Je, Chadema kuwa Na. 2 jimbo la Uzini Udini umeshindwa?

Chukuwa hii mwaka 2010 katika jimbo la Uzini Chadema walishika nafasi ya pili kwa kupata 7.6%.

Mwaka 2012 Chadema walishika tena nafasi ya pili Uzini kwa kupata 4%.

Sasa kama una akili tafakari chukua hatua.

Hoja yangu haipo kwenye asilimia? wanajamvi wanakuona unavyohangaika kujiokoa na dhambi yako ya udini.
 
Salaam kwa Malaria Sugu, Rejeo, Ritz, Faizay Fox na wengine wanaoamini katika udini.

Tumeaminishwa kwamba chadema ni chama cha wakristo lakini kimeshika namba 2 kwenye uchaguzi wa jimbo la Uzini, Zanzibar mbele ya CUF ingawa wapo wanaoamini kwamba CUF ni chama cha Waislamu kimekuwa namba 3.

Hakuna chama cha kidini nchi hii.

Uchaguzi huu umetusaidia kujua kwamba kauli mbiu ya udini inachochewa na kundi la watu wachache kwa maslahi yao binafsi lakini naapa hawatashinda. Wenye haki ya kuzuia udini watashinda.

Faizay Fox na wenzake wamejaribu sana kuitangaza chadema ni chama cha wakristo, mnasemaje kuhusu hili JF.

umemsahau Barubaru mkuu
 
we Hamza, siku ile kampeni zinaanza ulituambia chadema walikuwa kanisani wakihamasisha waumini wakitoka waelekee kwenye kampeni, leo unauliza nini!?


Mkuu wa Chuo.

Kumbuka kuwa sijakuambia bali niliandika. maana yake sikumbuki wapi nilikwambia.

Lakin kama ipo sehemu niliandika hivyo. nakuomba uiweke hapa ili tuijadili na kama ikithibitika hivyo nitakuwa wa kwanza kujipiga BAN milele pasi na kuwasubiri Mods.


 
Inna lillahi wainna ilaihi rajihunna.

Huu ni muswiba mkubwa sana.
Kwa kosa gani alilofanya mpaka kupigwa BAN ya maisha?

Inna lillahi wainna ilaihi rajihunna.





Tuacheni waislamu na wakristo tuwe na umoja hayo yameonekana uchaguzi wa uzini pelekeni porojo zenu za udini kwenye koo zenu zilizoacha wajibu wake wa kuwafunza hatari ya udini.
 
Huyo jamaa ana chuki kuu ya kidini

Molemo.
Chadema inabidi wajitafakur kama watakuwa chama makini na viongozi makini.

Wasitafute mchawi kwa kushindwa kwao. Mchawi ni kauli zao Bungeni na nje ya bunge kuhusu Znz na waZnz. Vile vile walitakiwa wasome alama za nyakati kuhusu siasa za Znz.

Lakin la mwisho viongozi wawe na huruma na pesa za posho walizo zoa kule Uzini. Kwani walijua kabisa wanashindwa bali waliongopa kuwa wana nafasi kubwa ya kushukua jimbo hilo.

Nafikiri sasa ni wakti wa kuwachukulia hatua kali viongozi walioweka kami Uzini na kuzoa posho bila kusema ukweli kuwa hakuna uwezekano wa kushinda. Chini ya 5% ni aibu kubwa sana ka Chadme na watendaji wakuu waliweka kambi huko.
 
Inna lillahi wainna ilaihi rajihunna.

Huu ni muswiba mkubwa sana.
Kwa kosa gani alilofanya mpaka kupigwa BAN ya maisha?

Inna lillahi wainna ilaihi rajihunna.




alikuwa ana maneno machafu, sasa Hamza naomba nikuulize eti kipindi kile ulipopata Div I point 10 ukachaguliwa Ilboru katibu wa necta alikuwa dini gani maana kuna sheikh ametoa sababu za kisayansi eti katibu ni sababu ya shule na wanafunzi wa kiislamu kufanya vibaya. Na watu wakampigia makofi.
 
CDM imepata ushindi mkubwa.Udini ziiiiiii...


Udini ziiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii, Malaria sigu na kundi lake ziiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii, wachochea udini ziiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
 
Sasa sijui mie takujibu nini hata historia ya Chadema huijui unasema Chadema hawakuwa na mgombea Uzini uchaguzi uliopita.

Nenda kawaulize viongozi wako watakuambia vizuri kama Chadema walikuwa hawana mgombea jimbo Uzini, wewe unaonekana ni Chadema-Kata.

Mie sio Chadema lakini najua kuwa Chadema walikuwa na mgombea Uzini uchaguzi uliopita. au kwa ili nalo unataka tuminyane?

Huelewi unachokisema.Utahadaa wajinga tu.Wagombea uwakilishi uchaguzi uliopita ni kutoka ccm,cuf na Appt Maendeleo
 
Mkuu wa Chuo.

Kumbuka kuwa sijakuambia bali niliandika. maana yake sikumbuki wapi nilikwambia.

Lakin kama ipo sehemu niliandika hivyo. nakuomba uiweke hapa ili tuijadili na kama ikithibitika hivyo nitakuwa wa kwanza kujipiga BAN milele pasi na kuwasubiri Mods.



kuna thread moja sema nimeisahau tena ilikuwa siku ya Jumapili, lakini hayo maneno yako hayakunifurahisha.
 
Salaam kwa Malaria Sugu, Rejeo, Ritz, Faizay Fox na wengine wanaoamini katika udini.

Tumeaminishwa kwamba chadema ni chama cha wakristo lakini kimeshika namba 2 kwenye uchaguzi wa jimbo la Uzini, Zanzibar mbele ya CUF ingawa wapo wanaoamini kwamba CUF ni chama cha Waislamu kimekuwa namba 3.

Hakuna chama cha kidini nchi hii.

Uchaguzi huu umetusaidia kujua kwamba kauli mbiu ya udini inachochewa na kundi la watu wachache kwa maslahi yao binafsi lakini naapa hawatashinda. Wenye haki ya kuzuia udini watashinda.

Faizay Fox na wenzake wamejaribu sana kuitangaza chadema ni chama cha wakristo, mnasemaje kuhusu hili JF.

"Waliofilisika kifikra na kihoja wakeshashindwa kujieleza, aidha huwa wanajikita katika kutafuta na kujitetea kwa hoja dhaifu za kikabila, kukanda, na mbaya zaidi kidini" - Quote: Mwl Myerere.

Kwa hiyo majibu ya wanaotumia mojawapo ya hizo hoja mfu juu, hatuna msaada kwao, ni muflisi! Hasa CCEM na wachumba wao KAF!
 
Molemo.
Chadema inabidi wajitafakur kama watakuwa chama makini na viongozi makini.

Wasitafute mchawi kwa kushindwa kwao. Mchawi ni kauli zao Bungeni na nje ya bunge kuhusu Znz na waZnz. Vile vile walitakiwa wasome alama za nyakati kuhusu siasa za Znz.

Lakin la mwisho viongozi wawe na huruma na pesa za posho walizo zoa kule Uzini. Kwani walijua kabisa wanashindwa bali waliongopa kuwa wana nafasi kubwa ya kushukua jimbo hilo.

Nafikiri sasa ni wakti wa kuwachukulia hatua kali viongozi walioweka kami Uzini na kuzoa posho bila kusema ukweli kuwa hakuna uwezekano wa kushinda. Chini ya 5% ni aibu kubwa sana ka Chadme na watendaji wakuu waliweka kambi huko.

Maneno hayo waambie CUF wenzako.Tunawapongeza makamanda wote wa CDM kwa kazi kubwa waliyofanya Uzini.Hongereni sana.
 
alikuwa ana maneno machafu, sasa Hamza naomba nikuulize eti kipindi kile ulipopata Div I point 10 ukachaguliwa Ilboru katibu wa necta alikuwa dini gani maana kuna sheikh ametoa sababu za kisayansi eti katibu ni sababu ya shule na wanafunzi wa kiislamu kufanya vibaya. Na watu wakampigia makofi.


Katibu wa baraza la mitihani (mkristo) anawajibika kwa Rais (mwislamu). Ni kweli hili linaweza kuachwa liendelee hata kwenye zama za rais Mwislamu? wakati wa Nyerere (mkristo) tuliambiwa haya!!!!!! Mwinyi (mwislamu) ikaelezwa hivi hivi kwa Mkapa (Mkristo) maneno haya haya.

Nitafurahi sana katibu wa baraza atakaefuata awe mwislamu tuone kama ndilo litakuwa jibu la mwanafunzi wa kiislamu kufanya vizuri mashuleni.
 
Acha uongo wako.CDM haikuweka mgombea kwenye nafasi ya uwakilishi

Wewe ni Chadema-kata hujui chochote muulize Mbowe kama Chadema hawakuweka na mgombea Uzini, uchaguzi uliopita.
 
kuna thread moja sema nimeisahau tena ilikuwa siku ya Jumapili, lakini hayo maneno yako hayakunifurahisha.

Mods,

nakuomba uwaombe Mods wakusaidie kutafuta hayo maneno aliyobainisha kwani mimi nasimamia hapo hapo.
Mkuu wa Chuo.

Kumbuka kuwa sijakuambia bali niliandika. maana yake sikumbuki wapi nilikwambia.

Lakin kama ipo sehemu niliandika hivyo. nakuomba uiweke hapa ili tuijadili na kama ikithibitika hivyo nitakuwa wa kwanza kujipiga BAN milele pasi na kuwasubiri Mods.

 
Mtoto wa Rais Mwanaasha Kikwete pia amefanya vibaya kumbe kwa sababu katibu wa baraza la mtihani ni Mkristo? Kama Rais ana hakika mtoto wake ana akili asingeliacha hili jambo la uonevu lipite hivi hivi. kumbuka katibu huyo ni mteule wa Rais. Tumuogope Mungu.
 
Wewe ni Chadema-kata hujui chochote muulize Mbowe kama Chadema hawakuweka na mgombea Uzini, uchaguzi uliopita.

Narudia tena acha uongo wako hapa CDM haikusimamisha mgombea uwakilishi.Nenda kwenye web ya ZEC.CDM walisimamisha mgombea ubunge aliyeshindana na Seif Khatib.Sasa niambie kati yangu mimi na wewe nani muongo.Umekalia uongo na udini unashindwa hata kusema kitu jinsi kilivyo.Shame on you
 
Tena mnaochochea udini siku yakitokea machafuko ya kwa ajli ya uchochezi wenu wa udini mtakuja kuhukumiwa kwa damu zitakazomwagika au haki itakayodhulumiwa.
 
Naomba niwaonye wadini wote kwamba Arumeru propaganda hiyo haitafua dafu.Chunguzeni watu wanaoishi Arumeru.Poleni sana.
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom