Je, Askari anaruhusiwa kukulazimisha ukiri kosa?

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
625
938
Je, Askari anaruhusiwa kukulazimisha ukiri kosa.png

Jibu la swali lililopo kwenye kichwa cha uzi huu ni HAPANA.

Melezo kwa uchache ni kama ifuatavyo;

Askari Polisi anayo haki na wajibu wa kukuhoji baada ya kukutajia haki zako na kukupa maelezo ya onyo, lakini hana
mamlaka ya kukulazimisha kuongea kitu chochote ambacho hutaki kusema/kukiri makosa ambayo hukufanya au kutoa maelezo.

Ikiwa mtuhumiwa amekataa kuongea ni wajibu wa Polisi kukupeleka Mahakamani ndani ya saa 24.

Ungamo la kosa litokanalo na kuteswa linalofanywa mbele ya Askari Polisi kwa namna yoyote ile halitakubalika Mahakamani kama ushahidi
 
Wengi tu wanawabutua na kwa vile vipigo watu hukazimika kukubali kosa kwa vyovyote vile!

Imekuwa ikisemekana hivyo!

Kama ni kweli basi inabidi jamaa waache kufanya hivyo!
 
Mahakama zina wataalam wa kuweza kubaini ukweli wa mambo hata kama mtuhumiwa alikataa kosa ktk ngazi ya Polisi na ngazi ya mahakama mwanzoni.
 
Viongozi wa Polisi wawakumbushe askari wao mpaka kule chini kabisa mikoani waache hivyo.

Wasitumie ujinga wa wananchi kama fimbo ya kuwachapia.

Yani kama mikoani huko vijijini duuh!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom