Vedasto Prosper
Member
- Jul 30, 2013
- 96
- 36
Bendera ya Tanganyika
Kabla ya Uchaguzi wa Mwaka 2015, CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), Zanzibar, kilieleza nia yake ya kutaka kuachiwa mamlaka ya kumchagua mgombea Urais wa Visiwa hivyo, badala ya utaratibu wa sasa unaoshirikisha wenzao wa Tanzania Bara.
Pamoja na hatua hiyo, chama hicho pia kilifikiria kurejea mtindo wa kupokezana kiti cha urais wa Tanzania kati ya bara na visiwani kama ilivyokuwa awali, ili kuweka usawa katika Muungano.
Hatua hiyo inaelezwa kuwa huenda ikazua mpasuko na malumbano mapya kuhusu suala la urais ndani ya CCM.
Vuai Ali Vuai
“Ndani ya CCM tuna utaratibu wetu wa kupata viongozi, lakini hilo suala la kuchaguliwa mgombea urais kutoka kwenye vikao vya Dodoma hata sisi limetugusa… Kwa sasa tuko kwenye mchakato wa kulijadili ili tupate ufumbuzi,” alisema Vuai na kuongeza:
“Siyo tu kuchaguliwa mgombea urais, hata suala la kupokezana urais na jinsi ya kupata viongozi wengine kama wabunge na wawakilishi tunalijadili kwa kina. Ninaamini tutapata ufumbuzi… Siwezi kusema lini kwa kuwa chama chetu ni kikubwa mno, lakini tunalijadili.”
Vuai alitoa kauli hiyo, huku kukiwa na malalamiko ya Wazanzibari wengi kuhusu Muungano, ambapo wengine wanahoji iwapo kuna haja ya kuendelea na utaratibu wa sasa kupata mgombea na Rais wa Zanzibar ambao ni lazima upate baraka za CCM Bara.
Bendera ya Tanganyika
Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Aliyekuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, alisema jambo hilo halijafikishwa kwenye vikao rasmi vya chama.
“Kama wao wanalifikiria hilo, acha waendelee, labda ungewauliza kama wameshalifikisha kwetu. Ukiniuliza mimi nitakujibu kuhusu utaratibu tulionao sasa, ila kama wao wana hoja nyingine, basi watazileta kwenye vikao husika zitajadiliwa,” alisema Nape.
Swali langu ni;
Je, Zanzibar mumeufyata au Msimamo bado upo Palepale?
Nawatakia Uchaguzi mwema.