Je, CCM waliyoianzisha akina Mwalimu Nyerere ingalipo?

Gellangi

JF-Expert Member
Apr 11, 2016
2,756
2,996
Nilikuwepo Februari 1977, nilishiriki paredi ya chipukizi wa chama kipya cha CCM, wakati ule hata Mwenyekiti na viongozi wenzake hawakujivika mavazi yenye rangi kama bendera.

Leo wanafiki wanavaa hadi boxer zao ni bendera lakini ni wezi, wala rushwa, wanajilimbikizia mali na madaraka kwa njia haramu.

Chama hiki cha sasa kimefilisika sera na hoja wanaanza kurejesha uchifu na ubaguzi wa kikabila ili wajirejeshee umaarufu.

CCM imekuwa ya kuogopa kukosolewa na kujitetea kwa ni kuua upinzani/wapinzani?
Unawezaje kujinasibu kuwa unakubalika ilhali hauthubutu kujadili Katiba ya nchi au kuundwa kwa tume huru ya uchaguzi?

Ndiyo maana najiuliza, Hivi CCM ile ya Wakulima na Wafanyakazi ipo au ilikufa pamoja na Azimio la Arusha?

Kwa kuwa Tanzania ni kubwa kuliko vyama, sisi Wananchi wa Tanzania tunataka kuandika Katiba yetu upya ili kuirudisha nchi kwa wenyewe kutoka mikono ya wanasiasa wanaotawala kwa utashi wao.
 
Tumebaki kushereheshwa maadhimisho ya kitu ambacho hakipo.Tutafakari upya mustakabali wa Tanzania badala ya vyama.
 
Nop, haipo, hii CCM ya siku hizi wanasema ina wenyewe, na wenyewe ni wale wenye kundi la kurithishana madaraka, wamekula na kuvimbiwa hata akili zao hazifanyi kazi tena.
 
Haipo. Kama ambavyo Mwanadamu hubadilika kupitia hatua mbali mbali vivho ndivyo vyama vya siasa navyo hubadilika.

Ni upuuzi kuendelea kufiki kwamba CCM ya wakati wa Nyerere iendelee kuwa ile ile ya Leo akina Manifongo na WemaSepetu!

Lazima kiwe na mabadiliko kulingana na nyakati mkuu. Kingeendelea kuwa kama kilivyokuwa wakati ule wa miaka ya mwanzo wa uhuru, Leo kisingekuwa na mwanachama hata mmoja!
 
Nop, haipo, hii CCM ya siku hizi wanasema ina wenyewe, na wenyewe ni wale wenye kundi la kurithishana madaraka, wamekula na kuvimbiwa hata akili zao hazifanyi kazi tena.
Ndiyo maana tunapozingatia historia hiyo,sasa ni dhahiri chini ya CCM hii ya kisasa hatuwezi kuendelea kwa sababu walishaachana na misingi ya uwajibikaji.
Watawala hawa wamepoteza moral authority and legitimacy.
Katiba mpya haiwezi kukwepeka.
 
Haipo. Kama ambavyo Mwanadamu hubadilika kupitia hatua mbali mbali vivho ndivyo vyama vya siasa navyo hubadilika.

Ni upuuzi kuendelea kufiki kwamba CCM ya wakati wa Nyerere iendelee kuwa ile ile ya Leo akina Manifongo na WemaSepetu!

Lazima kiwe na mabadiliko kulingana na nyakati mkuu. Kingeendelea kuwa kama kilivyokuwa wakati ule wa miaka ya mwanzo wa uhuru, Leo kisingekuwa na mwanachama hata mmoja!
Nakubaliana na mabadiliko chanya,nachukia mabadiliko ya kurejea tulikotoka.Kulikoni kuukumbatia uchifu na kukataa Katiba ya Wananchi?

Evolution ya kutoka sera ya Ujamaa na Kujitegemea kwenda kwenye Ujamaa wa Kiuchumi inawezaje kutekelezwa kwa Katiba ile ile ya enzi za Azimio la Arusha?

CCM inapofanya evolution zake nasi wananchi tusio wanachama wenu tunaililia Tanzania mpya itakayoongozwa kwa misingi tutakayoiweka kwenye Katiba mpya.Hatutaki machief wanaovaa nyara za serikali bila vibali halali-ngozi za chui kama mabotu.
 
Hili lichama limekuwa likiendekeza itikadi ya UTEUZI UTEUZI tu hakuna jipya humo CCM ,naona hata huyo SSH anavyoishi anafikiria atateuliwa lini akaamua ajiteue yeye mwenyewe kama HANGAYA.
 
Kuna kundi kimeiteka ccm wengine inaonekana km wakuja lkn yanamwisho haya
Wanaccm hawana cha kuwafanya hao waliokiteka chama zaidi ya kujipendekeza ili wateuliwe kwenye karamu ya kula keki ya taifa sirini.
Raslimali za taifa zinafujwa ila hakuna wa kuhoji wala kuzilinda.Ukithubutu unapotezwa na hakuna wa kuulizwa.
 
Nilikuwepo Februari 1977, nilishiriki paredi ya chipukizi wa chama kipya cha CCM, wakati ule hata Mwenyekiti na viongozi wenzake hawakujivika mavazi yenye rangi kama bendera.

Leo wanafiki wanavaa hadi boxer zao ni bendera lakini ni wezi, wala rushwa, wanajilimbikizia mali na madaraka kwa njia haramu.

Chama hiki cha sasa kimefilisika sera na hoja wanaanza kurejesha uchifu na ubaguzi wa kikabila ili wajirejeshee umaarufu.

CCM imekuwa ya kuogopa kukosolewa na kujitetea kwa ni kuua upinzani/wapinzani?
Unawezaje kujinasibu kuwa unakubalika ilhali hauthubutu kujadili Katiba ya nchi au kuundwa kwa tume huru ya uchaguzi?

Ndiyo maana najiuliza, Hivi CCM ile ya Wakulima na Wafanyakazi ipo au ilikufa pamoja na Azimio la Arusha?

Kwa kuwa Tanzania ni kubwa kuliko vyama, sisi Wananchi wa Tanzania tunataka kuandika Katiba yetu upya ili kuirudisha nchi kwa wenyewe kutoka mikono ya wanasiasa wanaotawala kwa utashi wao.
CCM YA NYERERE HAIPO TENA CCM YA NYERERE haikuogopa Upinzani iliruhusu
Haikubambikiziwa Wapinzani Kesi
Haikuzuia Mikutano ya Vyama


Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
 
Nilikuwepo Februari 1977, nilishiriki paredi ya chipukizi wa chama kipya cha CCM, wakati ule hata Mwenyekiti na viongozi wenzake hawakujivika mavazi yenye rangi kama bendera.

Leo wanafiki wanavaa hadi boxer zao ni bendera lakini ni wezi, wala rushwa, wanajilimbikizia mali na madaraka kwa njia haramu.

Chama hiki cha sasa kimefilisika sera na hoja wanaanza kurejesha uchifu na ubaguzi wa kikabila ili wajirejeshee umaarufu.

CCM imekuwa ya kuogopa kukosolewa na kujitetea kwa ni kuua upinzani/wapinzani?
Unawezaje kujinasibu kuwa unakubalika ilhali hauthubutu kujadili Katiba ya nchi au kuundwa kwa tume huru ya uchaguzi?

Ndiyo maana najiuliza, Hivi CCM ile ya Wakulima na Wafanyakazi ipo au ilikufa pamoja na Azimio la Arusha?

Kwa kuwa Tanzania ni kubwa kuliko vyama, sisi Wananchi wa Tanzania tunataka kuandika Katiba yetu upya ili kuirudisha nchi kwa wenyewe kutoka mikono ya wanasiasa wanaotawala kwa utashi wao.
Hata mimi nilipiga chipukizi nikiwa sekondari. Ilikuwa sherehe kubwa sana ya kuzaliwa CCM; Nyerere alianza kwa sherehe za miaka kumi ya Azimio pale Dar halafu mchana ule akenda Zanzibar kuzindua CCM. Kuzindulia CCM Zanzibar kumesababisha ichukue tabia za Zanzibar za kurithisha madaraka kwenye koo fulani tu; CCM nayo sasa ni mali ya Kikwete na Makamba pamoja na watu wao tu. mama yupo hapo kwa nguvu za hao wenyewe tu, hawezi kuwapinga hata kidogo hata kwa vipi. Kuna mmoja alitangaza wazi kabisa hadharani kuwa "sasa CCM imerudi kwa Wenyewe" wengine wote ni "viroboto" tu na akaukwaa uwaziri!

Mwanzilishi mkubwa wa CCM aliyebaki hai leo ni Pius Msekwa kwani ndiye aliyeandika katiba ya CCM akasimamia zoezi la ubunifu wa bendera, na pia uhakiki wa wimbo wa CCM, na akawa katibu mtendaji wa CCM wa kwanza. Yeye siyo mmoja wa wamiliki wa CCM leo, na hujasikia mtoto au mjukuu wake akilamba uteuzi wowote.
 
Siyo tena ya wakulima na wafanyakazi, ona watumishi wa umma walivyo sahaulika nyongeza ya mishahara miaka 7 sasa.Kweli hii ndiyo Ccm
 
Ile CCM iliamini kila mtu ana haki ya kuheshimiwa na kulinda utu wake .

Lakini hii ya sasa unapigwa risasi mchana kweupe tena ukitokea Bungeni Dodoma kutetea wananchi wako.
 
Siyo tena ya wakulima na wafanyakazi, ona watumishi wa umma walivyo sahaulika nyongeza ya mishahara miaka 7 sasa.Kweli hii ndiyo Ccm
Kutopandishwa mishahara,kuajiri na kulipa mafao yatokanayo na utumishi wa umma limefanywa jambo la kisiasa badala ya kisheria na CCM.
Wanafahamu kuwa watumishi wa umma hawakuwapa kura wakati wa uchaguzi wa 2015 pale CCM ilipogaragazwa na upinzani kote Tanganyika na Zanzibar,hilo linafahamika ila waliiba matokeo.
Huo utafiti wao uliwafumbua macho na yaliyojiri baadaye kwenye uchafuzi 2020 tuliyashuhudia.
CCM hawawezi kupandisha mishahara ya watumishi kama adhabu kwao hasa baada ya kujiridhisha kuwa Watanzania ni wapole na vyama vya wafanyakazi navyo vimetekwa kama na TLS walivyojisalimisha rasmi majuzi.
 
Back
Top Bottom