Prof Baregu alikuwa Mwenyekiti wa Kampeni ya Urais ya Bw. Mrema mwaka 1995 ambapo kulikuweko na uchakachuaji mkubwa wa kura uliomwezesha bwana Mkapa na CCM kuupora ushindi na kuwa Rais wakati Bw Marando amekuwa mtu wa ndani ya Usalama wa Taifa kwa muda mrefu. Kwa misingi hiyo, wote wawili wana uzoefu na swali la wizi wa kura: Baregu kwa kuibiwa tena mwaka 1995 na Marando kwa kujua undani wa utendaji wa UWT. Je, walitumiaje uzoefu wao na ujuzi wao kumtahadharisha Dr Slaa na kukiweka Chadema katika mkao wa kupambana na uchakachuaji huo? Au walikuwa wanasema "subiri tuone?"