Je, Bunge letu linaendeshwa kikada? Ili tuwe na Bunge la haki, lenye uwezo wa kuisimamia Serikali Kikamilifu, kuna haja Spika asitokane na vyama?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,443
113,452
Wanabodi

Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala fikirishi za "Kwa Maslahi ya Taifa".

Mada ya leo ni swali
Jee kuna uwezekano Bunge letu L
linaendeshwa kikada?. Ili tuwe na Bunge madhubuti la Haki, lenye uwezo wa kuisimamia serikali kikamilifu, jee kuna haja kwa Spika asitokane na vyama vya siasa na mawaziri wasiwe wabunge?

Baada ya kuvuliwa ubunge kwa Mbunge wa Arumeru Mhe. Joshua Nasari, kwa kosa ndogo tuu la kutotoa taarifa ya kutohudhuria mikutano zaidi ya mitatu bila ruhusa ya Spika, kuna wengi wanaona uamuzi wa Spika kama una some elements za ukada ukada!, mfano sijabahatika kumuona au kumsikia Prof. Mhongo akichangia hoja yoyote tangu alipotumbuliwa uwaziri, or let's assume taarifa ya kutoonekana kwake jee zipo mezani kwa Spika?!.

Japo mfumo wa Bunge letu ni mfumo wa Westminster wa Bunge la Uingereza na mabunge ya Commonwealth, lakini katika mfumo wa vyama vingi, ili haki itendeke na kuonekana kuwa haki inatendeka, jee mnaonaje kama tutabadili sheria ili Spika wa Bunge letu asiwe mwanachama wa chama chochote cha siasa, kama walivyo Majaji, ili kuepuka maamuzi ya kikada?.

Kuna uwezekano kabisa wa uamuzi huu wa Spika ni uamuzi wa haki kabisa uliofuata sheria, taratibu na kanuni za Bunge, lakini chama athirika bado kikaona kama kimeonewa, na kuwa haya ni maamuzi ya kikada kukibeba chama chake!. Mbona tunawasikia wabunge wa CCM wakitoa kauli za hovyo na za kiajabu ajabu mule Bungeni lakini sijawahi kusikia wakishurutushwa kufuta kauli au kutolewa nje, inamaana wabunge wakosefu ni wa upinzani tuu?!

Sambamba na hilo, ili tuwe na Bunge imara na madhubuti lenye uwezo wa kuisimamia serikali kikamilifu na ikibidi kuiwajibisha, mnaonaje kama mawaziri wasitokane na wabunge, ili kuutimiza ile dhana ya the principle of separation of powers, checks and balances?.

Bunge linapaswa kuisimamia serikali, na serikali inapoboronga, Bunge letu linatakiwa liwe na uwezo wa kuiwajibisha serikali!, hili bunge jipendekeza na Bunge jikombakomba linaweza kweli kuisimamia serikali?.

Inapotokea Wabunge wenye jukumu la kuisimamia serikali, halafu miongoni mwa Wabunge hao wanateuliwa kuwa mawaziri ambao sio tuu wanakuwa ni sehemu ya serikali, bali wanapokea ulaji, sasa katika mazingira kama haya, Wabunge hawa wanaweza vipi kuiwajibisha serikali wakati wao ni sehemu ya serikali?. Mtu unawezaje kulikata tawi la mtu ulilokalia, au mkono unaokulisha?.

Tena kazi ya Bunge sio tuu kuisimamia serikali au kuiwajibisha serikali, bali ndio mamlaka pekee yenye uwezo wa kumuwajibisha rais wa JMT kwa kumuondoa madarakani!, Bunge letu hili Bunge nyoronyoro, rais wa JMT akivunja katiba wanaweza kumuwajibisha?.

Lakini kwa mfumo wetu, rais ni sehemu ya Bunge kwa kuliunda, kulihutubia na kulivunja, pamoja na kuteua mtendaji Mkuu wa Bunge, ikitokea rais amefanya kosa kubwa mfano la uvunjaji wa Katiba, Bunge likaamua ku initiate impeachment process, lakini kwa mamlaka aliyokuwa nayo rais wa JMT kwa mujibu wa katiba yetu, kabla Bunge halijamuwajibisha rais, rais naweza kulivunjilia mbali Bunge, na kuitisha uchaguzi mwingine!.

Tukija kwenye uteuzi wa wakuu wa mihimili na vyombo vya dola, kama Waziri Mkuu, Jaji Mkuu, CDF, Mkurungezi Mkuu wa TISS, Takukuru, CAG, etc, rais aendelee kuwateua lakini waidhinishwe na Bunge ili kama rais amewateua rafiki zake tuu wasio na sifa au vigezo, Bunge limkatalie, au ikitokea rais amekwenda kinyume cha katiba, vyombo hivi viwe na meno ya kung'ata.

Kwa mfumo huu tulionao sasa wa Spika wa Bunge kutoka chama tawala, hata ikitokea ni kweli rais amevunja Katiba na anapaswa kuwajibishwa, hivi kweli Spika gani anaweza hata ku entertains such motion, yaani ipitishe hoja ya kujadili kumuondoa Mwenyekiti wa chama chake madarakani?, chama kilichokupa huo Uspika?.

Spika asipotokana na chama cha siasa, atakuwa na chance ya kuliendesha Bunge kwa haki bila kutokea hisia za ukada ukada, kama walivyo Majaji, hawana vyama, na kwenye nafasi za juu za utendaji Jaji Mkuu, na wakurugenzi wakuu wote wa taasisi za umma, nafasi zitangazwe, wenye sifa waombe, na sio watu hawana sifa lakini wanateuliwa kwa mserereko.

Nawatakia Furahi Dei Njema.

Wasalaam.
Paskali
Rejea
Wito: Wabunge Badilini Kanuni Kuondoa Udikteta wa Spika/N.Spika! - JamiiForums

Sheria ya Uchaguzi Ni Bad Law!, Kuendelea Kuitumia ni Ujinga?, Kuwabebesha Masikini Gharama za Uchaguzi ni Dhambi!. - JamiiForums

Swali: Jee Spika Anayo Mamlaka Kuzuia Muongozo wa Spika au ni Udikteta Tuu?! - JamiiForums
 
Nadhani moja kati ya vipengele amabavyo vinapaswa kuingizwa kwenye katiba, ni kutoruhusu spika au naibu soika na wasaidizi wake kuwa makada/wanachama wa chama Fulani hii itasaidia sana kulifanya bunge lifanye kazi ya kuisimamia serikali kikamilifu, lakini pia ikionekana spika au viongozi wengine hawafuati kanuni za kuongoza bunge basi, wawe na kipendele kinachowawajibisha.
 
Umetoa hoja konki lakini ukileta wakuu wa vyombo kama tiss mahakama n bunge mathalani katibu mkuu kuidhinishwa Na bunge linalotokana Na vyama vyenye itikadi fulqn Bado hatujatatua tatizo ungeundwa mfumo wa kikatiba viongoz wote km jaji ateuliwe n majaji wenzake kwa vigezo fulan n ubora hvo hvo tiss n majeshi ili mihhimili hii iwe huru Rev constitutional ya Kenya u will get point

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanabodi

Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala fikirishi za "Kwa Maslahi ya Taifa".

Mada ya leo ni swali
Jee Kuna Ewezekano Bunge Letu Linaeshwa Kikada?. Ili Tuwe na Bunge la Haki, Lenye Uwezo wa Kuisimamia Serikali Kikamilifu, Jee Kuna Haja kws Spika Asitokane na Vyama vya Siasa?.

Baada ya kuvuliwa ubunge kwa Mbunge wa Arumeru Mhe. Joshua Nasari, kwa kosa ndogo tuu la kutotoa taarifa ya kutohudhuria mikutano zaidi ya mitatu bila ruhusa ya Spika, kuna wengi wanaona uamuzi wa Spika una some elements za ukada, mfano sijabahatika kumuona au kumsikia Prof. Mhongo akichangia mada yoyote tangu alipotumbuliwa uwaziri, or let's assume taarifa ya kutoonekana kwake zipo kwa Spika.

Japo mfumo wa Bunge letu ni mfumo wa Westminster wa Bunge la Uingereza na mabunge ya Commonwealth, lakini katika mfumo wa vyama vingi, ili haki itendeke na kuonekana kuwa haki inatendeka, jee mnaonaje kama tutabadili sheria ili Spika wa Bunge letu asiwe mwanachama wa chama chochote cha siasa, kuepuka maamuzi ya kikada, na kuna uwezekano kabisa wa uamuzi wa Spika ni uamuzi wa haki kabisa uliofuata sheria, taratibu na kanuni, lakini chama athirika bado kikaona ni maamuzi ya kikada kukibeba chama chake.

Sambamba na hilo, ili tuwe na Bunge imara lenye uwezo wa kuisimamia serikali kikamilifu na ikibidi kuiwajibisha, mnaonaje kama mawaziri wasitokane na wabunge, ili kuutimiza ile dhana ya the principle of separation of powers, checks and balances.

Bunge linapaswa kuisimamia serikali, na inapoboronga, Bunge letu liwe na uwezo wa kuiwajibisha serikali .

Inapotokea Wabunge wenye jukumu la kuisimamia serikali, halafu miongoni mwa Wabunge hao wanateuliwa kuwa mawaziri ambao sio tuu wanakuwa ni sehemu ya serikali, bali wanapokea ulaji, sasa katika mazingira kama haya, Wabunge hawa wanaweza vipi kuiwajibisha serikali wakati wao ni sehemu ya serikali?.

Tena kazi ya Bunge sio tuu kuisimamia serikali au kuiwajibisha serikali, bali ndio mamlaka pekee yenye uwezo wa kumuwajibisha rais kwa kumuondoa madarakani.

Lakini kwa mfumo wetu, rais ni sehemu ya Bunge kwa kuliunda, kulihutubia na kulivunja, pamoja na kuteua mtendaji Mkuu wa Bunge, ikitokea rais amefanya kosa mfano uvunjaji wa Katiba, kabla Bunge halijamuwajibisha, analivunjilia mbali.

Tukija kwenye uteuzi wa Wakuu wa mihimili na vyombo vya dola, kama Waziri Mkuu, Jaji Mkuu, CDF, Mkurungezi Mkuu wa TISS, Takukuru, CAG, etc, rais aendelee kuwateua lakini waidhinishwe na Bunge ili ikitokea rais amekwenda kinyume, vyombo hivi viwe na meno ya kung'ata.

Kwa mfumo huu tulionao, la Spika wa Bunge kutoka chama tawala, hata ikitokea ni kweli rais amevunja Katiba na anapaswa kuwajibishwa, hivi kweli Spika anaweza hata ku entertains such motion, yaani ipitishe hoja ya kujadili kumuondoa Mwenyekiti wa chama chako kilichokupa Uspika?.

Spika asipotokana na chama cha siasa, atakuwa na chance ya kuliendesha Bunge kwa haki bila kutokea hisia za ukada ukada, kama walivyo Majaji, hawana vyama.

Nawatakia Furahi Dei Njema.

Wasalaam.
Paskali
Wewe huwa huelewekagi
 
Pascal suala la vyama ni Imani nikuulize uliwahi kuona wapi ktk maisha yako Dr Bashiru Ally kabla hajateuliwa kuwa mwenyekiti wa kamati ya kuhakiki Mali za Chama akijihusisha na Ukada wa ccm?
Kumbuka kazi ya Uspika ni ya kisiasa kwahiyo hakuna mtu ambaye anaweza kugombea Uspika bila kuwa mwanasiasa.
Spika ni Mbunge automatically kwa mantiki hiyo hakuna mtu anaweza kuwa Mbunge bila kuwa mwanasiasa.
Lakini hata upate Spika malaika kutoka mbinguni kwa vile ataongoza Bunge ambalo linatokana na vyama vya siasa bado maamuzi yake itafuata matakwa ya waliyowengi bungeni ambao kimsingi Ndiyo wapiga kura wake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nashukuru kwa pendekezo lako ambalo hata mimi nadhan nimewah kucomment katika hoja fulan humu ndan. ..lakin pale mwanzo umeongelea suala la Nassari huon kuwa bwana mdogo aliamua kuwachezea shere wenzie kwa akili nyingi na Kwa kujua hamna mwenye akili wa kutambua hilo mapema kwa chadema mana mwanzo CCM iliwasha taa mapema kwa wabunge wake ili waone kama wenzetu watashtuka ndio wakamaliza mchezo.





so Nassari kacheza zaid ya INIESTA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hayo yote ni baadhi ya mapendekezo yaliyotolewa wakati wa mchakato wa katiba mpya ambao licha ya kuligharimu taifa, tumeamua kwa makusudi kuutelekeza.

Inaashiria mfumo uliopo unawanufaisha wachache lakini hauna afya kwa taifa.
Nchi yoyote hata iwe na kanuni na sheria nzuri kiasi gani kama hakuna utashi wa viongozi kuzitii hazisaidii chochote. Kwa mfano sasa hivi msajili wa vyama siyo kada wa chama chochote lakini bado tunaona jinsi anavyofanya kazi zake! Hivyo hivyo hata kukiwa na sheria ya kwamba msajili asitokane na chama chochote lakini bado tu chama chenye nguvu eg CCM kitakuwa na nguvu ya kuweka pandikizi lake. Nadiriki hata kusema kama ingekuwepo sheria inayosema kuwa spika achaguliwe kutoka kwenye chama kikuu cha upinzani bado tu isingekuwa ni solution kwani angeweza ''kununuliwa'' na serikali iliyo madarakani! Demokrasia inataka ustaarabu wa hali ya juu na siyo huu ulafi wa viongozi wetu.
 
Wanabodi

Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala fikirishi za "Kwa Maslahi ya Taifa".

Mada ya leo ni swali
Jee Kuna Ewezekano Bunge Letu Linaeshwa Kikada?. Ili Tuwe na Bunge la Haki, Lenye Uwezo wa Kuisimamia Serikali Kikamilifu, Jee Kuna Haja kws Spika Asitokane na Vyama vya Siasa?.

Baada ya kuvuliwa ubunge kwa Mbunge wa Arumeru Mhe. Joshua Nasari, kwa kosa ndogo tuu la kutotoa taarifa ya kutohudhuria mikutano zaidi ya mitatu bila ruhusa ya Spika, kuna wengi wanaona uamuzi wa Spika una some elements za ukada, mfano sijabahatika kumuona au kumsikia Prof. Mhongo akichangia mada yoyote tangu alipotumbuliwa uwaziri, or let's assume taarifa ya kutoonekana kwake zipo kwa Spika.

Japo mfumo wa Bunge letu ni mfumo wa Westminster wa Bunge la Uingereza na mabunge ya Commonwealth, lakini katika mfumo wa vyama vingi, ili haki itendeke na kuonekana kuwa haki inatendeka, jee mnaonaje kama tutabadili sheria ili Spika wa Bunge letu asiwe mwanachama wa chama chochote cha siasa, kuepuka maamuzi ya kikada, na kuna uwezekano kabisa wa uamuzi wa Spika ni uamuzi wa haki kabisa uliofuata sheria, taratibu na kanuni, lakini chama athirika bado kikaona ni maamuzi ya kikada kukibeba chama chake.

Sambamba na hilo, ili tuwe na Bunge imara lenye uwezo wa kuisimamia serikali kikamilifu na ikibidi kuiwajibisha, mnaonaje kama mawaziri wasitokane na wabunge, ili kuutimiza ile dhana ya the principle of separation of powers, checks and balances.

Bunge linapaswa kuisimamia serikali, na inapoboronga, Bunge letu liwe na uwezo wa kuiwajibisha serikali .

Inapotokea Wabunge wenye jukumu la kuisimamia serikali, halafu miongoni mwa Wabunge hao wanateuliwa kuwa mawaziri ambao sio tuu wanakuwa ni sehemu ya serikali, bali wanapokea ulaji, sasa katika mazingira kama haya, Wabunge hawa wanaweza vipi kuiwajibisha serikali wakati wao ni sehemu ya serikali?.

Tena kazi ya Bunge sio tuu kuisimamia serikali au kuiwajibisha serikali, bali ndio mamlaka pekee yenye uwezo wa kumuwajibisha rais kwa kumuondoa madarakani.

Lakini kwa mfumo wetu, rais ni sehemu ya Bunge kwa kuliunda, kulihutubia na kulivunja, pamoja na kuteua mtendaji Mkuu wa Bunge, ikitokea rais amefanya kosa mfano uvunjaji wa Katiba, kabla Bunge halijamuwajibisha, analivunjilia mbali.

Tukija kwenye uteuzi wa Wakuu wa mihimili na vyombo vya dola, kama Waziri Mkuu, Jaji Mkuu, CDF, Mkurungezi Mkuu wa TISS, Takukuru, CAG, etc, rais aendelee kuwateua lakini waidhinishwe na Bunge ili ikitokea rais amekwenda kinyume, vyombo hivi viwe na meno ya kung'ata.

Kwa mfumo huu tulionao, la Spika wa Bunge kutoka chama tawala, hata ikitokea ni kweli rais amevunja Katiba na anapaswa kuwajibishwa, hivi kweli Spika anaweza hata ku entertains such motion, yaani ipitishe hoja ya kujadili kumuondoa Mwenyekiti wa chama chako kilichokupa Uspika?.

Spika asipotokana na chama cha siasa, atakuwa na chance ya kuliendesha Bunge kwa haki bila kutokea hisia za ukada ukada, kama walivyo Majaji, hawana vyama.

Nawatakia Furahi Dei Njema.

Wasalaam.
Paskali
There is significant mismatch between your topic and content.
Hivi wewe si mwandishi wa habari?
Content yako kwa kiasi kikubwa inaonyesha mambo mawili: Kwanza ni mwingiliano wa bunge na serikali; pili raisi kuwateua watendaji wakuu wa vyombo vya dola.
 
Wanabodi

Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala fikirishi za "Kwa Maslahi ya Taifa".

Mada ya leo ni swali
Jee Kuna Ewezekano Bunge Letu Linaeshwa Kikada?. Ili Tuwe na Bunge la Haki, Lenye Uwezo wa Kuisimamia Serikali Kikamilifu, Jee Kuna Haja kws Spika Asitokane na Vyama vya Siasa?.

Baada ya kuvuliwa ubunge kwa Mbunge wa Arumeru Mhe. Joshua Nasari, kwa kosa ndogo tuu la kutotoa taarifa ya kutohudhuria mikutano zaidi ya mitatu bila ruhusa ya Spika, kuna wengi wanaona uamuzi wa Spika una some elements za ukada, mfano sijabahatika kumuona au kumsikia Prof. Mhongo akichangia mada yoyote tangu alipotumbuliwa uwaziri, or let's assume taarifa ya kutoonekana kwake zipo kwa Spika.

Japo mfumo wa Bunge letu ni mfumo wa Westminster wa Bunge la Uingereza na mabunge ya Commonwealth, lakini katika mfumo wa vyama vingi, ili haki itendeke na kuonekana kuwa haki inatendeka, jee mnaonaje kama tutabadili sheria ili Spika wa Bunge letu asiwe mwanachama wa chama chochote cha siasa, kuepuka maamuzi ya kikada, na kuna uwezekano kabisa wa uamuzi wa Spika ni uamuzi wa haki kabisa uliofuata sheria, taratibu na kanuni, lakini chama athirika bado kikaona ni maamuzi ya kikada kukibeba chama chake.

Sambamba na hilo, ili tuwe na Bunge imara lenye uwezo wa kuisimamia serikali kikamilifu na ikibidi kuiwajibisha, mnaonaje kama mawaziri wasitokane na wabunge, ili kuutimiza ile dhana ya the principle of separation of powers, checks and balances.

Bunge linapaswa kuisimamia serikali, na inapoboronga, Bunge letu liwe na uwezo wa kuiwajibisha serikali .

Inapotokea Wabunge wenye jukumu la kuisimamia serikali, halafu miongoni mwa Wabunge hao wanateuliwa kuwa mawaziri ambao sio tuu wanakuwa ni sehemu ya serikali, bali wanapokea ulaji, sasa katika mazingira kama haya, Wabunge hawa wanaweza vipi kuiwajibisha serikali wakati wao ni sehemu ya serikali?.

Tena kazi ya Bunge sio tuu kuisimamia serikali au kuiwajibisha serikali, bali ndio mamlaka pekee yenye uwezo wa kumuwajibisha rais kwa kumuondoa madarakani.

Lakini kwa mfumo wetu, rais ni sehemu ya Bunge kwa kuliunda, kulihutubia na kulivunja, pamoja na kuteua mtendaji Mkuu wa Bunge, ikitokea rais amefanya kosa mfano uvunjaji wa Katiba, kabla Bunge halijamuwajibisha, analivunjilia mbali.

Tukija kwenye uteuzi wa Wakuu wa mihimili na vyombo vya dola, kama Waziri Mkuu, Jaji Mkuu, CDF, Mkurungezi Mkuu wa TISS, Takukuru, CAG, etc, rais aendelee kuwateua lakini waidhinishwe na Bunge ili ikitokea rais amekwenda kinyume, vyombo hivi viwe na meno ya kung'ata.

Kwa mfumo huu tulionao, la Spika wa Bunge kutoka chama tawala, hata ikitokea ni kweli rais amevunja Katiba na anapaswa kuwajibishwa, hivi kweli Spika anaweza hata ku entertains such motion, yaani ipitishe hoja ya kujadili kumuondoa Mwenyekiti wa chama chako kilichokupa Uspika?.

Spika asipotokana na chama cha siasa, atakuwa na chance ya kuliendesha Bunge kwa haki bila kutokea hisia za ukada ukada, kama walivyo Majaji, hawana vyama.

Nawatakia Furahi Dei Njema.

Wasalaam.
Paskali
Mkuu Mayalla,ni ukweli usiopingika kwamba juhudi za kuelekea huko unakoshauri tuelekee,zilishafutiliwa mbali na wanaojua kucheza na mbongo zetu!

Kama kumbu kumbu zangu zipo sawa sawa,ushauri wako ulijengwa vizuri kabisa katika rasimu ya pili ya iliyokuwa tume ya mabadiliko ya katiba,ikiongozwa na jaji mstaafu,Joseph Sinde Warioba,akisaidiana kwa karibu na wajumbe wengine kama Humphrey Pole Pole, na Prof. wa sheria,Palamagamba Kabudi.

Swali ninalojiuliza,ni je,ushauri wako unawezaje kutekelezeka,endapo juhudi kubwa zilizofanywa kwa utaratibu maalum wa kisheria chini ya watu makini,na matumizi makubwa ya rasilimali muda,na rasilimali fedha,lakini mwisho wa mchakato wote tunaujua,wengine wakatwambia hadharani kwamba habari ya katiba "si kipaumbele tena" sasa unadhani kwa hapa tulipo,nani anaweza kufanya mabadiliko ya sheria unazoshauri zifanyiwe mabadiliko?

Kwa maoni yangu, mfumo uliopo una mapungufu makubwa,lakini ndiyo unaowezesha kutawala kwa raha mustarehe,hivyo kuubadilisha ni "attempt" ya kupelekea kutawala kwa shida na hofu ya kushughulikiwana, je nani yupo tayari kujiingiza kwenye taabu hiyo?

Mzee wetu Jakaya,alijaribu ili akiondoka angalau wanaofuata waanze na mazingira hayo mapya,(kama unavyoshauri),kilichotokea wote tunakijua!
 
sasa hilo ndo swali gani la kuuliza, hivi kuna mtu ambae hajui kuwa bunge linaendeshwa kichama zaidi kuliko kitaasisi
hoja hujibiwa kwa hoja

Jenga hoja kubali au kataa

Nakufundisha kujenga hoja mfano :

Mimi Gussie sikubaliana na Pascal hata Kama spika akiwa si mbunge ni Raia tu bado Mamlaka yake kwa mbunge tunaowachagua ni makubwa Sana, Yatupasa Sisi wananchi kuwawajibisha wabunge wetu kwa kuandaa kura za kutokuwa na imani lakini sio spika kumfukuza mbunge

Sasa wewe Mkuu ulifikiri hapa JF ni Facebook, Jenga hoja wewe
 
Ishu ni "one man show"...hata kama adingetokana na vyama kuna jamaa mmoja juu kule ndio anaamua kila kitu kwa matakwa yake...

Ni wastage of time ikiwa huyo haeshimu Katiba na Sheria
 
Back
Top Bottom