Je bado mnafanya usafi kila mwisho wa mwezi.??

Adolph Jr

JF-Expert Member
Nov 5, 2016
5,548
8,616
Kwanza shukrani za dhati zimuendee Dr Pombe kwa kuwakumbusha raia kufanya usafi kila jumamosi ya mwisho wa mwezi hakika watu walikuwa wamebadilika sana.

Swali ni Je bado huu utaratibu unaendelea huko kwenu. ??

Maana huku mtaani kwetu Leo nimeamkia kazini mtaani sijakutana na kitu kama hicho na siyo Leo ni muda sasa sijaona hii kitu.

Huko kwenu vipi. .???
 
Kwanza shukrani za dhati zimuendee Dr Pombe kwa kuwakumbusha raia kufanya usafi kila jumamosi ya mwisho wa mwezi hakika watu walikuwa wamebadilika sana. ...
Swali ni Je bado huu utaratibu unaendelea huko kwenu. ??...maana huku mtaani kwetu Leo nimeamkia kazini mtaani sijakutana na kitu kama hicho na siyo Leo ni muda sasa sijaona hii kitu. ..
Huko kwenu vipi. .???
sisi tulifanya siku moja tu,tulivyopiga picha na kuzisambaza kwenye mitandao ya kijamii kutaka sifa basi tukatosheka mkuu!
 
Kwanza shukrani za dhati zimuendee Dr Pombe kwa kuwakumbusha raia kufanya usafi kila jumamosi ya mwisho wa mwezi hakika watu walikuwa wamebadilika sana. ...
Swali ni Je bado huu utaratibu unaendelea huko kwenu. ??...maana huku mtaani kwetu Leo nimeamkia kazini mtaani sijakutana na kitu kama hicho na siyo Leo ni muda sasa sijaona hii kitu. ..
Huko kwenu vipi. .???
Kwani ile sikukuu ya uhuru si ilifutwa ili tufanye Usafi, sasa walipoirudisha maana yake si walifuta usafi automatically!
 
Kwanza shukrani za dhati zimuendee Dr Pombe kwa kuwakumbusha raia kufanya usafi kila jumamosi ya mwisho wa mwezi hakika watu walikuwa wamebadilika sana. ...
Swali ni Je bado huu utaratibu unaendelea huko kwenu. ??...maana huku mtaani kwetu Leo nimeamkia kazini mtaani sijakutana na kitu kama hicho na siyo Leo ni muda sasa sijaona hii kitu. ..
Huko kwenu vipi. .???
Yule aliyetangaza mwenyewe Simuoni
 
Swala la kufanya usafi ni asili ya mtu.,kama watu wana hulka ya kuwa wachafu hata wasimamiwe na jeshi haitasaidia...hata hivyo mimi na boma langu tushafanya usafi si kwa sababu ilitangazwa na mkuu wa nchi ila ni tabia yetu..kuhusu huko mtaani sijui.
 
Bila ushabiki,usafi kila mwisho wa mwezi upo pale pale. Tembelea sokoni,stendi za mabasi na kwenye mikusanyiko ya watu madukani usafi lazima.
 
Swala la kufanya usafi ni asili ya mtu.,kama watu wana hulka ya kuwa wachafu hata wasimamiwe na jeshi haitasaidia...hata hivyo mimi na boma langu tushafanya usafi si kwa sababu ilitangazwa na mkuu wa nchi ila ni tabia yetu..kuhusu huko mtaani sijui.

Jibu zuri sana hili mkuu.....nadhani ifike sasa watu wapewe elimu ya uraia na kujitegemea....na nadhani suala la eti kuitwa wapinzani ni kupinga kila kitu nako huku kutazamwe....pamepwaya sana huku.
 
Siku hizi Juma mosi ya mwisho wa mwezi nisiku ya mazoezi sio usafi kasema Makamu wa Rais
 
Aliyepanga sera na kushindwa kuisimamia hajitambui hata kidogo.Anadhorotesha uchumi wa mtu mmojammoja na taifa kiujumla.
ANAYEBISHA AENDE
KARIAKOO Jumamosi aone watu wanavyochati na wengine kupiga stori tu huku wakisubiri muda wa kufungua biashara, au aende soko lolote hapa dar siku ya Jumamosi ajionee.
Please usiende na magari ya serikali ,maana watu watajifanya wako bize na usafi kumbe moyoni wanachukia.
Boresheni hii sera, sisemi pasiwe na siku ya usafi.TAFADHALI
 
Kawaida ya povu huwa halikai muda mrefu

Mkuu atapiga mkwara

"Walioficha mafagio ya kufanya usafi wajitaje wenyewe,vinginevyo......."
 
imebaki storii hata hawa wakusanya taka majumbani wamebaki kutuchangisha hela tu lakin taka zinazagaa sana maeneo tunapozikusanya
 
Back
Top Bottom