Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,480
- 30,152
Najua kuwa mazungumzo bado yanaendelea kati ya Chama kikuu cha upinzani nchini cha Chadema na Chama cha ACT Wazalendo ya namna ya kuachiana nafasi mbalimbali katika uchaguzi mkuu ujao.
Kwa mazingira niliyoyaona Leo kwa mgombea wa Urais wa chama cha Chadema, Tundu Lissu kuibuka kwenye mkutano mkuu wa ACT Wazalendo, natabiri kuwa mazungumzo ya kuachiana kwa nafasi mbalimbali, yanaendelea vizuri sana na yapo mategemeo makubwa sana ya kufikia muafaka kwa vyama hivyo.
Nafahamu pia hakuna mtanzania asiyefahamu nguvu ya kisiasa ya Maalim Seif, kule Zanzibar.
Kwa hiyo itakuwa kwa maslahi mapana ya upinzani wa nchi hii, kuweza kuunganisha nguvu kwa vile vyama makini, ambavyo kwa sasa naviona kuwa ni hivi vyama viwili vya Chadema na ACT Wazalendo, ili kuwezesha wasizigawe kura hizo kwa hao wagombea.
Nayatakia kila la kheri mazungumzo hayo yanayoendelea, ili hatimaye yafikie muafaka kwa maslahi mapana kwa upinzani nchini na naamini yatakuwa ni "maumivu" makubwa sana kwa jamaa zetu wa chama tawala cha CCM, iwapo mazungumzo hayo yatazaa matunda
Kwa mazingira niliyoyaona Leo kwa mgombea wa Urais wa chama cha Chadema, Tundu Lissu kuibuka kwenye mkutano mkuu wa ACT Wazalendo, natabiri kuwa mazungumzo ya kuachiana kwa nafasi mbalimbali, yanaendelea vizuri sana na yapo mategemeo makubwa sana ya kufikia muafaka kwa vyama hivyo.
Nafahamu pia hakuna mtanzania asiyefahamu nguvu ya kisiasa ya Maalim Seif, kule Zanzibar.
Kwa hiyo itakuwa kwa maslahi mapana ya upinzani wa nchi hii, kuweza kuunganisha nguvu kwa vile vyama makini, ambavyo kwa sasa naviona kuwa ni hivi vyama viwili vya Chadema na ACT Wazalendo, ili kuwezesha wasizigawe kura hizo kwa hao wagombea.
Nayatakia kila la kheri mazungumzo hayo yanayoendelea, ili hatimaye yafikie muafaka kwa maslahi mapana kwa upinzani nchini na naamini yatakuwa ni "maumivu" makubwa sana kwa jamaa zetu wa chama tawala cha CCM, iwapo mazungumzo hayo yatazaa matunda