Badilisha chama acha kukaririUelekeo wa awamu ya sita unaonesha upo Kwa ajili ya kurekebisha yaliyofanyika awamu ya tano.
Inavyoonekana kulikuwa na "makosa" mengi sana yaliyokwisha fanyika awamu ya tano ambapo jukumu la kwanza kwa awamu ya sita ni kurekebisha makosa ya awamu iliyopita.
Ukitazama safu ya uongozi katika awamu ya sita na tano haitofautiani sana.
Je, awamu ya sita inajificha nyuma ya kivuli Cha awamu ya Tano?
Je, ni rahisi Kwa awamu ya sita kubakia na clean file?
Je, ni lini hasa tutaona awamu ya sita ikifanya mambo yake bila kuyagusa yale ya awamu iliyopita? Inawezekana?
Je, ni lazima kwamba Kila jambo la awamu ya Tano libadiliashwe?
Je, Kila jambo lililofanyika awamu ya Tano lilikuwa baya?
Naamini awamu ya Saba ikifika yatashuhudiwa mengi ya awamu ya sita kama tulivyoona awamu ya tano Kwa ya sita.
Upanga ule ule unaotumika awamu ya SITA kuichinja awamu ya tano, unawezekana kutumika awamu ya Saba kuichinja awamu ya SITA.