Hivi macho yako yanaona kama mimi yanaona yanayoendelea CHADEMA? Chama kinachoomba ridhaa ya kuongoza Tanzania kwenye uchaguzi huu. Viongozi wa Chama hicho ni kama wamemsusia kila kitu mgombea wao wa kiti cha Urais bwana Tundu Lissu na kumwacha afanye mwenyewe kila kitu.
Hakuna anayejishugulisha, anayempa sapoti wala kuonyesha ushirikiano nae wowote ule.
Tumeshuhudia mikutano yote anayotembea Lissu yuko mwenyewe tu bila kuambatana na viongozi wowote waandamizi wa kitaifa wa Chama hicho. Hatumuoni Mbowe, hatumuoni Kigaila wala hatumuoni John Mnyika. Wote wamemuacha solemba Lissu.
Nenda kwenye mikutano ya waandishi wa habari ambayo kimsingi palitegemewa awe John Mrema kama Mkuu wa Kitengo cha Itikadi na Uenezi kutoa taarifa na kuzungumzia tathmini ya uchaguzi na kampeni za Chadema lakini badala yake Lissu anazunguka mwenyewe mikutano yake yote na pakitokea jambo la kuzungumza analazimika tena huyohuyo mwenyewe Lissu kama mgombea kuzungumza na waandishi wa habari, tofauti na inavyotakiwa na hata tunavyoona kwenye vyama vingine vilivyojipambanua kama taasisi kuwa na kitengo cha uratibu wa kampeni kila mmoja. Hii ndio kali ya mwaka naiona.
Hata ratiba ya kampeni na mikutano ambayo kimsingi ilitakiwa kutolewa na idara ya Itikadi na Uenezi, Lissu anatoa mwenyewe. Kila mtu amemsusia Lissu kampeni zote. Hii ndio maana Lissu amekuwa na mlolongo wa makosa ya uvunjifu mkubwa wa maadili ya uchaguzi ya kujirudia rudia kwenye kila mkutano anaoufanya jambo lililosababisha mpaka akafungiwa kufanya kampeni siku 7. Hii inatokana na ukweli kwamba hakuna anayemfunga kengere tena Lissu na kumnyosha kimaadili na kufuata sheria na taratibu mana Chama chake kimemsusia.
Sasa hapa Watanzania wanaweza kupata picha ya aina ya upinzani na vyama vyetu vya upinzani. Hao ndo tuwape nchi kweli? Watu ambao wao kwa wao tu wenyewe hawapatani na wala hawaelewani, vipi itakuwa kwa Watanzania? Yani ndani ya Chama kimoja kila mtu na lake. Mwenyekiti wa Chama na Katibu wake hakuna anayeonekana kwenye mikutano ya mgombea wao na wala hajui kinachoendelea.
Lissu sasa wamemuacha kisiwani asijue cha kufanya. Kama tulivyozoea kuona kwenye mikutano ya vyama vingine vyenye taasisi imara pakiwa na safu nzima ya uongozi wa Chama kitaifa, viongozi waandamizi na wale wa maeneo husika, kwa Lissu mambo ni tofauti kabisa. Wao kwa wao hawana connection na wala huoni tafsiri ya utaasisi wa vyama vyao. Ni kama kikundi tu cha watu fulani wajanja wajanja wameamua kuhadaa na kurubuni watu ili wapate ruzuku ya Serikali ambayo wakishaipata wamekuwa wakigawana kama mchele mbele ya kuku.
Tukawanyime kura watu hawa Oktoba 28 kwenye sanduku la kura. Nchi hii si ya kuchezea chezea na kuleta usanii. Watanzania wanataka maendeleo na si vinginevyo.
Ni Mimi Kijana Wa Newala, Mtwara.
Hakuna anayejishugulisha, anayempa sapoti wala kuonyesha ushirikiano nae wowote ule.
Tumeshuhudia mikutano yote anayotembea Lissu yuko mwenyewe tu bila kuambatana na viongozi wowote waandamizi wa kitaifa wa Chama hicho. Hatumuoni Mbowe, hatumuoni Kigaila wala hatumuoni John Mnyika. Wote wamemuacha solemba Lissu.
Nenda kwenye mikutano ya waandishi wa habari ambayo kimsingi palitegemewa awe John Mrema kama Mkuu wa Kitengo cha Itikadi na Uenezi kutoa taarifa na kuzungumzia tathmini ya uchaguzi na kampeni za Chadema lakini badala yake Lissu anazunguka mwenyewe mikutano yake yote na pakitokea jambo la kuzungumza analazimika tena huyohuyo mwenyewe Lissu kama mgombea kuzungumza na waandishi wa habari, tofauti na inavyotakiwa na hata tunavyoona kwenye vyama vingine vilivyojipambanua kama taasisi kuwa na kitengo cha uratibu wa kampeni kila mmoja. Hii ndio kali ya mwaka naiona.
Hata ratiba ya kampeni na mikutano ambayo kimsingi ilitakiwa kutolewa na idara ya Itikadi na Uenezi, Lissu anatoa mwenyewe. Kila mtu amemsusia Lissu kampeni zote. Hii ndio maana Lissu amekuwa na mlolongo wa makosa ya uvunjifu mkubwa wa maadili ya uchaguzi ya kujirudia rudia kwenye kila mkutano anaoufanya jambo lililosababisha mpaka akafungiwa kufanya kampeni siku 7. Hii inatokana na ukweli kwamba hakuna anayemfunga kengere tena Lissu na kumnyosha kimaadili na kufuata sheria na taratibu mana Chama chake kimemsusia.
Sasa hapa Watanzania wanaweza kupata picha ya aina ya upinzani na vyama vyetu vya upinzani. Hao ndo tuwape nchi kweli? Watu ambao wao kwa wao tu wenyewe hawapatani na wala hawaelewani, vipi itakuwa kwa Watanzania? Yani ndani ya Chama kimoja kila mtu na lake. Mwenyekiti wa Chama na Katibu wake hakuna anayeonekana kwenye mikutano ya mgombea wao na wala hajui kinachoendelea.
Lissu sasa wamemuacha kisiwani asijue cha kufanya. Kama tulivyozoea kuona kwenye mikutano ya vyama vingine vyenye taasisi imara pakiwa na safu nzima ya uongozi wa Chama kitaifa, viongozi waandamizi na wale wa maeneo husika, kwa Lissu mambo ni tofauti kabisa. Wao kwa wao hawana connection na wala huoni tafsiri ya utaasisi wa vyama vyao. Ni kama kikundi tu cha watu fulani wajanja wajanja wameamua kuhadaa na kurubuni watu ili wapate ruzuku ya Serikali ambayo wakishaipata wamekuwa wakigawana kama mchele mbele ya kuku.
Tukawanyime kura watu hawa Oktoba 28 kwenye sanduku la kura. Nchi hii si ya kuchezea chezea na kuleta usanii. Watanzania wanataka maendeleo na si vinginevyo.
Ni Mimi Kijana Wa Newala, Mtwara.