Je, CHADEMA imenufaika au imepata hasara na ujio wa Mawaziri Wakuu wastaafu? Je, ina la kujifunza?

CalvinKimaro

JF-Expert Member
Sep 11, 2017
244
312
Nadhani huyu ndiye atakuwa Waziri Mkuu mstaafu wa mwisho kuwepo Chadema. Nikitizama Salim, Warioba, Msuya, Pinda na hata Majaliwa sioni uwezekano wowote wa Chadema kupewa fursa ya kumhifadhi Waziri Mkuu mstaafu tena.

Ukichunguza kwa makini utabaini kuwa ujio wa mawaziri wakuu umeiumiza mno chadema. Wanaweza kupuuza kama ilivyo desturi yao lakini hakika majeraha ni makubwa mno.

Ukianza na Lowasa hasara aliyowatia mwaka 2015 katikati ya uchaguzi mkuu ilikuwa kubwa. Nitaje Tu hasara chache.

CHADEMA ilipoteza hoja ya ufisadi. CHADEMA ilipata mshika bendera ambaye hakika hakuwasaidia sana kwenye kampeni. CCM ilipata fursa ya kuibomoa CHADEMA kutokana na mgombea wao.

Ukija kwa Sumaye ni hivyo hivyo. Hoja ya ufisadi isingesimama. Lakini Sumaye kaongeza jeraha baya mno. Kadhihirisha kuwa CHADEMA hakuna demokrasia.

Watamkashifu wee lakini kawaumbua. Jina haliendani na matendo ndani ya chama. Zile tuhuma kuwa Mbowe ndie kila kitu zimethibitika! Zile tuhuma kuwa kuna "inner cabinet" imethibitika. Hiki ndio kimemkimbiza Profesa Safari!

Je, CHADEMA itathubutu tena kupokea wakubwa kutoka CCM? Hakika sasa watakuwa na hofu. Je walioko Chadema na walitoka CCM wako salama? Haswa Nyalandu! Je kuna waliopo CCM watatamani kwenda CHADEMA? Mhhhh!
Hakika Chadema badala ya faida imeambukia hasara! Sasa wataelewa msemo wa "oil chafu"?

Badala ya kumshambulia Sumaye ni vyema wayafanyie kazi mapungufu ambayo Petrobus, Prof Safari na Sumaye wameyaonyesha. Tayari kuna dalili za mpasuko kanda ya Pwani!

Wana UKAWA mtaweza kwenda na CHADEMA? Kama ndani mwao ndio hivi vipi nyie wakuja?
 
Nadhani huyu ndiye atakuwa Waziri Mkuu mstaafu wa mwisho kuwepo Chadema. Nikitizama Salim, Warioba, Msuya, Pinda na hata Majaliwa sioni uwezekano wowote wa Chadema kupewa fursa ya kumhifadhi Waziri Mkuu mstaafu tena.

Ukichunguza kwa makini utabaini kuwa ujio wa mawaziri wakuu umeiumiza mno chadema. Wanaweza kupuuza kama ilivyo desturi yao lakini hakika majeraha ni makubwa mno.

Ukianza na Lowasa hasara aliyowatia mwaka 2015 katikati ya uchaguzi mkuu ilikuwa kubwa. Nitaje Tu hasara chache.

CHADEMA ilipoteza hoja ya ufisadi. CHADEMA ilipata mshika bendera ambaye hakika hakuwasaidia sana kwenye kampeni. CCM ilipata fursa ya kuibomoa CHADEMA kutokana na mgombea wao.

Ukija kwa Sumaye ni hivyo hivyo. Hoja ya ufisadi isingesimama. Lakini Sumaye kaongeza jeraha baya mno. Kadhihirisha kuwa CHADEMA hakuna demokrasia.

Watamkashifu wee lakini kawaumbua. Jina haliendani na matendo ndani ya chama. Zile tuhuma kuwa Mbowe ndie kila kitu zimethibitika! Zile tuhuma kuwa kuna "inner cabinet" imethibitika. Hiki ndio kimemkimbiza Profesa Safari!

Je, CHADEMA itathubutu tena kupokea wakubwa kutoka CCM? Hakika sasa watakuwa na hofu. Je walioko Chadema na walitoka CCM wako salama? Haswa Nyalandu! Je kuna waliopo CCM watatamani kwenda CHADEMA? Mhhhh!
Hakika Chadema badala ya faida imeambukia hasara! Sasa wataelewa msemo wa "oil chafu"?

Badala ya kumshambulia Sumaye ni vyema wayafanyie kazi mapungufu ambayo Petrobus, Prof Safari na Sumaye wameyaonyesha. Tayari kuna dalili za mpasuko kanda ya Pwani!

Wana UKAWA mtaweza kwenda na CHADEMA? Kama ndani mwao ndio hivi vipi nyie wakuja?
Cha kujifunza kwa chadema na viongozi wake ni 1. Kuacha papara inapofanya maamuzi yake.
2. Kutoendekeza tamaa ya mali au pesa.
3. Kutoendekeza uchu wa madaraka.
4. Kuiishi kwa vitendo falsafa ya demokrasia.

Haya mambo yanayoendelea ndani ya chama kwa sasa yanatutia aibu sisi tunaojimwambafy kama wanachama damu wa CHADEMA
 
Una ufinyu wa mawazo na hujui siasa-my dear politics is game of chance ndio maana dunaiani kote unaitwa mchezo mchafu.Kwa maono yako unadhani kuwa kama Chadema wangekuwa na hoja ile ya ufisadi 2015 wangeshindda kiti cha uraisi Big No.
Hata hao akina mbowe wanajua fika kwa mazingira ya kikatiba ya nchi yetu ni ngumu sana chama cha upinzani kuja kupata nafasi ya uraisi-Nadhani lengo lao kubwa la Lowassa kuja ilikuwa ni kutengeneza mgogoro ndani ya CCM ili upinzani iweze kupata viti vingi bungeni,kitu ambacho walifanikiwa.
 
Think tank ya CDM ilikua ni Chacha, Zito, mkumbwa na Dr. Slaa. Hao wengine huwa awatumii ubongo hivo ata uwaeleze vipi, kwao muhimi ni kwenda chooni tuu.
 
Think tank ya CDM ilikua ni Chacha, Zito, mkumbwa na Dr. Slaa. Hao wengine huwa awatumii ubongo hivo ata uwaeleze vipi, kwao muhimi ni kwenda chooni tuu.
Kweli akutukanae hakuchagulii tusi.
 
Mbona huzungumzii faida ya lowassa kusaidia Ruzuku kwa chadema kuongezeka kwa zaidi ya 50% ?

Au hujui kupitia lowassa ndio chadema imepata wabunge wengi na kuongoza halmashauri nyingi toka mfumo wa vyama vingi uanze?

Usihesabu mabaya tu mkumbuke na mazuri mengi aliyowasaidia

Leo chadema mnatamba sababu ya Ongezeko la ruzuku ,mnadhan ni wanachama wenu peke ndio wamewawezesha ,

Mnasahau lowassa alitoka na kundi kubwa CCM ambalo liliongeza idadi ya kura kutoka mil 2 hadi million 6
 
Think tank ya CDM ilikua ni Chacha, Zito, mkumbwa na Dr. Slaa. Hao wengine huwa awatumii ubongo hivo ata uwaeleze vipi, kwao muhimi ni kwenda chooni tuu.
Aisee na CCM ikawachukua waenda chooni kama Prof Mkumbo,Waitara (waziri TAMISEMI) DC Dodoma,Shonza,DAS Kisarawe,na Wabunge waliounga nia ...na wengineo !
Wakati wa kuabudu na kusifu usinyime akili kazi yake ,na kuukabidhi moyo,utaonekana ni kituko!
 
Mbona huzungumzii faida ya lowassa kusaidia Ruzuku kwa chadema kuongezeka kwa zaidi ya 50% ?

Au hujui kupitia lowassa ndio chadema imepata wabunge wengi na kuongoza halmashauri nyingi toka mfumo wa vyama vingi uanze?

Usihesabu mabaya tu mkumbuke na mazuri mengi aliyowasaidia

Leo chadema mnatamba sababu ya Ongezeko la ruzuku ,mnadhan ni wanachama wenu peke ndio wamewawezesha ,

Mnasahau lowassa alitoka na kundi kubwa CCM ambalo liliongeza idadi ya kura kutoka mil 2 hadi million 6

Acha upotoshaji wa mchana kweupe, Lowassa aliikuta Cdm ikiwa imekolea, hata cdm ingesimamisha mbuzi bado ingepata kura nyingi. Watu wengi walijiandikisha kwa hasira kwakuwa walijua Lowassa ndio atachaguliwa na ccm. Hakuna tawi wala mwanachama yoyote aliyeletwa na Lowassa zaidi ya mkewe na genge lake. Baada ya uchaguzi wa 2010 cdm ndio chama kilichowafakia wananchi wengi na kufanya, mikutano na operesheni mbali mbali nchi nzima. Hayo yote yalifanyika Lowassa akiwa ccm akizurura kwenye nyumba za ibada na kugawa hela ili kupata uungwaji mkono.

Neno la kitambulisho cha kura kuitwa kichinjio lililetwa na wapinzani likimaanisha ni kichinjio cha kumchinja Lowassa, kwani wote tulijua kabisa Lowassa ndio atakuwa chaguo la ccm. Alaaniwe Mbowe na genge lake kumpokea huyo tapeli, baada ya kupokea hela yake kisha kumpa nafasi adhimu. Leo hii chama kimeishia kupoteza haiba yake kwa ajili ya hizo taka ngumu toka ccm, kisha unataka kupotosha eti Lowassa ndio alifanya cdm ipate kura nyingi? Huo upotoshaji wapelekee wasiojua lolote.
 
Think tank ya CDM ilikua ni Chacha, Zito, mkumbwa na Dr. Slaa. Hao wengine huwa awatumii ubongo hivo ata uwaeleze vipi, kwao muhimi ni kwenda chooni tuu.

walipoondoka hao DETERIORATION AT RAPID RATE IKAANZA, walipiisha hao, IKAZIKWA,

KWA SASA IMEBAKI YA WAPAYUKAJI TU NA WANAOBISHA KILA KITU MPAKA UKWELI HUU
 
Back
Top Bottom