Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,498
- 51,090
Mwaka 2017 rais Museveni kupitia mitandao ya kijamii alitoa taarifa kuwa lile bomba la mafuta litakaotoka nchini mwake kupitia Tanzania litaweza kupita kwenye baadhi ya maeneo nchini ambayo ni hifadhi ya barabara zetu
Majuzi hapa baada ya kukutana kwa raisi Museveni na Magufuli wamekubaliana mpango wa ujenzi wa bomba la mafuta kupitia nchini mwetu uendelee.
Hata hivyo sisi wananchi tungependa kujua
1. Je, kwa nini mkataba wa makubaliano baina yetu na Uganda katika suala hilo unakuwa siri?
2. Kama bomba linapita katika hifadhi ya barabara, je sheria ya hifadhi za barabara imezingatiwa vyema?
3. Tatu, Je, tukipitisha bomba hilo kwenye hifadhi za barabara je hatujifungi sisi wenyewe kushindwa kupanua barabara zetu?
4. Tumebomolea wananchi wetu maelfu kwa maelfu nyumba zao kisa wamejenga katika hifadhi za barabara, Je iweje leo tufunge macho kuhusu kupitisha bomba hilo kwenye hifadhi za barabara hizo wakati hizo hifadhi hazikutengwa makhsusi kwa ajili ya bomba hilo, Au ndo falsafa ya kuhusudu vitu ila linapokuja suala la watu hatujali?.
5. Tunataka kujua, ikitokea umwagikaji wa mafuta kwa bomba kutoboka au kupasuka njiani na uharibifu wa mazingira yetu ukatokea, ni nani atakuwa responsible kugharamia usafishaji wa mazingira na kulipa gharama za majanga ya moto kama ukitokea na kuunguza maelfu ya hekari za misitu na mimea yetu, nyumba na mali za wananchi!
6. Na katika maeneo ya wananchi ambayo hilo bomba litapita, wamewahusishaje wananchi ili kujua haki zao kabla ya kuwekeana mkataba?
Tunataka serikali iweke wazi mikataba ya rasilimali zetu inayoingia kwa niaba yetu
Hii hapa ni tweet ya Museveni akiishukuru serikali ya Tanzania kumpa hifadhi za barabara yake apitishe bomba!
Majuzi hapa baada ya kukutana kwa raisi Museveni na Magufuli wamekubaliana mpango wa ujenzi wa bomba la mafuta kupitia nchini mwetu uendelee.
Hata hivyo sisi wananchi tungependa kujua
1. Je, kwa nini mkataba wa makubaliano baina yetu na Uganda katika suala hilo unakuwa siri?
2. Kama bomba linapita katika hifadhi ya barabara, je sheria ya hifadhi za barabara imezingatiwa vyema?
3. Tatu, Je, tukipitisha bomba hilo kwenye hifadhi za barabara je hatujifungi sisi wenyewe kushindwa kupanua barabara zetu?
4. Tumebomolea wananchi wetu maelfu kwa maelfu nyumba zao kisa wamejenga katika hifadhi za barabara, Je iweje leo tufunge macho kuhusu kupitisha bomba hilo kwenye hifadhi za barabara hizo wakati hizo hifadhi hazikutengwa makhsusi kwa ajili ya bomba hilo, Au ndo falsafa ya kuhusudu vitu ila linapokuja suala la watu hatujali?.
5. Tunataka kujua, ikitokea umwagikaji wa mafuta kwa bomba kutoboka au kupasuka njiani na uharibifu wa mazingira yetu ukatokea, ni nani atakuwa responsible kugharamia usafishaji wa mazingira na kulipa gharama za majanga ya moto kama ukitokea na kuunguza maelfu ya hekari za misitu na mimea yetu, nyumba na mali za wananchi!
6. Na katika maeneo ya wananchi ambayo hilo bomba litapita, wamewahusishaje wananchi ili kujua haki zao kabla ya kuwekeana mkataba?
Tunataka serikali iweke wazi mikataba ya rasilimali zetu inayoingia kwa niaba yetu
Hii hapa ni tweet ya Museveni akiishukuru serikali ya Tanzania kumpa hifadhi za barabara yake apitishe bomba!