue ya kifamilia zaidi ila public interest sababu Baba ni Mhe. Analipwa kwa taxpayers money hivyo anapoteza sehemu ya his right to privacy ili wananchi wajue public na private conduct yake.
Kuzika kwa kuchoma ni moja ya njia za kisasa za body disporsal with body dignity kuliko decent burial with psychologil comfort on the eyes followed by ghasly decomposition in the cofin as long as it takes place iside the burial chamber and no foul smell comes out, hivyo its ok.
Uamuzi wa creamation naamini merehemu mwenyewe ndiye aliyeamua. Msimlaumu Mrema.
The last factor ni 'the Kenyan wife'. Jamani wanawake wa Kenya ni wakorofi sijapata kuona na kwenye misiba ni wababe mfano hakuna. Nilipota kushuhudia kisa cha Maehemu Mzee John Ondolo pale Sinza.
Mzee Ondolo ni Mjaluo wa Tanzania alioa Mkikuyu wa Kenya wakapata watoto 3. Wawili wa kike na mmoja wa kiume. Mwaka 1967, akahamia Tanzania na kununua eneo kubwa pale Sinza. Miaka ya 70 akatengana na mkewe, mama akarudi Kenya na watoto wa kike, baba akabaki Tanzania na mtoto wa kiume. Baadaye baba akaoa mke mwingine Mtanzania na kupata watoto wengine 3.
Mpaka mauti yalipomkuta, alikuwa na familia mpya na mwanae mkubwa wa kiume akijitegemea na familia yake ila wakati anaumwa, akamgawiya kila mtoto ardhi yake na kusisitiza atazikwa Dar.
Baada ya kutokea msiba, akatoka amri Kenya msizike mpaka Mke wa marehemu afike toka Kenya. Tulingoja for Two weeks tukiambiwa mke anawasubiri mabinti zake toka Marekani ndipo waandamane.
After 14 days, akaibuka binti,pekee na wakati huo tumeshatangaziwa mazishi ni kesho. Siku ya Mazishi, yule binti kwa ujasiri mkubwa na macho makavu, akatangaza, wametumwa na mama yao kuichukua- maiti ya mumewe kumpelekea Kenya kwa mazishi, akitoa hoja yeye ndiye mke wa ndoa in total disregard of subsisting family. Ni ugomvi tena ukalipuka na ugomvi mwingine wakitaka hati za ardhi na milki ya mali zake zote!. Baada ya vuta nikuvute, uamuzi ulifikiwa mazishi yakafanyika Dar lakini maiti ilikaa mortual zaidi ya mwezi, kisa Mke Mkenya. Mrema hili ameamua kuliepuka kwa kumake a long story short kwa kumalizia kila kitu Marekani.


Inawezekana ikiwa ni hivyo ila ukweli utabaki pale pale kwamba katika hilo alimnyima haki yake ya msingi Mkewe (Milcah) maana alitakiwa kumjulisha katika maamuzi hayo kutokana na nafasi yake katika hilo.
 
Pasco! Umetoa mfano usiolingana na ishu inayozungumzwa. Ninatofautiana na wewe katika yafuatayo:

1) Umewakumu waKenya wote kwa kitendo cha Mrs Ondolo. Umehukumu taifa lote kwa kitu ambacho kinaongozwa zaidi na mila za kabila na hulka ya mtu anayehusika. Haukuwatendea haki waKenya.

2) Unadai MKE wa Kikuyu amemtuma BINTI yake aende kwa wakwe zake akadai mwili wa mume waliyetengana miaka mingi iliyopita! Unataka kutuambia kuwa kwa wakikuyu mume anazikwa kwa mke? Huyo mzee Ondolo hakuwa na ndugu wa kiume hadi wakamwachia huyo binti awachanganye? Au unatufanya sisi wote hapa si waafrika? Hatuzipendi baadhi ya mila zetu lakini tunazijua!

3) Unasema mwili ulikaa mortuary kwa zaidi ya mwezi wakati umesema kuwa mlimsubiri mke mkubwa kwa wiki 2! Kwa msisitizo umesema binti aliwasili baada ya 14 days na mazishi yalikuwa kesho yake! Au mwezi wako una siku 14?

4) Kutaka kujua mali za mzazi wako marehemu ni kitu cha kawaida. Wewe kama mtu uliyebobea katika sheria ni lazima ujue kuwa hata wangechukua hati isingewasaidia kitu maana wengine wangeweza kuweka pingamizi katika mabidiliko yoyote ya hati. Unapaswa kujua vile vile kuwa mtu hawezi kuchukua milki mazikoni. Kuna taratibu na kama ndugu wamesoma kidogo wanajua kuna sheria za mirathi. Lakini sishangai kwa mtu ambaye hakuwa karibu na baba yake kutaka kujua mali alizomiliki marehemu. Yeye kama mtoto ana haki unless mzazi wake amemfuta kimaandishi katika mirathi yake!

5) Haujatuambia vile vile kama walipotengana waligawana walichochuma wakati wa ndoa yao? Je, huyo mama alikatiwa sehemu ya lile eneo kubwa la pale Sinza au kama kawaida yetu alitolewa nje na mzee akabaki na eneo lake? Haujatuambia kama marehemu katika mgao aliofanya wa hilo eneo kama aliwakumbuka binti zake?

6)Huyu mama wa marehemu hajaomba mwili wa marehemu ukazikwe kwao Kenya bali anataka ukazikwe kwa mumewe waliyetengana. Mume ndiye anayedai mtoto wake azikwe ugenini. Huyu ni mtu anayetoka katika kabila ambalo hata kuzika Dar es Salaamu wanaona shida hadi wamrudishe marehemu kwao!

7) Mara nyingi sisi wanaume tunajisahau kuwa mwenye uhakika wa uzazi wa mtoto ni mwanamke. Yeye ndiye aliyembeba na ndiye aliyemzaa. Sisi ni wasindikizaji tuu. Kwa hali hiyo si haki kumzuia mama wa mtoto hata kama mmekorofishana vipi kumzika mwanae! Kwa bahati mbaya tabia anayoonyesha huyu mheshimiwa ni kawaida mno kwetu wanaume wakiafrika. Arrogance na ubabe usio na sababu wala mpaka!

Kama alivyosema WomenofSubstanc, mara nyingi tunatumia kisingizio cha mambo ya kifamilia kufanya dhulma. Na mara nyingi tunafanya hivyo kumkomoa yule tuliyetofautiana.

Hata mseme vipi, this thing stinks!

Amandla.....

Kwanza nimekubali makosa ya blind generalization. Korrection sio wanawake wote wa Kenya ni wakorofi bali baadhi ya Wanawake ni wakorofi. Mistake regrated.
The first 14 days za kumsubiri Mke na mabinti toka Marekani. Mke hakuja bali Binti toka Marekani ndiye kaja. Kwa vile alikuwa akisubiriwa mke, baada tuu ya kuwasili dada mtu, jamaa wakatangaza mazishi yangefanyika kesho yake. Na ndipo dada akatangaza ujumbe wa mke kutaka mwili wa mumewe. Siku 14 za pili ni mgogoro wa wanandugu, mwili uende Kenya ama uzikwe hapa.
Masuala ya mali ni mambo ya familia.
Tuendelee na Janvi.
 
Back
Top Bottom