Je, atakuwa ananipenda?

SuperHb

JF-Expert Member
Mar 21, 2016
897
697
Kuna binti nilimtongoza akanichomolea nje kwa kusema tayari ana BOY FRIEND japo alisema hivyo ila tuliendelea kuwasiliana kama kawaida coz nilikuwa na mawasiliano yake.

SASA KINACHONITATIZA.
Kila siku mimi ndie ninayeanzisha mazungumzo ya kuwasiliana, hajawai hata siku moja kuanza yeye.

Siku moja nilimpigia simu akawa hakupokea, tangu siku hiyo nilijua kuwa amenipuuzia, labda anaona najipendekeza kwake, nikaamua kama WIKI 2 kuwa kimya bila kumjulia hali.

Siku moja nikakutana nae face to face, tukasalimiana baada ya hapo akaanza kulalamika. (ETI SIKU HIZI NIMEANZA KUMCHUNIA), akaniuliza KWANINI? Nikamjibu nakuwa BUSY tu wala sijamchunia.

SWALI LANGU
Je, huyo binti ana elements za kunipenda ama?
 
Hapana
Hana elements za kukupenda

Angekupenda lazima ungeona ana 'shobo' na wewe siku moja moja
shobo anazo tukionana live...maana kuna wakati ananiita ofisini kwake tuzungumze
 
Mwanamke akiwa interested na wewe utajua tu
Kwa maelezo yako hapo juu huyo mwanamke hakupendi

Trust me
tukiwa tunaongea face to face interest zinaonekana kwa 80%..kwa ananipenda..maana hata nikiwa wapi anifata mwenyw na kuniomba kampani ya lunch au break fast ,,mpaka apo nakuwa sielewi apo kama ananipenda au la
 
i have agreed according to your views,sina jinsi
Pole mkuu
Mpotezee kuanzia sasa hivi
Kama yupo na the same feelings kama zako am sure atakutafuta

Views zetu zinaweza kuwa sio za kweli so tunasubiri huyo mwanamke atuprove uongo

Stay strong
 
tukiwa tunaongea face to face interest zinaonekana kwa 80%..kwa ananipenda..maana hata nikiwa wapi anifata mwenyw na kuniomba kampani ya lunch au break fast ,,mpaka apo nakuwa sielewi apo kama ananipenda au la
Kwani izo lunch na breakfast nani analipia?km ni ww basi ujue anakua na njaa na hana pesa na ashakusoma unamzimia so lazima bills utalipia tu
 
ngoja nami nishindilie msumari, kaka jua kwamba HUPENDWI! wewe ni kama joker tu kwake na kizuga muda anapokuwa ana msongo! we elewa hivyo maana wengine wameshapitia hali yako
 
Kwani izo lunch na breakfast nani analipia?km ni ww basi ujue anakua na njaa na hana pesa na ashakusoma unamzimia so lazima bills utalipia tu
bills nalipa mimi,siku nyingine yeye,,wakati mwingine tunachangia bills kuilipa
 
Hapo uliposema unaanzisha mawasiliano, basi kaa vumilia uone kama na yeye atakumisi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom