Uchaguzi 2020 Je, CHADEMA itamuunga mkono Maalim Seif kule Zanzibar na Membe atamuunga mkono Tundu Lissu katika nafasi ya Urais huku Bara?

Kwa kauli yako hii,maana yake hata wewe uliletwa bahati mbaya na mama Karibu Sana ,na pia unauwezo wa kumchagulia mume mama yako na kumuozesha!.
Basi nawe jitahidi usipate mimba kwa bahati mbaya kwa tabia yako ya kukaribisha karibisha hovyo wanaume,maana imani yako ipo kwa mwanaume aliyefungua mlango.
K vant inakuchanganya Nini mbona unatoka nje ya mada,ukiona umelewa sio lazima uni qoute unaweza kusoma tu comment na ukapita kimya kimya mnakwama wapi bawacha?
 
Hiyo ni timu ya propaganda "waliowewezeshwa" na hao jamaa wa kijani, ili wamchafue Mbowe

sasa bahati mbaya mtazamo wa wote waliopo apo wote hawamtaki, amebaki anshangaa tu nn kimetokea yaani mwaka mtam sana huu, cdm tushawaambia hakuna mtu anataka kuwaskia mnalazimisha hilo ni moja bado mengine yanakuja
 
Niwaambie kitu kimoja tu, haiwezekani vyama viwili tofauti viongoze Tanzania na Zanzibar bila nyufa za Muungano kuanza kuleta athari ya kuporomosha Muungano mzima. CCM haipo tayari kuruhusu hilo, na juu chini chini juu CCM Zanzibar lazima ilindwe.
 
Hiyo ni timu ya propaganda "waliowewezeshwa" na hao jamaa wa kijani, ili wamchafue Mbowe
Ili kuthibitisha kama hizo ni propaganda, wewe toa point zako za kuwapinga hao wanaomlalamikia. Vyenginevyo hakuna propaganda zaidi ya ukweli.
 
Are you serious Mtanzania?

Hivi hujui alichokifanya huyo mtu wenu Jecha katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015?

Hivi mtu aliyewahenyesha mno katika uchaguzi mkuu wa 2015, ndiyo leo umuite si lolote wala chochote?
Kwanza itakuwa vizuri kama utanitaka radhi kwa kunituhumu kuwa Jecha ni mtu wangu. Mimi hunijui na wala sikujui. Mimi si mwana chama wa chama chocote kile. Sikjiandikisha kupiga kura na sina lengo la kupiga kura. Nipo hapa kutoa mawazo yangu tu. Pia sijamuita mtu yeyete yule katika post yangu kuwa si lolote wala chochote, hayo ni maneno yako. Usitie maneno yako kwenye kinywa changu.

Sijui mwenzangu kiswahili ni lugha yako ya pili au vipi? Mimi nilichosema ni kuwa mrithi wa urais ameshajulikana, nikimaanisha kabisa kuwa rais anaefuata ni wa ccm hata kama wakishindwa katika kura. Hayo ndio maoni yangu na hata ndugu zangu tupige kelele vipi wazanzibari hatuna umoja wa kuweza kuiondoa ccm zanzibar.

labda niongezee kidogo juu ya kwa nini naamini ccm watarithisha rais wao Zanzibar. Kuna watu wengi zanzibar bado wanakumbuka aliyoyafanya seif sharif wakati wa utawala wa Aboud Jumbe pale walipokwenda bara kutaka kuwepo na serikali tatu. Kuna watu Zanzibar walio ccm na wasio ccm hawamuamini Seif kwa kile alichikifanya walipofika bara. Kadhalika Kuna watu wengi bado wanakumbuka namna issue ya upemba na uunguja iliposhamiri pale Seif alipokuwa waziri wa elimu na baadae waziri kiongozi.

Labda mwenzangu wewe ni mdogo, lakini na wapo watu wengi wanayakumbuka na ingawa wanataka mabdiliko zanzibar, lakini hawamuamini Seif. Ili kuweza kuiondoa ccm zanzibar anahitajika m tu ambae wana ccm wa zanzibar sio tu watampa kura zao bali pia watakuwa tayari kusimama bega kwa bega kudai uhalali wake, na kwa Seif Sharifu hilo ni muhali.



[/QUOTE]
 
Niwaambie kitu kimoja tu, haiwezekani vyama viwili tofauti viongoze Tanzania na Zanzibar bila nyufa za Muungano kuanza kuleta athari ya kuporomosha Muungano mzima. CCM haipo tayari kuruhusu hilo, na juu chini chini juu CCM Zanzibar lazima ilindwe.
chilubi
Naku-quote ulivyosema

Ni lazima CCM ilindwe Zanzibar!

Kwa maana hiyo kwa uliyoyasema, hakuna haja ya uchaguzi Zanzibar!

Nikuambie tu kuwa Maalim Seif ameshaonya kuwa hatakuwa tayari kwa yale aliyoyaona 2015, kwa Jecha "kupindua" matokeo

Hivi unadhani nini kitatokea kwa nyinyi CCM kujiapiza kuwa NI LAZIMA ZANZIBAR ILINDWE?

Tunamuomba Mungu atuepushe na hali hiyo na awape busara nyinyi CCM, kuwa mheshimu uamuzi utakaofanywa na wananchi wa Zanzibar kupitia sanduku la kura. OVA
 
Time will tell
Ukweli upo palepale ningependa sana mabadiliko sababu najua uzuri wake kwa kuishi muda mrefu kwa wenzetu. Lakini ukweli upo palepale sijamuona mwanasiasa serious anayetaka mabadiliko zaidi ya upigaji tu. Miaka miwili mfululizo makada wa Chadema wamemtukana sana Zitto kuwa ni ccm b. Mwaka jana Yericko kampasua vibaya sana hapa na twitter. Leo zimebaki siku chini ya 90 ndiyo akili inawajia na wewe dada yangu unaingia kwenye mkenge huu. CCM wana mtaji tayari wa watu mil 16 mmepigwa pin msifanye mikutano miaka 4 na nusu halafu wenzenu wamepita wakitoa rushwa kuanzia 2018 leo mnataka kujidanganya hapa kua mtashinda.

2015 mpaka juzi tu dada yangu kanielewa. Nilimwambia hivihivi kuhusu mafuriko mpaka akaniblock kwenye simu akidhani nafagilia ccm wakati nilikua namwambia ukweli.
 
Waungane wasiungane hawawezi kushinda watamsindikiza magufuli kwenye ushindi wake wa kishindo,wao wataendelea kuitwa wapinzani mpaka kufa kwao,nje na CCM wakukamata dola hajazaliwa

Hivi vyombo vya dola hupiga kura mara ngapi ?
 
Shauri la Zanzibar, chadema hawana ushawishi hata wa 0.001%, kwa hivyo sio jambo hata la kuletwa mezani, ila kama publicity itapendeza, but not a negotioation agenda.

Bara ipo sababu kubwa yao kukaa kitako na kujadili, lakini chadema wakijua kuwa chadema ya leo sio ya 2015, chadema imekutana na misukosuko mingi ya nje na ndani, na umaarufu wake umetetereka kidogo, na hali ACT umaarufu wake umepanda sana.

Hapa uzuri utakuwa vyama hivi viwe na busara ya kuelewana na sio kuonyeshana misuli.
 
Back
Top Bottom