Je, CCM Inapaswa Kulaumiwa kwa Vijana Kupoteza ari ya Siasa nchini? Tafakari Kuhusu Elimu ya Siasa Tanzania

Apr 8, 2023
24
15
Uko msamiati miongoni mwa wanazuoni wa Kikoloni kuelezea mtu ambaye kwa juhudi na maarifa yake pekee, bila usaidizi wa mtu ama mifumo au jamii fulani ya watu, huweza kufanikisha ama kufanikiwa kuinua maisha yake kwa viwango vya kushangaza. Hili laweza kuwa katika biashara, siasa na kadhalika, na wakoloni humuita mtu wa aina hii "self made" ama aliyejitengeneza mwenyewe.

Baada ya makala yangu juu ya niliyoipa jina "Millennials na GenZ na Siasa za Nchi yetu" kwenye majukwaa tofauti mtandaoni, wengi wamekuja na maoni tofauti. Wakati baadhi wamekuja na kashfa na mitusi (siwalaumu, naelewa hii ni dalili ya kukata tamaa hata kujaribu kutafakari juu ya hili), wako waliosema lawama zinapaswa kuelekezwa kwa chama kinachotawala nchini Tanzania cha CCM kwa "kuua Upinzani" na hivyo kufanya vijana wa sasa kupoteza dira ya mambo yahusuyo siasa. Wako waliodai serikali kupitia mkono wa Dola imewavunja moyo wengi na baadhi wakisingizia madhila yaliyomkuta mwanamuziki "Roma Mkatoliki" kuwa chanzo cha wasanii wetu kuogopa ama kuchukia kuzungumza siasa.

Ebu tutafakari. Kwanza ni je CCM inapaswa kulaumiwa kwa vijana kupoteza hari ya kujihusisha siasa za nchi yao!!? Jibu langu mimi ni "ndiyo". Kwa sababu hari na mapenzi ya siasa miongoni mwa vijana siyo na haijawahi kuwa "self made", mara zote hili limekuwa moja ya mazao bora kabisa ya huyu "Baniani mbaya" aitwaye CCM kupitia mfumo wake wa UVCCM kuandaa viongozi wajao; ni kutoka huko waliandaliwa wanasiasa wote waliowahi na hata wanaoendelea kuwa maarufu katika siasa za Tanzania. Ni CCM iliyoanzisha utamaduni wa kufundisha siasa mashuleni tangu shule za msingi, sekondari, vyuo na hata kwenye majeshi miaka mingi kabla ya ujio wa "Demokrasia" ya kimagharibi na kurejesha sera za vyama vingi, na hivyo siasa kugeuka sumu badala ya somo kwenye elimu msingi.

Wahenga tunakumbuka siasa likiwa somo tangu shule za msingi ambapo ufaulu katika masomo kama sayansi, kilimo, maarifa na siasa vilimpa mtu nafasi ya kwenda sekondari akiwa amejengewa uwezo wa msingi kushiriki vyema mfumo wa maisha wa jamii yake huko aendako. Baada ya 1995, tukabadili (nadhani tulipaswa kuboresha) mitaala na kuondoa kabisa baadhi ya masomo ambayo kimsingi ndiyo yaliyotusaidia wakati huo tukiwa watu milioni kumi na kidogo, tukiwa na wasomi wasiozidi 100 kujenga taifa la watu bora Afrika Mashariki na Afrika nzima, wenye makabila na lugha zaidi ya 120 na bado wanaweza kumaliza tofauti zao kwa majadiliano badala ya mtutu wa bunduki, walau kwa takribani miaka 60 sasa tangu uhuru wa bendera.

Wengi wetu (hata taliokuwapo wakati huo) hatufahamu kwamba hiki kiitwacho "upinzani" hakikuwapo Tanzania isipokuwa tu kwa ridhaa ya waasisi wa CCM baada ya mataifa ya magharibi wakati huo kutishia kutunyima "mikopo na misaada" hadi tutakaporuhusu aina yao ya "demokrasia. Ujamaa ukiwa umeanguka na ukomunist umedhoofu, wazee wetu wakaamua kuwaita kando vijana wao akina Mabere Marando, Mtei, Seif Sharif Hamad na wengine na kuwaagiza "kuanzisha vyama vya upinzani" ili kukidhi matakwa ya kidemokrasia ili pamoja na mambo mengine tuvuke kwenye hali ngumu ya uchumi wa dunia na wa kwetu hasa baada ya vita ya 1978 na Uganda.

Hapo "vikazaliwa" tena vyama vya upinzani na ukawa mwisho wa siasa mashuleni na nyimbo kama "Chama chetu cha Mapinduzi chanjenga Nchi, Nyerere ahaa na Mwinyi na Mwinyi, wajenga nchi.....". Sisemi tulipaswa kuendelea kuimba CCM, nasema tulipaswa kuendelea kuwafundisha watoto na vijana wetu siasa mashuleni kwa faida ya vizazi vijavyo. Labda ndiyo maana fikra tunduizi za siasa zinaonekana kukomea Generation X kwa sasa ndiyo pekee waliokuwa wa mwisho "kufaidi" masomo ya siasa.

Nasema lawama zote ni kwa CCM. Ndiyo, ni CCM aliyekuwa "mzazi" wa wataalamu ambao pia walikuwa na fikra tunduizi za kisiasa. Watu kama Profesa Baregu, Profesa Safari, Daktari Lwaitama ama Padre Willbroad Slaa, walikuwa mazao ya CCM na mafundisho yake ambao hata katika kuanzisha na kuongoza vuguvugu kubwa kabisa la "Uamsho wa kisiasa" kuwahi kuonekana hapa Tanzania kupitia CDM, walikopa karatasi moja ama mbili kutoka kitabu cha CCM, asomaye na afahamu.

Wakati walipoanzisha mfumo wa kushawishi vijana wasomi vyuoni kujiunga na siasa hazaza za upinzani na kuwapa majukwaa ya kufanya "recruitment" ya wenzao, ndipo wakazaliwa wanasiasa waliohamasisha wengi wa Generation X na hata baadhi ya Millennials kuingia siasa. Watu kama Zitto Kabwe, Halima Mdee, John Mnyika na wengine, ni mazao ya juhudi hizi ambazo nazo ni mazao ya mbinu na ubunifu wa CCM. Kwa hiyo ikiwa siasa zetu zimewakinai vijana, wazazi lazima kulaumiwa na wazazi ni CCM.

Nitarejea kujadili ikiwa serikali kwa mkono wa dola imewavunja moyo wengi wa vijana kujihusisha na siasa, ila kwa sasa hizi ni salaam nawasalimia!
 
Hapa tulipofikia ni machafuko au mapinduzi tu ndio yataondoa mfumo CCM. Hakuna kijana yuko tayari kushiriki siasa za kuitukuza CCM ambacho ni chama kizee. Vijana wanataka mambo mapya, sio za hicho chama wanachoona ni cha babu zao.

Chaguzi zetu zimeshapuuzwa rasmi baada ya CCM kulazimisha kukaa madarakani kwa shuruti kwa mbeleko ya vyombo vya dola. Kwa vyovyote vijana watafanya mabadiliko kwa machafuko baada ya ugumu wa maisha kuzidi.
 
Wa kulaumiwa ni chadema. Wakati ule ccm ya kikwete na mzee ndovu ilipokuwa imepoteza ushawishi kwa wananchi, vijana wengi walikuwa na mwamko wa kisiasa kupitia chadema. Tangu chadema ilipoanza kuzorota baada ya ule usaliti wa 2015, vijana wengi walivunjika moyo na mwamko wa kisiasa ukashuka.
 
Wengi wameona siasa ni upuuzi ukizingatia yale yaliyojidhihirisha katika siasa zetu,miaka ya hivi karibuni. Hivyo kijana mwenye akili na weledi zaidi atachukua na kuidharau siasa🤔
 
wazee wetu wakaamua kuwaita kando vijana wao akina Mabere Marando, Mtei, Seif Sharif Hamad na wengine na kuwaagiza "kuanzisha vyama vya upinzani"

mazao ya CCM na mafundisho yake ambao hata katika kuanzisha na kuongoza vuguvugu kubwa kabisa la "Uamsho wa kisiasa"

Wakati walipoanzisha mfumo wa kushawishi vijana wasomi vyuoni kujiunga na siasa

kuwapa majukwaa ya kufanya "recruitment" ya wenzao, ndipo wakazaliwa wanasiasa waliohamasisha wengi wa Generation X

baadhi ya Millennials

Watu kama Zitto Kabwe, Halima Mdee, John Mnyika na wengine, ni mazao ya juhudi hizi

ni mazao ya mbinu na ubunifu wa CCM.

Kulaumiwa kwa Vijana Kupoteza ari ya Siasa nchini?​

ni mazao ya mbinu na ubunifu wa CCM.
Watu kama Zitto Kabwe, Halima Mdee, John Mnyika na wengine, ni mazao ya juhudi hizi
 
Wa kulaumiwa ni chadema. Wakati ule ccm ya kikwete na mzee ndovu ilipokuwa imepoteza ushawishi kwa wananchi, vijana wengi walikuwa na mwamko wa kisiasa kupitia chadema. Tangu chadema ilipoanza kuzorota baada ya ule usaliti wa 2015, vijana wengi walivunjika moyo na mwamko wa kisiasa ukashuka.
Acha kujiroa ufahamu. Kama ni kweli usemavyo (japo sio kweli) ni CDM pekee ndicho Chama cha Upinzani??

Ukweli ni kwamba wakati wa utawala wa Jiwe, aliwatishia Vijana wa Vyuo Vikuu kuwaondolea sifa ya mikopo au kuwafukuza Vyuoni kabisa endapo tu watajihusisha na masuala ya siasa. Na wale wachache walioona hakuna uvunjaji wa sheria hivyo kuendeleza juhudi zao, walikumbwa na misukosuko hata kunusurika vifo. Mfano Abdul Nondo.
 
Kipindi Cha kupigania Uhuru Tanganyika ilikuwa chini ya mfumo wa vyama vingi chini ya utawala wa mkoloni mwengereza(beberu) Cha kushangazaa baada ya nchi kupata Uhuru chini ya TANU na Baadaye CCM (TANU+ASP) wakaanzisha mfumo wa chama kimoja ambao haukuwahi kuwepo kabla sababu kuu ya mabadiliko haya yalikuwa ni uroho na tamaa ya madaraka kama ilivyo hulka kwa viongozi wengine wa Afrika nacha kushangazaa licha ya kuwa chini ya mfumo wa vyama vingi bado wizi wa Kura ulijotokeza wazi wazi mfano ni Kigoma Kura za ndio za Mzee Mwinyi zilizidi idadi ya wapiga Kura.

Twende mbele turudi nyama hotuba ya P.W.Botha licha kwamba ni mbaya iliyo jaa dharau dhidi ya waafrika ila aliongea ukweli mchungu kuhusu Afrika,ni kijana mjinga tu ndio atakuwa bize kufuatilia siasa za kijinga za chama Cha mapinduzi ndani ya hii ,Kolimba kasha wahi sema CCM imepoteza dira kama chama tawala kimepoteza dira unategemea siasa zake nazo zitakuwa na dira gani kwa taifa ? ambazo zinaweza leta mageuzi ya kiuchumi,kisiasa,kijamii nk
 
Ccm wanaogopa ukweli kama kifo na kwa kuwa uongo hubomoa basi kuendekea ni vigumu. Vijana haeatanusurika katika muktadha huu.
 
Wa kulaumiwa ni chadema. Wakati ule ccm ya kikwete na mzee ndovu ilipokuwa imepoteza ushawishi kwa wananchi, vijana wengi walikuwa na mwamko wa kisiasa kupitia chadema. Tangu chadema ilipoanza kuzorota baada ya ule usaliti wa 2015, vijana wengi walivunjika moyo na mwamko wa kisiasa ukashuka.
Sio kweli vijana walijitokeza kwa wingi kupiga kura 2020 zilipoibiwa na CCM wengi walikata tamaa.
 
Sio kweli vijana walijitokeza kwa wingi kupiga kura 2020 zilipoibiwa na CCM wengi walikata tamaa.

Mkuu sio kukata tamaa, bali ni kuzipuuza siasa. Aina ya siasa za kishenzi zilizoletwa na yule mlevi wa madaraka wa awamu ya tano, kisha wawakilishi wa upinzani kwenda kuunga juhudi, kumechangia sana watu kuzipuuza siasa.

Na itachukua muda mrefu watu kurudi kwenye siasa hasa za ushindani, na ili watu warejee kwenye siasa ni lazima yafanyike mabadiliko, na mabadiliko ya kweli sioni yakitokea bila machafuko, ama mapinduzi. Hizi porojo za kina Mbowe za maridhiano naona ni utapeli mtupu.
 
CHADEMA walaumiwe kwa kutumia chama kuwalaghai vijana kwamba Tanzania kuna upinzani😂😂😂
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom