Je, eti open university programs hutoa elimu isiyokidhi kiwango cha kimataifa?

SOLOGWIGABA

Member
Aug 9, 2011
22
0
Jamani kuna mdogo wangu amemaliza Form six HGL mwaka juzi akapata Division 3 akiwa na principle tatu.Hata hivyo kulingana hali ya maisha kuwa ngumu niliamua kumtafutia kibarua amudu kujikimu mahitaji yake.Kwa sasa anaendelea na kibarua na nimemshauri mwaka huu ameomba Open University na amepata Mass Communication.Sasa tatizo kuna rafiki zake walioko vyuo mbalimbali kama UDOM,UDSM na kwingineko wanamshauri asisome Open eti kuwa kiwango cha elimu inayotolewa haikidhi kiwango cha kimataifa na kuwa OUT ni wasumbufu na hawaratibu vizuri Programs zao.Ndogo amekata tamaa na mimi napenda asome huku akifanya kazi kwa ajili ya kujikimu.Naomba ushauri wenu wakuu na ukweli kuhusu Open kwa wanaofahamu kwa kina hasa waliosoma au wanaoendelea kusoma OUT.
 
mpendwa,

usiwe na hofu, ukishasikia inaitwa "university" tena ya umma, iko kimataifa, labda mwanafunzi mwenyewe aboronge, kumbuka hiyo ni open na kama yuko katika open/distance mode anatakiwa kuwa na self discpline zaidi kwenye masomo vinginevyo itakuwa kazi kwelikweli. mi nawafahamu wengi tu wamesoma hapo na wapo walipata hata zile scholarship zenye ushindani mkali sana na kuendelea na masomo nje ya nchi na wakafanya vizuri tu huko

so kwa kifupi, binafsi sina wasiwasi na elimu ya pale!

ubarikiwe sana
 
Mwenye record za OUT kuhusu performance ukilinganisha ni vyuo vingine TZ ampe huyu bwana tafadhali dogo amuondoe hofu na fikra potovu.
 
Amina ubarikiwe pia na ninashukuru sana kwa ufafanuzi wako mzuri.Kama hautajari ningependa kujua location na addresse yako tafadhali
mpendwa,<br />
<br />
usiwe na hofu, ukishasikia inaitwa &quot;university&quot; tena ya umma, iko kimataifa, labda mwanafunzi mwenyewe aboronge, kumbuka hiyo ni open na kama yuko katika open/distance mode anatakiwa kuwa na self discpline zaidi kwenye masomo vinginevyo itakuwa kazi kwelikweli. mi nawafahamu wengi tu wamesoma hapo na wapo walipata hata zile scholarship zenye ushindani mkali sana na kuendelea na masomo nje ya nchi na wakafanya vizuri tu huko<br />
<br />
so kwa kifupi, binafsi sina wasiwasi na elimu ya pale!<br />
<br />
ubarikiwe sana
<br />
<br />
 
Mwenye record za OUT kuhusu performance ukilinganisha ni vyuo vingine TZ ampe huyu bwana tafadhali dogo amuondoe hofu na fikra potovu.
in what sense??
maana hakuna utofauti na vyuo vingine, people graduate and acquire jobs, scholarships, promotion etc. tatizo wa tz sisi ni wagumu wa kufanya utafiti, utakuta mtu anaongea kuhusu ishu fulani bila ushahidi wala ukweli na usishangae wengine hata website ya OUT hawajapitia. duh tz hili jamani
wenzetu wanakimbia sisi tunatambaa tu..... namshauri huyo dada afanye utafiti, tembelea website, fika hata campus ilipo uone hata customer services yao, maktaba, na takwimu mbalimbali. hapo utajiridhisha kwamba ujiunge au usijiunge vinginevyo nawewe upo kwenye mkumbo wa wa tz tusiopenda kusoma, kutafakari, kutafiti ila tunapenda unafiki, majungu, wivu, na pia si wazalendo.....
 
Mpeleke dogo akasome OUT, Wenzio tulimalizia hapo na tukiwa kazini performance yetu iko juu sana, maana miaka yote anayosoma out vile vile ni kama anakuwa field akifanya research na ku-solve matatzo in real life situation. Dogo akasome Out bwana!
 
open haina tatizo,mi nmefundshwa chuo fulan hapa bongo na malecturer wa2 ambao wamesoma OUT first degree na masters na walikuwa safi sana kuliko hata wale waliosoma wapi cjui...akasome tu
 
in what sense??
maana hakuna utofauti na vyuo vingine, people graduate and acquire jobs, scholarships, promotion etc. tatizo wa tz sisi ni wagumu wa kufanya utafiti, utakuta mtu anaongea kuhusu ishu fulani bila ushahidi wala ukweli na usishangae wengine hata website ya OUT hawajapitia. duh tz hili jamani
wenzetu wanakimbia sisi tunatambaa tu..... namshauri huyo dada afanye utafiti, tembelea website, fika hata campus ilipo uone hata customer services yao, maktaba, na takwimu mbalimbali. hapo utajiridhisha kwamba ujiunge au usijiunge vinginevyo nawewe upo kwenye mkumbo wa wa tz tusiopenda kusoma, kutafakari, kutafiti ila tunapenda unafiki, majungu, wivu, na pia si wazalendo.....

Wiki iliyopita kuna mtu alipost thread hapa kuonyesha ranking za vyuo hapa Afrika.
Katika vyuo vikuu vya Tanzania, OUT ilisimama katika nafasi ya NNE!!
DOGO kaza buti, Open ni chuo kizuri tu, fuata maoni ya hapo juu, quote.
 
Wiki iliyopita kuna mtu alipost thread hapa kuonyesha ranking za vyuo hapa Afrika.
Katika vyuo vikuu vya Tanzania, OUT ilisimama katika nafasi ya NNE!!
DOGO kaza buti, Open ni chuo kizuri tu, fuata maoni ya hapo juu, quote.

kwa kifupi, kila nyanja hapa nchini ina regulator. mfano; mabenki regulator ni BOT, usafiri-SUMATRA, nishati-EWURA, mawasiliano-TCRA na elimu ya juu ni TCU. sasa kila chuo hapa nchini kinatambuliwa na TCU na hawawezi kuanzisha kozi, idara, faculty bila kupeleka proposal TCU. tunakoelekea hata exams zitakuwa znapitiwa na TCU b4 hazijafanywa(TCU wanaendelea kujipanga katika hili).
kuhusu rankings za vyuo; hapa criteria/vigezo vinavyotumika ni vingi.mfano, idadi ya walimu, ubora wa learning facilities eg library, no of students graduating per yr, ushirikiano wa chuo na vyuo vya nje, idadi ya academic/research paper or publishments/machapisho yaliyotolewa na chuo mfano, udsm ni kubwa ilianza 1961 na tumaini 2002, OUT 1994....how can u rate them???
suala la uwezo wa mwanafunzi wa chuo ni juhudi za mwanafunzi kwa 75%, wewe unatakiwa ujisomee, utafiti, uwe curious, nk. utakuta mtu anamaliza chuo hajui kuzungumza english, hapa ni chuo au yeye???
tafakari
 
Dah, hakika katika thread hii hata mimi nimepata faida kubwa kwa maana watu wanapenda sana kupotosha wenzao.
 
Naomba kujua Foundation Course huwa yanafundishwa masomo gani? Ngugu yangu aliomba akasome degree ya Environmental Science, lakini amepata ya kusomea Foundation.
 
Naomba kujua Foundation Course huwa yanafundishwa masomo gani? Ngugu yangu aliomba akasome degree ya Environmental Science, lakini amepata ya kusomea Foundation.

foundation ina parts 3 nazo ni arts, science na business studies
SCIENCE
1. communication skills
2. physics
3. chemistry
4. biology
5. development studies
arts;
1. english
2.comm skills
3.history
4. geography
5. dev studies
pia tembelea www.out.ac.tz upate prospectus kwa ufafanuzi zaidi
 
Back
Top Bottom