Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,480
- 30,152
Tupo katika kipindi muhimu sana cha kuelekea kwenye uchaguzi mkuu, mwishoni mwa mwaka huu.
Ni matarajio ya Watanzania wote kuwa vyombo vyetu vya habari vya Umma vitatekeleza wajibu wao kwa usawa bila kupendelea chama chochote cha siasa.
Tumeshuhudia chombo cha habari cha television ya Taifa cha TBC, kikirusha mubashara mkutano mkuu wa chama cha CCM, uliofanyika jijini Dodoma siku chache zilizopita.
Tumeshuhudia chombo hiko cha Umma cha TBC "kikiwagomea" chama kikuu cha upinzani nchini cha Chadema, kurusha matangazo mubashara walipofanya mkutano wao mkuu, mwanzoni mwa wiki, pale katika ukumbi wa Mlimani city.
Tumeshudia pia chombo hicho cha Umma cha televisheni ya Taifa ya TBC "kikigoma" kwa mara nyingine tena kurusha mubashara mkutano mkuu wa chama cha ACT Wazalendo, uliofanyika pale katika ukumbi wa Diamond Jubilee hapo jana.
Hata hivyo nimeshangaa sana kuona chombo hicho cha Umma cha televisheni ya Taifa kikirusha LIVE mkutano mkuu wa chama "kidogo" cha NCCR, ambao unafanyika katika ukumbi wa Diamond hivi leo.
Ndipo hapo nilipojiuliza hivi hii TBC inatumia vigezo gani vya kuchagua chama kipi kiwape LIVE coverage na chama kipi cha siasa kisiwape hiyo nafasi?
Tujikumbushe pia kuwa hiyo TBC inaendeshwa kwa kodi za watanzania wote bila kujali itikadi zetu za kisiasa, kwa maana chimbo hicho kinahudumiwa na walipa kodi wote wa nchi hii, yaani wanachadema,.wanaccm na wa vyama vingine vya siasa bila kujali itikadi zetu za kisiasa.
Kwa hiyo kitendo kinachofanywa na TBC cha "kupendelea" vyama fulani fulani kwa "maagizo" ya watawala wetu wa CCM ni makosa makubwa sana na kitasababisha mpasuko mkubwa sana kwa Taifa hili.
Ni matarajio ya Watanzania wote kuwa vyombo vyetu vya habari vya Umma vitatekeleza wajibu wao kwa usawa bila kupendelea chama chochote cha siasa.
Tumeshuhudia chombo cha habari cha television ya Taifa cha TBC, kikirusha mubashara mkutano mkuu wa chama cha CCM, uliofanyika jijini Dodoma siku chache zilizopita.
Tumeshuhudia chombo hiko cha Umma cha TBC "kikiwagomea" chama kikuu cha upinzani nchini cha Chadema, kurusha matangazo mubashara walipofanya mkutano wao mkuu, mwanzoni mwa wiki, pale katika ukumbi wa Mlimani city.
Tumeshudia pia chombo hicho cha Umma cha televisheni ya Taifa ya TBC "kikigoma" kwa mara nyingine tena kurusha mubashara mkutano mkuu wa chama cha ACT Wazalendo, uliofanyika pale katika ukumbi wa Diamond Jubilee hapo jana.
Hata hivyo nimeshangaa sana kuona chombo hicho cha Umma cha televisheni ya Taifa kikirusha LIVE mkutano mkuu wa chama "kidogo" cha NCCR, ambao unafanyika katika ukumbi wa Diamond hivi leo.
Ndipo hapo nilipojiuliza hivi hii TBC inatumia vigezo gani vya kuchagua chama kipi kiwape LIVE coverage na chama kipi cha siasa kisiwape hiyo nafasi?
Tujikumbushe pia kuwa hiyo TBC inaendeshwa kwa kodi za watanzania wote bila kujali itikadi zetu za kisiasa, kwa maana chimbo hicho kinahudumiwa na walipa kodi wote wa nchi hii, yaani wanachadema,.wanaccm na wa vyama vingine vya siasa bila kujali itikadi zetu za kisiasa.
Kwa hiyo kitendo kinachofanywa na TBC cha "kupendelea" vyama fulani fulani kwa "maagizo" ya watawala wetu wa CCM ni makosa makubwa sana na kitasababisha mpasuko mkubwa sana kwa Taifa hili.