Je, ardhi hawana gharama rasmi ya upimaji ramani ya nyumba au ardhi?

Tyupa

JF-Expert Member
Aug 11, 2013
802
653
Kila Mtanzania ana haki ya kupata hati ya kumiliki nyumba au ardhi, vitu ambavyo vinaweza kumsaidia baadae kupata mikopo katika taasisi za Serikali au binafsi.Lakini hadi sasa ni asilimia kumi na tano ( 15 % ) tu ya Watanzania wote wenye kumiliki hati hizi.

Asilimia themanini na tano ( 85 % ) hawana hati za nyumba.Hawa 85 % ambao hawana hati sio kwamba hawapendi kupata hati hizo bali inatokana na ugumu uliojengwa na watu ardhi ambao hutaja gharama kubwa za kutisha.

Ukubwa wa gharama hizo ni moja ya bomu ambalo waziri wa ardhi Mh.Lukuvi hajawahi kulitegua na wala hajui kama lipo.

Kupata hati ya nyumba ugumu wake ni sawa na tajiri alienenwa kwenye biblia kuwa ugumu wa kuuona au kuingia kwenye ufalme wa Mungu ni sawa na ngamia asivyoweza kupenya tundu la sindano.

Taasisi zote za Serikali zina utararatibu maalum uliowekwa wazi juu ya gharama katika kutoa huduma mbali mbali.

Kwa mfano wizara ya afya ina bei elekezi katika kuchangia gharama za matibabu, TANESCO nao wana gharama maalum katika kila huduma wanayotoa, idara ya maji nayo ina mfumo mzuri unaonyesha gharama katika kila huduma wanayotoa.Lakini wizara ya ardhi haina huo utaratibu bali kila mtumishi ana gharama zake ambazo ameziweka kichwani.

Mimi nina nyumba ilioko katika ukubwa wa hatua au mita 70 kwa 40 lakini nimeshindwa kupata hati kwa muda mrefu kwa sababu wahusika wanadai kulipwa milioni tatu hadi tano ( 3, 000,000/= ).

Gharama hizi ni pamoja na kusafirisha vifaa vya kupimia ambavyo wao hudai ni delicate na vinathamani kubwa kupindukia, posho ya wapimaji na usumbufu mwingine.

Gharama hizo zimenishinda na hadi leo sina hati ya nyumba.Gharama hizi ndio hizi hizi ambazo huwakwamisha na watu wengine.

Wizara ilipaswa kuweka bayana gharama zote kuanzia ukubwa fulani wa eneo hadi ukubwa fulani ikiwa na pamoja na kutoa risiti ya Serikali.

Hivi karibuni hapa katika mji mdogo wa Mlandizi idara ya ardhi imetoa tangazo kwa wanainchi wote wa Mlandizi kuwa wajiandikishe kwa ajili ya kupimiwa ardhi au nyumba kwa ajili ya kupata hati ya nyumba.

Gharama zilizotajwa ni aina moja kwa watu wote, uwe una eka moja, nusu eka au robo gharama ni moja.Ikiwa gharama ni moja kwa kila mtu basi wahusika wana uhakika wa kuvuna mabilioni ya hela.

Tunamwomba waziri Lukuvi afike Mlandizi aje atueleze ni vigezo gani hutumika katika upimaji huo na je ikiwa yeye ndie mwenye dhamana na wizara hiyo kwa nini ameshindwa kupanga gharama za upimaji ziwe aina moja na zijulikane pote nchini kwa manufaa ya wote.
 
Naunga mkono hoja. Being tena iwekwe kwenye website kila mwenye ardhi ajue. Hii inaitwa kurahisisha ulipaji bila shuruti
 
Pole sana Mkuu, hao jamaa wa ardhi huwa wanakuwa na makampuni yao binafsi wanayatumia sana, ukienda kama Mserikali au mtu fulani wa kunyoosha maelezo huwa wanakusoma halafu wanakuzingua kama walivyofanya kwa kukuwekea gharama ambayo mwisho wa siku utanawa mikono bila kula mwenyewe.

Sijajua eneo lako ulipo ulipo jenga kama kulishakuwa surveyed, kuna mchoro au eneo limeshapimwa au ni eneo la skwata/ambalo halijapimwa kabisa na watu walishajenga.

Kutegemea na eneo ulilopo jitahidi uwashawishi wenzako wanaokuzunguka mchangie gharama hii ita rahisisha mgawane gharama na itapelekea kupunguza mzigo wa gharama. Mfano jamaa wakileta mashine kwako tu kupima ni milioni tatu ila kukiwa na wenzako kumi au kumi na tano wenye nia kama yako gharama inaweza kuwa milioni kumi ambapo mkishea unakuta mzigo unapungua sana, tulijaribu kufanya hivyo ikatusaidia sana.
Makampuni mengi ya upimaji ardhi huwa hawaweki gharama zao halisi isipokuwa wanaweka katika asilimia, mara nyingi watakuambia utachangia asilimia 25 ya gharama ya ardhi katika upimaji, nitaelezea jinsi wanavyo kokotoa hesabu zao.
Kwa mfano una hekari moja ambayo haijapimwa na zoezi la upimaji, mchoro, kuweka mawe hadi hati litatakiwa vitoke viwanja vinne vya ujazo mdogo au wa kati( low or medium density) kampuni ya upimaji wanachukua kiwanja kimoja katika vinne ambapo ndio asilimia 25 ya gharama yao ya ardhi na wewe unabakiwa na asilimia 75 viwanja vitatu, hii njia nimeona makampuni mengi ya upimaji kwa hapa Dar es salaam sijajua nje ya Dar ipoje.

Kwa eneo ulilokuwepo kama lina ukubwa wa 70 kwa 40 ina maana ukitafuta eneo lako katika mita za mraba ni sawa na 2800 mita za mraba/ square meters, kutegemeana na gharama za mita moja ya mraba katika eneo ulilopo mfano kama wanauza square mita moja kwa shilingi elfu kumi katika eneo lililopo ina maana 2800 mara 10000 ina maana inakuja milioni 28( ambayo ni asilimia mia moja) ya gharama, ukikotoa asilimia 25 ya gharama ya upimaji inakuja milioni 7 inabidi uilipe kampuni.

Ushauri wangu waelimishe wadau wanaokuzunguka muunganishe nguvu muweze kuchangia gharama, vinginevyo utaumia sana Mkuu.
 
Pole sana Mkuu, hao jamaa wa ardhi huwa wanakuwa na makampuni yao binafsi wanayatumia sana, ukienda kama Mserikali au mtu fulani wa kunyoosha maelezo huwa wanakusoma halafu wanakuzingua kama walivyofanya kwa kukuwekea gharama ambayo mwisho wa siku utanawa mikono bila kula mwenyewe.

Sijajua eneo lako ulipo ulipo jenga kama kulishakuwa surveyed, kuna mchoro au eneo limeshapimwa au ni eneo la skwata/ambalo halijapimwa kabisa na watu walishajenga.

Kutegemea na eneo ulilopo jitahidi uwashawishi wenzako wanaokuzunguka mchangie gharama hii ita rahisisha mgawane gharama na itapelekea kupunguza mzigo wa gharama. Mfano jamaa wakileta mashine kwako tu kupima ni milioni tatu ila kukiwa na wenzako kumi au kumi na tano wenye nia kama yako gharama inaweza kuwa milioni kumi ambapo mkishea unakuta mzigo unapungua sana, tulijaribu kufanya hivyo ikatusaidia sana.
Makampuni mengi ya upimaji ardhi huwa hawaweki gharama zao halisi isipokuwa wanaweka katika asilimia, mara nyingi watakuambia utachangia asilimia 25 ya gharama ya ardhi katika upimaji, nitaelezea jinsi wanavyo kokotoa hesabu zao.
Kwa mfano una hekari moja ambayo haijapimwa na zoezi la upimaji, mchoro, kuweka mawe hadi hati litatakiwa vitoke viwanja vinne vya ujazo mdogo au wa kati( low or medium density) kampuni ya upimaji wanachukua kiwanja kimoja katika vinne ambapo ndio asilimia 25 ya gharama yao ya ardhi na wewe unabakiwa na asilimia 75 viwanja vitatu, hii njia nimeona makampuni mengi ya upimaji kwa hapa Dar es salaam sijajua nje ya Dar ipoje.

Kwa eneo ulilokuwepo kama lina ukubwa wa 70 kwa 40 ina maana ukitafuta eneo lako katika mita za mraba ni sawa na 2800 mita za mraba/ square meters, kutegemeana na gharama za mita moja ya mraba katika eneo ulilopo mfano kama wanauza square mita moja kwa shilingi elfu kumi katika eneo lililopo ina maana 2800 mara 10000 ina maana inakuja milioni 28( ambayo ni asilimia mia moja) ya gharama, ukikotoa asilimia 25 ya gharama ya upimaji inakuja milioni 7 inabidi uilipe kampuni.

Ushauri wangu waelimishe wadau wanaokuzunguka muunganishe nguvu muweze kuchangia gharama, vinginevyo utaumia sana Mkuu.
Waziri wa ardhi Mh Lukuvi aje Mlandizi atuambie yeye hizo milioni tatu au saba kwa ukubwa wa hatua au mita 70 kwa 40 ni kwa kigezo gani na hizo mashine za kupimia ambazo ni ghali sana kuliko kitu lingine chochote inakuaje hadi iwe hivyo.Je hayo makampuni ya kupima ardhi yanafanyeje kazi zao ambazo asilimia 85 ( 85 % ) wanashindwa kumudu gharama za upimaji. NI lazima hawa wakifuatiliwa wataonekana wahuni tu. Hospitali mbona kuna mashine delicate na ghali sana kama X ray , MRI, Ct scan ultrasound lakini gharama zake kila mgonjwa anamudu.Hivi hizi mashine za kupimia ardhi kama zinanunuliwa na serkali inakuaje serkali ikikabidhi kwa makampuni yenye hila na ujanja wa kuaibia Watanzania?
 
Adverse effect naona wewe ni mojawapo wa watu ardhi ambao wanakula pesa za watu bila jasho.Kupima hatua 70 x 40 gharama zake iwe milioni saba kama ulivyosema huo ni wizi uliopitiliza ambao ni sawa na unyang'au.
 
Waziri wa ardhi Mh Lukuvi aje Mlandizi atuambie yeye hizo milioni tatu au saba kwa ukubwa wa hatua au mita 70 kwa 40 ni kwa kigezo gani na hizo mashine za kupimia ambazo ni ghali sana kuliko kitu lingine chochote inakuaje hadi iwe hivyo.Je hayo makampuni ya kupima ardhi yanafanyeje kazi zao ambazo asilimia 85 ( 85 % ) wanashindwa kumudu gharama za upimaji. NI lazima hawa wakifuatiliwa wataonekana wahuni tu. Hospitali mbona kuna mashine delicate na ghali sana kama X ray , MRI, Ct scan ultrasound lakini gharama zake kila mgonjwa anamudu.Hivi hizi mashine za kupimia ardhi kama zinanunuliwa na serkali inakuaje serkali ikikabidhi kwa makampuni yenye hila na ujanja wa kuaibia Watanzania?
Mkuu Tyupa, kwanza ningependa uelewe kuwa mimi sio mpimaji wa ardhi na wala sina maslahi yoyote isipokuwa nimetoa mchango kama mdau ambaye pia nilishapitia hiyo kero uliyokuwa nayo ambayo pia wengine inawasumbua pia, kwa hiyo nimechangia mjadala kwa wengine wajifunze pia.

Utekelezaji wa mipango ya wizara ya ardhi inategemea sana na bajeti ya fedha ikiyokuwepo, zoezi na michakato ya upimaji ya ardhi hadi kupata hati linahitaji fedha, vifaa vya upimaji, magari ya kuendea saiti, mafuta, rasilimali watu( ambao ni wataalamu) n.k. Kwa mantiki hii utakuta idara zinazohusika na upimaji ardhi na kutoa hati zinashindwa kutekeleza mipango yake kutokana na ufinyu wa bajeti na ukosefu wa fedha.

Namkubali sana, mheshimiwa Lukuvi waziri wa ardhi kwa juhudi zake, ingawa bado hataweza kufikia malengo ya wizara yake kama inavyotakiwa kutokana na bajeti finyu katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo .

Pia kuhusu gharama za mashine za kupimia ardhi na zile za hospitali kama CT scan, MRI na ultrasound ni kuwa ni vitu viwili tofauti( ambavyo sio sawa kuvilinganisha au kuvifananisha) kwa vigezo ulivyoainisha.
CT scan, MRI haziwafuati wagonjwa au wateja bali wateja au wagonjwa ndio wanazifuata hospitali pale wanapoumwa au kuhitaji hivyo vipimo.

Mwisho ila bado sijamaliza, endelea kumsubiri waziri Lukuvi hapo mlandizi ili aje kutatua kero zinazowakabili
 
Pole sana Mkuu, hao jamaa wa ardhi huwa wanakuwa na makampuni yao binafsi wanayatumia sana, ukienda kama Mserikali au mtu fulani wa kunyoosha maelezo huwa wanakusoma halafu wanakuzingua kama walivyofanya kwa kukuwekea gharama ambayo mwisho wa siku utanawa mikono bila kula mwenyewe.

Sijajua eneo lako ulipo ulipo jenga kama kulishakuwa surveyed, kuna mchoro au eneo limeshapimwa au ni eneo la skwata/ambalo halijapimwa kabisa na watu walishajenga.

Kutegemea na eneo ulilopo jitahidi uwashawishi wenzako wanaokuzunguka mchangie gharama hii ita rahisisha mgawane gharama na itapelekea kupunguza mzigo wa gharama. Mfano jamaa wakileta mashine kwako tu kupima ni milioni tatu ila kukiwa na wenzako kumi au kumi na tano wenye nia kama yako gharama inaweza kuwa milioni kumi ambapo mkishea unakuta mzigo unapungua sana, tulijaribu kufanya hivyo ikatusaidia sana.
Makampuni mengi ya upimaji ardhi huwa hawaweki gharama zao halisi isipokuwa wanaweka katika asilimia, mara nyingi watakuambia utachangia asilimia 25 ya gharama ya ardhi katika upimaji, nitaelezea jinsi wanavyo kokotoa hesabu zao.
Kwa mfano una hekari moja ambayo haijapimwa na zoezi la upimaji, mchoro, kuweka mawe hadi hati litatakiwa vitoke viwanja vinne vya ujazo mdogo au wa kati( low or medium density) kampuni ya upimaji wanachukua kiwanja kimoja katika vinne ambapo ndio asilimia 25 ya gharama yao ya ardhi na wewe unabakiwa na asilimia 75 viwanja vitatu, hii njia nimeona makampuni mengi ya upimaji kwa hapa Dar es salaam sijajua nje ya Dar ipoje.

Kwa eneo ulilokuwepo kama lina ukubwa wa 70 kwa 40 ina maana ukitafuta eneo lako katika mita za mraba ni sawa na 2800 mita za mraba/ square meters, kutegemeana na gharama za mita moja ya mraba katika eneo ulilopo mfano kama wanauza square mita moja kwa shilingi elfu kumi katika eneo lililopo ina maana 2800 mara 10000 ina maana inakuja milioni 28( ambayo ni asilimia mia moja) ya gharama, ukikotoa asilimia 25 ya gharama ya upimaji inakuja milioni 7 inabidi uilipe kampuni.

Ushauri wangu waelimishe wadau wanaokuzunguka muunganishe nguvu muweze kuchangia gharama, vinginevyo utaumia sana Mkuu.
Tumeshajiandikisha Mlandizi nzima lakini tuna mashaka nao, tunamtaka Mh Lukuvi aje au atoe maelezo kwenye vyombo vya habari kuwa huo ndio utaratibu wa serkali wa kuwatoza mamilioni ya pesa hata kama kakiwanja kina hatua 40 x 40.Mh.Lukuvi atueleze pia ni kwa nini ukishapimiwa kiwanja au nyumba hati zinapatikana baada ya miaka mingi.Je kweli ni kwa sababu zinachapishwa mbali Marekani na husafirishwa kwa meli? Mimi binafsi sijawahi kuona wizara ya ajabu kama wizara ya ardhi.
 
Mkuu Tyupa, kwanza ningependa uelewe kuwa mimi sio mpimaji wa ardhi na wala sina maslahi yoyote isipokuwa nimetoa mchango kama mdau ambaye pia nilishapitia hiyo kero uliyokuwa nayo ambayo pia wengine inawasumbua pia, kwa hiyo nimechangia mjadala kwa wengine wajifunze pia.

Utekelezaji wa mipango ya wizara ya ardhi inategemea sana na bajeti ya fedha ikiyokuwepo, zoezi na michakato ya upimaji ya ardhi hadi kupata hati linahitaji fedha, vifaa vya upimaji, magari ya kuendea saiti, mafuta, rasilimali watu( ambao ni wataalamu) n.k. Kwa mantiki hii utakuta idara zinazohusika na upimaji ardhi na kutoa hati zinashindwa kutekeleza mipango yake kutokana na ufinyu wa bajeti na ukosefu wa fedha.

Namkubali sana, mheshimiwa Lukuvi waziri wa ardhi kwa juhudi zake, ingawa bado hataweza kufikia malengo ya wizara yake kama inavyotakiwa kutokana na bajeti finyu katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo .

Pia kuhusu gharama za mashine za kupimia ardhi na zile za hospitali kama CT scan, MRI na ultrasound ni kuwa ni vitu viwili tofauti( ambavyo sio sawa kuvilinganisha au kuvifananisha) kwa vigezo ulivyoainisha.
CT scan, MRI haziwafuati wagonjwa au wateja bali wateja au wagonjwa ndio wanazifuata hospitali pale wanapoumwa au kuhitaji hivyo vipimo.

Mwisho ila bado sijamaliza, endelea kumsubiri waziri Lukuvi hapo mlandizi ili aje kutatua kero zinazowakabili
Tanesco huafuata wateja wake wote majumbani kuwawekea nguzo za umeme na shughuli zingine zinazoendana na kupakiwa umeme lakini gharama zao zote ni fixed na kila mtu anazijua.Idara ya maji kila siku huafuata wateja majumbani kuwafungia maji na gharama zao zinajulikana na kila mtu.Ni idara ya ardhi tu ambayo wafanyakazi wake wanalipwa na serkali lakini linapokuja swala la kupima ardhi wanadai posho nyingine na malipo mengine ya ajabu ajabu kama eti gari ya kubebea vyombo vya kupimia ambavyo ni delicate na expensive kuliko kitu lingine chochote.Nasema hivi kwa sababu nimewahi kuambiwa.Halafu gharama za kupimia zinatofautiana kila sehemu walioko wahudumu wa ardhi hapa nchini.Kama wizara hii hupewa bajeti finyu inakuaje waziri anaehusika asipanga bajeti yake kulingana na mahitaji yake ?
 
Tanesco huafuata wateja wake wote majumbani kuwawekea nguo za umeme na shughuli zingine zinazoendana na kupakiwa umeme lakini GHARAMA zao zote ni fixed na kila mtu anazijua.Idara ya maji kila siku huafuata wateja majumbani kuwafungia maji na gharama zao zinajulikana na kila mtu.Ni idara ya ardhi tu ambayo wafanyakazi wake wanalipwa na serkali lakini linapokuja swala la kupima ardhi wanadai posho nyingine na malipo mengine ya ajabu ajabu kama eti gari ya kubebea vyombo vya kupimia ambavyo ni delicate na expensive kuliko kitu lingine chochote.Nasema hivi kwa sababu nimewahi kuambiwa.Halafu gharama za kupimia zinatofautiana kila sehemu walioko wahudumu wa ardhi hapa nchini.Kama wizara hii hupewa bajeti finyu inakuaje waziri anaehusika asipanga bajeti yake kulingana na mahitaji yake ?
Nafikiri ni kamfumo kaupigaji,kama watu wanalipwa kwa kodi zenu hawakupaswa kulipwa ziada hata magari yanasafiri kwa kodi zetu ndomana kuna huduma nyingi zinatufuata with no extra payment kama polisi,tanesco,maji,nk
 
Pamoja na juhudi za Mh. Lukuvi huko ardhi nadhani bado kuna wapigaji kama huyo hapo juu ingawa anajaribu kujitetea sana. Maelezo yake yamenyooka sawa sawa na yale yanayotolewa na wateule wa Idara ya Ardhi. Kwa mtindo huu ..Squater.. zitaendelea kuota kama uyoga tu.
 
Back
Top Bottom