Gavana
JF-Expert Member
- Jul 19, 2008
- 33,233
- 8,779
Naona umekuwa msemaji mpaka wa Lucifer 😂😂😂😂Hapana Mungu ndiye muasisi wa Demokrasia.
Hivi kuna demokrasia bila kuruhusu upinzani ?
Watanzania si mlichagua kuwa na vyama vingi na sasa mnalilia Katiba Mpya ili muimarishe Demokrasia ?
Mosi.
Mungu hataki kuwa
Dikteta kama Kim-Jong Un, Raisi wa Korea Kaskazini, ambaye anaua raia wake ili kuwatisha ili wamsikilize yeye tu.
Mungu hataki hivyo, kwakuwa kuna watu hawamtaki Mungu kabisa, anawaheshimu sana, na amewapa muda ili wamrudie kumtii yeye kwa hiari yao.
Ibirisi Lucifer, Shetani Mkuu naye ni mungu pia, na ana miungu yake na waumini anaowaongoza.
Nenda YouTube bofya " Satanic Church" utayaona makanisa ya Shetani na waumini wake.
Shetani hatakiwi kuuwawa, kwakuwa ana wafuasi wengi tu, kwa kujua au kuto kujua. Na wanapenda maisha ya Kishetanishetani, wanataka kuwa huru, hawataki kuamrishwa amrishwa, waache hiki na watende kile.
Pili
Mungu ndiye Muumba wa kila kitu.
Huwa hashauriwi na yeyote. Anafanya kile anachoona kinampendeza Yeye.
Ni kama wewe unapochonga kinyago cha mti wa mpingo, unaweza kukipamba maua na kikiweka kama pambo sebureni.
Siku ikikupendeza unaweza ukakigeuza kuni na kukichoma moto kikaungua kabisa.
Atakuuliza nani ?
Tatu.
Mungu haui mtu, bali unamuondoa duniani na kumpeleka anako ona yeye kunafaa.
Yesu Kristo alimnyanyua na kumpeleka Mbinguni.
Na hakuna namna ya kumchukua mtu zaidi ya Njia ya Kifo. Kwakuwa inabidi auache mwili wake ndipo achukuliwe.
Mwili ni jumba linalokuwezesha kuishi hapa duniani tu.
Mungu akikuchukua unatakiwa uondoke bila mwili, ndio maana unauacha mwili wako na watu wanaufukia.
Wewe huyoooo, unaondoka.