Je, Dini Zote Zinaelekeza Watu kwa Mungu Yuleyule?

allagail

Member
Dec 25, 2016
7
6
“Mimi nina dini yangu mwenyewe, na siwezi kuiacha. Isitoshe, dini si hoja, kwa kuwa dini zote zinaelekeza watu kwa Mungu yuleyule.”

JE, UMEWAHI kumsikia mtu akisema hivyo? Watu wengi wanaamini kwamba dini yoyote inaweza kumsaidia mtu kumjua Mungu na kuelewa maana ya maisha. Vivyo hivyo, wengine wanaamini kwamba kila dini ina ubaya na uzuri wake, na kwamba hakuna dini inayoweza kudai kuwa hiyo tu ndiyo ya kweli au ndiyo inayoelekeza watu kwa Mungu.

Maoni hayo yameenea sana kati ya watu wanaodai kwamba hawapingi imani za wengine na wanaofikiri dini zote ni sawa. Mara nyingi wale walio na msimamo tofauti wanaonwa kuwa wenye maoni finyu, au wenye imani kali. Una maoni gani? Je, unafikiri kwamba dini zote zinaelekeza watu kwa Mungu yuleyule? Je, ni sawa tu hata kama mtu anafuata dini gani?

Je, Kweli Mafundisho ya DiniYanapatana?

Ensaiklopidia moja inasema kwamba sasa kuna dini 9,900 duniani. Baadhi ya dini hizo zimesambaa sehemu nyingi ulimwenguni na zina mamilioni ya wafuasi. Inakadiriwa kwamba asilimia 70 ya wanadamu ni wafuasi wa dini tano kubwa ambazo ni dini ya Kiyahudi, Ubudha, Uhindu, Uislamu, na Ukristo. Ikiwa dini zote zinaelekeza watu kwa Mungu yuleyule, bila shaka dini hizo tano zinapaswa kuwa na mambo mengi yanayopatana katika mafundisho yao, na ufafanuzi wao kumhusu Mungu na kusudi lake. Lakini ukweli ni nini?

Hans Küng, mwanatheolojia wa Kanisa Katoliki, anasema kwamba dini kubwa zinapatana katika mafundisho fulani ya msingi kuhusu jinsi watu wanavyopaswa kutendeana. Kwa mfano, dini nyingi zinapinga kuua, kusema uwongo, kuiba, na kufanya ngono na mtu wa ukoo, na zinafundisha kwamba watoto wanapaswa kuwaheshimu wazazi, nao wazazi wanapaswa kuwapenda watoto wao. Lakini katika mambo mengine, na hasa ufafanuzi wao kumhusu Mungu, dini hizo kubwa hazipatani hata kidogo.

Kwa mfano, Wahindu wanaabudu miungu mingi sana, na inasemekana kuwa Wabudha hawana uhakika kwamba Mungu ni halisi. Waislamu wanafundisha kwamba Mungu ni mmoja na ndivyo na makanisa yanayodai kuwa ya Kikristo. Hata hivyo, mengi ya makanisa hayo yanadai pia kwamba Mungu ni Utatu. Isitoshe, makanisa hayo yanafundisha mambo mengi yanayotofautiana. Wakatoliki wanamtukuza Maria, mama ya Yesu, katika ibada yao, lakini Waprotestanti hawafanyi hivyo. Kwa jumla, Wakatoliki wanakatazwa kutumia njia za kuzuia kupata mimba lakini Waprotestanti wengi hawakatazwi. Waprotestanti hawakubaliani ikiwa ni sawa au si sawa kwa watu wa jinsia moja kufanya ngono.

Je, ni jambo linalopatana na akili kufikiri kwamba wafuasi wa dini hizo zote zinazofundisha mambo ambayo yanatofautiana kadiri hiyo, wanaweza kuwa wanamwabudu Mungu yuleyule? Hapana. Kinyume chake, watu hao wanaweza tu kuchanganyikiwa wasijue ukweli kumhusu Mungu na jinsi anavyotaka aabudiwe.

Dini Zinaunganisha Watu au Zinawagawanya?

Ikiwa dini zote zinaelekeza watu kwa Mungu yuleyule, bila shaka tungeona kila moja ikijitahidi sana kuunganisha watu wawe na amani. Je, mambo ya hakika yanathibitisha wanafanya hivyo? Historia inaonyesha kwamba badala ya dini kuunganisha wanadamu inasababisha mgawanyiko na vita. Hebu tuone mifano kadhaa.

Kuanzia karne ya 11 hadi ya 13, mataifa yanayodai kuwa ya Kikristo yalipigana na serikali za Kiislamu katika vita mbalimbali vya dini. Katika karne ya 17 Wakatoliki na Waprotestanti walipigana katika vile Vita vya Miaka 30. Mwaka wa 1947, mara tu Uingereza ilipozipa uhuru nchi za bara Hindi, Wahindu na Waislamu walianza kupigana. Hivi karibuni, Wakatoliki na Waprotestanti wamepigana kwa miaka mingi huko Ireland Kaskazini. Huko Mashariki ya Kati, Wayahudi na Waislamu hawaishi kwa amani. Isitoshe, Vita vya Pili vya Ulimwengu vilipiganwa na dini zote tano kubwa, hata wafuasi wa dini ileile walipigana wakiwa pande tofauti za majeshi ya nchi zilizokuwa zikipigana

Mambo hayo yanaonyesha waziwazi kwamba diniza ulimwengu zimeshindwa kuleta amani na umoja. Pia zimeshindwa kuwaelekeza wanadamu kwa Mungu yuleyule. Badala yake, zimewagawanya na kuwachanganya wasielewe ukweli kumhusu Mungu na jinsi ya kumwabudu. Kwa hiyo, lazima yeyote anayetaka kuwa na uhusiano na Mungu wa kweliachague kwa uangalifu njia atakayofuata. Hilo linapatana na shauri la Biblia, ambayo ni kitabu cha dini cha kale zaidi kinachojulikana na wanadamu.

Jichagulieni Yule Mtakayemtumikia

Biblia inaonyesha wazi kwamba ili kuipata njia itakayokuelekeza kwa Mungu unahitaji kufikiria kwa makini na kufanya uamuzi kwa uangalifu. Yoshua, mtumishi wa Yehova Mungu, aliliambia hivi taifa la kale la Israeli: “Jichagulieni leo yule mtakayemtumikia, kama ni miungu ambayo waliitumikia mababu zenu waliokuwa ng’ambo ile nyingine ya Mto au kama ni miungu ya Waamori ambao mnakaa katika nchi yao. Lakini mimi na nyumba yangu, tutamtumikia Yehova.” Miaka mingi baadaye, nabii Eliya aliwahimiza watu wafanye uamuzi kama huo aliposema: “Mtayumba-yumba juu ya maoni mawili tofauti mpaka wakati gani? Ikiwa Yehova ndiye Mungu wa kweli, mfuateni yeye; lakini ikiwa ni Baali [mungu wa Wakanaani], mfuateni yeye.”—Yoshua 24:15, 16; 1 Wafalme 18:21.

Maandiko hayo na mengineyo yanaonyesha waziwazi kwamba wale waliotaka kumtumikia Mungu wa kweli walihitaji kufanya uamuzi kwa uangalifu. Ndivyo ilivyo leo. Ikiwa tunataka kumtumikia Mungu wa kweli, lazima tufanye uamuzi unaofaa. Lakini ni nini kinachoweza kutusaidia kufanya uamuzi huo kuhusu ibada? Tunaweza kuwatambua waabudu wa kweli jinsi gani?
 
Hapana;

Kuna Dini ambayo ukitoa adhabu ya kuua mwenzako, ndio unapata swawabu (sijui thwawabu; anyway wanajua wenyewe waislamu)
Halafu, kuna ambao Dini zao haziruhusu kuua, hao ni wakristo.

Hapo lazima kila Mmoja ana Mungu wake..
 
Hapana;

Kuna Dini ambayo ukitoa adhabu ya kuua mwenzako, ndio unapata swawabu (sijui thwawabu; anyway wanajua wenyewe waislamu)
Halafu, kuna ambao Dini zao haziruhusu kuua, hao ni wakristo.

Hapo lazima kila Mmoja ana Mungu wake..
So tutaitambuaje ipi ni dini ya kweli au ipi ni ya Mungu wa kweli?
 
Uchambuzi wako ungeenda mbali zaidi mpaka kwenye madhehebu ya dini. Hapa nadhani ndio ingekuwa rahisi kwako kupata conclusion isiyotia shaka.
Dini zote zimejikita kwenye upendo. Hii elimu nimeipata baada ya kuzisoma dini za kibudha, ukristo, uislam na dini za jadi (African Traditional Religion).
 
Hapana;

Kuna Dini ambayo ukitoa adhabu ya kuua mwenzako, ndio unapata swawabu (sijui thwawabu; anyway wanajua wenyewe waislamu)
Halafu, kuna ambao Dini zao haziruhusu kuua, hao ni wakristo.

Hapo lazima kila Mmoja ana Mungu wake..
Kama Yesu ni Mwana wa Mungu maana yake Mungu ni Mkristo, kwa hiyo Ukristo ni Dini ya Kweli, utabisha tu kwa sababu ya ushabiki.
 
Dini zinaelekeza kwa miungu,

Kila dini ina kijiMUNGU chake inachokipigania tofauti na dini nyingine, ndio maana maelezo ya misaafu ya kidini havipatani, km dini zingalikuwa zinaelekeza kwa Mungu mmoja basi misaafu ya kidini yote ingalikuwa inafafa

Mungu si Dini, Dini si Mungu,

Dini ni mawazo ya wanadamu juu ya Mungu,

Asili ya dini zote ni ujinga

Mwisho
Dini ni tegemeo la watu wa jinga na wapumbavu, Bali ni tegemeo la watu wenye Hekima, Busara na Maarifa
 
“Mimi nina dini yangu mwenyewe, na siwezi kuiacha. Isitoshe, dini si hoja, kwa kuwa dini zote zinaelekeza watu kwa Mungu yuleyule.”

JE, UMEWAHI kumsikia mtu akisema hivyo? Watu wengi wanaamini kwamba dini yoyote inaweza kumsaidia mtu kumjua Mungu na kuelewa maana ya maisha. Vivyo hivyo, wengine wanaamini kwamba kila dini ina ubaya na uzuri wake, na kwamba hakuna dini inayoweza kudai kuwa hiyo tu ndiyo ya kweli au ndiyo inayoelekeza watu kwa Mungu.

Maoni hayo yameenea sana kati ya watu wanaodai kwamba hawapingi imani za wengine na wanaofikiri dini zote ni sawa. Mara nyingi wale walio na msimamo tofauti wanaonwa kuwa wenye maoni finyu, au wenye imani kali. Una maoni gani? Je, unafikiri kwamba dini zote zinaelekeza watu kwa Mungu yuleyule? Je, ni sawa tu hata kama mtu anafuata dini gani?

Je, Kweli Mafundisho ya DiniYanapatana?

Ensaiklopidia moja inasema kwamba sasa kuna dini 9,900 duniani. Baadhi ya dini hizo zimesambaa sehemu nyingi ulimwenguni na zina mamilioni ya wafuasi. Inakadiriwa kwamba asilimia 70 ya wanadamu ni wafuasi wa dini tano kubwa ambazo ni dini ya Kiyahudi, Ubudha, Uhindu, Uislamu, na Ukristo. Ikiwa dini zote zinaelekeza watu kwa Mungu yuleyule, bila shaka dini hizo tano zinapaswa kuwa na mambo mengi yanayopatana katika mafundisho yao, na ufafanuzi wao kumhusu Mungu na kusudi lake. Lakini ukweli ni nini?

Hans Küng, mwanatheolojia wa Kanisa Katoliki, anasema kwamba dini kubwa zinapatana katika mafundisho fulani ya msingi kuhusu jinsi watu wanavyopaswa kutendeana. Kwa mfano, dini nyingi zinapinga kuua, kusema uwongo, kuiba, na kufanya ngono na mtu wa ukoo, na zinafundisha kwamba watoto wanapaswa kuwaheshimu wazazi, nao wazazi wanapaswa kuwapenda watoto wao. Lakini katika mambo mengine, na hasa ufafanuzi wao kumhusu Mungu, dini hizo kubwa hazipatani hata kidogo.

Kwa mfano, Wahindu wanaabudu miungu mingi sana, na inasemekana kuwa Wabudha hawana uhakika kwamba Mungu ni halisi. Waislamu wanafundisha kwamba Mungu ni mmoja na ndivyo na makanisa yanayodai kuwa ya Kikristo. Hata hivyo, mengi ya makanisa hayo yanadai pia kwamba Mungu ni Utatu. Isitoshe, makanisa hayo yanafundisha mambo mengi yanayotofautiana. Wakatoliki wanamtukuza Maria, mama ya Yesu, katika ibada yao, lakini Waprotestanti hawafanyi hivyo. Kwa jumla, Wakatoliki wanakatazwa kutumia njia za kuzuia kupata mimba lakini Waprotestanti wengi hawakatazwi. Waprotestanti hawakubaliani ikiwa ni sawa au si sawa kwa watu wa jinsia moja kufanya ngono.

Je, ni jambo linalopatana na akili kufikiri kwamba wafuasi wa dini hizo zote zinazofundisha mambo ambayo yanatofautiana kadiri hiyo, wanaweza kuwa wanamwabudu Mungu yuleyule? Hapana. Kinyume chake, watu hao wanaweza tu kuchanganyikiwa wasijue ukweli kumhusu Mungu na jinsi anavyotaka aabudiwe.

Dini Zinaunganisha Watu au Zinawagawanya?

Ikiwa dini zote zinaelekeza watu kwa Mungu yuleyule, bila shaka tungeona kila moja ikijitahidi sana kuunganisha watu wawe na amani. Je, mambo ya hakika yanathibitisha wanafanya hivyo? Historia inaonyesha kwamba badala ya dini kuunganisha wanadamu inasababisha mgawanyiko na vita. Hebu tuone mifano kadhaa.

Kuanzia karne ya 11 hadi ya 13, mataifa yanayodai kuwa ya Kikristo yalipigana na serikali za Kiislamu katika vita mbalimbali vya dini. Katika karne ya 17 Wakatoliki na Waprotestanti walipigana katika vile Vita vya Miaka 30. Mwaka wa 1947, mara tu Uingereza ilipozipa uhuru nchi za bara Hindi, Wahindu na Waislamu walianza kupigana. Hivi karibuni, Wakatoliki na Waprotestanti wamepigana kwa miaka mingi huko Ireland Kaskazini. Huko Mashariki ya Kati, Wayahudi na Waislamu hawaishi kwa amani. Isitoshe, Vita vya Pili vya Ulimwengu vilipiganwa na dini zote tano kubwa, hata wafuasi wa dini ileile walipigana wakiwa pande tofauti za majeshi ya nchi zilizokuwa zikipigana

Mambo hayo yanaonyesha waziwazi kwamba diniza ulimwengu zimeshindwa kuleta amani na umoja. Pia zimeshindwa kuwaelekeza wanadamu kwa Mungu yuleyule. Badala yake, zimewagawanya na kuwachanganya wasielewe ukweli kumhusu Mungu na jinsi ya kumwabudu. Kwa hiyo, lazima yeyote anayetaka kuwa na uhusiano na Mungu wa kweliachague kwa uangalifu njia atakayofuata. Hilo linapatana na shauri la Biblia, ambayo ni kitabu cha dini cha kale zaidi kinachojulikana na wanadamu.

Jichagulieni Yule Mtakayemtumikia

Biblia inaonyesha wazi kwamba ili kuipata njia itakayokuelekeza kwa Mungu unahitaji kufikiria kwa makini na kufanya uamuzi kwa uangalifu. Yoshua, mtumishi wa Yehova Mungu, aliliambia hivi taifa la kale la Israeli: “Jichagulieni leo yule mtakayemtumikia, kama ni miungu ambayo waliitumikia mababu zenu waliokuwa ng’ambo ile nyingine ya Mto au kama ni miungu ya Waamori ambao mnakaa katika nchi yao. Lakini mimi na nyumba yangu, tutamtumikia Yehova.” Miaka mingi baadaye, nabii Eliya aliwahimiza watu wafanye uamuzi kama huo aliposema: “Mtayumba-yumba juu ya maoni mawili tofauti mpaka wakati gani? Ikiwa Yehova ndiye Mungu wa kweli, mfuateni yeye; lakini ikiwa ni Baali [mungu wa Wakanaani], mfuateni yeye.”—Yoshua 24:15, 16; 1 Wafalme 18:21.

Maandiko hayo na mengineyo yanaonyesha waziwazi kwamba wale waliotaka kumtumikia Mungu wa kweli walihitaji kufanya uamuzi kwa uangalifu. Ndivyo ilivyo leo. Ikiwa tunataka kumtumikia Mungu wa kweli, lazima tufanye uamuzi unaofaa. Lakini ni nini kinachoweza kutusaidia kufanya uamuzi huo kuhusu ibada? Tunaweza kuwatambua waabudu wa kweli jinsi gani?

Very complicated
 
Back
Top Bottom