Je, duniani tumekuja kama adhabu baada ya kufanya makosa Mbinguni?

Zero IQ

JF-Expert Member
Dec 21, 2016
13,917
24,674
Je, Duniani tumekuja kama Adhabu baada ya kufanya Makosa mbinguni?

Kabla ya baadhi yetu kuja Duniani inawezekana sisi binadamu wote makazi yetu na Nyumbani kwetu kwa Asili ni mbinguni,
Na hapa duniani ni kama Gerezani tu tunakuja baada ya kufanya makosa huko tunaletwa hapa ili kutumikia kifungo cha Adhabu (Gerezani).

inaonekana Nyumbani kwetu kwa Asili ambako ni mbinguni kuna Teknolojia ya Hali ya juu na ndio maana ukihukumiwa kifungo chako unaletwa gerezani ambako ni duniani kwa namna ya Ajabu bila kujitambua

Kwanza unafutwa kumbukumbu zako zote halafu unaletwa duniani (kifungoni) kama mtoto, utaishi kulingana na muda uliohukumiwa kutumikia

Na baada ya kumaliza kifungo chako Unakufa na kurudi utokako (Mbinguni) kama Roho alafu kwa sababu ya ukubwa wa Teknolojia iliyopo kule Roho yako inarudishwa kwenye umbo lake na kuruhusiwa kuendelea kuishi na jamii yako,

Wapo watakaouliza kama hii ni kweli inakuaje kwa wale watoto wanaotolewa mimba kabla ya kuzaliwa kifungo chao kilikuwaje?

Hapa jibu ni kwamba kule mbinguni kwenye Nchi yetu ya Asili hukumu zake zinatolewa kulingana na ukubwa wa kosa ulilolitenda,
Mfano kuna Ambao waliohukumiwa wiki mbili Gerezani, Mwezi, siku na ndio hao (Mimba) zinazotolewa(kifungo kimeisha wanarudi mbinguni )

Na kuna ambao waliohukumiwa miaka kadhaa (Ndio sisi tuliozaliwa ishi na wengine kuzeeka). Kifungo kikiisha tunakufa tunarudi tulikotoka.

Kuna ambao wamehukumiwa kifungo na Mateso makubwa, Kuna wa vifungo tu, pia kuna wale wamehukumiwa vifungo na kazi nzito.

Na ndio maana Duniani (Gerezani ) kila binadamu anaeishi ana Shida zake, ndio maana binadamu hatuko sawa tunatofautiana,

Ni kwa sababu hapa ni Gerezani kila binadamu anatumikia kifungo chake kwa mujibu wa hukumu na makosa aliyoyafanya akiwa Mbinguni.

Siku tukimaliza Vifungo Vyetu tunarudi kule tulikotoka kujumuika na Jamaa zetu.
 
Kwanza unafutwa kumbukumbu zako zote alafu unaletwa duniani(kifungoni) kama mtoto,utaishi kulingana na muda uliohukumiwa kutumikia
Tatizo ni kuwa kama tunafutwa kumbukumbu zote tusikumbuke tulikotoa manake hiyo ni siri nzito, ambayo imewekwa na hao wenye technolojia ya hali ya juu sana.

Sasa kwa nini teknolojia hiyo ikawa imeshindwa kuwazuia watu kama zero IQ Wasiweze kufikiria jambo hilo ?
 
Kwa nini umekuwa na mtazamo huo?
Hii ni baada ya kusoma na kupitia vitabu vingi vya kumuelezea Mungu ambae kwa mujibu ni Muumbaji wa yote,
Maandiko hayo yote yanaelezea sifa, na ukarimu wa mungu,
"Kwamba yeye ni wa haki,hana upendeleo,anatoa kwa wote"

Kwa kupitia hoja ya hapo juu ndio nikaja na Reason hii kwamba Duniani hapa ni Gerezani, Kwa maana hiyo kama "mungu ni wa haki, hana upendeleo, anatoa kwa wote".

Basi binadamu wote tungeumbwa sawa bila upendeleo,wote tungeumbwa kwa usawa kusingekuwa na walemavu, Maskini,wala madaraja ya Rangi,(weusi, weupe, orange na Nk. )

Ila kwa kuwa duniani ni Gerezani ndio maana tumekuja hivyo kwa Categories mbali mbali ni kama Adhabu ili kutumikia vifungo kulingana na Makosa tuliyoyatenda.
 
Tatizo ni kuwa kama tunafutwa kumbukumbu zote tusikumbuke tulikotoa manake hiyo ni siri nzito,ambayo imewekwa na hao wenye technolojia ya hali ya juu sana.

Sasa kwa nini teknolojia hiyo ikawa imeshindwa kuwazuia watu kama zero IQ Wasiweze kufikiria jambo hilo ?
Ok technologia hiyo imenifuta kila kitu ila kwa kuwa tunaletwa na kuwa Na Akili ndio maana nimepata uwezo wa kureason, lakini kwa kuwa nimefutwa na kupewa Akili ndio maana nimereason lakini sina ushahidi na wala uhakika kama hayo ninayosema ni ya kweli kwa maana nyingine Nimebashili tu.
.
 
Ok technologia hiyo imenifuta kila kitu ila kwa kuwa tunaletwa na kuwa Na Akili ndio maana nimepata uwezo wa kureason, lakini kwa kuwa nimefutwa na kupewa Akili ndio maana nimereason lakini sina ushahidi na wala uhakika kama hayo ninayosema ni ya kweli kwa maana nyingine Nimebashili tu.
.
hahahah poa mkuu.

Sina shida na kubashiri mkuu.

Mawazo ni mapana sana.

Ila dhana inakuwa ileile kwamba"ukijiona upo duniani basi jua utaishi milele"
 
Aisee nilkua naskia watu wanakusifia ila kwa uzi huu nimekukubali.


Hii hoja ni nzito na fikirishi sana. Ndo maana duniani hapajawahi kua na raha. Ni mwendo wa fujo.
Nawasubiri watu wazito wazito waje tujadili hapa
 
Sikubaliani na wewe MKUU,, kama dunia ni gereza mbona watu wanaendelea kufanya makosa? mfano kuua,,kudhulumu,,uzinzi? Nk..na kama ni kweli tumehukumiwa kwa makosa ya nyuma huko mbingunj hawa MITUME NA MANABII LUKUKI WALILETWA HUKU GEREZANI KUFANYA NN?
Hayo makosa uliyoyaeleza ni kama Fujo za gerezani tu hizo mkuu(Refer matukio yanayotokea magerezani hapa hapa duniani ) then rudi kwenye Hoja yako.
 
Back
Top Bottom